Leo CCM wanafanya Mkutano Mkuu maalum kidijitali . Niseme ukweli huu mkutano hautakuwa na matokeo chanya kama CCM wanavyotarajia. Asilimia kubwa ya Wajumbe hawajui dhana ya mtandao na hasa kule vijijini. Mfano Mjumbe wa Mkutano Mkuu toka kule Itilima, Rorya, madaba, Mlangali je wana uelewa na mtandao?. Nimesoma kupitia Youtube kuwa Wajumbe toka Mkoa wa Simiyu hawatashiriki mkutano huu wa kidijitali badala yake wanataka mkutano wa uso kwa uso ili kuwawezesha kuuliza maswali pale panapotakiwa.
Ushauri wangu:- Mkutano Mkuu Maalum uitishwe upya na Wajumbe wote waitwe Dodoma ili wakutane uso kwa uso ili watoe ushauri wao na kuuliza maswali kama itabidi.
Nawasilisha.
Ushauri wangu:- Mkutano Mkuu Maalum uitishwe upya na Wajumbe wote waitwe Dodoma ili wakutane uso kwa uso ili watoe ushauri wao na kuuliza maswali kama itabidi.
Nawasilisha.