Mkishangaa ya Chato msisahau ya Msoga

Mkishangaa ya Chato msisahau ya Msoga

platozoom unataja maeneo ambayo wala hayapo kwenye mada yangu.. Naona kwenye mada nzima na kila nilichoandika havijadiliwi tena bali tumebaki na ukabila.. Rudia kusoma tena pls

Jr
Mbona sijaandika kabila, nimetumia neno 'Kaskazini' kama ulivyolianzisha. Na sisi Watu wazima tafsiri tunaijua labda utuambie Kaskazini ipi uliyomaanisha
 
Mshana bhana! Kwahiyo hii hoja yako point yake ni ipi sasa? Wakati umesema katika sehemu zote zilizopendelewa kiuchumi bado watu wa Kas kazini wameshika nafasi za juu?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli kwan uongo?
Sehemu yoyote mtu wa kaskazini alipo lazma kuendelee, ukienda mkuranga,kisarawe wachaga wamenunua karibu maeneo yote na maendeleo ni makubwa mno,ila mwanzoni wenyeji hawakuona fursa hii hii ndio mantiki ya mshana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watu wa Kaskazini hasa Kilimanjaro ubaguzi ndio asili yao.
Wanasema wanashushwa, sijajua lini walipandishwa?

Hao watu wanapenda kila kitu kizuri kiwe chao hivyo wakikosa ndio wanaanza porojo

Kuiba maofisini, ufisadi, ujambazi , utapeli ndio mambo wanayoweza sasa Magufuli kawabana kwote huko ndio wanakuja kutema nyongo kwa ID fake hapa JF
Kwani kila kitu kizuri kikijengwa kaskazini ndiyo nchi itakuwa imeendelea?

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ndo nilileta tetemeko? Ndo majibu waliyopewa watu wa kagera walipopatwa na majanga.

Kagera kila mtu anapambana na Hali yake ukilima kahawa ukapata upenyo Uganda ndo umetajirika hivyo.

Ukiangalia mkoa wa kagera maendeleo ya watu binafsi yako juu kuliko general maana ya miundombinu ambayo ni KAZI ya serikali.


Nyumba ni nzr vijijin lakin barabara za vijijin serikali haitaki kujenga

Sent using Jamii Forums mobile app
Noted
Kaskazini ameshindwa kuidumaza maana watu wa kule Wana akili nyingi ametumia kila nguvu lakin Cha ajabu kaskazini haitetereki kila mahali tz ukienda unakuta wakaskazin wameshika fursa,hata chato wakaskazin wameshakamata fursa kitaambo huku wenyeji wakichunga ngombe,hii ndio faida ya elimu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda tukuchukue ramani then tuangalie upande wa kaskazini kuna nani na nani... Hii itasaidia kuondoa mazoea na kukariri jambo ambalo ni baya sana... Na katika maisha tumefeli ama kupotosha mara nyingi kutokana na mazoea na kukariri... We are not specific...
Mbona sijaandika kabila, nimetumia neno 'Kaskazini' kama ulivyolianzisha. Na sisi Watu wazima tafsiri tunaijua labda utuambie Kaskazini ipi uliyomaanisha

Jr
 
Jamaa wa manispaa ya moshi wanajiona wajanja sana wakati Dodoma imewapita hivi hivi na kuwa jiji.

Sent using Jamii Forums mobile app
Dodoma hiyo ya ku boostiwa?
Mbona Dodoma wananchi ni maskini Sana?
Kilimandjaro ni mkoa wa pili watu wake kuishi maisha Bora na makazi Bora kwa 90%
Wakati kule Dodoma wanalala nyumba zimefanana na banda lá kuku kule moshi
PILI kilimanjaro Hakuna shida za maji,umeme, zahanati lkn dodoma ndio sasahv wanajengewa na serikali ndio ufananishe na kilimanjaro?
Kilimanjaro wananchi wanajitoa sana ktk maendeleo,mfano vunjo mwaka jana wananchi walichanga bilion 7 kukarabati barabara zote za jimbo dodoma wana uwezo huo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uko sahihi, huyo mshana anajaribu ku compromise ila anajua ameshakosea na mada yake ya kitoto na ubaguzi.

