Nadhani mpk hapo ndugu yangu MpiganiaUhuru kesi imeisha, kumbe ana haki ya kufanya hivyo hasa kwa kua umesema mnaishi mbalimbali lkn pia mlishawahi kusuluhisha tatizo la mchepukoNashukuru, kweli wewe ni Kubwa Lao. In fact alianza tabia ya kunichunguza kwa kutumia watu tulio kuwa nao karibu kama vile majirani zangu na wafanyakazi wenzangu na baadaye akagundua kuwa hao hao wanamgeuka kwa kuja kuniambia hivyo akabadili style. Tatizo kubwa lililopelekea yeye kuanza tabia hiyo ni baada ya yeye kugundua kuwa nina kamchepuko ingawa hili tulishalijadili kama wanandoa na kulimaliza yapata miaka 3 sasa.
Amekataa kabisa kuweka wazi, yeye ameng'ang'ania kuomba msamaha na kudai yaishe. Yataishaje bila kujua methodology aliyotumia?Unaweza kumuuliza mke wako ka hack vipi na mimi nihack Ya baba watoto wangu? Tuletee humu
Ni mkeo wa ndoa, na tena mna watoto wawili tayari halafu unataka kumfungulia kesi ili afungwe kisa kaingilia mawasiliano yako, aisee Wewe ni mpumbavu sana mkuu, hujui kuwa mkeo ndo Wewe mwenyewe? ninyi ni mwili mmoja kwa hiyo ana haki ya kujua privacy zako zote Na Wewe ndo una makosa huwezi kutuma pesa popote bila mkeo kujua, ni lazima umshirikishe kwa kila jambo ndo maana ya mke, huyo si hawara yako ni mkeo sasa unakuwaje na akili ya kivuta bangi eti umshtaki mkeo?Habari wanajamvi,
Katika hali isiyo ya kawaida nimegundua kuwa mke wangu wa ndoa ame-hack simu yangu na kuweza ku-access mawasiliano yangu yote hasa ya sms tokea mwezi wa 10 mwaka jana 2015 na kuzihifadhi kwenye simu yake. Sina uhakika kama aliweza kupata mawasiliano mengine tofauti na sms. Ninasema ku-hack kwa sababu tunaishi mikoa tofauti na hivyo hakuwa na namna yoyote ya ku-access simu yangu physically toka wakati huo, pia cmu yangu ambayo ni smart phone ina security (password) in case angetumia mtu aliye karibu yangu. Nimegundua hii hacking baada ya kuwa na hali ya kutoelewana kati yetu kwa muda sasa ambapo pamoja na mambo mengine niligundua kuna taarifa zangu za siri anazozifahamu ndipo nilipoanza uchunguzi na kugundua kuwa ana hizo sms. Miongoni mwa sms anazoshikia bango ni zile zinazohusiana na miamala ya Mpesa ambapo nimewatumia pesa ndg, jamaa na marafiki ambao ckuona umuhimu wa kumtaatifu hivyo akazijengea hoja mbali mbali ikiwemo ya uhusiano wa kimapenzi wakati si kweli! Nimejaribu kumbana aseme amewezaje ku-access "private communications" zangu ila amegoma kabisa kuweka wazi. Cha kushangaza zaidi ni kuwa hana utaalam wowote wa masuala ya mawasiliano!
Kwa kuzingatia usumbufu uliojitokeza kwa kuingilia mawasiliano yangu ya siri hasa kupitia mis-perception ya taarifa alizokutana nazo, nimepata wazo la kumshtaki kwa mujibu wa ile SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO, 2015 ila nikaona kabla cjafanya hivyo nililete suala hili hapa ili nipate michango yenu ya mawazo hasa juu ya nini cha kufanya. Suala hili limenichanganya sana hasa ukizingatia kuwa tumekuwa kwenye ndoa takribani miaka 8 sasa na tuna watoto 2. Naombeni michango yenu ya mawazo.
Ahsante!
Hivi ndugu zangu watanzania kwa nini tunakosa kuaminiana ktk ndoa zetu? wewe una familia yako na watoto bado unalalamika unataka kumshitaki mkeo kisa kaingilia privacy yako... sasa nini maana yakuoa unaoa ili iweje? unajua maana na umuhimu wa ndo kweli wewe nakushauri kabla hujamshitaki mkeo nenda aidha kwa mchungaji wako aliyefungisha ndoa yenu ama uende msikitini kama ndoa yako ilifungishwa na Sheikh.. utapata solusheni sahihi ndg yangu usitake kuharibu ndoa yako kwa jambo lenye kushaurika.Sehem za siri zenu mnaonyeshana hadi kuzaa watoto wawili, Ila sim inakufanya umshtaki!
hebu mwambie, maana mimi mwenyewe nimekua na wasiwasi kuhusu maturity ya huyu jamaa anayejiita Nyani Ngabukumfanya mke ajue kila kitu sawa na kuuza ramani ya vita kwa adui wewe!!
