Mkulo anatuongopea?

Mkulo anatuongopea?

Mkulo: Serikali haijafilisika

na Mwandishi wetu, Dodoma
Source: Hapa

WAZIRI wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo, amesema serikali haijafilisika na haijawahi kukopa fedha kwa ajili ya kulipa mishahara ya watumishi wake.

Mkulo alisema hayo mjini Dodoma jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari akijibu tuhuma za Naibu Katibu Mkuu wa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kabwe Zitto, aliyesema kuwa serikali imefilisika kiasi cha kukopa kwenye mabenki ya ndani kwa ajili ya kulipa mishahara ya watumishi wake na wabunge.

"Napenda kutumia fursa hii kukanusha vikali madai hayo kuwa ni uongo mtupu na upotishaji unaofanywa kwa maksudi kwa lengo la kujitafutia umaarufu wa kisiasa… napenda kuwaeleza wananchi kuwa taarifa hizo si sahihi. Serikali inalipa watumishi wake mishahara kwa kutumia mapato yake ya ndani pia ina uwezo wa kugharamia shughuli zake nyingine ikiwemo kuendesha Bunge," alisema Mkulo.

Alisema mishahara ya watumishi wa serikali katika kipindi cha kuanzia Desemba hadi Aprili mwaka huu, makusanyo na mapato ya ndani ni malipo ya mishahara ya watumishi wa serikali.

Akifafanua hilo Mkulo alieleza kwamba Desemba mwaka jana serikali ilikusanya sh bilioni 594 ambapo kiasi cha sh bilioni 243.80 kilitumika kulipa mishahara na ziada ya sh bilioni 350.20 ilipatikana wakati Januari mwaka huu makusanyo yalikuwa sh bilioni 433.50 na mishahara iliyolipwa ni sh bilioni 240 huku ziada ya sh bilioni 193 ikiendelea kuwepo.

Mkulo aliendelea kufafanua kuwa Februari mwaka huu walikusanya sh bilioni 430 na ikalipa mishahara sh bilioni 266 na ikabaki na ziada ya sh bilioni 163.70 huku Machi serikali ikikusanya sh bilioni 567 na ikalipa mishahara sh bilioni 249 na kubaki na ziada ya sh bil. 317 wakati Aprili walikusanya sh bilioni 432 na ikalipa mishahara sh bilioni 246.70 na kubaki na ziada ya sh bilioni 185.40.

"Uchambuzi huu unaonyesha dhahiri kuwa serikali inayo mapato ya kutosha ambayo yanakidhi kulipa mishahara ya watumishi wa serikali kwa ukamilifu na tunayo ziada ya kutosha kugharamia shughuli nyingine za serikali… kwa kawaida serikali inatumia fedha taslimu kulipa gharama zake.

"…Kwa hiyo mapato ya Desemba yanalipa mishahara na matumizi ya Januari. Mapato ya Januari yanalipa matumizi ya Februari na kadhalika, kwa utaratibu huu hakuna hata mwezi mmoja ambao wafanyakazi wa serikali wamekosa mshahara.

"Wanaotoa uongo huo wanatafuta umaarufu wa kisiasa, wamekosa uzalendo kwa taifa lao," alisisitiza Mkulo na kuongeza kwamba posho mbalimbali za wabunge zimelipwa kwa wakati licha ya ongezeko la wawakilishi hao na kutaja stahili zao kuwa ni kwa ajili ya shughuli za kamati za Bunge, posho majimboni, mishahara na mafuta ya kila mwezi.

Aliongeza kuwa mwezi uliopita mishahara ya wabunge ilitolewa Aprili 22 mwaka huu na fedha kwa ajili ya posho mbalimbali nazo zimeshatolewa kwenye ofisi za Bunge. Hivyo alisisitiza na kuelewesha umma kuwa serikali haijashindwa kulipa mishahara ya wabunge na posho zao tofauti na taarifa zilizotolewa na Zitto akidai wabunge hawajalipwa.

Akizungumzia mikopo ya serikali na malengo yake, Mkulo alisema pamoja na kutumia mapato ya ndani kugharamia shughuli zake, hukopa kutoka vyanzo mbalimbali ili kugharamia shughuli za maendeleo. Mikopo hiyo inahusisha ile yenye masharti nafuu na kibiashara.

