Ni kama stori ya kutunga iviii.. ila ni kwamba, ulimuoa akiwa bado mdogo na hakuwa amefanya chaguo sahihi. Ila shida zake ndo zikapelekea kukubali kuolewa mapema akijua anapunguza ugumu wa maisha na alichachungulia fursa. Ni hivi, bado ataendelea kukucheat ikiwa atapata upenyo. Na cku akipata chaguo sahihi lake atasepa huku unaugulia maumivu ya moyo na majuto. Tuliza akili nenda nae taratibu, ikiwezekana mpe ufree ili umsome vzr. Maana ukimbana utajiumiza we mwenyewe. Mpe uhuru afanye mambo yake ili palipo na ubovu upajue mapema na uchukue hatua mapema. Ukijitia kumbana sana utapoteza muda wako, utapoteza pesa, na hutakuwa na amani ya moyo maana muda wote kiroho juu kutaka kujua nn kafanya tena. Siku zote ukweli utakufwata nyuma