Sasa hapo ndo tujiulize, ilikuwaje 'kiama' kikatangazwa na mhusika asichukulie serious...alijua makosa yake
Baada ya kuona mtuhumiwa haelewi somo, ilibidi bimkubwa aje amuonyeshe kuwa alikuwa serious..nadhani mume hakuzingatia terms za kwenye namba moja
Nadhani mtuhumiwa hakujua namna ya kupooza hali ya hewa, na ukute ndio alizidi kuichafua
Bado nakataa kama ni mpango mahsusi, kwa sababu hata thread inavyojieleza inaonekana ni hasira za bibie tu
Mkuu hebu msome huyu jamaa kwa makini hapa chini.....
wadau naomba mawazo yenu kwa hili jambo nifanyeje mimi na mke wangu kwenye ndoa yetu tuna miaka sita na tumejaaliwa kupata mtoto mmoja wa kiume,kama ujuavyo mambo ya ndoa hamuwezi kuishi kama malaika ugomvi hutokea.ila kwa bahati mbaya siku moja kama miaka miwili tumewahi kugombana kidogo ila mke wangu alinitamkia kwamba siku moja ataniua kwa kisu au kwa sumu,
wiki mbili zilizopita nilikuwa nimekuja mkoa mwingine kikazi ila alikuja ghafla usiku saa tano akakuta nimelala tukalala mpaka asubuhi,
asubuhi akanambia kwamba anataalifa kwamba nina mahusiano na mwanamke mmoja na nimemfungulia duka,nikamkatalia kwamba jambo hili halina ukweli kabisa
tulibishana kwa mda wa masaa sita tukiwa chumbani lodge wakati huo alikuwa kafunga mlango wa chumba na funguo kaficha,baada ya mimi kuendelea kukataa ghafla alichomoa kisu alichomeka kwenye suluali na kutaka kunichoma ikabidi tuendelee kupokonyana kile kisu bahati mbaya kikanikata mkononi naomba ushauri madau nifanyeje?
Ukisoma kwa makini utatambua kuwa huyu mwanamke ana matatizo.
1. Wana miaka sita ya ndoa, mara ya mwisho kugombana imeshapita miaka miwili!!
2. Anamtuhumu jamaa ana mwanamke mwingine na kamfungulia duka (ANAMTUHUMU KWA KUWA HANA UHAKIKA... Hajathibitisha pasopo shaka)
3.Amefanya ziara ya ghafla akitegemea angemkuta mmewe ana kimada ndani, ili labda awaue wote lakini kamkuta mmewe yuko peke yake na wakalala mpaka asubuhi
4. Kafunga mlango na funguo kaficha ili jamaa asipate mwanya wa kutoroka..... Oh Gosh!
5. Kachomoa bisu mfukoni tayari kumshindilia mmewe....
Hata kama ni hasira za namna gani, kwa mtiririko wa matukio haya, isingempasa kufikia hatua ya kutaka kumuua mmewe.
Ndio maana namtahadharisha jamaa, akae mbali na huyu kichaa. Atajamuua kweli si masihara!