Ajabu kuna vitoto vimeshadakia mada vinataka ligi bila Kujua historia ya utawala wa hii nchi
Mbona sijaandika kabila, nimetumia neno 'Kaskazini' kama ulivyolianzisha. Na sisi Watu wazima tafsiri tunaijua labda utuambie Kaskazini ipi uliyomaanisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Natambua wingi wa matukio na harakati za maisha vinatufanya kuangalia mapya bila kutafakari yaliyopita..
Wiki hii kulikuwa na mjadala mwingine baada ya kuzinduliwa Mahakama ya mwanzo CHATO ikitajwa kama mahaka kubwa na nzuri kulinganisha na Mahakama nyingine za mwanzo TANZANIA

Tangu awamu hii ishike hatamu mambo mengi ya kimaendelea yamefanyika CHATO... Kwa kutaja chache tu

Traffic lights
Jengo kubwa la Bank ya CRDB
Jengo la mamlaka ya mapato TRA
Mbuga ya wanyama
Uwanja wa ndege
Uwanja wa mpira
Msikiti mkubwa nknk
Malalamiko yamekuwa mengi kuwa kuna upendeleo unafanywa kuipa CHATO maendeleo isiyostahili
Ni lazima tukumbuke kanuni hii muhimu ya BINADAMU kwamba MWAMBA NGOMA NGOZI HUVUTIA KWAKE... Ni baba wa Taifa pekee hayati Mwalimu J. K. Nyerere ambaye alienda tofauti na kauli hii na kidogo akafuatiwa na Mzee Mwinyi na Mzee Mkapa

Alipoingia madarakani brother Jakaya mambo yakawa tofauti... Akaamua kutumia nafasi yake kuwasaidia watu wa kwake.. Aamejitahidi kadiri alivyoweza kuiamsha Pwani.. Miradi mingi ikipelekwa huko ama Pwani ikipewa kipaumbele... Ombwe halikuonekana sana kwakuwa pia Pwani ni eneo MKAKATI kwa ajili ya kuingia na kutoka Dar.

Hata hivi viwanda vya leo Pwani zilikuwa ni juhudi zake.. Lakini kuna mengine yakawa ni kama hayakuwa na ullazima wa kuyafanya... Leo hii kuna njia mbili za lami mpaka mlangoni kwake pale Msoga... Lakini kuna Msikiti mkubwa mzuri ulijenga pale Msoga barabarani siku hizi umezungukwa na nyasi. Hauhudumiwi tena

Natambua dhima ya kila kiongozi kutaka kusaidia eneo lake ili walau lifanane na kwingine... Natambua fika mawazoni mwao wanataka kuona maeneo yao yakifanana na kaskazini hasa ukanda wote wa Tanga, Moshi mpaka Arusha... Lakini huu ni mchakato mrefu wenye kuhitaji maandalizi na mpango MKAKATI a kina... Kielimu na kubadili mtazamo wa wenyeji wake

Watu wa kaskazini wako vizuri juu na chini pia na wnapenda sana kutumia vizuri fursa zilizopo, ni wabunifu na ni wachapakazi.. Hawana majungu na wanathamini kila kitu kizuri.. Wanapenda UMOJA na kushirikishana... Wanajua vizuri thamani ya elimu ardhi na rasilimali watu....

Maendeleo yaliyojaribu kupelekwa CHATO na PWANI yangepelekwa kaskazini... kisinheharibika hata kitu kimoja na kingetumiwa kwa weledi mkubwa na kuleta matokeo chanya zaidi... Lakini la zaidi huko kote wanaosimania na kujaribu kuleta matokeo hayo chanya bado ni wale wale wa kaskazini!

Kwa mfano Pwani ya JK wenyeji wamebaki kuwa viibarua wapagazi na kazi zisizo na taaluma huku wakiendelea kuuza ardhi zao kwa bei sawa na bure.. Wao wakipata pesa kidogo ni starehe na KUONGEZA wake.

Siwezi kuizungumzia CHATO kwasasa lakini haina tofauti sana na Pwani... Na kuna uwezekano mkubwa sana awamu hii ikiheshimu Katiba na kuondoka madarakani kila kitu kitakufa kule.... Labda wa kaskazini wafanye jitihada kuokoa jahazi kwakuwa maono yao ni makubwa na uelewa wao uko deep zaidi...

Kuna tofauti kubwa sana kati ya mtoto aliyekulia nyumba ya nyasi na aliyekulia nyumba ya bati na sakafu...

Nimemaliza...!!!!

Jr
Rubbish, ulitaka fursa zipelekwe Mwanga? hamjaridhika na aliyowafanyia Msuya?
Siku hizi umekuwa mtaalam wa kuandika pumba
 
Nimekuelewa Sana mkuu hongera
Kwa kawaida ya kabira yetu ulitakiwa kusifiwa kwa tusi au salazo ila tuuachane na hayo,
Kuhusu vingine vilivyojengwa harafu havina muendelezo si kweli kuota nyasi msiti wa msoga inatokana na kijji kilivyo kwa msoga ilivyo Kama kule kilipo Kijiji kukawa kumejengwa msikiti mwengine Basi hapana budi ule msikiti wa barabarani kuota nyasi
Nilichojifunza kwa
Watu wa kaskazin kikubwa ubinfs (ukabila) migogoro ya mipaka aridhi mkiwa na mtu wa kutoka kaskazin kjijin kwenu maendeleo anataka yawe kwake tu mi nilishaamishiwa nguzo ya umeme kisa kaenda kulipa yeye hapo ilipowekwa nguzo na tanesko wote tungepata umeme mini na yeye lakini yeye akawambia iwekwe kwenye kiwanja chake sio hapo barabarani
nakubali kuwa aridhi iliuzwa na inauzwaa Bei Chee kweli lakini utakuta kaya moja yenye familia ya watu 10 Wana pori la heka 100 Kila wanalima heka 12 au 15 Kuna heka nyingi zinabaki hazifanyiwi kazi hujauza Bei Chee unangoja Nini,matapeli wakuuzie
Pwani kikwete kaacha alama kapandisha aridhi thamani na maendeleo yanayoendelea


Sent using Jamii Forums mobile app
Kisarawe, mkuranga,bagamoyo wachaga wameinunua karibu yote wanaona fursa ya miaka 20 mbele
Yaan Hawa watu kwa maendeleo nawapa hongera

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waache watu wa Chato wajiletee maendeleo yao wenyewe kwa juhudi zao wakijua wanafanya nini na nini gharama ya maendeleo kuliko kuletewa maendeleo wasiyojua yanatoka wapi. Wazaramo ni watu wa asili ya Dar es Salaam. Hawa wangepaswa kuwa ndio watu walioendelea zaidi ya wengine wote Tz. Lakini kwasababu waliletewa kila kitu mlangoni hawakufanya chochote cha kujiendeleza, wakabaki wakifikiri kwamba maendeleo ni kitu cha kuletewa na wengine kama zawadi. Angalia leo hii wazaramo miaka 200 baada ya kuishi na waarabu, wajerumani, waingereza, wahindi na wapare, wachagga, n.k. bado ni primitive na wanazidi kuuza ardhi na kusogea mbali na jiji huko Mkuranga na kwingineko.
N'a kule mkuranga,kisarawe , bagamoyo wachaga wameshanunua karibu yote tunawasogeza tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Eti wa kaskazini maono yao makubwa blah blahh blahh

Kwahio kanda zingine vilaza?.nchi hii imefika hapa kwa sababu yenu tu?

mnasahau hii iko hivyo kwa sababu ya kihistoria ya umishenari na ukoloni?.
Kama hamuamini watch and see ....everyone is educated this days na kila mtu ni mfanya biashara siku hizi

Sikutegemea kuona mindset kama hii kutoka kwako...ohh na we ni wa Kaskazini i forgot
But niwakumbushe ukabila hauna nafasi tena nchini kwa sasa..
Acha wivu jifunze kwa walioendelea
Kwan ni uongo tangu enzi na enzi kilimanjaro ni mwalimu wa maendeleo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata ningekua mimi ningekumbuka nyumbani aisee! Uzuri hata Waziri Mkuu mstaafu anayetokea Kaskazini Cleopa Msuya, mpaka leo kuna baadhi ya wadau wanamshutumu kupeleka barabara ya lami kwao huku maeneo mengi ya kimkakati yakipotezewa.

Sema tu kuna umuhimu wa kubalance kwa namna yoyote ile! maana too much is harmful.
 
Back
Top Bottom