Kweli wewe ni Cipro~, povu jiingi! Sababu kuu ya kuleta huu uzi hapa ni kupata ushauri na ndio maana ckukimbilia mahakamani kwanza kutokana na side effects zake, hiyo mitusi vipi? Mtu maakini akishasoma uzi huu atajua kuwa tayari ndoa yetu ina mgogoro, usijidai huoni!Ni mkeo wa ndoa, na tena mna watoto wawili tayari halafu unataka kumfungulia kesi ili afungwe kisa kaingilia mawasiliano yako, aisee Wewe ni mpumbavu sana mkuu, hujui kuwa mkeo ndo Wewe mwenyewe? ninyi ni mwili mmoja kwa hiyo ana haki ya kujua privacy zako zote Na Wewe ndo una makosa huwezi kutuma pesa popote bila mkeo kujua, ni lazima umshirikishe kwa kila jambo ndo maana ya mke, huyo si hawara yako ni mkeo sasa unakuwaje na akili ya kivuta bangi eti umshtaki mkeo?
Tatizo watu hamjui thamani ya ndoa na maana ya mke, hapo unajiona Wewe uko sawa sana kwa utumbo uliofanya wa kumficha mkeo, hivi angekuwa yeye anatuma pesa anakuficha ungemwelewa? au kwa kuwa yeye ni mwanamke basi hana haki, Nakushauri usijaribu kabisa kumshtaki labda kama umeamua kuvunja ndoa na halafu akifungwa utawaambia nini hao watoto? kwamba mama yao ulimfunga!
Nakushauri tena usijaribu kabisa huo upuuzi, cha kufanya uonane na mkeo haraka myamalize matatizo yenu, ugomvi ktk ndoa ni jambo la kawaida pote duniani ila siyo tena kumfunga mwenzako, mkishindwana mwachane salama msije kutesa watoto wasio na hatia kwa upumbavu wenu.
Nipo kwenye ndoa kwa miaka 6 sasa Wewe una makosa huwezi kumficha mkeo, ndoa ni zaidi ya unavyofikiri Wewe, ndo maana wengi ndoa zimewashinda, Wewe unataka kuishi kwa chenga kivipi? mkiendelea hivyo hiyo ndoa itakufa.Ningependa zaidi kupata michango toka kwa wazoefu wa ndoa kuliko wale wenye ndoa za "kufikirika" vichwani.
Kwa hiyo kwa upande wako kosa hapa ni kumficha mke wangu baadhi ya taarifa ambazo infact sio tangible na sio ujasusi aliofanya?Nipo kwenye ndoa kwa miaka 6 sasa Wewe una makosa huwezi kumficha mkeo, ndoa ni zaidi ya unavyofikiri Wewe, ndo maana wengi ndoa zimewashinda, Wewe unataka kuishi kwa chenga kivipi? mkiendelea hivyo hiyo ndoa itakufa.
Watu mnaingiaga kwenye ndoa huku mkiwa hata hamjielewi.
Inavyoonekana mnaingiaga tu ili kukidhi matakwa potofu ya jamii.
Sasa wewe unalalamika eti mkeo anazifahami taarifa zako za siri.
Siri gani hizo ilhali mko kwenye ndoa?
Au mliwekeana makubaliano ya mipaka kwenye ndoa yenu kabla hamjaifunga?
Iwapo hiyo simu unayoitumia ulipewa zawadi na mkeo, basi bila shaka alijiandaa kupata taarifa zako kwa njia ya siri. Kama ni mkeo wa ndoa haina haja kumshitaki mahakamani kwani yote hayo yamejengeka juu ya kuwa na wivu nawe. Na wivu ndio mapenzi.Kuhack simu bila kupata simu yako ningumu sana,labda mkeo nae kama anakabuzi kampuni moja ya simu ambako ndio kanampa taarifa zote,ivyo nimoja ya kutafuta njia ya kuachana na wewe sasa kajamaa kanajitahid kumpa hiyo miamala na text ili ajue pa kuanzia
Afadhali umenisaidia kumweleza ukweli,maana anajiona yeye pekee ndo mwenye ndoa humu, anataka kuweka limit ya ndoa wakati kuvuliana nguo na kufanya mapenzi ndo mwisho wa yote, eti ku hack mawasiliano yake ndo amshtaki mwanamke, mbona hakumshtaki alipo hack dushelele lake hadi wakazaa watoto wawili, Tatizo la kudandia ndoa bila kujua uzito wake ndo hili sasa .Sehem za siri zenu mnaonyeshana hadi kuzaa watoto wawili, Ila sim inakufanya umshtaki!
Hakuna, vinginevyo nisingepata ujasiri wa kusema kuwa nafikiria kumshtaki na yeye kuishia kuomba msamaha!Naomba nikuulize swali mdau, kwenye hizo texts alizo nazo hakuna text za kumkwaza yeye?( michepuko yako).....kabla ujafikiria kwenda kumshitaki