Mkishangaa ya Chato msisahau ya Msoga

Mkishangaa ya Chato msisahau ya Msoga

Ukizungumzia maendeleo ya kanda ya Kaskazini usisahau kuna kanda ya ziwa pia.

Siku zote ni huwa Mwanza vs Arusha na Moshi vs Kagera na si Chato vs Kaskazini.

Lakini kwanini haya yote ni chato kama si ubinafsi wakati Kagera hawana hata stendi ya mabasi ya kueleweka.

Jr
 
Wachaga na watu wa Kas kazini acheni kuishi Tanznaia ya Miaka 30 iliyopita!

Sasa hivi kila mtanzania ana exposure, amesoma, siyo kama zamani mchaga pekee ndio alikuwa biashara anajua yeye, kazi za maofisini anajua yeye tu!

Sasa hivi kila mtu ni mjanja. Fursa ikijitokeza kila Kabila linaiona na kuifanyia kazi.

Sasa ndugu zangu wa Kas kazini bado mna akili za miaka ya nyuma hamtaki kukubali ukweli kwamba fursa mlizokuwa mnazi fanya ninyi siku hizi kila mtanzania anamudu kuzifanya! Ndio maana mnaona kama mnaonewa na utawala huu maana kila mnapoenda mnakuta watu wameshawahi

Kubalini kwamba watanzania wa kila Kabila wanasoma na wamejanjaruka siku hizi.

Hakuna kinachodumu milele. Poleni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio maana mnaona kama mnaonewa na utawala huu maana kila mnapoenda mnakuta watu wameshawahi
Kuna mahali nimetaja uonevu? Kuna mahali nimetaja kabila lolote? Anyway ni mjadala hivyo una mengi ndani yake
Wachaga na watu wa Kas kazini acheni kuishi Tanznaia ya Miaka 30 iliyopita!

Sasa hivi kila mtanzania ana exposure, amesoma, siyo kama zamani mchaga pekee ndio alikuwa biashara anajua yeye, kazi za maofisini anajua yeye tu!

Sasa hivi kila mtu ni mjanja. Fursa ikijitokeza kila Kabila linaiona na kuifanyia kazi.

Sasa ndugu zangu wa Kas kazini bado mna akili za miaka ya nyuma hamtaki kukubali ukweli kwamba fursa mlizokuwa mnazi fanya ninyi siku hizi kila mtanzania anamudu kuzifanya! Ndio maana mnaona kama mnaonewa na utawala huu maana kila mnapoenda mnakuta watu wameshawahi

Kubalini kwamba watanzania wa kila Kabila wanasoma na wamejanjaruka siku hizi.

Hakuna kinachodumu milele. Poleni.

Sent using Jamii Forums mobile app

Jr
 
Sawa but huko chato imekuwa too much asee ,msoga cyo saana alafu kikwete hakukandamiza maeneo mengine kwa kiburi na kujiskia Kama huyu meko ,jamaa namfananisha kwa mbaali na mobutu sese seko kuku ngwendu wazabanga ,,kwa mambo yake anayoyafanya
But hapa ni heri aliyenacho aingezewe tu yaani kwa kuwa Kanda ya kaskazini tulishaejielewa mapema na mind u that hatuna kibur ,next time urais utoke kaskazi Sasa ,,,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwanza nasikitika saana kuona baadhi
ya watanzania kujiona wajanja kuliko wengine wakati wamekalia kuti kavu..nadhani ni kiburi cha mamlaka au kuvimbiwa tu ..Maendeleo ya Tz ni historical..kwa German kushindwa vita..maendeleo lazima yawe hivi yalivvyo..kwani tumezungukwa na maadui wasio tayari kufanya biashara nasi..hata kwa hali ya kawaida hatupo vizuri na majirani zetu..sehemu pekee yenye nafuu kimasilahi kwa Tanzania ni Kenya yenye connection NATO na UsD..naam uwekezaji wa kikolon ulilenga British East Afrika yenye himaya Nairobi..kwa upepo huu wa hulka zetu za kikabila itachukua muda mrefu mikoa mingine kuipita Kaskazini kiuchumi..labda kwa maamuzi sahihi ya viongozi wetu lakini kwa mawazo ya AU,SADC na EAC tunapoteza muda tu na hatutoweza toka kamwe..Kuna mzingira ya aina tatu yanaweza kubadili Uchumi wa Tanzania.
1.Tuungane na Burundi,DRC na ANGOLA..Burundi ni njia kufika kwa hao tunaofanana kimaliasili.
2.BRICS isimame kama West block..tutapata mbadala wa access ya mafuta..naam bidhaa na technology.
3.Uhusino na nchi za Asia iwe kipaumbele.
Kwa hali hiyo mambo yatakuwa shwari Tanzania..kwa sasa kaskazini wanaconnection asili. Wengine tulie tu.
 
Ndio maana mnaona kama mnaonewa na utawala huu maana kila mnapoenda mnakuta watu wameshawahi
Kuna mahali nimetaja uonevu? Kuna mahali nimetaja kabila lolote? Anyway ni mjadala hivyo una mengi ndani yake

Jr
Mshana bhana! Kwahiyo hii hoja yako point yake ni ipi sasa? Wakati umesema katika sehemu zote zilizopendelewa kiuchumi bado watu wa Kas kazini wameshika nafasi za juu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukizungumzia maendeleo ya kanda ya Kaskazini usisahau kuna kanda ya ziwa pia.

