Mke wangu bado anawasiliana na Ex wake

Mke wangu bado anawasiliana na Ex wake

MOYO WANGU UNAUNGUA, SINA RAHA TENA!

Nimeoa mwanamke ambaye nimeishi naye miaka mitano hadi sasa. Wakati tunaingia katika mahusiano nilimkuta tayari ana mtoto ambaye alizalishwa na mwanaume mwingine na akamkimbia.

Kwa kuwa nilimpenda sana naye akanipenda sikuona mtoto kama kikwazo katika mahusiano yetu. Niliendelea kumpenda yeye pamoja na mtoto wake na kuwatunza wote vizuri.

Maisha yetu yalikuwa ya furaha sana, lakini miaka miwili iliyopita niligundua kumbe bado anawasiliana na mwanaume ambaye alimzalisha akamkimbia.

Nilimkanya, akaniambia hakuna chochote zaidi ya kutaka kujua hali ya mwanaye. Siku moja wakati nachungulia simu yake niliona kuna ujumbe kutoka kwa huyo mzazi mwenzie ambaye anamsifia kuwa sasa hivi amekuwa mtamu na anajua kukatika mauno.

Moyo ulinienda kasi sana, kwa ujasiri niliamua kumuuliza ambapo alikubali kuwa ni kweli amefanya naye mapenzi ila nimsamehe hatarudia tena.

Kuanzia hapo, nimekuwa sina raha katika ndoa yangu, moyo wangu unaungua kwa sababu mara kadhaa naendelea kuona wakiwasiliana.

Naomba ushauri wako, nifanyeje? Nitasoma comment zote kwani nahitaji kuokoa moyo wangu

Au nikanyage tu maisha yaendelee?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mambo ya kuvumiliana kwenye ndoa ni mawili tu,
1. Mpolomoko wa uchumi
2. Maradhi
haya mengine wanaume wenzangu sijui mnayatoa wapi tu.
 
Kosa kubwa ulilofanya ni kuoa mke wa mtu mwingine, yes you got married to another man's wife. Ukweli ni kuwa ni wazazi(me na ke) wachache sana wenye watoto nje ya ndoa watakuwa sio wasaliti
 
Maoni yangu:
1. MUACHE HUYO KILAZA hajui wapi anapendwa wapi anachezewa yupo tu kustarehesha yoyote ubongo wake umesinzia.
2. Mtu malaya awe amezaa au hajazaa ila kuendelea na ma X zake au mabwana wapya haachi.
3. Usipanic, usione ulikosea wapo waliooa vigori ila yanawakuta zaidi ya haya just relax umia kwa muda utazoea utapata mwanamke anayejua kupendwa akajiheshimu.
4. Watakuambia uvumilie ila ndoa nikuvumiloa sasa jipime utavumilia kuchapiwa miaka 20 ijayo yote? Hakuna tabia mbaya kama mtu anayeweza kurejesha mapenzi kwa X akiwa nao 5 ataliwa/kula sana na kila atakayempa nafasi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baba umebeba gunia la mvi, wenzenu wakilalamika kuhusu masingle mother nyie ndio mnajikutaga mna maupendo yenu. Aya baba kazana kupenda. Maana hao hawatakaa waache lbda mtoto afe, ni uongee tu kiutuzima na mwanume mwenzio muelewane myamalize tofaut na hapo utaumia sana.
Au fanya maamuzi ya mtoto aende kwa baba ake na komaa mpk mtoto aondoke lasivyo aman isiwepo ndani. Upooo?!!!
 
mkuu hujui ufanyeje, wanaume tunapungua sana aiseee.....

Sasa nakupa ushauri huu.
Muite huyo EX wake muishi nae kwako muwe mnapokezana kulala na huyo mke wenu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]wew ni kiboko cha matatizo ya kipuuzi kama hayo.
 
MOYO WANGU UNAUNGUA, SINA RAHA TENA!

Nimeoa mwanamke ambaye nimeishi naye miaka mitano hadi sasa. Wakati tunaingia katika mahusiano nilimkuta tayari ana mtoto ambaye alizalishwa na mwanaume mwingine na akamkimbia.

Kwa kuwa nilimpenda sana naye akanipenda sikuona mtoto kama kikwazo katika mahusiano yetu. Niliendelea kumpenda yeye pamoja na mtoto wake na kuwatunza wote vizuri.

Maisha yetu yalikuwa ya furaha sana, lakini miaka miwili iliyopita niligundua kumbe bado anawasiliana na mwanaume ambaye alimzalisha akamkimbia.

Nilimkanya, akaniambia hakuna chochote zaidi ya kutaka kujua hali ya mwanaye. Siku moja wakati nachungulia simu yake niliona kuna ujumbe kutoka kwa huyo mzazi mwenzie ambaye anamsifia kuwa sasa hivi amekuwa mtamu na anajua kukatika mauno.

