Naomba nitoe ushuhuda kidogo,
Kuna dogo wa kike sikusoma nae ila tulikutana huko, alikua kadogo dogo ila kazuri ka sura na rangi na kakishua sana(ushua nilikuja kuujua tulipofika chuo)
Sasa kazi nyingi ngumu zilikua zinamshinda japo alikua na morali na anapambana haswa, tumekaa kama mwezi kuna wakati akapotea pale kombania kama siku mbili hivi
Kwakua mm nilikua rafiki yake ikabidi nimuulize rafiki yake mwingine wa kike kua fulani mbona sijamuona kama siku mbili hv, aisee alichonijibu kiliniacha mdomo wazi na nilisikitika sana,
Akaniambia unamjua afande fulani, nikasema ndiyo, akaniambia alikuaga anamtaka dogo na kumtisha kumpa doso akikataa, si unakumbuka kuna wakati tulikua tukipewa utawala dogo anabaki nyuma kidogo, ndo alikua anamtongoza na kumuahidi kua atakua anahakikisha dogo anapunguziwa majukumu, basi msoto ulipokua mkali hasa zile wiki sita za mwanzo naona dogo akajaa,
Na zile siku mbili ambazo hawakuwepo jamaa alimchukua akapeleka gheto kakuta demu bikra kapiga sana dogo karudi yuko hoi, anableed tu, kwahiyo yuko ndani kalala tu, jamaa kamletea antibiotics na ilibidi usiku ule ampeleke pale dispensary ya kambini akapigwa drip tatu za maji,
Baadae dogo mwenyewe alikuja kuniambia kua ni kweli, na anatamani kujimaliza maana amekua ni kujuta kila siku,
baadae tumepangiwa chuo kimoja dogo akawa wakati mwingine analia tu mwenyewe na kudai lile tukio lilimwachia kumbukumbu mbaya sana maana siku hiyo waliopolewa wawili na hao jamaa wawili, ila mwenzake ambae yupo chuo tofauti yeye alivyoanza chuo kwenye ile miezi ya mwanzo alianza kuugua ugua homa haziishi, kwenda kuchek akakuta tayar kaukwaa, kwa sasa ni marehemu(Mwenyezi Mungu ailaze roho ya C*****y mahala pema peponi




)
Ni miaka mingi imepita, lakini namimi ile kitu imeniacha na kumbukumbu mbaya sana, hasa nikimuona au kuwasiliana na yule dada, na nikimkumbuka na marehemu pia
Sisemi kule ni kubaya maana hata mm nilipita lakini kuna wachache wanawageuza madogo wa kike kama kifuta jasho,