"Kwa mfano katika mwaka wa fedha wa 2010/2011 serikali ilipanga kukopa kiasi cha dola za Marekani milioni 525 ambapo kati hizo dola za Marekani 250 zitagharamia miuondombinu wakati kiasi cha dola za Marekani milioni 175 zitatumika kununua mitambo ya kufua umeme wenye uwezo wa kuzalisha megawati 100 kwa ajili ya Dar es Salaam na megawati 60 kwa ajili ya Mwanza," alisema.

Mkulo alisema ameamua kutoa ufafanuzi huo ili kuonyesha kwa kifupi kuwa serikali ina uwezo wa kulipa mishahara ya wafanyakazi wake, mishahara na gharama zote za kuendesha Bunge kutokana na mapato yake ya ndani. Sio kweli na ni upotoshaji wa makusudi wenye malengo ya kujitafutia umaarufu wa kisiasa.

Alipoulizwa hatua gani atachukuliwa Zitto kutokana na kutoa taarifa za uongo kwa Watanzania, alijibu kuwa yeye alichofanya ni kueleza kile ambacho ndicho sahihi kwa serikali na kwamba wanaoweza kumchukulia hatua Zitto kwa kusema uongo ni Bunge lenyewe. Kutokana na ufafanuzi huo, Mkulo alisema kuwa kikubwa kinachotakiwa hata kama ni mtu wa chama chochote cha kisiasa ama kiongozi kuchuja mambo na kuangalia athari zake kwa kina na si kukurupuka kwa kutafuta umaarufu ambao hauna tija kwa taifa zaidi ya kusababisha matatizo.



My Take:

1. Mkulo anataka kutuaminisha kwamba kazi ya mapato ya serikali ni kulipa mishahara basi. Sasa sijui hata hivyo vikao vya bajeti wanakaa kwa ajili ya nini.

2. Kwa takwimu za mkulo ina maana mpaka sasa serikali ina ziada ya shillingi bilioni elfu moja mia mbili na nane au Shillingi Trilioni 1 na bilioni mbili

3. Inakuwaje sasa serikali yenye ziada ya mihela yote hiyo halafu inaenda kukopa tena?

4. Hivi huu si uwendawazimu? Februari mwaka huu walikusanya sh bilioni 430 na ikalipa mishahara sh bilioni 266 na ikabaki na ziada ya sh bilioni 163.70 . Mishahara tu ni 62%, hiyo serikali iakuwaje na hela?

5. Kwa mapato hayo na matumizi hayo kwa mishahara tu, si ni indicator ya wazi kabisa kwamba tuna liserikali likuubwa tena lisilo na manufaa yeyote.

6. Hiyo trend ya matumizi hainekani kabisa kwamba jamaa wanajali kubana matumizi wao ni kutumia tu!

7. Kama hizi data nni za kweli, basi Mkulo, JK and the government are failing us miserably.

8. Bunge linaingiajae hapa kumchukulia hatua Zitto kama amesema uwongo?


NI kweli hali ya serikali kifedha sio nzuri kabisa. Mfano mshahara wa mwezi uliopita (April) kwa UDSM umelipwa kuanzia tarehe 05 May , kitu ambacho hakijawahi tokea katika historia ya UDSM. Na hali halisi ya kipesa ni mbaya saana.
 
Tatizo ninaloliona mimi ni kwamba jana kikwete amewaagiza wawe wanajibu mapigo. sasa wao bila kujipanga wanakurupuka na matokeo yake ndio haya. Mh. Zito ni mbunge na ni ushahidi tosha kwamba hawajalipwa posho kwa sababu serikali ina ukata. angekuwa amelipwa posho asingesema hayo. Je Mh. zito akiamua kuanika mengine kuhusu ukata wa serikali sijui Mkulo atajibuje!!!!!

mimi naona hiyo ndio sababu cz walimpigia simu akiwa Kenya akasema ajibu hoja za mitahani.
 
Kwa wastani hapa ni kuwa kila mwezi serikali hutumia 244.875bn kwa mishahara....ikiwa tufanye wastani wa mishahara kwa kada zote ni 1,000,000 ina maana serikali ina watumishi 244,875?
duh,mkuu nimekusoma,mbona hali inatisha??ina maana kila mtu sh 1milion pay teh teh,hii ni serikali ya wachache asee..
 
