...Vip wajameni?
Hivi nani hapa asiyeju kuwa kwa katiba yetu wananchi uchagua chama kuunda serikali, na kwa sasa serikali imeundwa na CCM?
Actually, mfano ulikuwa MWENYE DUKA(aliyeingia mkataba wa kutoa huduma kwa wanunuzi aka wananchi ni CCM), na MUUZA DUKA(anayewajibika kuwahudumia wananchi ni serikali kupitia viongozi wake), na kama WAUZA DUKA(viongozi wa serikali) wataharibu, na hivyo kuwakera WANUNUZI(wananchi), WANUNUZI watamchukia MWENYE DUKA(CCM) na kutokwenda tena dukani kwake(KUCHAGUA CHAMA KINGINE).
Kwa mantiki kuwa, wananchi wameichagua CCM iongoze serikali kwa terms zilizoahinishwa kwenye ilani ya uchaguzi ya CCM, 2010/15, hivyo ni wajibu wa viongozi wa CCM kuisimamia serikali kwa ukaribu sana katika kuhakikisha inatekeleza ahadi zake kwa wananchi, pale wanapomuona kiongozi yeyote wa serikali asiyetimiza wajibu wake na kuitumia nafasi yake serikalini kujinufaisha binafsi na kuwaonea wananchi wasimuonee haya, wachukue hatua stahiki za kutoa taarifa ili aondolewe haraka, wasipofanya hivyo na kuwaacha viongozi wa serikali wasiowajibika kwa wananchi,wananchi wataichukia CCM na kuihukumu katika uchaguzi, hivyo kabla CCM haijawajibishwa na wananchi, itawawajibisha viongozi hao wa serikali kupitia serikali yake, na hivyo kuendela kubeba imani ya wananchi kama chama kinachoweza kuwaletea maendelea na mtetezi wa kweli wa wanyonge.
Sioni tatizo lolote hapa hapa..