Mke wangu ananiumiza kichwa

Mke wangu ananiumiza kichwa

Kirahisi hivyo! He! Kwetu wana methali inasema "Akushabilila katafile tomanya nka akelekela" literal translation: Mtu anayetembea na mke/mme wako kama bado yuko hai huwezi jiaminisha ameacha! Msamehe, ameacha au jifanye hakuna jambo kama hilo? Anyway ni vizuri kuvumilia lakini inahitaji moyo! Ushauri wako ni mzuri anyway
iwe kumbe olyo'womuka?? mpola wamawe'!!!
 
Yaaaaah Unaenda kugongewa tu Huko chuoni kama Akienda Wake za Watu chuoni Warahisi sanaaaa labda km ameshazeeka Watu hawana time naye ila km bado damu inachemka Jua unaenda kugawa na atakuletea na wewe km Movie ya Adam na Hawa.... Wambulu ni Wagawaji AKA si Wachoyooo
 
Pole ndugu, ila nliwahi shauriwa kuwa kama huna kifua kaa mbali na simu ya mwenza wako, mi nakuomba fanya yafuatayo, toka naye out siku moja jua wewe na yeye, ikiwezekana hata chukua weekend moja hotelini, wakati mnainjoi embu jaribu kupeleleza kama kuna kitu ana miss kwako, nini anatamani uongeze katika mapenzi yenu, kama vipo hivyo vitu then in a polite way jaribu kumuuliza kama ndo vinafanya anachat ujinga fb, kama havipo jaribu kumuuliza politely why anafanya anayoyafanya?

Ongea naye tatua in a polite way mpe another chance, niliwahi salitiwa na mpenzi wangu niliumwa hadi kulazwa, alikuja akitubu na msamaha analia hadi alizimia ila sikuwa tayari, baadae nilijiuliza hivi ningekuwa ni mimi nimefanya hilo kosa si ningetaka kusamehewa? I believe ingehappen kwako ungetaka na wewe kusamehewa na mwenzako akupe fursa ya kujieleza why ulianguka, kama yeye amechangia au lah, na upewe a chance to make things fresh.

Victor j (MC mtumishi)
Inspirational and motivational speaker/master of ceremony
Am not so far from what you had said, women need special attention katika kuuliza kile alichokikosea na ni wepesi Sana kujutia and so on.
 
tumblr_o2macjGBaB1uvwvnho1_500.gif
 
Pole sana mkuu.... hawa watani wetu wa jadi hawatabiriki hata kidogo. tena pale utapomuonesha kuwa unamuamini anatumia mwanya huo kufanya yake...mwanamke isimwambie nakuamin hata kama unamtania atakuliza.......Mwanamke kumuamin ni sawa na kumpa ramani ya vita unapigana nae.....
 
Halafu cha ajabu kajamaa ambako kanampa jeuri Facebook nimeview account yake ni kasanii ka muziki underground hakajatoka...yaani vivulana vya kipuuzi puuzi kabisa roho inaniuma kupita maelezo
Pole saaana mkuu,jaribu kutafuta chanzo,usisahau wewe na mkeo ndio wenye uwezo wa kujenga au kubomoa ndoa yenu;bado una nafasi ya kurejesha heshima ya ndoa yako

Pia mara nyingi kukaa mbali na mkeo ni hatari saana kaka,jitahidi kutengengeneza mazingira ya kuwa karibu na mkeo atapunguza kutafuta faraja nje ya ndoa
 
Pole ya kawaida hayo, ongea nae delete hiyo account Facebook, jipe muda maumivu yapungue msamehe maisha yaendelee.....
Siungi mkono ushauri wako kaka. Huyo mwanamke si wa kumsamehe la sivyo yatamkuta ya sajenti kinyogori
 
Wanaposema "hakuna ndoa isiyo na matatizo" wanamaanisha mambo kama hayo. pia ulikula kiapo " kwa shida kwa raha" hiyo ndiyo shida uliyoapa kuila.
Ukioa/olewa halafu ukalalamikia matatizo ya ndoa ni upumbavu, kwani uliingia ndoani ukijua hakuna ndoa isiyo na shida. Hasara za ndoa ni nyingi kuliko faida.
 