Hivi sijui mnashangaa nini!!! Ni lini Mkulo alishawahi kuongea ukweli??? Si ni huyu huyu jamaa ndiye aliyekwenda na bajeti feki kwa wahisani na kudai kuwa ni bajeti halisi??
 
Jinsi inavyoonyesha kwamba Kibonde ni kada wa CCM, leo katokwa mishipa yake ya shingo kwenye kipindi cha Jahazi na cloud fm kumtetea Mkulo kuhusu kukopa.....eti.. Hata Marekani nayo inakopa....du.....uchumi upi huo!
 
This is interesting. I havent had enough time to examine his statement but what is wrong with borrowing if it is justified? kwanini uoga kuelezea bayana kama serikali imekopa kama ni kweli sababu from an economic standpoint, it is not a never happen issue. Even in his own ministry, there is a statement regarding the activities of the ministry of finance in our economy including borrowing to pay salaries. It is a clear indication that the government borrows from time to time to pay salaries. Below is a quote from the ministry's website. Ntarudia mjadala huu next time.

The ministry says in its website:
Why does the Government borrow?

The Government spends money to finance its various activities. The activities include building of infrastructure, defence of a country's national boundaries, provision of social services such as health, education, maintenance of security, payments of salaries for its employees and many others. To meet these expenditures the Government needs to have financial resources (revenue). Essentially the Government would use its domestic revenue arising from tax and non-tax sources. However, these resources may not be enough to meet these expenditures. This means that the expenditures will be greater than revenue hence creating a gap. This gap is called a deficit. To bridge this gap the Government is compelled to borrow from either domestic sources or external sources. This is referred to as Budget Financing. Sometimes the Government may have balance of payments problems, whereby the country's exports can not pay for imports. In this case the Government may borrow to solve this problem. This is sometimes referred to as balance of payments (BOP) financing.
 
Nyambala nimerudia hizo hesabu na kujiuliza:

Mwezi Disemba mishahara 243.80 bilioni
Mwezi Januari mishahara 240 bilioni (punguzo la bilioni 3)
Mwezi Machi Mishahara 249 bilioni (ongezeko la bilioni 9)
Mwezi Aprili Mishahara 246.70 (punguzo la bilioni 3 hivi)

Najiuliza kulikuwa na tatizo gani la Ajira huko serikalini? wanaajiri sana au wanatimuana sana? Au mishahara inabadilika mara kwa mara? au hii inajumlisha na posho zote n.k? Vyovyote vile ilivyo sijui kama hesabu hizi zinaakisi ajira halisi iliyopo serikalini.

Good questions Mwanakijiji. Hii ndiyo aina ya watenda kazi wa jk walivyo dhaifu ktk kufikiri. kwao ujanja ujanja na kutaka kudanganya umma ndiyo kazi yao. wanadhani watanzania hawana uwezo wa kufikiri na kuchanganua hoja inayo tolewa kiyakinifu. Huyu Mkulo hana uwezo wowote kiutendaji. hii ndiyo maana unaona hakuna hata consistency ktk data zake alizo toa. Ngoja nikuambie Mwanakiji mdogo wangu, hapo ni wizi tu ndugu yangu. siyo kitu kingine.
 
Hivi sijui mnashangaa nini!!! Ni lini Mkulo alishawahi kuongea ukweli??? Si ni huyu huyu jamaa ndiye aliyekwenda na bajeti feki kwa wahisani na kudai kuwa ni bajeti halisi??

Mustafa Mkulo ni mwongo hata kwenye mambo yanayomhusu:

1. Yeye ni Mmalawi ana sema sio, UONGO
2. Ametetea uizi wa Group endowment wa PPF kuwa ni halali wakati sio kweli. Kadanganywa na Erio naye kalisema bungeni. Kadanganya Bunge, kambishia Mh. Zitto aliyelifanyia kazi

3. Amesema alipokuwa NSSF alilipwa Group Endowment wakati NSSF hawana malipo haya, UONGO
4. Akiwa Arusha kwenye Mkutano wa wadau wa PPF alisema PSPF itakufa very soon, Bungeni kapinga ushauri Mh. Zitto

Huyu alimchongea kwa uongo Zakia Megji kwa JK ili aachiwe Hazina. Ataendelea kudanganya mpaka lini?

