Mkutano wa CCM Mbeya

wamepata ujasiri wa kuongea mbele za watu baada ya RA kuvua gamba. Wanakula allowance za chama tu hawa hamna lolote.

Nnadhani 6 anautaka urais 2015, anaona EL anakwamishwa basi anadhani atapewa yeye. Tunavyomjua kwa hasira zake akiukosa basi atahama ccm japo hata umri utakuwa haumruhusu tena.
 
Mkutano wa CCM utangazwa magwanda, halafu mnasubiri habari kwa hamu. Hii kali.
 
Jama habari za kujivua gamba zimeongelewa? maana nape alikuwa anapiga domo sana je kaliongelea hilo?
 
Mkutano umemalizika salama na nilifanikiwa kuhudhuria katika mkutano huo

Mkutano ulitanguliwa na Maandamo ambayo kwa asilimia kubwa yaliwashirikisha Wana CCM wengi kutoka Ileje,Mbozi, Chunya na maeneo ya Pembezoni mwa mji ambao walisombwa na kuletwa Mbeya na Malori na wale wachache waliletwa na na Coaster, Hiiace, Bajaji pamoja na Landcruiser za Mikonga maarufu kama hardtop. Kwa kweli naweza kuzungumza bila ushabiki kwamba Wanambeya wengi walikiwa pembeni na baadhi wenye ujasiri walikuwa wanaonesha alama za vidole viwili maana kulikuwa na Ulinzi mkali sana.

Mkutano ulihudhuriwa na watu wengi ila walikuwa katika makundi mawili. Kundi la kwanza ni lile ambalo lilikuwa na wazee wengi na vijana wachache waliokuwa wamevalia sare ambao wengi wao waliletwa kwa malori na ambao walikuwa wakishangilia

Kundi la pili ni lile ambalo wengi wao ni wakazi wa Mby mjini,hawa walikuwa ni wengi na ambao muda wote walikuwa kimya ila kulikuwa na baadhi ya vijana ambao walikuwa wanashangilia huku wakionesha vidole viwili.

Kwa kifupi ni kwamba CCM bado wana kazi kubwa Mby mjini kama si kuleta watu kutoka majimbo mengine hakika wangeandamana peke yao
 
Nape amezungumzia kisa cha Maalim seif, amesema baada ya kuona Njaa imemzidi ikabdi aombe muafaka na CCM wakampa Umakamu wa rais akasema baada ya seif kupata Cheo sasa anapendeza, anang'ara ha ha ha dongo kwa CUF
 
Kwa makadirio ya harakaharaka, kulikuwa na watu takriban 1200, nusu wakiwa wameletwa na magari kutoka maeneo mbalimbali na hawa walikuwa wamevalia sare za CCM na walikuwa wanashangilia mara kwa mara. Nusu ingine ni wakaazi, ambao muda wote walikuwa kimya wakinong'onezana hili na lile wakati mkutano ukiendelea. Kwa ujumla, muitikio wa watu sio mkubwa na wananchi wengi hususan wakaazi wa mbeya hawaonekani kuvutiwa na CCM.
 
J Muhagama hamna kitu, hilo ni kundi la kushindwa hawajawai kushinda move yoyote ile, Sitta aseme kwanza kwanini alikosa U-Spika.

