Mkishangaa ya Chato msisahau ya Msoga

Mkishangaa ya Chato msisahau ya Msoga

Dah, haya mkuu yetu macho uliyosema yana ukweli wake. Jengo la mahakama wilaya ya Chato ni hatari kuliko mikoa mingi niyotembelea na hakika muendelezo wa hayo yote itakuwa ni changamoto kwani rasilimali watu haijaendelezwa kabisa
Yeye kasema mahakama ya mwanzo. Naona anaandika kwa mzuka na hisia kali. Kitu ambacho si kizuri kwa calibre ya mtu kama Mshana.
 
Naomba unirekebishe Rwebo kama nimekosea tafadhali
Yeye kasema mahakama ya mwanzo. Naona anaandika kwa mzuka na hisia kali. Kitu ambacho si kizuri kwa calibre ya mtu kama Mshana.

Jr
 
Vyote kwa pamoja vinahitajika i mean uwezeshwaji wa rasilimali watu na vitu ili kufanikisha maendeleo ya jamii husika.

Ila swali la msingi ni je, kipi kianze kati ya uwezeshwaji wa rasilimali watu au vitu..?
 
Viende sawia na bila agenda ya siri... Maslahi ya wengi yawe ndio kipaumbele bila kuwa na agenda za kisiasa na kujijenga binafsi
Vyote kwa pamoja vinahitajika i mean uwezeshwaji wa rasilimali watu na vitu ili kufanikisha maendeleo ya jamii husika.

Ila swali la msingi ni je, kipi kianze kati ya uwezeshwaji wa rasilimali watu au vitu..?

Jr
 
Naomba unirekebishe Rwebo kama nimekosea tafadhali

Jr
Hujakosea sana, mahakama inayozungumziwa ni ya wilaya, lakini wewe ukasema ni ya mwanzo kitu ambacho kinaweza amsha hasira za wananchi. Other wise uko vizuri Mshana Jr. Bravo!!
 
Nimekuelewa Sana mkuu hongera
Kwa kawaida ya kabira yetu ulitakiwa kusifiwa kwa tusi au salazo ila tuuachane na hayo,
Kuhusu vingine vilivyojengwa harafu havina muendelezo si kweli kuota nyasi msiti wa msoga inatokana na kijji kilivyo kwa msoga ilivyo Kama kule kilipo Kijiji kukawa kumejengwa msikiti mwengine Basi hapana budi ule msikiti wa barabarani kuota nyasi
Nilichojifunza kwa
Watu wa kaskazin kikubwa ubinfs (ukabila) migogoro ya mipaka aridhi mkiwa na mtu wa kutoka kaskazin kjijin kwenu maendeleo anataka yawe kwake tu mi nilishaamishiwa nguzo ya umeme kisa kaenda kulipa yeye hapo ilipowekwa nguzo na tanesko wote tungepata umeme mini na yeye lakini yeye akawambia iwekwe kwenye kiwanja chake sio hapo barabarani
nakubali kuwa aridhi iliuzwa na inauzwaa Bei Chee kweli lakini utakuta kaya moja yenye familia ya watu 10 Wana pori la heka 100 Kila wanalima heka 12 au 15 Kuna heka nyingi zinabaki hazifanyiwi kazi hujauza Bei Chee unangoja Nini,matapeli wakuuzie
Pwani kikwete kaacha alama kapandisha aridhi thamani na maendeleo yanayoendelea


Sent using Jamii Forums mobile app
 
asante kwa masahihisho nitarekebisha...!!!
Hujakosea sana, mahakama inayozungumziwa ni ya wilaya, lakini wewe ukasema ni ya mwanzo kitu ambacho kinaweza amsha hasira za wananchi. Other wise uko vizuri Mshana Jr. Bravo!!

Jr
 
Hujawa muwazi mkuu ni nini hasa kifanyike kuiinua chato
Waache watu wa Chato wajiletee maendeleo yao wenyewe kwa juhudi zao wakijua wanafanya nini na nini gharama ya maendeleo kuliko kuletewa maendeleo wasiyojua yanatoka wapi. Wazaramo ni watu wa asili ya Dar es Salaam. Hawa wangepaswa kuwa ndio watu walioendelea zaidi ya wengine wote Tz. Lakini kwasababu waliletewa kila kitu mlangoni hawakufanya chochote cha kujiendeleza, wakabaki wakifikiri kwamba maendeleo ni kitu cha kuletewa na wengine kama zawadi. Angalia leo hii wazaramo miaka 200 baada ya kuishi na waarabu, wajerumani, waingereza, wahindi na wapare, wachagga, n.k. bado ni primitive na wanazidi kuuza ardhi na kusogea mbali na jiji huko Mkuranga na kwingineko.
 
