Mkoa wa Mbeya ndio nchi ya ahadi?

Utitiri wa makanisa kwa uchunguzi wako;Lakini umeshawahi kusikia mtu analazimishwa kuingia kwenye hayo makanisa?Au unasema tu kujifurahisha
 
wingi wa madhehebu ya makanisa ya kikristo mbeya ni suala la kihistoria.kipindi cha ukoloni kuna makanisa (independent churches) yaliyoanzzishwa na waafrika yakiwa na lengo la kutetea haki na uhuru wa waafrika pamoja na kupinga shughuli za makanisa ya wamishionari,sasa kwa tanganyika makanisa hayo hayakuwa mengi.pale malawi kuikuwa na kanisa la chilembwe lililoanishwa na mch.john chilembwe (1871-1915) raia wa malawi.kwakuwa ukristo ulisambaa sana malawi ilikua rahisi sana kwa ukristo kuingia mapema mkoani mbeya kwani mbeya na malawi ni jirani.
nawasilisha
 
Utitiri wa makanisa kwa uchunguzi wako;Lakini umeshawahi kusikia mtu analazimishwa kuingia kwenye hayo makanisa?Au unasema tu kujifurahisha

Mkuu nimeuliza nini sababu ya huo utitiri,sijalaumu pls soma nilicho kiandika
 
Tatizo lenu ndio hilo, badala ya kusoma upande wa pili wa shilingi nyinyi mmeng'ang'ania na agano tu. Mimi ndio nakwambia kwenye uislam hakuna dhehebu linaloitwa shia.


Mkuu kama shia sio waislamu ni nani basi.?!
 
Sababu kuu ya wingi wa madhehebu kwa mkoa wa mbeya ni kukosekana ama udhaifu wa madhehebu makubwa ya kikristo yaani Roman Catholic, Lutherani na Anglican. Haya madhehebu yalichelewa sana kufika mbeya na kukuta wenzao wa Moravian wameshatawala eneo kubwa sana la huko mbeya. Kanisa la Moravian linashabihiana sana na makanisa ya kilokole yaani kipentekoste. Makanisa ya kipentekoste hujulikana kwa wachungaji wao. Hivyo wengi walioshika dini sana mbeya walijikuta wanaanzisha makanisa yao mahali wanapokua. Hali kama hii haipo kwa mikoa ambayo ni ngome ya makanisa makubwa mfano. mwanza - RC, Songea - RC, Sumbawanga - RC, Arusha - Lutheran, Dodoma - Anglican, Bukoba - RC.

Pia wanyakyusa wana vipaji sana hasa uimbaji. Kama unyakyusani ingekua ngome ya RC tusingewasikia sana wakitoa nyimbo au kuwa wachungaji kila sehemu wanapokua. Madhehebu hayo mengine (ya kilokole) yanathamini sana nyimbo na ni sehemu kubwa sana ya ibada zao, ndio maana vipaji hivyo hukua kirahisi kwa mkoa wa mbeya.
hiyo ndiyo sababu kubwa. wakoloni wa kijerumani waligawa maeneo kwa wamishionari ili wasijekugombana. mbeya walipewa moravian wakati iringa na sumbawanga walipeewa RC. sasa moravia hawabrainwash sana waumini wao hivyo wengi kuwa open minded. mi nililelewa moravian ila sasa nina kanisa langu.
 
Sio makanisa tuu hata vyakula Mbeya inazarisha chakula kwa wingi ili kulisha mikoa mingine Mby inebarikiwa kwa kweli karibuni sana Mbeya.!!!!!
 
Ni sawa na kuuliza hivi; Tanzania ina Makabila takribani 125 lakini zaidi ya 50 Asilimia ya makabila hayo yanapatikana mkoa wa Mara, je MARA NDIKO KULIJENGWA MNARA WA BABERI?
 
Back
Top Bottom