Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,252
- 113,647
Huyu RC ameanzisha hii operesheni dhidi ya dada poa. Hakuna jipya na hatofanikiwa kamwe. Yeye si wa kwanza na si wa mwisho.
Hana lolote jipya kwenye hiyo operesheni. Nilichokiona labda kilicho na ubunifu [kwa viwango vyao vya akili] ni badala ya askari kupiga doria kwenye maeneo yenye dada poa wengi kwa difenda, badala yake wanajazana kwenye Noah, Bajaji, na vi Ist kwenda kuwastukiza hao wachuuzi. Ni mbinu za kijima na haziko sustainable.
Biashara haijaisha. Ipo na inaendelea vizuri tu. Wachuuzi wamebadili tu namna ya kuifanya kwa muda mfupi halafu watarudia hali yao ya kawaida siku si nyingi zijazo.
Sasa anachofanya huyu RC Chalamila ni microcosm ya kushindwa kuongoza kwa CCM kwa zaidi ya miaka 60 sasa. CCM hawana kabisa mbinu mpya za kutatua matatizo.
Angalia tu hata Rais wao, Kila baada ya muda fulani, anabadili baraza la mawazi.
Wewe mdau toka umeanza kufuatilia mabadiliko ya Mabaraza ya Mawaziri, umeona tofauti gani iliyo ya msingi?
Chama kinachofanya mambo yaleyale na kutegemea yatokee mabadiliko, ni chama kilichofilisika kifikra.
Governor Chalamila hawezi kuua ukahaba kwa kufanya yaleyale ambayo yalishafanywa kabla yake yaliyokuwa na lengo hilo hilo.
Hana lolote jipya kwenye hiyo operesheni. Nilichokiona labda kilicho na ubunifu [kwa viwango vyao vya akili] ni badala ya askari kupiga doria kwenye maeneo yenye dada poa wengi kwa difenda, badala yake wanajazana kwenye Noah, Bajaji, na vi Ist kwenda kuwastukiza hao wachuuzi. Ni mbinu za kijima na haziko sustainable.
Biashara haijaisha. Ipo na inaendelea vizuri tu. Wachuuzi wamebadili tu namna ya kuifanya kwa muda mfupi halafu watarudia hali yao ya kawaida siku si nyingi zijazo.
Sasa anachofanya huyu RC Chalamila ni microcosm ya kushindwa kuongoza kwa CCM kwa zaidi ya miaka 60 sasa. CCM hawana kabisa mbinu mpya za kutatua matatizo.
Angalia tu hata Rais wao, Kila baada ya muda fulani, anabadili baraza la mawazi.
Wewe mdau toka umeanza kufuatilia mabadiliko ya Mabaraza ya Mawaziri, umeona tofauti gani iliyo ya msingi?
Chama kinachofanya mambo yaleyale na kutegemea yatokee mabadiliko, ni chama kilichofilisika kifikra.
Governor Chalamila hawezi kuua ukahaba kwa kufanya yaleyale ambayo yalishafanywa kabla yake yaliyokuwa na lengo hilo hilo.