Moisemusajiografii
JF-Expert Member
- Nov 3, 2013
- 49,734
- 89,327
Video zao zitendewe haki.Hii ni kwa sababu aina za nyimbo wanazoimba zinahitaji uchezaji mahiri hasa.Wako poa kabisa!
Hii ngoma naipenda sana kwa kweli. Hao madogo wana vipaji haswa.
Dogo Aslay kaiua hiyo aya ya kwanza.
Beka naye kaitendea haki kabisa hiyo aya ya pili.
Maromboso naye kafanya kweli.
Halafu hako kabinti kalikovaa spandex na kikaptula cha jeans juu yake nimetokea kukapenda. Yaani kanavyonengua..aaah.
Yaani wimbo umetulia kuanzia mashairi, mpangilio wa ala, hadi dance routine.
Kisura wangu ingawa haelewi wanachoimba lakini anaipenda sana hiyo choreography.
Kukupenda, imekuwa kero
Kutwa kucha kunitenda, mi mwana wa mwenzio
Nachofanya mi sikioni, ila masikio yanasikia wee
Nachofanya mi sikioni, ila masikio yanasikia wee
Kupenda na kupenda kweli, ah sikatai
Uwepo wako ni mzuri, maishani nafurahi
Kupenda na kupenda kweli, ah sikatai
Uwepo wako ni mzuri, maishani nafurahi
Ila ya moto, ya moto mapenzi
Mapenzi ya kitoto, ya kitoto mie siwezi
Ila ya moto, ya moto mapenzi
Mapenzi ya kitoto, ya kitoto mie siwezi
Hii ngoma acha kabisa.
Tayari nshaiweka kwenye iPod.