Tutachukua Maasai kutoka Ngorongoro kuwahamishia burigi
Hakuna lisilowezekana katika Awamu hii
Angalia eti unajengwa uwanja wa ndege wa kimataifa porini, halafu kwasababu watu wanahoji ujenzi huu, basi serikali ndio inageuza mapori ya akiba yaliyo karibu na uwanja kuwa national parks ili kuhalalisha ujenzi wa uwanja wa ndege. Ndivyo waafrika tunavyofanya ndio maana hatuendelei.

Uwanja wa ndege wa kimataifa aliojenga Mobutu kijijini kwake sasa ni pango la popo na panya. Uwanja huu zilikuwa zinatua hata ndege aina ya Concorde. Lakini sasa angalia uwanja ulivyo hapa.
1576843104536.png
 
Eti wa kaskazini maono yao makubwa blah blahh blahh

Kwahio kanda zingine vilaza?.nchi hii imefika hapa kwa sababu yenu tu?

mnasahau hii iko hivyo kwa sababu ya kihistoria ya umishenari na ukoloni?.
Kama hamuamini watch and see ....everyone is educated this days na kila mtu ni mfanya biashara siku hizi

Sikutegemea kuona mindset kama hii kutoka kwako...ohh na we ni wa Kaskazini i forgot
But niwakumbushe ukabila hauna nafasi tena nchini kwa sasa..
 
.
Waache watu wa Chato wajiletee maendeleo yao wenyewe kwa juhudi zao wakijua wanafanya nini na nini gharama ya maendeleo kuliko kuletewa maendeleo wasiyojua yanatoka wapi. Wazaramo ni watu wa asili ya Dar es Salaam. Hawa wangepaswa kuwa ndio watu walioendelea zaidi ya wengine wote Tz. Lakini kwasababu waliletewa kila kitu mlangoni hawakufanya chochote cha kujiendeleza, wakabaki wakifikiri kwamba maendeleo ni kitu cha kuletewa na wengine kama zawadi. Angalia leo hii wazaramo miaka 200 baada ya kuishi na waarabu, wajerumani, waingereza, wahindi na wapare, wachagga, n.k. bado ni primitive na wanazidi kuuza ardhi na kusogea mbali na jiji huko Mkuranga na kwingineko.


Jr
 
Angalia eti unajengwa uwanja wa ndege wa kimataifa porini, halafu kwasababu watu wanahoji ujenzi huu, basi serikali ndio inageuza mapori ya akiba yaliyo karibu na uwanja kuwa national parks ili kuhalalisha ujenzi wa uwanja wa ndege. Ndivyo waafrika tunavyofanya ndio maana hatuendelei.

Uwanja wa ndege wa kimataifa aliojenga Mobutu kijijini kwake sasa ni pango la popo na panya. Uwanja huu zilikuwa zinatua hata ndege aina ya Concorde. Lakini sasa angalia uwanja ulivyo hapa.View attachment 1298155

Jr
 
LadyRed kuna mahali nimezungumzia makabila na ukabila? Ninaposema kaskazini unapata tafsiri gani?
Je si kweli kwamba pamoja na Pwani kubebwa vilivyo lakini wenyeji wake wameshindwa kabisa kujitambua..?
LadyRed rafiki toka kwenye hilo box la fikra finyu uione hii post katika mtazamo mpana zaidi utanielewa
Eti wa kaskazini maono yao makubwa blah blahh blahh

Kwahio kanda zingine vilaza?.nchi hii imefika hapa kwa sababu yenu tu?

mnasahau hii iko hivyo kwa sababu ya kihistoria ya umishenari na ukoloni?.
Kama hamuamini watch and see ....everyone is educated this days na kila mtu ni mfanya biashara siku hizi

Sikutegemea kuona mindset kama hii kutoka kwako...ohh na we ni wa Kaskazini i forgot
But niwakumbushe ukabila hauna nafasi tena nchini kwa sasa..