Kweli magamba wanayo kazi. Hivi huyu Six huwa hachoki na mabo yake ya unafiki? Ukiangalia historia yake tokea yuko Chuo UDSM alikuwa ni miongoni mwa vijana waliosumbua na kutokea kusimamishwa masomo. Ingawa ni miongoni mwa wasomi wa zamani hapa Tz haioneshi kama ana uwezo kwa kustahimili mikiki mikiki ya siasa za vyama vingi hivi sasa. Ni mtu wa vituko huyu. Kwa wale waliokuwepo miaka ya 80 mtakumbuka vituko alivyofanya alipoteuliwa kuwa waziri inayosimamia uhamishaji wa Makao Makuu CDA. Alivuruga sana pale na kusababisha wataalamu vijana wakati ule waliokuwa wameajiriwa katika mradi huo kusambaratishwa na kuiacha Dodoma bila muelekeo uliotarajiwa. Alipendelea sana mambo ya ngono na wakati mwingine kutia aibu kuona Waziri aliyeheshimika akifanya mapenzi na watumishi wa kike wafagiaji ambao katu haikupaswa iwe hivyo. Hajatokea kuonesha kama analo la kujisifia alipokuwa katibu wa CCM kwenye Mikoa ya Iringa na Kilimanjaro na pale alipokumbukwa na Ben kupewa Kituo cha uwekezaji inaonesha wawekezaji akina Richmond ndo walijitokeza kwenye ngwe yake na punde tu anaonesha kuwa hawajui!! Alipopata kigoda cha Uspika alikitumia kwa muda mrefu akisaidiana na washirika wake CCJ kupambana na maadui zake akina RA na ikiwa ni pamoja na suala la Dowans lililopelekea kukosa umakini wa kufanya maamuzi na kusababisha nchi kukaa gizani wakati mitambo ya kuwashia umeme ikiwa pango la nyuki pale Ubungo. Zito, Makamba na Njeleja walijaribu kuwa na mawazo mbadala lakini wapi kwa kisiki cha Six!! Hivi sasa CCJ wanaendeleza mapambano dhidi ya akina RA kwa kwenda Mbeya alikokulia mburushi huyu ili kushinikiza magamba yaliyochojolewa yasiote tena. Ni visasi vya kuukosa Uspika. Hivi kazi za Jumuia ya Afrika Mashariki siyo nyingi kiasi kwamba Six anapata nafasi ya kufanya itikadi zinazotakiwa zifanywe na akina Nape?
 
Kwa makadirio ya harakaharaka, kulikuwa na watu takriban 1200, nusu wakiwa wameletwa na magari kutoka maeneo mbalimbali na hawa walikuwa wamevalia sare za CCM na walikuwa wanashangilia mara kwa mara. Nusu ingine ni wakaazi, ambao muda wote walikuwa kimya wakinong'onezana hili na lile wakati mkutano ukiendelea. Kwa ujumla, muitikio wa watu sio mkubwa na wananchi wengi hususan wakaazi wa mbeya hawaonekani kuvutiwa na CCM.
Yote uliyoyazungumza naweza kabisa kuyakubali ila kwenye hiyo namba utanisamehe
 
Yote uliyoyazungumza naweza kabisa kuyakubali ila kwenye hiyo namba utanisamehe

Trust me, the aproximation error is plus or minus 100 peoples. My secondary school had 1000 students so its easy for me to approximate.
 
Mkutano umemalizika salama na nilifanikiwa kuhudhuria katika mkutano huo Mkutano ulitanguliwa na Maandamo ambayo kwa asilimia kubwa yaliwashirikisha Wana CCM wengi kutoka Ileje,Mbozi, Chunya na maeneo ya Pembezoni mwa mji ambao walisombwa na kuletwa Mbeya na Malori na wale wachache waliletwa na na Coaster, Hiiace, Bajaji pamoja na Landcruiser za Mikonga maarufu kama hardtop. Kwa kweli naweza kuzungumza bila ushabiki kwamba Wanambeya wengi walikiwa pembeni na baadhi wenye ujasiri walikuwa wanaonesha alama za vidole viwili maana kulikuwa na Ulinzi mkali sana.Mkutano ulihudhuriwa na watu wengi ila walikuwa katika makundi mawili. Kundi la kwanza ni lile ambalo lilikuwa na wazee wengi na vijana wachache waliokuwa wamevalia sare ambao wengi wao waliletwa kwa malori na ambao walikuwa wakishangiliaKundi la pili ni lile ambalo wengi wao ni wakazi wa Mby mjini,hawa walikuwa ni wengi na ambao muda wote walikuwa kimya ila kulikuwa na baadhi ya vijana ambao walikuwa wanashangilia huku wakionesha vidole viwili.Kwa kifupi ni kwamba CCM bado wana kazi kubwa Mby mjini kama si kuleta watu kutoka majimbo mengine hakika wangeandamana peke yao
Si muda mrefu hizo gharama za kusomba watu na kuwalipa zitawashinda na hapo ndo moto utawawakia. Demokrasia ya kununua watu siyo ya kudumu ina gharama kubwa. Watawapata watu kwa sababu wanashida na pesa lakini hawataweza kulazimisha wawapende toka mioyoni mwao kama chadema.Ni kazi kwa cdm kulifanyia kazi hili la demokrasia ya kununua watu. Elimu tu inatosha watu bado wanaogopa kuwa wakipokea hela kisha wakaacha kwenda watakuja kufatiliwa.Kuna jirani yetu ni mwalimu walionja joto ya jiwe wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2010. Walidanganywa kuwa jk anataka kuongea na walimu wa dar es salam hivyo waende uwanja wa sabasaba. Walipofika sabasaba wakaingizwa kwenye ukumbi na kulikuwa na mshushu kibao wakajikuta wako pale wametekwa hawaruhusiwi kutoka nje, hamna chakula na wala hamna cha kuongea na JK. Muda wa mkutano wa JK pale Jangwani ulipofika wakatolewa na kuingizwa kwenye daladala kupelekwa kwenye mkutano jangwani. Yule mama aliniambia kiherehere kilimwisha maana walishindishwa njaa na hawakurudishiwa hata nauri maana walijikusanaya wakakodisha costa asubuhi saa kumi na mbili. Alishangaa kitendo cha kulazimishwa kuhudhuria mkutano kwa nguvu akasema ccm ni mamafiaHaya ndo huwa yanawapata watu wengi wakati wa uchaguzi hasa akina mama wanaopenda kuwa kwenye vikundi vikundi sijui vya sacos sijui nini. Vi balozi ndiyo huwa vinawashawishi akina mama.Nadhani cdm inabidi wawe na wawakilishi wao angalau kila nyumba 20 ili kupambana na hawa mabalozi maana huwa vinawarubuni mno mama zetu.
 
