Mkutano wa CCM Mbeya

Mkutano wa CCM Mbeya

A13.JPG
 
nimeangalia taarifa ya habari ya TBC TV, CCM walikua kwenye mkutano wao jijini Mbeya wamempiga kijembe EL kuhusu kauli yake ya maamuzi magumu wakisema maamuzi yanatakiwa yawe ya makini na ya tija na yatolewe na kiongozi makini. waliotoa kauli hizo ni mwakyembe na ole sendeka.
MY TAKE:
EL. nawe jivue gamba kama mwenzako RA jamaa zako hawakutaki
 
hii picha imepigwa kimtindo na magari nayaona kwa karibu ina maana hapo ndipo mwisho wa watu, kama kuna mtu anapicha aweka sio tunaongea tuu ndio maana magamba wanapiga kelele hiyo nimeitoa michuzi
 
EL alishasema wao wakimwaga ugali yeye anamwaga mboga....haha hi sinema tamu tusubili tuone kama sterling atakufa
 
Hao ni CCJ wanapambana na CCM Mtandao sijui nani atashinda.
 
six anajaribu kusawazisha c aliharibu bungeni kusema wanaopinga posho wanafiki sasa leo kakiri mgao wa umeme serikali inastahili kulaumiwa
 
Diwani wa kata ya nzovwe mby mjini amejiunga ccm kwa kununuliwa kwa ADA ya 7m.Hizi ni habari rasmi kutoka kwa mdogo wake kabisa
 

Kweli Chama Cha Magamba wamefulia!!!!

Hivi wanataka kuwaambianini wana wa MBY????Je ni HIZI SIASA UCHWARA-GUTTER POLITICS kama alivyoziitz jamaa yao RA???

Kwa hesabu za haraka haraka hapa waliovaa magwanda ya magamba wakiandamana hawazidi hata 100. Hapa mbele naona wachovu walewale wa CCM: SS,Nnape,Ole Sendeka,Anne Kilango,Nyalandu,na wengineo.Nyuma hakuna mwanachama yeyote zaidi ya watu walioko pembezoni mwa barabara wakiwashangaa hawa wana Magamba!!!

Wasitegmee chochote pale Mbeya mjini. LILE NI JIMBO LA CHADEMA chini ya uongozi wa Mhe.Sugu.Wao walie tu. Vichwani mwao pale walipo hawana 1 au 2 vichwani mwao kuhusu matatizo sugu yanayowakabili Watanzania kama UKOSEFU WA UMEME na UMASKINI wa kupindukia.

Sana sana wanaweza POSHO MILL ZA MJENGONI TU. Basi.
Na pengine wangelipata akili ya ziada wangemfuata RA kule Igunga wakamchukua na kwenda naye MBY ili kupata kitu cha kuzungumza kuhusu kujivua gamba. Bila shaka watu wangelikwenda mkutanoni kumwona Mpakistani aliyewatukana CCM kuwa WANAENDESHA SIASA UCHWARA-GUTTER POLITICS!!!!!!
Acha washangae jiji la Mbeya lakini hawapati kitu hapa.
 
Kumekucha,naona EX-Chairman wa Chadema anafanya kazi yake kama alivyonunuliwa na kuahidi kuwa ataisambaratisha Chadema Mbeya.
 
Wasitegmee chochote pale Mbeya mjini. LILE NI JIMBO LA CHADEMA chini ya uongozi wa Mhe.Sugu.Wao walie tu. Vichwani mwao pale walipo hawana 1 au 2 vichwani mwao kuhusu matatizo sugu yanayowakabili Watanzania kama UKOSEFU WA UMEME na UMASKINI wa kupindukia.
Acha washangae jiji la Mbeya lakini hawapati kitu hapa.

Not so fast...

Kama ungekuwepo uwanjani ungefikiri upya kuhusu hilo...
 
CDM saizi pesa hamna yote wamemalizia kwenye maandamano yasiokuwa na tija kwa taifa letu, kwa kugawana posho ndio kisa cha huyo diwani kikimbia CDM
 
Watachukua pesa, watachukuwa card, watavaa rangi za kijani saa zote lakini kwenye ballot box watafanya kinyume including huyo Shitambala.
Kwa ushauri wangu ccm wangeacha kabisa hii tabia ya kununua watu maana ndio imewafikisha hapo walipo. Hela ina ukomo! Ni afadhali wabakie na wanachama 5 wa kweli kuliko milini 5 wa kununua.
 
Not so fast...

Kama ungekuwepo uwanjani, ungefikiri upya kuhusu, naamini Sugu kama kweli anabebeka, leo atakuwa amepata onyo kubwa...
Wanafunzi walalamika kulazimishwa kuhudhuria maandamano ya CCM leo


Na Emmanuel Lengwa 16th July 2011

Wanafunzi wa shule za Sangu, Meta na Ivumwe zinazomilikiwa na Jumuiya ya Wazazi mkoani Mbeya, wamelalamikia hatua ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani hapa kuwalazimisha kuhudhuria maandamano ya chama hicho yanayotarajiwa kufanyika leo jijini Mbeya.
Wakizungumza na gazeti hili kwa sharti la kutotajwa majina yao, wanafunzi hao wamedai kuwa viongozi wa CCM wamekwenda kwenye shule zao na kuwaamuru walimu wawashinikize wanafunzi kuhudhuria maandamano hayo.
Walisema viongozi hao wa CCM wameahidi kuwapelekea magari yatakayowabeba kutoka kwenye shule zao kwenda mahali pa kuanzia maandamano na kisha kuwarejesha shuleni baada ya maandamano kumalizika.
Walisema kitendo hicho cha kuwalazimisha sio kizuri kwa kuwa na wao wanayo hiyari ya kwenda au kutokwenda kwenye maandamano hayo.
"Pamoja na kwamba hizi shule za wazazi zinamilikiwa na Jumuiya ya Wazazi ambayo ipo chini ya CCM, lakini watambue kuwa na sisi tunazo itikadi zetu za kisiasa ambazo zinapaswa kuheshimiwa," alisema mmoja wa wanafunzi hao.
Mwanafunzi huyo ambaye alionekana kuwa kiongozi wa kundi kubwa la wanafunzi waliofika katika ofisi za gazeti hili kulalamika, alisema wao hawako tayari kuhudhuria maandamano hayo kwa kuwa wanayo kazi moja tu ya kujisomea.
"Wao kama wanataka wanafunzi waongeze idadi ya watu kwenye maandamano yao, wawachukue wale wa O- level, lakini sisi kwanza ni watu wazima wenye maamuzi yetu na pia tunajiandaa na mitihani kwani sisi tunaona kama muda hautututoshi," alisema.
Mwalimu mmoja wa shule ya Sekondari Meta ambaye pia hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alithibitisha kuombwa na viongozi wa CCM ili wawaruhusu wanafunzi wa shule hiyo kuhudhuria maandamano hayo.
"Ni kweli viongozi wa CCM wamefika hapa na kutuomba wanafunzi waende kwenye maandamano yao, kwa kuwa wao ndio wamiliki wa shule hizi na ndio waajiri wetu, sisi hatuna uwezo wa kuwakatalia, lakini pia sioni ubaya wowote kwa wanafunzi kwenda kwenye maandamano hasa ukizingatia kuwa kesho (leo) sio siku ya masomo," alisema.
Katibu wa CCM Mkoa wa Mbeya, Verena Shumbusho, alisema suala hilo sio la kwake na kama lipo wanaopaswa kuulizwa ni walimu wa wanafunzi hao au viongozi wa Jumuiya ya Wazazi.
"Hilo mimi halinihusu, kawaulize walimu wao na kama hutaridhika waone viongozi wa Jumuiya ya Wazazi kwa sababu wao ndio wamiliki wa shule hizo," alisema Shumbusho.
Maandamano cha CCM yanayotarajiwa kufanyika leo yamepangwa kuanzia eneo la Mafiati na kuishia viwanya vya Rwandanzovwe.



CHANZO: NIPASHE
 
Nasikia wamekusanya watu toka ipinda,bhujonde,kyela,usale,ushirika,masoko,rungwetukuyu etc ili angalau kuambulia nyomi kama la chadema
 
CCJ wemeandamana leo kujibu mapigo ya CCM. Nani atashinda? Mbeya kwa hakika safu yote ni CCJ
 
Back
Top Bottom