Mkuu wa Wilaya ya Mlele, Majid akerwa kukuta mifuko ya saruji imeganda

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,989
Mkuu wa Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi, Majidi Mwanga amekerwa kwa kutelekezwa mradi wa kutengeneza tanki la maji lenye ujazo wa lita milioni moja ambapo saruji ilinunuliwa kwa ajili ya kutekeleza mradi huo ilihifadhiwa vibaya na hatimaye kukutwa imeganda.

Majidi amefanya ziara ya kutembelea vyanzo vya maji katika Kata ya Mamba iliyoko Halmashauri ya Mlele ambapo amekerwa kwa kuona mifuko ya saruji iliyotakiwa kutekeleza mradi wa kutengeneza tanki la maji imeganda kwa sababu ya kuhifadhiwa bila utaratibu mzuri.

Musitafa Kipeta ambaye ni Diwani wa Kata ya Mamba amesema kucheleweshwa kwa mradi huo kitaisababishia Serikali gharama huku Joshua Mbwana ambaye ni Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Mlele amesema fedha za Serikali inatoa pesa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi lakini baadhi ya watu si waaminifu katika kuthamini pesa za serikali.

Mradi huo wa tanki endapo utakamilika utanufaisha Kata ya Mamba, Kata ya Kasansa na Maji Moto ambapo ni zaidi ya wananchi laki mbili.
 
Picha za cement mgando tuzione.... mepita bagamoyo road kwa mbali maeneo ya dawasco Pana Lori kubwa limetelekezwaaa kwa muda mrefu sanaaa, nadhani ni mifuko ya saruji ilogandamana
 
Back
Top Bottom