Duh laiti ingekuwa mbeya ni moshi au arusha! Ningewapa vidonge vyao hao magamba hadi wakimbie. Tungewapokea na mabango ya liyobeba ujumbe wa kutaka umeme maji na bei ya mafuta na sement na nondo za kujengea pia hali ya afya na elimu kama hawana suluhisho ni kipi wanakuja kutuambia magamba yao wayapeleke igunga wakayavulie huko. Sisi hatuyahitaji
 
Kwa makadirio ya harakaharaka, kulikuwa na watu takriban 1200, nusu wakiwa wameletwa na magari kutoka maeneo mbalimbali na hawa walikuwa wamevalia sare za CCM na walikuwa wanashangilia mara kwa mara. Nusu ingine ni wakaazi, ambao muda wote walikuwa kimya wakinong'onezana hili na lile wakati mkutano ukiendelea. Kwa ujumla, muitikio wa watu sio mkubwa na wananchi wengi hususan wakaazi wa mbeya hawaonekani kuvutiwa na CCM.

Trust me, the aproximation error is plus or minus 100 peoples. My secondary school had 1000 students so its easy for me to approximate.

Duh..naona ndugu yangu una zaidi ya makengeza, nakushauri uende ukamwone daktari wa macho haraka sana.

Kwa picha... http://michuzi-matukio.blogspot.com/2011/07/mkutano-wa-nape-mjini-mbeya-wafunika.html#links
 
Mkutano umemalizika salama na nilifanikiwa kuhudhuria katika mkutano huo

Mkutano ulitanguliwa na Maandamo ambayo kwa asilimia kubwa yaliwashirikisha Wana CCM wengi kutoka Ileje,Mbozi, Chunya na maeneo ya Pembezoni mwa mji ambao walisombwa na kuletwa Mbeya na Malori na wale wachache waliletwa na na Coaster, Hiiace, Bajaji pamoja na Landcruiser za Mikonga maarufu kama hardtop. Kwa kweli naweza kuzungumza bila ushabiki kwamba Wanambeya wengi walikiwa pembeni na baadhi wenye ujasiri walikuwa wanaonesha alama za vidole viwili maana kulikuwa na Ulinzi mkali sana.

Mkutano ulihudhuriwa na watu wengi ila walikuwa katika makundi mawili. Kundi la kwanza ni lile ambalo lilikuwa na wazee wengi na vijana wachache waliokuwa wamevalia sare ambao wengi wao waliletwa kwa malori na ambao walikuwa wakishangilia

Kundi la pili ni lile ambalo wengi wao ni wakazi wa Mby mjini,hawa walikuwa ni wengi na ambao muda wote walikuwa kimya ila kulikuwa na baadhi ya vijana ambao walikuwa wanashangilia huku wakionesha vidole viwili.

Kwa kifupi ni kwamba CCM bado wana kazi kubwa Mby mjini kama si kuleta watu kutoka majimbo mengine hakika wangeandamana peke yao
Kweli tupu hata mimi nilikuwepo na nimeona hivyo
 
Mungu akiamua kukuacha uendelee kutesa watuwake si kwamba hawezi kukufanya lolote, CCM wamekuwa wakitutesa sana sasa hii ni nguvu ya Mungu, Mungu amekisikia kilio chetu na ameshawawekea pingamizi CCM na hivyo ndivyo ilivyo. Mara nyingi mtu akipata ajali hua haamini kama kaumia na hujaribu kurukaruka ili aonekane yeye ni hodari hivyo ndivyo ilivyo sasa kwa CCM
 
hakuna mtu mnafiki kama sitta..kigeu geu sana yule mzee

Kwa ufupi, idadi ya watu ilikuwa kubwa sana, hii ni ishara kuwa CCM yenye uelekeo wa kipiganaji ni tishio kubwa kwa uhai wa Chadema mjini Mbeya.

Yaliyoongelewa kwa ufupi.

MWAKYEMBE:

...Aliahidi kuwa Wabunge wa CCM Mbeya hawataukacha mji wa Mbeya, watautetea na kufanya kila liwezavyo kuleta maendeleo katika mji huu, kwa sababu Mji wa Mbeya ni kioo cha mkoa wa Mbeya.
..Alisikitishwa na kauli za Sugu, kuwaponda Mwandosya, Mwakyusa na yeye, amemponda Sugu kwa kutoshiriki katika harakati za kuupigania mkoa na badala yake kupoteza muda mwingi akizungukazunguka tu kisanii.
...Alimsifu Rais Kikwete na kuwahakikishia wananchi wa mbeya kuwa ana nia ya dhati ya kuibadisha CCM, na kuwa Mafisadi na ufisadi hauna nafasi sasa ndani ya CCM
...Alimkejeli Lowasa (bila kumtaja jina) kuwa maamuzi magumu si ajabu na ata majambazi pia uyafanya kwa kuchukua uamuzi mgumu kuvamia nyumba bila kujua mwenye nyumba ana zana gani ndani, alisema jambo la muhimu zaidi kuliko maamuzi magumu ni maamuzi MAKINI NA SAHIHI, na kuwa CCM iliyojivua gamba siku zote italizingatia hili.
...Aliwahakikishia wananchi wa Mbeya kuwa katika mwaka huu wa fedha, Km 28 za lami zitawekwa mjini Mbeya kwa msaada wa Benki ya Dunia.

MARY MWANJELWA

...Alitangazwa kuwa anafanya kazi sasa kama Mbunge wa Mbeya Mjini, na kupitia uwakilishi wake Serikali ya CCM itatekeleza ilani ya CCM katika mji wa Mbeya.

HILDA NGOWI

...Alikitaja CHADEMA kama chama cha kikanda, na chenye ubaguzi, na kuwa pamoja na Mbeya kuwa mkoa wa pili kwa kumpa kura Dr.Slaa, kura zilizotumika kuteulia Wabunge wa Viti Maalumu, lakini CHADEMA iliwajaza wabunge kutoka Kaskazini na Mkoa wa Mbeya haukupewa ata Mbunge mmoja.

OLE SENDEKA.

...Aliwamasisha sana wananchi kwa kuelezea mwelekeo wa CCM mpya iliyojivua gamba katika kupambana na vitendo vya dhuruma na kujali maslahi ya umma.
...Alisikitishwa na tuhuma za kupika zinazoelekezwa kwa Kikwete na Mtoto wake.

LAZARO NYALANDU.

...Kwa hisia kubwa aliitaja miaka 50 ya uhuru kuwa ni alarm ya kuuanza mwanzo mpya wenye mwelekeo wa kuongeza nguvu zaidi katika kuwaletea wananchi maendeleo.
...Aliahidi kuwa serikali kupitia wizara yake itajizatiti katika kuwaongezea wananchi uwezo wa kipato na kuwa uwanja wa Ndege wa Mbeya utakaokamilika kabla ya December, utatumiwa kama chachu ya kuufungua mkoa wa Mbeya kiuchumi.
...Aliahidi kuwa serikali itawanyang'anya wote waliochukua viwanda vilivyokuwa vya serikali na kushindwa kuviendeleza.

SAMWELI SITTA.

