Mke wangu anatuma post za kunisimanga Facebook

Mke wangu anatuma post za kunisimanga Facebook

Daka mchepuko and huyo wife mchane suspension ya miez 3 ajirekebishe kwanza
 
Very sad,amekuwa akiweka ujumbe wa ajabu ajabu kwenye wall yake ya Facebook, na sasa hii ndio profile picture yake.
Hii amenza kufanya kama miezi miwili na nusu nyuma, na mbaya zaidi ni kwamba yeye ni mlokole na amehama Kanisa letu lilotulea na kuhamia kwenye makanisa ya miujiza.

Yeye yuko very demanding, ukimwambia mshahara hautoshi, kwake ni maneno, nimejaribu kufungua biashara na yeye ndiyo msimamizi mkuu.Bado faida haionekani licha ya kuwa sichukui chochote toka kwenye biashara hizo.

Analalamila kisa eti kila mwezi namtumia mama kijijini laki 3, what is laki tatu by the way ni sawa na elfu kumi kwa siku.
ukimuelewesha haelewi, anataka mama yake nimtumie laki tano,mpaka sasa nahisi amegeuka kero na mzigo.

Sina mengi, ila namshukuru Mungu kwa yote.

10927928_359236227594237_347315041_n.jpg


Mnafanana na wewe umeleta umbea huku!
 
mnh! haya bhana... manake hizi nyumba hizi, zinaficha mengi ile mbaya sasa inapofikia kuanikwa hadi hadharani...
 
Vurugu zote za nini au umeambia ukimuacha utakufa? Au ndio mfunga pingu za maisha?
 
umeongelea upande mmoja tuu hapa.....kipato chako ni kiasi gani? isije kuwa pesa yote unatuma kwa mamako alafu unamtesa mke. hizo post zake fb inaweza kuwa matokeo ya stress unazompa
 
tatizo ni laki 3 tu unazotuma kwa mama au kuna kingine?
wakati mwingine ni muhimu sana ujue aina ya mwanamke uliyenaye, mwanamke wa hivyo hafai hata kujua jumla ya kipato chako, muhimu kwake ni huduma, matumizi na mapenzi tu, siyo kila kitu unamfungukia, ATAKUSUBUA!
 
umeongelea upande mmoja tuu hapa.....kipato chako ni kiasi gani? isije kuwa pesa yote unatuma kwa mamako alafu unamtesa mke. hizo post zake fb inaweza kuwa matokeo ya stress unazompa

Amesema hiyo laki3 ni sawa na elfu10 TU kwa siku, kwa maana kuwa ni insignificant ukilinganisha na kipato chake. Mke kapewa na biashara na hahojiwi matumizi bado anatolea jicho elfu kumi anayopata mama mkwe! anataka jamaa atume ukweni mara mbili ya anachotuma kwao....kazi ipo!
 
Amesema hiyo laki3 ni sawa na elfu10 TU kwa siku, kwa maana kuwa ni insignificant ukilinganisha na kipato chake. Mke kapewa na biashara na hahojiwi matumizi bado anatolea jicho elfu kumi anayopata mama mkwe! anataka jamaa atume ukweni mara mbili ya anachotuma kwao....kazi ipo!

ndoa za kimaslahi hizo
 
Ushauri mwingine bhana ni kama tusi,

aliyekuambia mtoa mada alikuwa mwanamke ni nani?

huelewi nini hapo?
mwanamume ina weza kutumika kama Nomino na wakati mwingine kama Kivumishi cha sifa,
ametumia kama kivumishi, Nini huelewi hapo? watu wengine bhana...
 
hatuko interested kujua mama yako umamtumia kiasi gani, mbona husemi huyo mkeo umemfungulia biashara ya mtaji wa sh. ngapi?
 
Uyo anasunbuliwa na roho mbaya tuuu...zinamuuma ela unazotuma Kwa mama yako....sasa acha kabisaa kuwapa kwao eka afu ukiwaunatuma ela kwenu usimshirikishe tima kimya kimya....kuwa makini akikutana na wadada Wa mjin wakamfundisha uchawi umekwisha Kwa libwata...utatuma mshahara wote kwao maana ndo anachokitaka....wanawake wachoyo sana sasa kwan ulimuoa hili uhudumie familia yao? Eti laki tano wamekusomesha wao...anataka kukupanda kichwani uyo
 
Mke Facebook! Hawezi kuongea na wewe? Facebook ndio atapata majibu? Sitaki kusikia ulokole kabisa, nakumbuka mama yangu aliingia huko ilikuwa kazi kumtoa. Alikuwa kama nusu Mwehu, yesu hivi, yesu vile! Hata Ndugu zake alikuwa hawataki kuwaona ni Aidha wakimtembelea ni wachawi au washirikina na sisi watoto na baba yetu ni rc hataki kusikia! Kiguu na njia kanisani tangu asubuhi mpaka jioni, wao ndio wasafi kiroho na wanaojua kumwabudu Mungu kwa roho na kweli ila pole sana ndugu.
 
Very sad,amekuwa akiweka ujumbe wa ajabu ajabu kwenye wall yake ya Facebook, na sasa hii ndio profile picture yake.
Hii amenza kufanya kama miezi miwili na nusu nyuma, na mbaya zaidi ni kwamba yeye ni mlokole na amehama Kanisa letu lilotulea na kuhamia kwenye makanisa ya miujiza.

Yeye yuko very demanding, ukimwambia mshahara hautoshi, kwake ni maneno, nimejaribu kufungua biashara na yeye ndiyo msimamizi mkuu.Bado faida haionekani licha ya kuwa sichukui chochote toka kwenye biashara hizo.

Analalamila kisa eti kila mwezi namtumia mama kijijini laki 3, what is laki tatu by the way ni sawa na elfu kumi kwa siku.
ukimuelewesha haelewi, anataka mama yake nimtumie laki tano,mpaka sasa nahisi amegeuka kero na mzigo.

Sina mengi, ila namshukuru Mungu kwa yote.

10927928_359236227594237_347315041_n.jpg

Hiyo ni shida kubwa na inabidi suala hili ulipeleka kwa third party maana inaelekea aidha hamna mawasilano mazuri au nyote mnazungumza lugha tofauti na hakuna anayemuelewa mwenzake.
Na hiyo ikishindikana basi you have to make a hard decision on this kwa sababu sidhani kama nyinyi mnaenda safari moja
 
Mmmh laki tatu kwa mwezi?? Kijijini!!?

TZS Milioni 3.6 kwa mwaka, huyo mama wa kijijini ni tajiri sana, na sijui ana mudu vipi kuimaliza hiyo hela kila mwezi, mi naona wife wa jamaa yuko sahihi, kwa kuwa ukokotoaji wa mgawanyo wa keki kwa wazazi haujakaa sawa.
 
Back
Top Bottom