Siku zote ni huwa Mwanza vs Arusha na Moshi vs Kagera na si Chato vs Kaskazini.

Lakini kwanini haya yote ni chato kama si ubinafsi wakati Kagera hawana hata stendi ya mabasi ya kueleweka.
Mimi ndo nilileta tetemeko? Ndo majibu waliyopewa watu wa kagera walipopatwa na majanga.

Kagera kila mtu anapambana na Hali yake ukilima kahawa ukapata upenyo Uganda ndo umetajirika hivyo.

Ukiangalia mkoa wa kagera maendeleo ya watu binafsi yako juu kuliko general maana ya miundombinu ambayo ni KAZI ya serikali.


Nyumba ni nzr vijijin lakin barabara za vijijin serikali haitaki kujenga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Natambua wingi wa matukio na harakati za maisha vinatufanya kuangalia mapya bila kutafakari yaliyopita..
Wiki hii kulikuwa na mjadala mwingine baada ya kuzinduliwa Mahakama ya mwanzo CHATO ikitajwa kama mahaka kubwa na nzuri kulinganisha na Mahakama nyingine za mwanzo TANZANIA

Tangu awamu hii ishike hatamu mambo mengi ya kimaendelea yamefanyika CHATO... Kwa kutaja chache tu

Traffic lights
Jengo kubwa la Bank ya CRDB
Jengo la mamlaka ya mapato TRA
Mbuga ya wanyama
Uwanja wa ndege
Uwanja wa mpira
Msikiti mkubwa nknk
Malalamiko yamekuwa mengi kuwa kuna upendeleo unafanywa kuipa CHATO maendeleo isiyostahili
Ni lazima tukumbuke kanuni hii muhimu ya BINADAMU kwamba MWAMBA NGOMA NGOZI HUVUTIA KWAKE... Ni baba wa Taifa pekee hayati Mwalimu J. K. Nyerere ambaye alienda tofauti na kauli hii na kidogo akafuatiwa na Mzee Mwinyi na Mzee Mkapa

Alipoingia madarakani brother Jakaya mambo yakawa tofauti... Akaamua kutumia nafasi yake kuwasaidia watu wa kwake.. Aamejitahidi kadiri alivyoweza kuiamsha Pwani.. Miradi mingi ikipelekwa huko ama Pwani ikipewa kipaumbele... Ombwe halikuonekana sana kwakuwa pia Pwani ni eneo MKAKATI kwa ajili ya kuingia na kutoka Dar.

Hata hivi viwanda vya leo Pwani zilikuwa ni juhudi zake.. Lakini kuna mengine yakawa ni kama hayakuwa na ullazima wa kuyafanya... Leo hii kuna njia mbili za lami mpaka mlangoni kwake pale Msoga... Lakini kuna Msikiti mkubwa mzuri ulijenga pale Msoga barabarani siku hizi umezungukwa na nyasi. Hauhudumiwi tena

Natambua dhima ya kila kiongozi kutaka kusaidia eneo lake ili walau lifanane na kwingine... Natambua fika mawazoni mwao wanataka kuona maeneo yao yakifanana na kaskazini hasa ukanda wote wa Tanga, Moshi mpaka Arusha... Lakini huu ni mchakato mrefu wenye kuhitaji maandalizi na mpango MKAKATI a kina... Kielimu na kubadili mtazamo wa wenyeji wake

Watu wa kaskazini wako vizuri juu na chini pia na wnapenda sana kutumia vizuri fursa zilizopo, ni wabunifu na ni wachapakazi.. Hawana majungu na wanathamini kila kitu kizuri.. Wanapenda UMOJA na kushirikishana... Wanajua vizuri thamani ya elimu ardhi na rasilimali watu....

Maendeleo yaliyojaribu kupelekwa CHATO na PWANI yangepelekwa kaskazini... kisinheharibika hata kitu kimoja na kingetumiwa kwa weledi mkubwa na kuleta matokeo chanya zaidi... Lakini la zaidi huko kote wanaosimania na kujaribu kuleta matokeo hayo chanya bado ni wale wale wa kaskazini!

Kwa mfano Pwani ya JK wenyeji wamebaki kuwa viibarua Papaya's na kazi zisizo na taaluma huku wakiendelea kuuza ardhi zao kwa bei sawa na bure.. Wao wakipata pesa kidogo ni starehe na KUONGEZA wake.

Siwezi kuizungumzia CHATO kwasasa lakini haina tofauti sana na Pwani... Na kuna uwezekano mkubwa sana awamu hii ikiheshimu Katiba na kuondoka madarakani kila kitu kitakufa kule.... Labda wa kaskazini wafanye jitihada kuokoa jahazi kwakuwa maono yao ni makubwa na uelewa wao uko deep zaidi...

Kuna tofauti kubwa sana kati ya mtoto aliyekulia nyumba ya nyasi na aliyekulia nyumba ya bati na sakafu...

Nimemaliza...!!!!

Jr
Mimi nadhani dhana hizo hazipo tena kwasababu kupata taarifa ni rahisi na watu wameingiliana sana ..hapo ni jamii husika kutumia mitaji ili kukua basi
 
Back
Top Bottom