...Kwanza aliwaomba msamaha wa wananchi wa Mbeya kwa niaba ya Serikali ya CCM kwa kuwa kwenye mgawo wa umeme kwani nchi yenye rasilimali kama zetu, haistahili kuwa kwenye matatizo ya umeme.
...Alisema mgawo huu ni matokeo ya vitendo vya kifisadi vilivyokuwa vinalitafuna taifa.
...Alisema CCM iliyojivua gamba, itaitazama mikataba yote ya umeme yenye ishara za kifisadi na kutafuta vyanzo vipya vya umeme, na kuahidi kuwa ndani ya miaka 4 hii kabla ya uchaguzi ujao, tatizo la umeme litakuwa historia.
...Alieleza changamoto ambazo yeye na wapiganaji wengine walikumbana nazo katika kupambana na ufisadi ata kufikia hatua ya kutaka kuvuliwa uanachama wa CCM, ata hivyo alisema kuwa waliamua kupambana ndani ya CCM na matokeo yake sasa yanaonekana.
...Alisikitishwa na kitendo cha vyama vya upinzania ambavyo vilimuomba sana agombee Uraisi kupitia vyama hivyo, leo hii vinamsimanga na kumponda kwa uzalendo wake wa kuusimamia ukweli.
...Alizungumzia kauli yake aliyoitoa Bungeni wiki iliyopita kuhusu unafiki wa Wabunge wa vyama vya upinzani kuhusu posho, na kuahidi kuwa serikali ipo mbioni kuboresha posho za Madktari, Manesi, waalimu n.k ili kuwafanya waboreshe utendani wao wa kazi na kuwa posho zisizo za lazima zitafutwa kama ilivyoainishwa katika mpango kazi wa miaka 5.
...Aliiponda Chadema kuwa bado haina uwezo wa kuongoza nchi, alisema wana viongozi wachache sana wenye uwezo.

NAPE NNAUYE.

...Alifafanua zana nzima ya kujivua gamba, CCM iliyojivua gamba itakuwa na sumu kali zaidi kuiwezesha kupambana vikali zaidi na vitendo vyote vinavyohatarisha maslahi ya umma na kupambana na watendaji wote wa serikali wanaozitumia nafasi zao kujinufaisha.
...Aliahidi kuwa CCM mpya itasimama kwenye misingi ya Mwl Nyerere, na haitalivumilia kundi la wenye pesa kukiodhi chama.
...Aliahidi kuwa CCM iliyojivua gamba kuisimamia Serikali kwa ukaribu katika kuhakikisha kuwa inatekeleza kwa umakini mkataba wa chama na wananchi(ilani ya uchaguzi), kiongozi yeyote wa serikali atakayeshindwa kutekeleza kazi kwa ufanisi hatavumiliwa.
...Alidokeza kuwa kampeni hii ya kujivua gamba sio yake binafsi bali ni ya chama, na kuwa kama ingelikuwa ni yake binafsi, basi wale wanaoshutumiwa wasingeanza kujiondoa wenyewe kama walivyoanza kufanya, amewaahidi wananchi kuwa chama kitawaondoa wale ambao hawatachukua hatua za kujiondoa kwa hiari yao.
...Amemponda Dr.Slaa kwa uchu wake wa madaraka, na kumtaka ayaweke mbele maslahi ya wananchi kuliko uchu wake binafisi.Aliwatahadharisha wananchi kutokubali kutumiwa na watu wachache wenye uchu wa madaraka walio tayari kuwatoa wananchi wauawe au kupata vilema kwa ajili ya maslahi yao ya kisiasa kama ilivyotokea Arusha.

PRINCE MWAIHOJO, MGOMBEA UBUNGE WA CUF 2010.

...Alisikitishwa na kitendo cha Mbunge wa Mbeya kuhamasisha vurugu kwa kauli yake ya kuwataka wananchi wa Mbeya wawapige mawe viongozi wa Serikali,alisema kauli kama hizo hazina maslahi kwa wananchi wa Mbeya na zinapaswa kupingwa na wana Mbeya wote.

...Alihoji uadilifu wa Dr.Slaa kwa kutaka kuingia Ikulu na mke wa mtu.
...Alihojji ufisadi uliopo Chadema katika uteuzi wa viti maalumu, amehoji uhalali wa wabunge wengi wa viti maalumu Chadema kutoka wilaya tatu za Kilimanjaro.
 
Back
Top Bottom