JK chukua hatua
 
Mkullo ni mwongo mwongo mwongo hasa, mie nim mtumishi wa Umma na sijalipwa mshahara hiyo 22/04/2011. Mie nimelipwa mshahara wa April 2011 tarehe 5/5/2011, Hapa wafanyakazi wengi wa serikali tumesherehekea siku kuu ya wafanyakazi tukiwa mifuko mitupu
 
Haya mambo yanashangaza sana. Bajeti hutangazwa,mapato hukusanywa,na pengine fedha za wahisani na mikopo hupatikana pia. Sasa hizi kauli za "Serikali haina hela" au "Hazina haina hela kabisa" labda mpaka bajeti ijayo zinatoka wapi??? Nchi haiko/haikuwa vitani,hakuna majanga makubwa ya asili,madeni hayalipwi maana hatuambiwi kama yanalipwa,sasa huu upungufu wa hela hivi huwa unatokeaje? Inawezekana kuna sababu za kitaalamu(kiuchumi) zinazosababisha mapungufu hayo,ila kwa case hii nadhani kuna jambo jingine la kizembe na kibinafsi zaidi. Yani ni uongo uongo tu,ujanja ujanja wa kipuuzi na kupigwa chenga ya mwili(wananchi),then maisha yanakuwa ghali kuyamudu na serikali inakosa hela(ambazo bado sijui zinakosekana vipi),na badaye Mkulo anakuja juu na kusema hela ipo tena nyingi tu. Haya mambo yanakera kiasi kwamba mtu anaweza kuandika kitabu kuelezea dukuduku lake. Ila mi najua ipo siku tu... kutakuwa na kilio na kusaga meno!!
 
Mkulo anasema pesa imekusanywa ya kotosha kulipa wafanyakazi na surplus. Makusanyo ya pesa si kwa kulipa wafanyakazi wa serikali pekee na kama ukisema surplus ni kwamba kuna pesa ambayo haina matumizi baada ya budget. Hii si kweli hatuna umeme na pesa ya generator, hatuna maji vijijini, hatuna madawati mashuleni, hatuma barabara mijini na vijijini na tunategemea misaada kwa 30% ya budget yetu sasa hiyo surplus anayosema iko wapi???. Ni aibu kuanza kusema Tanzania tuna surplus wakati hatuna hata umeme kwenye miji yetu!!!. Hawa jamaa sijui wanapata vipi kazi


“Between December and April this year, revenue collection trend and payment of salaries to public servants was impressive, as the government through TRA collected 594bn/- out of which 243bn/- was for the salaries of the public servants and 350bn/- was surplus money,” he explained.
In January this year, he said internally-generated revenue collected stood at 433.50bn/- out of which 240bn/- was public servants’ salaries and 193bn/- was surplus money. In February this year, 430.40bn/- was collected of which 266.70bn/- was paid as salaries of public servants and 163.70bn/- remained as surplus. In March 567bn/- was collected out of which public servants’ salaries stood at 249.50bn/- and 317.60bn/- was surplus.
“Last month we collected 432bn/-, paid 246bn/- to public servants and we remained with 185bn/- as surplus. These statistics are a clear testimony that the government is not bankrupt, as speculated by the opposition MP,” clarified Mkulo, adding: “It also testifies to the fact that the government has enough internally-generated funds for paying salaries to public servants and financing other government operations,” clarified Mkulo.
 
Kama goma la mchiriku, data hazifikiriki, zinapanda na kushuka ovyo ovyo, je namba ya wafanyakazi huko sirikalini na yenyewe influctuate hivyo! 62% ya pato la mwezi inakwenda kwenye mishahara, vipi elimu, maji, nishati, madawa, nk. Kwa nini tusiamini kuwa kuna ukata wa kufa mtu huko sirikalini!
Hizi semeni za kuwambia kujibu bila kufanya analysis ya unachokuja kujibu itatupa uondo wa kujua mengi, yetu macho na masikio.
 
This is interesting. I havent had enough time to examine his statement but what is wrong with borrowing if it is justified? kwanini uoga kuelezea bayana kama serikali imekopa kama ni kweli sababu from an economic standpoint, it is not a never happen issue. Even in his own ministry, there is a statement regarding the activities of the ministry of finance in our economy including borrowing to pay salaries. It is a clear indication that the government borrows from time to time to pay salaries. Below is a quote from the ministry's website. Ntarudia mjadala huu next time.

