hilo tatizo litakuwa na history yake. mwanzo uliliona dogo, ukalilea mpaka lilipofika. lazima kuna sehemu walipishana (mkeo na nduguzo), na labda kwa kuwa wote hawakuwa na busara kila upande ulijiona una nafasi kwako wewe kuliko mwingine, ndugu wanategemea uwe upande wao na mke anataka uwe upande wake. na wewe kwa kuhofia kuwaudhi wote ukaamua kukaa kimya
ndugu ni zako, na mke ni wako pia. wewe ndiye ulitakiwa usome pande zote 2 na uwaelewe wanachogombania na kuwaweka sawa (bila kupendelea upande wowote). pale ambapo unaona ndugu wanakosea, usiogope kuwaambia ukweli. wakikwambia mkeo yupo hivi na vile, waambie yule ni mke wangu nitakwenda kumuweka sawa mwenyewe.
mkeo naye mpe facts zake. kaa ongea naye, mwambie hana sababu yoyote ya kushindana na ndugu maana yeye ndio ubavu wako. lakini na wewe play part yako kama mume/ baba wa familia.
mi kwanza nashangaa, ilikuwaje mpaka ndugu wa pande zote 2 mkawagombanisha na wao. kila mtu alikuwa anaenda kushtaki kwa wazazi wake? sometimes ni ukweli mgumu kuumeza kwamba ndugu/ wazazi nao wanakosaga busara.
kumuacha mke uliyekaa naye miaka zaidi ya 10 won't make life better. hao wanaokwambia uache mke ikifika jioni wao wanaingia chumbani na wake zao kulala, wewe utabaki unang'aa macho (sijui utamuita mama/ kaka/ dada mpige story wakati wa kulala). na hao wanaosema wanawake ni wengi utaoa mwingine, what if kama ndugu zako na wewe mna tatizo kweli, nayeye si yatamshinda? utaoa wa tatu
umeongea kweli, mimi ninaishi na ndugu za mume wangu hadi leo, na miaka yote nimekuwa nikiishi nao, wengine ni wazuri hawana shida wengine wakorofi kidogo ila tunaishi vizuri,.. sasa kuna mdogo wa mume wangu mmoja alikuwa mjeuri sijawahi ona, hana adabu hana heshima, kiburi mwanzo mwisho...nilishi nae kwa miaka kama 8 ivi kuanzia yupo sekondari hadi alipomaiza chuo akapanga na kuondoka kwenda kwake...sikumtilia kinyongo, nilimfanyia bonge la graduation, nikamnunulia mazawadi n.k hakuamini..
baada ya kukaa kwake alikopanga baadae sana akanitafuta kwa maongezi maalumu, akaniambia shemeji naomba msamaha, nilikufanyia mambo ya ajabu sana wakati ule nakaa kwako, sijui ni shetani au utoto..akaniambia dhamira yake inamsuta sana na ili awe na amani ameamua kuja kuniomba msamaha...nikamwambia mimi nilishakusamehe zamani,..na mpaka leo ni rafiki yangu wa karibu kuliko hata ndugu wengine wa mume wangu...
kwa hiyo inawezekana kabisa mke wa huyu kaka akawa hana damu ya kupendwa na wakwe, lakini yeye hatakiwi kuwaonyesha wazi kuwa kuna tofauti, awasalimie, awape vizawadi, zile hasira zitaisha tu..sio lazima wawe mabest lkn ule uelwano wa kawaida unatosha kabisa