Moyo ulinienda kasi sana, kwa ujasiri niliamua kumuuliza ambapo alikubali kuwa ni kweli amefanya naye mapenzi ila nimsamehe hatarudia tena.

Kuanzia hapo, nimekuwa sina raha katika ndoa yangu, moyo wangu unaungua kwa sababu mara kadhaa naendelea kuona wakiwasiliana.

Naomba ushauri wako, nifanyeje? Nitasoma comment zote kwani nahitaji kuokoa moyo wangu

Au nikanyage tu maisha yaendelee?

Sent using Jamii Forums mobile app
Unavyo andika huu uzi bado uko naye??
 
Acha kuwa mpumbavu ndugu, mwache huyo mwanamke akaendelee maisha yake na mwanaye pamoja na mzazi mwenza. Kadri unavyomuona kila siku itakuletea shida na kuna siku utafanya jambo ambalo utajutia maisha yako yote kutokana na kujeruhiwa moyo wako.
Wanawake huwa hawana upendo kama tulivyo sisi wanaume yaani huwa mwanaume humpenda mwanamke kama mtu alivyo labda kwa muonekano wake au ukarimu wake, kwa mwanamke ni tofauti kabisa wao hupenda kifursa zaidi yaani nani anaweza kumtatulia shida zake kwa wakati husika.
Mwanamke akipoteza heshima kwako mruhusu aondoke nyumbani kwako achana na ujinga sijui nampenda sana sijui hakuna kama huyu sijui nimezaa nae watoto kumi sijui nini kwa sababu ukiendelea kukaa na mwanamke asiye na utii kwako kuna siku atakugeuza kuwa mtu katili sana, wapo wengi sana hawa usijifunge kwenye kifungo cha kifikra.
 
MOYO WANGU UNAUNGUA, SINA RAHA TENA!

Nimeoa mwanamke ambaye nimeishi naye miaka mitano hadi sasa. Wakati tunaingia katika mahusiano nilimkuta tayari ana mtoto ambaye alizalishwa na mwanaume mwingine na akamkimbia.

Kwa kuwa nilimpenda sana naye akanipenda sikuona mtoto kama kikwazo katika mahusiano yetu. Niliendelea kumpenda yeye pamoja na mtoto wake na kuwatunza wote vizuri.

Maisha yetu yalikuwa ya furaha sana, lakini miaka miwili iliyopita niligundua kumbe bado anawasiliana na mwanaume ambaye alimzalisha akamkimbia.

Nilimkanya, akaniambia hakuna chochote zaidi ya kutaka kujua hali ya mwanaye. Siku moja wakati nachungulia simu yake niliona kuna ujumbe kutoka kwa huyo mzazi mwenzie ambaye anamsifia kuwa sasa hivi amekuwa mtamu na anajua kukatika mauno.

Moyo ulinienda kasi sana, kwa ujasiri niliamua kumuuliza ambapo alikubali kuwa ni kweli amefanya naye mapenzi ila nimsamehe hatarudia tena.

Kuanzia hapo, nimekuwa sina raha katika ndoa yangu, moyo wangu unaungua kwa sababu mara kadhaa naendelea kuona wakiwasiliana.

Naomba ushauri wako, nifanyeje? Nitasoma comment zote kwani nahitaji kuokoa moyo wangu

Au nikanyage tu maisha yaendelee?

Sent using Jamii Forums mobile app
Swali; je alitumia protection alivyolala na huyo ex?
Na je tangu umemsamehe, kuna mabadiliko yoyote amefanya kuonyesha kweli msamaha alioomba anauthamini?

Kama matendo yake bado yanaashiria kutojali hisia zako, na pia kama alilala na jamaa bila mpira, dude hapo huna mke. Pengine umpe mda ajitathmini kwanza. Inaezekana bado anampenda jamaa na hili litakua tatizo kubwa kwako. Pia ogopa magonjwa.
 
Huwa tunasema, any man who decides to wife-up a single-mother deserves all the consequences that come with such a stupid decision. Childbirth is the closest a woman gets to seeing death with her own two eyes. You CANNOT erase the stamp that a man who impregnates a woman for the first time leaves in her life. YOU CANNOT!
Men should get this idea of love out of their heads, I think the pursuit of this dream (being loved) is what most men who marry single-mothers chase. Even a young and virgin 20-year old can never love you. What women love is your ability to provide for them, not you. Single-mothers know how to con men who chase love, they're experts in this.
Men should stop chasing love and the idea of being loved. If they stop doing this, then hii story ya kuoa single-mothers itaisha.
 
Back
Top Bottom