Du hiyo ni FB tu bado huko QT na hiko diploma alipopita! Huko Degree bado bado kitaa, oh nimesahau humu JF
 
Du hiyo ni FB tu bado huko QT na hiko diploma alipopita! Huko Degree bado bado kitaa, oh nimesahau humu JF
 
Habari za jumatano wanajamvi, bila shaka mmeamka salama kabisa.

Leo nimekuja huku kuomba ushauri maana tangu usiku sijalala kichwa kinawaka moto.Nimeoa miaka minne ilitopita, kabla ya hapo niliambiwa kabila la Mbulu sio la kuoa mie moyo ukawa umenasa hivyo na pete kanisani ikavaliwa. Nimebarikiwa mtoto mmoja wa kike.

Mwaka 2011 nilimfungulia account facebook mchumba kabla sijamuoa na nilikuwa namuamini sana.Tatizo Jana (Jumanne nikiwa kazini akaniambia account yake imesumbua halafu njia ndio mie hivyo nikiwa kazini nikalog in kwenye account yake (ikumbukwe tangu nimuunge sijawahi ingia kwenye inbox wala kugusa simu yake) baada ya kumrekebishia tatizo lake nikaona niingie inbox kwa mara ya kwanza.

Ukweli mie sinywi pombe lakini Jana nilijikuta naondoka kazini mapema na kwenda kuzimua kichwa. Nimekuta message nyingi anachat na vijana za ajabu ajabu mara mume wangu nitamuaga naenda kwa ndugu nitakuja kwako, mara mume wangu hayupo halafu nipo kitandani peke yangu baridi kali, Mara nimetoka kuoga ndio najifuta now, halafu anagawa namba yake ya simu kirahisi kwa kila anayemuomba namba. Yaani nusura nianguke ofisini maana mpaka wenzangu wamejua kuna tatizo ila sijafungua mdomo wangu.

Nimerudi nimemkuta ananichekea yani sijaongea kitu roho inaniuma vibaya, nahangaika kutoa jasho kwaajili ya kumpendezesha na mtoto wetu ila kaniona boya. Wakati naanza uhusiano nae nilikuta akiwa na elimu ya darasa la saba tu, nikamuendeleza QT na kumfundisha mpaka now ana diploma na October anaingia degree, sijui hata nifanye nini haki ya Mungu inanitesa sana.
Pole kwa kupitia masumbuko makubwa ya kuumizwa na mwenzi wako!
Kweli kuna sehemu anakosea Ila inabidi uelewe tu kuwa social media zina ushawishi wake pia! Ulikuwa umemfungulia mwenyewe account FB ambapo ulitaka asocialize na watu! Kwa kweli kwa watu wenye umri mdogo hupelekwa sana na hisia na. Hilo ni jambo la kawaida!
Lakini vipi kama yeye pia angeweza kuingia inbox ktk simu yako, FB, WhatsApp, Instagram Twitter etc, je asingekutana na ujumbe hata mmoja wa kumsononesha! Hizi tevhnolojia kuna time zinaleta utundu wa kujitongozesha au kutongoza bila hata ya sababu! Just cool down, ni vema ukaanza kuelewa tu kuwa mwenzi wako inawezekana ameanza uhusiano nje ya ndoa Ila tumia busara kunusuru familia yako!
Unaweza kuvumilia na kumwambia ulichokiona, pia kudemand asiendelee na uhusiano na mwingine wowote (ingawa ngumu)! Just try ukiwa na faith na ukipresent hoja bila mihemko ya ghadhabu unaweza kumfanya akuelewe!
 
Pole ya kawaida hayo, ongea nae delete hiyo account Facebook, jipe muda maumivu yapungue msamehe maisha yaendelee.....
Hiyo ni Tabia yake halisi na jamaa ana bahati kuijua, hata kama akimfutia Hiyo facebook hawezi kamwe kumfutia hiyo tabia,
 
Halafu cha ajabu kajamaa ambako kanampa jeuri Facebook nimeview account yake ni kasanii ka muziki underground hakajatoka...yaani vivulana vya kipuuzi puuzi kabisa roho inaniuma kupita maelezo
Blaza usipanic sana mkeo .....itakuwa anajifurahisha tu na hajawahi wala hana mp ango wa kufanya lolote baya.... just a chatting
 
Back
Top Bottom