The ministry says in its website:
Why does the Government borrow?

The Government spends money to finance its various activities. The activities include building of infrastructure, defence of a country's national boundaries, provision of social services such as health, education, maintenance of security, payments of salaries for its employees and many others. To meet these expenditures the Government needs to have financial resources (revenue). Essentially the Government would use its domestic revenue arising from tax and non-tax sources. However, these resources may not be enough to meet these expenditures. This means that the expenditures will be greater than revenue hence creating a gap. This gap is called a deficit. To bridge this gap the Government is compelled to borrow from either domestic sources or external sources. This is referred to as Budget Financing. Sometimes the Government may have balance of payments problems, whereby the country's exports can not pay for imports. In this case the Government may borrow to solve this problem. This is sometimes referred to as balance of payments (BOP) financing.

This is what surprises me, is as if borrowing is a mega sin and has never been done before. It seems the minister was addressing the matter in a political avenue more than to the reality.
 
Zitto promises to expose govt over salaries saga Tuesday, 10 May 2011 22:58

By The Citizen Reporter
Sumbawanga.

The deputy secretary general of the Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, Mr Zitto Kabwe, has said he will prove in Parliament how the government had borrowed money from banks. The Kigoma North MP said his evidence in parliament was aimed at making the minister for Finance and Economic Affairs, Mr Mustafa Mkulo, to bear the responsibility for refusing to tell the truth.

He reiterated that the government was bankrupt and quoted March 2011 reports by the Bank of Tanzania (BoT) which indicated that the government had failed to collect taxes by 15 per cent.Mr Kabwe said that the reports showed that the government failed to collect 15 per cent of taxes except for customs duty.

He said the government borrowed money from Exim Bank and other commercial banks in March in order to pay for civil servants' salaries."Mr Mkulo should show us a government in the world that borrows from commercial banks… This is a very dangerous trend," warned Mr Kabwe.

He said the government's budget for the 2010/11 financial year was Sh11trillion but it failed to meet its projections by Sh1.6trillion due to the shortfall created by its failure to collect taxes fully. He asked the minister to stop misleading Tanzanians that revelations that the government was broke amounted to lack of patriotism which could scare away investors.

"The government is broke and there is no argument about it. There is nothing like lack of patriotism... Lack of investment has been caused by poor policies by the ruling Chama Cha Mapinduzi," said Mr Kabwe.

Addressing Chadema supporters in Mbozi over the weekend, Mr Kabwe said the government in power was in dire financial straights and was unable to pay salaries for its civil servants. The lawmaker said the government was being forced to borrow money from commercial banks to cater for employees' salaries. He said that the dire situation saw the government fail to pay April salaries for civil servants and MPs, noting that it only did so on May 7, this year.

"The government has even failed to pay allowances for MPs," said Mr Zitto.He said the government has borrowed Sh540billion to cater for salaries, instead of building infrastructure such as railways, roads and ports.

 
"Finance and Economic Affairs minister, Mr Mustafa Mkulo, told a press conference in Dodoma that no loans had been secured from commercial banks to pay the salaries for any of its employees or fund recurrent expenditure as claimed by some Opposition politicians".

In fact Government actual revenue and expenditure reports for the July 2010 to Feb 2011 period indicate that:

Total expenditure amounted to 6 trillion shillings, of which
1.6 trillion was development expenditure & net lending; the remainder being recurrent
1.1 trillion shillings were received in foreign grants (i.e. aid from donors), and
1.4 trillion shillings were borrowed (61% on foreign and 39% on domestic markets)

Since grants are generally given for development projects, only 500 billion shillings of the 1.6 trillion development expenditure was financed by the government (1.6 trillion - 1.1 trillion), thus 900 billion shillings of the 1.4 trillion borrowed had in fact to have been spent on recurring expenditure (including presumably on salaries).

Of course, it could be that donor grants where given to finance government recurrent expenditure, which is highly improbable.

Obviously, goverment did not borrow solely from commercial banks, so in fact Mr. Mkulo may be right when saying that money borrowed specifically from commercial banks was not used to pay salaries, but the fact remains that hundreds of billions were borrowed to pay for recurrent expenditures, including salaries.
 
Back
Top Bottom