Mkishangaa ya Chato msisahau ya Msoga

Atleast Pwani ni karibu na Dar, watu wanahama kwenda mkoa wa pwani kupanua mji.

Huko Chato nani atakaa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Siongei kishabiki, ila kasi ya ukuaji wa miji ambayo ipo kandokando ya ziwa Victoria na karibu na miji mikubwa huwa kubwa sana. Kilichokuwa kinaleta shida ni mpangilio mbovu wa Miji.

Nani atakaa Chato? Kwanza wapo waliopo lakini pia itategemea kasi ya ukuaji wa kiuchumi. Ki-nchi tunaweza kusema eneo hilo si landlocked kwa sababu linapakana na ziwa Victoria (kuna bandari kongwe ambayo iliwekwa na Wakoloni, na nafikiri unajua sehemu mkoloni alipoweka miundombinu kama hiyo alikuwa anafikiria mbali kiasi gani), Mji wa Geita, Mkoa wa Kagera na urahisi wa kufika Nchi za Rwanda na Uganda.

Kwani kipi cha kushangaza kuanzishwa Chato? Barabara? Majengo ya huduma za kijamii? Uwanja wa ndege.

Kwa hili la Uwanja wa ndege ni vyema kujikumbusha ilipoanzishwa Kia eneo ulipo Uwanja halafu rudi miaka zaidi ya 30 nyuma, Mtu angejiuliza 'unajenga vipi Kiwanja cha Kimataifa porini!' Kumbuka wakati huo zao linaloingiza fedha nyingi za kigeni ni Pamba, Katani na Korosho.

Hapa ndipo inakuja hoja hii aspect ya 'Kaskazini' ndo wenye maono kama Mtanzania mzalendo siwezi kuiunga mkono, ni kuchochea chuki.

Na ushauri wangu, Chama chochote cha siasa kisije kujinasibisha na hili
 
Sema tu kuna umuhimu wa kubalance kwa namna yoyote ile! maana too much is harmful. [emoji736][emoji736][emoji736][emoji736][emoji736]
Jr[emoji769]
 
Ukitaka kuwatoa nyoka shimoni walimojificha mwaga mafutataa.... Halafu kaa pembeni ushuhudie mahangaiko.... [emoji124][emoji124][emoji124][emoji124][emoji124][emoji124]

Jr[emoji769]
 
Kuna neno umenifurahisha mkuu.....' kuna tofauti ya mtoto aliyekulia kwenye nyumba ya nyasi na aliyekulia kwenye nyumba ya bati na sakafu'..... hayo maneno yamebeba ujumbe mzito na ndiyo hayo pekee yamenifanya kuchangia mada hii.

Kwingine kote nimetofautiana kidogo na mawazo yako.

Sisi tunaunga mkono chochote kinachojengwa popote kwa gharama yoyote!

Huu mwamko wa uungaji mkono wa aina hii umetokana na matendo ya tawala zilizopita, za siasa za maneno, kupiga pesa hadi nchi ikachakaa kama dampo la taka na tukakosa wa kumlaumu!

Miradi yoyote ile ijengwe kaskazini, kusini, mashariki ama magharibi kwa gharama yoyote sisi twaiunga mkono, maana hii ni Tanzania moja hatuhitaji vibali vya uhamiaji kwenda kuishi popote upapendapo.

Kuanza kusema matabaka ya wa kaskazini, sijui mashariki, mawazo hayo yana harufu ya ukabila na ni sumu kwa kizazi cha leo.

Mawazo ya namna hiyo yalikwisha kufutwa zamani na baba wa taifa kwa kutoa elimu ya uraia iliyomaliza ujima huo wa ukabila, sasa tusirejelee huko

Aheri kujenga kuliko kutojenga na hela iliyopo kuishia kupigwa na wajanja!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120]tafsiri imekuwa ngumu kidogo.... Kaskazini ilikuwa kachumbari ya mada lakini msingi ulikuwa hizo sehemu mbili.. Na nikasema wazi kabisa kwamba CHATO tuiweke kando hebu turudi Pwani.. Hebu nisome tena nilichoandika Kuhusu Pwani..
Jr[emoji769]
 
Ungekuwa ushafika Chato afu unaandika uwo upuuzi wako, nafikiri ungejishangaa sana.......jaribu kuandika kitu ulichokiona kwa macho usiwe mtu wa kusimuliwa simulizi, kama hadithi za abunuawasi.
Sasa kwa taharifa yako NMB wamejenga bonge la jengo zaidi ya CRDB na hospitali kubwa sana inajengwa km mloganzila......
Najua ayo pia ujui.....tembea na fact.....kaka
 
Kanda gani sikuhizi haina elimu?...
 
Sasa huo ni uonevu au ni uhalisia IDEGENDA
Nijibu pia na swali la ukabila
?

Jr[emoji769]
Kwenye huu uzi wako unataka kuwaambia watu kwamba pamoja na kwamba wanalalamika chato kupendelewa kuliko mikoa ya Kas kazini, bado hiyo miradi iliyopelekwa huko kiupendeleo, watakaoiendesha ni watu wa Kas kazini maana ndio wenye maono.

Hii si Tanznaia ya miaka ya enzi kina Mwinyi na kina Mkapa mkuu.

Akili walizonazo watu wa Kas kazini ndio walizonazo watu wa kusini, magharibi na Mashariki.

Enzi za watu wa Kas kazini kujimwambafy kila kona katika nchi hii zimeahapita mkuu. Ni ukweli unaouma na wala hamuonewi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
N
Nani anajenga hayo yote huko kwa siri, jpm?
 
Mshana Jr mtizamo mpana ni kwamba kila mtu anasoma siku hizi na kila mtu ana biashara sikuhizi

Sio tu makabila yaliyokaririwa

Hamjajifunza tu bado?..
Kuna service gani special Kaskazini ambayo Kanda zingine hawana?.
Hao bado hawajazinduka mkuu! Makabila yote siku hizi wameelimika wanajua dunia inaendaje.

Enzi za wewe mtoto wa shirima basi nenda dar kuna shirima kwenye shirika flani utapata kazi zimeisha.

Ndio maana wakienda maofisini siku hizi wanakutana na rundo la watu kutoka kila Kabila wana cv Sawa na yake na wote wanataka kazi hiyo hiyo,
Akikosa anaishia kulaumu eti Magu anapendelea na kubagua watu wa Kaskazini. [emoji23][emoji23][emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anafikiri wote hapa ni wajinga, sipendi mijitu ambayo bado inaabudu ukabila

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkakati wa kichadema

M/kiti MCHAGA
Katibu MCHAGA
M/kiti bawachha MCHAGA
M/kitu Bavicha nijuzeni

Sent using Jamii Forums mobile app
Na hapo ndo wanapofeli
Ina maana ktk makada nchi nzima hamna wa kanda nyingine mwenye uwezo?..

Zama hizi u will win me kama unatizama mbele kama nchi tunaendaje na sio ukanda
 
Hali hiyo inaondoka kwa kasi ndio maana mnahisi mnaonewa!
Hamtaki kukubali ukweli kwamba hizo fursa kila Kabila linazigombania siku hizi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…