Wewe acha upotoshaji kabisa, kwanza hapo umeandika mawazo yako na wala sio maandiko, kwa faida ya wengi ngoja ninukuu maandiko yenyewe ni Matayo 19:8-9, "Akwaambia, 'Musa Musa kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwapa ruhusa ya kuwaacha wake zenu, lakini tangu mwanzo haikuwa hivi. Nami nawaambia ninyi: Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini."Watu wengine bwana!! ni kwa nini unaoa kama akili yako bado haijakomaa na hujui ni nini maana ya maamuzi magumu? yani hili nalo linahitaji Ushauri?
Kama wewe ni Mkristo soma hapa:
Mwalimu ( Yesu ) Musa alitufundisha kuhusu talaka je ni kwa vipi wewe unatufundisha kwamba aliyewaunganisha Mungu basi binadamu asiwatenganishe?
Mwalimu ( Yesu ) akawajibu, zamani haikuwa hivi ila kutokana na ugumu wa mioyo yenu ndio maana Musa aliwaruhusu kuwapa talaka wake zenu, basi na mimi nasema mtu na asimuache mke wake isipokuwa kwa kosa la uzinzi tu." Mwisho wa kunukuu.
Kama kuna mtu au padri wako au Mchungaji wako anakudanganya eti Wakristo hawana talaka pole sana. Kosa la uzinzi halina msamaha kamwe.
Wewe acha upotoshaji kabisa, kwanza hapo umeandika mawazo yako na wala sio maandiko, kwa faida ya wengi ngoja ninukuu maandiko yenyewe ni Matayo 19:8-9, "Akwaambia, 'Musa Musa kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwapa ruhusa ya kuwaacha wake zenu, lakini tangu mwanzo haikuwa hivi. Nami nawaambia ninyi: Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini."
Yesu anasema Musa alitoa ruhusa kwa sababu watu walikuwa na mioyo migumu yaani walikuwa wanapenda kuoa na kuacha hata Musa akawaambia basi fanyeni mnayotaka wenyewe lakini sio kwamba ilikuwa ni mpango wa Mungu. Hata pale Yesu anaposema isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati hamaanishi kwamba kama umeoa mke kihalali basi akitembea nje ya ndoa basi unaruhusiwa kumwacha hapana. Kwanza ni muhimu kufahamu maana ya maneno haya mawili yaani UZINZI na UASHERATI. Uzinzi unahusisha watu walio katika ndoa, na uasherati unahusisha watu ambao hawajaoana.
Kwa hiyo, uasherati unaozungumziwa katika maandiko ni pale watu wanapokuwa wanaishi pamoja kwa uasherati yaani hawajafunga ndoa halali, maana yake hao ni mke na mume lakini kwa sababu ya uasherati, hivyo wanaweza kuachana tu, na wanapoachana kila mmoja anakuwa huru kuoa. Lakini kamwe si kwa yule ambaye ameoa au ameolewa katika ndoa halali.
Kwa hiyo, tusidanganyane kwenye Ukristo hakuna TALAKA, kama kuna Askofu, Mchungaji au kiongozi yeyote anaruhusu watu kuachana na kuoa au kuolewa na wenza wengine, huyo anawakatia tiketi ya jehanamu kwa bei rahisi kabisa maana wanaishi maisha ya uzinzi, na wazinzi hawatauona ufalme wa Mungu, 1Kor 6:9-10.
nakiri kuwa aibu na mateso yanayotokea kwa kuvunja makubaliona ya ndoa ukilinganisha na raha unayoipata baada ya kutoka nje ni vitu viwili tofauti kama mbingu na dunia!"...........anachofanya ni usaliti wa ndoa?"Mmmmmmh utamu uliomo kwenye haya mambo,binadamu wengi huja kukumbuka hizi sentence wakiishavaa nguo.God bless us out of this*?*
Tangu uzaliwe uliwahi kusikia au kuona Mwanamke ameolewa na Waume wawili? je umewahi kuona Mwanaume mwenye mke zaidi ya mmoja? ukijijibu swali hili ndio utaelewa ni kwa nini Mwanaume akisaliti ndoa yake ni rahisi kusamehewa lakini si mwanamke. na naomba usinipe hadithi za kufikirika za mfumo dume.Samahani sana ninaomba niangalie upande wa pili jee wewe hujawahi kusaliti ndoa yako?[hata kama mkeo hajui lakini mungu ndiye shahidi] jee hypothetically angepata ushahidi kuwa ni kweli ulifanya usaliti angekubali kukusamehe?????
Hapa issue ni kusamehe na siyo suala jingine na kama unataka twende utakavyo jee unafahamu kwa nini kafanya hivyo??? unajuaje pengine wewe ndiye chanzo cha usaliti wake??? ndiyo maana nasema suala kubwa hapa ni kusamehe au kutosameheTangu uzaliwe uliwahi kusikia au kuona Mwanamke ameolewa na Waume wawili? je umewahi kuona Mwanaume mwenye mke zaidi ya mmoja? ukijijibu swali hili ndio utaelewa ni kwa nini Mwanaume akisaliti ndoa yake ni rahisi kusamehewa lakini si mwanamke. na naomba usinipe hadithi za kufikirika za mfumo dume.
Caa muhimu hapo atleast alitumia condom!!! binafsi nikigundua ndio mwisho wetu huo