mke wangu alitaka nichoma kisu

mke wangu alitaka nichoma kisu

mahango... Nafikiri ili upate ushauri mzuri, ingekuwa poa ukawa muwazi with what is
happening with ya marriage.

Nafikiri kuna tatizo kubwa sio hyo mikwaruzano midogo midogo unayosema. Inaweza kuwa ni usaliti au tatizo lingine linaloumiza sana nafsi kiasi cha kufanya mtu awe na hasira na asiwaze nini kitatokea out ya hasira zake.

Sidhani kama huyo mke wako ni mjinga kiasi hicho akutishie kisu without reason, akufate tu ulikosafiri kikazi tena aje na silaha mkononi without reason????

Whatch your ways gentleman.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Kumbe bado kuna watu wavulimu kiasi hicho....Unasubiri mpaka akuchinje? Alishakwambia atakuua na sasa amekukosakosa na kisu. Brother, huyo ndiye anayekupikia, akiku Mwakyembe je? Kama hujatudanganya mimi nakushauri rudisha kwao mara moja kwa muda wa miezi 6 hivi na uwaeleze wazazi wake ni kwanini umechukua uamuzi huo

Itakuwaje kama wazazi wake wapo behind this....wanajua kila kitu na ndiyo washauri wakubwa....inawezekana dada amechukua hatua kubwa zaidi lkn they know....
 
Tafuta bastola ndugu, mwambie kuwa akifanya tena utakrushia bullet, atatulia!
 
Mwanamke anayeishi kwa tetesi si mzuri kabisa kwani ktk ndoa wako watu wakiona mnapendana huwa huanzisha maneno ya uchonganishi na hata wapo watu watakao dai unawataka ikiwa hata huwajui.La muhimu ni mke kuwa na busara ktk mambo kama hayo!Sasa yeye akisikia umefungulia mwanamke duka anaushahidi?Na je wewe kwako hakuna maendeleo au uwa hujali familia?Inabidi umwambie akupeleke ktk hilo duka ulilofungua ili athibitishe na kama akikataa mwambie akutajie aliyempa hizo taarifa!Na jaribu kuangalia marafiki wa pande zote yaani wa kwake na wko kwani wengine huwa si wema na hawafurahii kuona mna amani.Hiyo sio kwako tu ni kwa watu wengi inatokea.
 
Mimi nafikili jamaa ndio mwenye matatizo si mkewe, hapa hatuelezi kila kitu - na wala sioni kama huyo mwanamke ana nia thabiti ya kuua, anatishia tu baada ya kuchoshwa na nyenedo za jamaa.

Mkuu kumbuka wanawake wana inbuilt instinct za ajabu sana, sio za maternal peke yake wanaweza vile vile kuhisi by 99.5% kama mwanamume ana mahusiano nje ya ndoa - Sasa ku-act/react kunategemea hulka ya mwanamke zilivyo, kuna wanao weza kuhisi wakakaa kimya au kupeleleza pole pole wakisha pata uhakika na wao wanalipiza kisasi kwa kuanzisha mahusiano nje ya ndoa bila ya kujali wajihi/sura/class na anaye tembea naye - yeye anachotafuta ni kulipiza kisasi basi!!! Sasa wengine kama huyu dada hawafanyi hivyo, wanastick kwenye ndoa zao bila ya kuteteleka, lakini wakihisi wanasalitiwa na waume zao wana-react kwa hisia kali sana, oh yes wakati mwingine wanaweza kuua bila ya kukusudia.
 
Ndoa ina miaka sita anakuchomolea bisu je ikifika miaka ishirini itakuwaje, fikiria chukua hatua.
 
Si ujiweke pembeni uepushe msongamano, yaani unakufa unajiona hivihivi, kisa? Mke akhaa!
 
Kutishia na kujaribu kuua hai-justify kwamba alikuwa na hasira zilizopitiliza, huyo anaonekana ana wivu kupita kiasi na ndio maana ana wasiwasi na ndoa yake kuingiliwa. huyu hafai kuitwa mke.
Dada Zinduna yangu story nzima mm naipinga kwani hawa walikuwa wanaishi Mkoa mwingine jamaa aliposafiri Mke akamfuata na Guest anayofikia anaijua akaingi-amo.
LIGWARIDE na HONEYMOON kila mtu wa Ndoa anajua hizo mechi za viwanja vya nje huwa zinawapatanisha wagombanao na kuirudisha NDOA
Mtoa Mada ni Lodge ya wapi watu wanapigana kwa visu hadi Damu bila ya kuwaamulia?
Ni Lodge ya Kijiji gani inaruhusu kupigana ndani ya vyumba bila kuwapeleka POLISI
Ni Mwana-ume kweli unafungiwa ndani na kudundwa na bado mkarejea wote kwenu bila Revenge au Mshataka kwa Washenga hadi kuja kushtaki humu JF
 
Last edited by a moderator:
Kaka tatizo la hapo mlipofikia mnalijua nyie wawili hta mkienda kusuluhisha mtapoteza mda kaa chini na mwenzi wako muyazungumze yaishe
 
mwanamke -------- uvunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe,be careful atakuua uyo ckumoja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom