Wazazi wako ni wazazi wako na hakuna wa kukutenga nao. Walikuelekeza jinsi ya kuishi hadi ukawa kijana morani na ukaja kuoa. Weka issue za familia yako mbali na issues za wazazi wako. Timiza wajibu wako nyumbani, na wajibu wako kwa wazazi.
Wa kulaumiwa ni wewe. Unashindwa jinsi ya kuwasiliana na wote. Hivi kuna siku ulishasema home 'jane yule receptionist, kaniambia friji za zec ndo nzuri kwa hiyo nitanunua' ? Kuwa muangalifu na taarifa unazopeleka kati yao. Namaanisha kuwa mwanaume. Jipange.
isije ikawa yeye, mwanaume, ndiye anayetakiwa kurudishwa kwao akafunzwe jinsi ya kuishi na mke.. ni ngumu ku-judge kutokana na jinsi alivyoileta sory yenyewe, haijakamilika.
isije kuwa ni yule mwanaume anayemwambia mkewe "mama kasema tusinunue gari tununue shamba, mama kasema mtoto asiende shule hii aende ile, mama kasema bla bla bla...". atueleze vizuri
Huyo mkeo inaonesha unamuendekeza sanaaaa...we miaka tisa yote unapandwa kichwani tu!!!
Rudisha kwa wazazi wake huko wakamfunze namna ya kuheshimu mume na wazaa chema asilete umajinuni...
Kwa hiyo mume akifanya hayo ndio mke anaruhusiwa kuwachukia wakwe zake???
Sidhani kama inafaa kutoa hukumu hiyo wewe Watu8 just kwa kusikia story from one side. Haya matatizo huwa magumu sana kuyatolea hukumu pasipo kujua chanzo cha tatizo. Kwa nini awachukie wazazi? Yaani from nowhere tu awachukie! There is a strong reason my dear.
sisemi kama awachukie wakweze. ila mwanaume ukiambiwa huwezi amua kwenye family yako, kila kitu unafanyiwa maamuzi na wazazi wako, hiyo ni serious issue na unatakiwa ujitazame mara mbili.
huyo jamaa naye alitakiwa atuambie kwa nini mkewe anadai anafanyiwa maamuzi na ndugu zake.
atueleze pia je anaishi na mkewe kwa wazazi wake au? maana mkiishi kwa wazazi wote wawili mnapoteza nafasi ya kuwa baba/ mama mwenye nyumba.
unaweza kuta mume anatokea makabila ya ombaomba haya,kiasi kwamba mke hayupo komfotabo kuona ndugu wwa mume wanamkamua ndugu yao huku familia yake ikiwa haipigi hatua.
Mimi ni muhanga wa tabia kama hiyo ya wanawake, wengi wao wala huwa hawana sababu yoyote ya msingi bali huwa wamejaa CHOYO, UBINAFSI n.k.
Na kumrudisha mke kwa wakwe akajifunze adabu hiyo wala sio hukumu bali ni utaratibu wa kimila za kibantu...unless uniambie hufahamu vizuri mila za Kitanzania.
Jamani wana JF naomba ushauri wenu,niko ndani ya ndoa zaidi ya miaka kumi tuna watoto 3,kinachofanya niombe ushauri ni kwamba baada ya kufunga ndoa ndani ya mwaka 1 familia yangu ilianza kuwa na migogoro isiyoisha,tatizo mke wangu hapendi ndugu zangu hasa wazazi wangu,imefikia ndugu wa pande zote mbili wazazi wa mke na wazazi wangu hawasalimiani,kisa anadai mie nafanyiwa maamuzi na wazazi wangu,imefikia mahala sasa hataki kuwasalimia hata wazazi wangu,nifanyeje?
Lazima yalianzia mbali na wewe kiunganishi cha hizi pande mbili ulizembea sehemu!
Wewe na mkeo wote ni watoto kwa wazazi wako na wake,hebu jishusheni na mjifunze kunyenyekea hata kama hamuwategemei kwa chochote. Ongea na mkeo asahau yaliyopita,kawaombeni radhi wazazi maisha yaendelee kila mmoja akiwa kwake,mkikutana msalimiane ikipita 2weeks na zaidi watoto pigeni simu kuwajulia hali basi.
Usikubali kuwa katika nafasi ya kuchagua kati ya wazazi na mkeo na watoto maana kila kundi lina nafasi yake kwako na hakuna kundi rahisi wewe kulitelekeza hapo.
Mwambie mkeo Sikio Halizidi Kichwa!