Mke wangu kanitoroka kisa kubadili Dini

Mke wangu kanitoroka kisa kubadili Dini

Jamani kabla sijatoa maoni yangu nakujikuta nimetoa ushauri usiofaa.

Naomba kufahamu Dini ni kitu gani?, faida zake ni zipi? Ni upi utofauti wa Dini na imani, naje aliye naimani ni lazima awe na dini?
 
Mkuu katika maisha hamna silaha kubwa ya kujivunia kama ukweli! kama since day 1 ungemuambia ukweli huyo mwenza wako kwamba wewe ni Muslim na kama amekupenda kweli haya mambo yote unayo taka ushauri humu JF yasingekuwepo

Kweli nilifeli sana ila kibinadamu imetokea na sikuwahi jua kama itakuja nigharimu
 
NIMESIKIA SIKIA KUWA KUNA WATU WAMETUMWA KUZALISHA WANAWAKE WA DINI NYIGINE ILI KUONGEZA IDADI YAO. JE WEWE N MMOJAWAPO? KAMA KAGUNDUA IMEKULA KWAKO

Mkuu sijakuelewa nieleweshe vizuri
 
Mkuu kwanza nashukuru u-mzima kabisa maana dhambi kama yako (uongo) imeshawapoteza wengi. (Dada neema alimchoma ndani kamanda mwenzetu.)

Pili, kubali tu kulipa gharama ya dhambi yako na jaribu sana kutuliza akili na kufikiri ipaswavyo maana swala lako linahitaji uamuzi binafsi.

Tatu, mpe muda bidada, usikurupuke kwenda kubadilisha dini, kaeni kuyajadili na mpange mipango jinsi mtakavyo ishi kila mtu akiwa karidhika.
 
Umekosea kuzaa nje ya ndoa, na unataka ukosee zaidi kubadilisha imani.

Hakuna ndoa ya watu wenye imani tofauti/mmoja anaebadili kwa ajili ya ndoa. Kama kuna ulazima mwanamke anapaswa kukufuata mwamba.

Kwa vile ameondoka wekeni mkakati wa kulea mtoto wenu, kisha kila mmoja atafute mtu wa dini yake kwa ajili ya maisha ya ndoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe koma,tumia hiko kichwa vizuri kufikiri acha kufuata upepo na vijana mtakaopita hapa muisome post iliyo ktk link hapo chini muelewe kilichoandikwa humo dini haibadilishwi kwa sababu za kitoto toto eti mapenzi...ndo kitu gani hicho?


Mshkaji kamshauri ushauri mbaya sana, eti aukane uislamu aende ukristoni,, na asipojiangalia huyo kijana atapotezwa humu.
 
Habari wana jamii forums mimi ni Kijana eg yangu
29 nilianza mahusiano na mwana Dada eg 26
Tulianzisha mahusiano mwaka 2015 tukiwa Dsm

Tulifanikiwa kupata mtoto wa Kike mwaka huo huo

Lakini kwa kuwa nilikuwa nataka kumpata anikunalie nilimdanya jina na
Dini yangu ili akubali

na sikujua kama nitaishi naye miaka mingi
Nilimwambia naitwa Rich
ni mkiristo ivo ikawa rahisi kuwa naye pia

Lakini kadiri muda unavyokwenda alikuja jua ukweli na nilimwambia anisamehe maisha yakaendelea

Yeye alipendelea sana kwenda kanisani na hakutaka kuwa mbali na Maombi

Ilifika kipindi anataka nimuoe lakini alitaka nimuoe kupitia Dini yake dhehebu Anglican

Nilimzungusha sana ila nilikuwa nampenda sana hata yeye alinipenda sana
Sijawahi hata ona mwanaume akipita pita kwake

Miaka niliyoishi naye imetosha kumuamini lakini kilichokuja kuleta tofauti ni Dini tu

Kuna kipindi nilienda nae kanisani kwao kwa mchungaji wake nikaomba anipe muda wa kufikiria ili swala la kubariki ndoa nikapewa muda wa kufikiria

Lakini haikutosha nikaja kuongea na Mke nikamwambia naona ubadilishe wewe au tukafunge ndoa ya Kiserikali hakunijibu ila alionekana kukasirika sana

Mwisho wa siku nilikuwa ofisini yeye anafanya kazi sehemu nyingine kwa hiyo tunatofautiana kurudi

Nilikuta kachukua vitu vyake tu kaondoka nikamtafuta akaniambia unavyoona ndo ivo nimechoka ruhusu maisha mengine yaendelee

Kwa kweli nilichoka sana niliumia mno ukizingatia alinivumilia sana kwenye shida nyingi nilizopita nae ila now sipo nae

Nilimtumia mesej na nikaongea nae pia kuwa nipo tayari kufanya ivo na nikaenda kwa mchungaji nikamwambia maoni yangu

Lakini yeye anasema hata ukija church siwezi rudi kwako lakini kwa moyo wangu najua ana hasira sana na mimi

Na kwao niliwaambia kuhusu kuondoka kwake pia
wakasema wataongea naye lakini hawakurudisha majibu sahihi

Sasa ndugu zanguni msinicheke kwa Mapenzi yangu ila naomba mnishauri je anaweza rudi nikamuoa nikienda church kwao? au ndo kama alivosema hata nikienda church kwao harudiani na mimi nitafute msichana mwingine wa kumuoa?

Naombeni ushauri ndugu marafiki [emoji120]

Unaishinae, unazaanae, unataka bado umuowe na isitoshe ni kafiri na bado unaomba ushauli wa kwenda church kumuoa wakati wewe ni muisilamu!!!! Unashangaza sana kijana,,, mapenzi yamekutia upofu, sitoshangaa uka-ritadi kwa sababu ya uyo dada wa kikafiri.


ولا تقربوا الزنا انه كان فاحشة وساء سبيلا
 
Umekosea kuzaa nje ya ndoa, na unataka ukosee zaidi kubadilisha imani.

Hakuna ndoa ya watu wenye imani tofauti/mmoja anaebadili kwa ajili ya ndoa. Kama kuna ulazima mwanamke anapaswa kukufuata mwamba.

Kwa vile ameondoka wekeni mkakati wa kulea mtoto wenu, kisha kila mmoja atafute mtu wa dini yake kwa ajili ya maisha ya ndoa.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sawa Mkuu[emoji120]
 
eg 29 wewe, yeye eg 26 maana yake nini!?

Hivi nyinyi mmeshaona dini ndio maisha ee? Huo upumbavu wa kuwatenganisha sijui mimi wa dini fulani siwez kuoa au kuolewa na wa dini fulani mnautoa wapi!?.

Niwaombe wazazi wote, wafundisheni watoto wenu hasa wa kiume kuwa na maamuzi Thabiti.
 
Back
Top Bottom