Mke wangu katembea nje ya ndoa, nimsamehe?

Mke wangu katembea nje ya ndoa, nimsamehe?

Watu wengine bwana!! ni kwa nini unaoa kama akili yako bado haijakomaa na hujui ni nini maana ya maamuzi magumu? yani hili nalo linahitaji Ushauri?

Kama wewe ni Mkristo soma hapa:
Mwalimu ( Yesu ) Musa alitufundisha kuhusu talaka je ni kwa vipi wewe unatufundisha kwamba aliyewaunganisha Mungu basi binadamu asiwatenganishe?

Mwalimu ( Yesu ) akawajibu, zamani haikuwa hivi ila kutokana na ugumu wa mioyo yenu ndio maana Musa aliwaruhusu kuwapa talaka wake zenu, basi na mimi nasema mtu na asimuache mke wake isipokuwa kwa kosa la uzinzi tu." Mwisho wa kunukuu.

Kama kuna mtu au padri wako au Mchungaji wako anakudanganya eti Wakristo hawana talaka pole sana. Kosa la uzinzi halina msamaha kamwe.
 
angalia aina ya toba yake
je, ni kweli yaani anajutia kitendo alicho kifanya na ana maanasha hata rudia tena hicho kitendo

mwisho uamuzi una wewe
 
............Msamehe samehe kwanza hadi akikuletea Ukimwi ndo umuache, umesikia enheee mtoto mzuri!!
 
angalia aina ya toba yake
je, ni kweli yaani anajutia kitendo alicho kifanya na ana maanasha hata rudia tena hicho kitendo

mwisho uamuzi una wewe

Mkuu, hakuna cha toba wala nini hapo hao viumbe wanajua maigizo, anaweza akaomba msamaha na kuangua kilio semester nzima ila ukimsamehe tu, wembe ule ule............Askari wa wanyama pori wakipata taarifa kuwa Simba kamla binadamu huwa wanamtafuta na kumuuwa sababu wanaamini ataendelea kula binadamu tu!!. PIGA CHINIIIIIIIIIIIIIIIIII!!!!!!!!!!!!!!!
 
ww unampenda ndio maana unajiuliza. pili jiulize ww hujawahi fanya hivyo? usije tuletea story nyingene hapa huko mbeleni ''oh.. namataka mtaliki wangu nsijui nifanyeje?'' fanyha maamuzi yako mwenyew kwa kushirikisha moyo na akili nyingi isiyo changanyikiwa under stress.
 
Heshima mbele wana MMU,

Nami nimeona sio mbaya kupitia huku walau mara moja. Hoja yenyewe ni kama ilivyo:
Mke wangu ametubu kutembea nje ya ndoa nilipokuwa safarini. Hii ilikuwa baada ya kukuta kondomu iliyotumika ambayo pia ndio aina ambayo huwa nami natumia. Nimsamehe? Tumekuwa kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka sita na tumejaaliwa watoto wa kiume wawili.
For more:
My wife admitted cheating on me, should I forgive her? - DN2 - nation.co.ke
My wife admitted cheating on me, should I forgive her? - DN2 - nation.co.keView attachment 65970




Mkuu ni kweli kabisa unahaki ya kumuacha, sababu ya kumuacha unayo, uwezo waumuach unao na vilevile inawezekana labda hata nia ya kumuacha unayo, na pia vile vile sidhani kama ni dhambi kumuacha mtu wa namna hii, ila naomba utambue mkuu kwa kuwa amekiri kosa na ametubu kweli.........basi katika swala kama hili msamaha unasisitizwa zaidi ndugu yangu.........msamehe mkeo bwana, najua kiukweli inauma sana na kutomsamehe sio dhambi katika swala kama hili ila na yeye ni binadamu yule na anakosea kama binadamu wengine, jitahidi tu umsamehe mkuu.............MIMI NI HAYO TU NDUGU YANGU
 
''Mipango na Mikakati imekamilika na sasa tuko kwenye mchakato wa mazungumzo na wafadhili"- M Pinda

Hii nayo kasema lini??


Ha ha ha ha haaaa Kongosho hiyo nadhani ilikua kwenye maswali ya papo kwa papo... ila binafsi nachukizwa sana na hayo maneno.. Mchakato, mkakati!!!
 
Last edited by a moderator:
Watu wengine bwana!! ni kwa nini unaoa kama akili yako bado haijakomaa na hujui ni nini maana ya maamuzi magumu? yani hili nalo linahitaji Ushauri?

Kama wewe ni Mkristo soma hapa:
Mwalimu ( Yesu ) Musa alitufundisha kuhusu talaka je ni kwa vipi wewe unatufundisha kwamba aliyewaunganisha Mungu basi binadamu asiwatenganishe?

Mwalimu ( Yesu ) akawajibu, zamani haikuwa hivi ila kutokana na ugumu wa mioyo yenu ndio maana Musa aliwaruhusu kuwapa talaka wake zenu, basi na mimi nasema mtu na asimuache mke wake isipokuwa kwa kosa la uzinzi tu." Mwisho wa kunukuu.

Kama kuna mtu au padri wako au Mchungaji wako anakudanganya eti Wakristo hawana talaka pole sana. Kosa la uzinzi halina msamaha kamwe.
ndugu yangu, mambo tunayoyafahamu katika maisha ni machache sana zaidi ya tunayoyafahamu.
Hayajakukuta!

 
mambo ya mke kupakuliwa hayo!! nawahurumia sana wanaume, mwenyewe unaona umezungushia uzio, kumbe wenzio wanajisevia, ila na sisi! mmmhhhhh!
 
wala usiwaze maana hio siku hizi sio kosa tena maana kama supermarket kila mtu anaingia basi ni sawa na duka la kawaida hata wewe waweza ingia supermarket nyingine na ukapata unachokitaka ukarudi home
 
wala usiwaze maana hio siku hizi sio kosa tena maana kama supermarket kila mtu anaingia basi ni sawa na duka la kawaida hata wewe waweza ingia supermarket nyingine na ukapata unachokitaka ukarudi home
huo mwendelezo ndio unanichanganya akili mkuu. Maana ukifikiria pale ambapo wote tulipaswa kusimama kutokana na kiapo cha miaka 6 iliyopita ni kuwa tulishateleza. Lakini kama comments zilivyo, mwafrika ni mwafrika na hasa mwanamme lakini pia linaibuka na suala la imani juu ya kusamehe! Ugumu bado unaendelea kutamalaki
 
Hiyo condom ilikuwa na mavuno ndani (sperm)?
kama hakuna, ujue aliivua na kupiga kavu. nenda kampime kwanza halafu maamuzi baadae.
 
INAVONEKANA UMESHAMSAMEHE, ila uyo mwanamke hadi amekubali ninapata shaka hao ni jamii ya wanawake wasiofundwa. Mwanamke aliyefundwa labda awe amefumwa adhawizi hawezi kubali Kamwe.
 
Uzuri alikumbuka kutumia condom, ila tujiulize Tupo wangapi?
 
Wewe ndio unamjua zaidi mkeo raha zake na ubaya wake,na pia vile vile jiulize jee wewe hujawahi kumsaliti hata mara moja
iwe wakati wachumba au mmeshaowana? je kama uliwahi kumsaliti ulimwambia kama umemsaliti? nadhani jibu kaka utakuanao............
 
Back
Top Bottom