Jr
 
Wewe ni mtu mzima, acha ushamba na mawazo ya kitoto.
Umeshajiuliza mada hii ya kijinga ikiyo na upumbavu na ubaguzi itasaidia nini vijana?
Natambua wingi wa matukio na harakati za maisha vinatufanya kuangalia mapya bila kutafakari yaliyopita..
Wiki hii kulikuwa na mjadala mwingine baada ya kuzinduliwa Mahakama ya mwanzo CHATO ikitajwa kama mahaka kubwa na nzuri kulinganisha na Mahakama nyingine za mwanzo TANZANIA

Tangu awamu hii ishike hatamu mambo mengi ya kimaendelea yamefanyika CHATO... Kwa kutaja chache tu

Traffic lights
Jengo kubwa la Bank ya CRDB
Jengo la mamlaka ya mapato TRA
Mbuga ya wanyama
Uwanja wa ndege
Uwanja wa mpira
Msikiti mkubwa nknk
Malalamiko yamekuwa mengi kuwa kuna upendeleo unafanywa kuipa CHATO maendeleo isiyostahili
Ni lazima tukumbuke kanuni hii muhimu ya BINADAMU kwamba MWAMBA NGOMA NGOZI HUVUTIA KWAKE... Ni baba wa Taifa pekee hayati Mwalimu J. K. Nyerere ambaye alienda tofauti na kauli hii na kidogo akafuatiwa na Mzee Mwinyi na Mzee Mkapa

Alipoingia madarakani brother Jakaya mambo yakawa tofauti... Akaamua kutumia nafasi yake kuwasaidia watu wa kwake.. Aamejitahidi kadiri alivyoweza kuiamsha Pwani.. Miradi mingi ikipelekwa huko ama Pwani ikipewa kipaumbele... Ombwe halikuonekana sana kwakuwa pia Pwani ni eneo MKAKATI kwa ajili ya kuingia na kutoka Dar.

Hata hivi viwanda vya leo Pwani zilikuwa ni juhudi zake.. Lakini kuna mengine yakawa ni kama hayakuwa na ullazima wa kuyafanya... Leo hii kuna njia mbili za lami mpaka mlangoni kwake pale Msoga... Lakini kuna Msikiti mkubwa mzuri ulijenga pale Msoga barabarani siku hizi umezungukwa na nyasi. Hauhudumiwi tena

Natambua dhima ya kila kiongozi kutaka kusaidia eneo lake ili walau lifanane na kwingine... Natambua fika mawazoni mwao wanataka kuona maeneo yao yakifanana na kaskazini hasa ukanda wote wa Tanga, Moshi mpaka Arusha... Lakini huu ni mchakato mrefu wenye kuhitaji maandalizi na mpango MKAKATI a kina... Kielimu na kubadili mtazamo wa wenyeji wake

Watu wa kaskazini wako vizuri juu na chini pia na wnapenda sana kutumia vizuri fursa zilizopo, ni wabunifu na ni wachapakazi.. Hawana majungu na wanathamini kila kitu kizuri.. Wanapenda UMOJA na kushirikishana... Wanajua vizuri thamani ya elimu ardhi na rasilimali watu....

Maendeleo yaliyojaribu kupelekwa CHATO na PWANI yangepelekwa kaskazini... kisinheharibika hata kitu kimoja na kingetumiwa kwa weledi mkubwa na kuleta matokeo chanya zaidi... Lakini la zaidi huko kote wanaosimania na kujaribu kuleta matokeo hayo chanya bado ni wale wale wa kaskazini!

Kwa mfano Pwani ya JK wenyeji wamebaki kuwa viibarua wapagazi na kazi zisizo na taaluma huku wakiendelea kuuza ardhi zao kwa bei sawa na bure.. Wao wakipata pesa kidogo ni starehe na KUONGEZA wake.

Siwezi kuizungumzia CHATO kwasasa lakini haina tofauti sana na Pwani... Na kuna uwezekano mkubwa sana awamu hii ikiheshimu Katiba na kuondoka madarakani kila kitu kitakufa kule.... Labda wa kaskazini wafanye jitihada kuokoa jahazi kwakuwa maono yao ni makubwa na uelewa wao uko deep zaidi...

Kuna tofauti kubwa sana kati ya mtoto aliyekulia nyumba ya nyasi na aliyekulia nyumba ya bati na sakafu...

Nimemaliza...!!!!

Jr

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom