Mke wa Rais naye kawa Kiongozi !????

unakumbuka na Regina Lowasa nae alivyokuwa anafunika? sasa hivi chali... maskini sijui mama wa watu kapotelea wapi. kumbuka msemo wa mbowe.."nyuma ya mwanaume fisadi.........."
Ehh, mwenzenu sielewi kitu labda sababu sipo Dar es Salaam. Haya mambo ya kukaa sana Sikonge yana madhara yake unapitwa na wakati. Sasa Mbowe alisema kukaa nyuma ya Fisadi ndiyo itakuwaje tena? HAlafu mnasema anasubiri kwenda LEBA sasa ina maana anategemea kujifungua? Si wengine wanaandika kuwa mapenzi yamefifia? Au ina maana historia inajirudia tuje tusikie kuwa Muungwana nayeye kapata Mramba wake? Pia hii ya mpwaye Rostam Azziz ni kuwa Muungwana Kaowa au kimada tu?
Mie najua kuwa Mama wa Kwanza ni mke wa kwanza tu. Ndiyo maana Monica Lewinski hatambuliki rasmi kama Bi Clinton. Mie nilisoma kuwa Kikwete anaikacha ndege yake na Mkewe anatesa nayo. Hivi hii ikoje? Tanzania nchi yangu kweli poa sana. Ni nchi kama nchi nyingine zilizo kwenye mwelekeo wa kuendelea ila zinasubiri MUSA wake aje azitoe Misri na kuzipeleka kwenda KULIPULIWA NA MABOMU na kuangukia na Rocket za Waarabu.
 
enhe ... my dear tell me! ... didnt know that she was in that state ... she is really over running the engine ... mkunga hapa atusaidie to advise her ...

wanira raha naimaomari.
Yaani we acha tu.mwaka huu watakukoma.
 
unakumbuka na Regina Lowasa nae alivyokuwa anafunika? sasa hivi chali... maskini sijui mama wa watu kapotelea wapi. kumbuka msemo wa mbowe.."nyuma ya mwanaume fisadi.........."

LOL!!!...Kuna mwanamke fisadi!!!!...:)
 
Naichukulia hii issue ni kama ABUSE ya kodi za wananchi.

Nafikiri huu ni wakati muafaka zaidi kuanza kumwandama na maswali magumu dizaini ya aliyoulizwa Chelsea Clinton wakati akimpigia kampeni mamaye. This will be a good lesson kwa watu wanaokimbilia mambo yasiyowahusu.
 
Urais Wa Kikwete Una Ubia Na Mke Wake ,na Hivyo Rais Alitudanganya Aliposema Kuwa Hana Ubia Na Mtu.

Huyu Mama Lazima Atulie Na Akae Chini Kwani Hana Mamlaka Ya Kufanya Hicho Anachofanya Huyu.

Mke Wa Rais Ni Chumbani Na Njiani Akiwa Na Mumewe Na Sio Vinginevyo.
 
Tunajiuliza na kushangaa kuona kwamba mke wa Rais sasa naye anafanya ziara nchi nzima bila mumewe.

Katiba yetu haimtambui mke wa Rais kama ilivyo kwa US. Inakuwaje huyu mama sasa anahangaika kuliko Makamu wa Rais? Anaweza akasikika kama atakuwa akiandamana na mumewe.

JK yabidi amu-kontroo mukewe bwana sisi hatukumchagua.

Mkuu,

Katiba ya US inamtambuaje mke wa rais na yetu haimtambui vipi? Unaweza kutoa vifungu vya reference?

Mimi nafikiri kama kuna mjadala uwe ni juu ya umuhimu wa safari na kama haingiliii kazi za kiutendaji ambazo zingetakiwa kuwa a strict domain ya watendaji wa serikali na siyo juu ya kwamba First Lady anasafiri mwenyewe.Kusema kuwa First Lady hawezi kusafiri mwenyewe kutakuwa ni hatua ya kwanza kuelekea kusema kwamba dada zetu hawatakiwi kutoka nje ya nyumba bila kusindikizwa na kaka, mume au ndugu wa kiume. First Lady anaweza kutumika vizuri sana katika "ceremonial duties" kama kufungua Zahanati na ku officiate mashindano ya uzuri.Siafiki First Lady kuwa na nafasi katika ushauri wa sera.

Sioni tatizo la First Lady kusafiri kivyake, anaweza kutumika vizuri kuhamasisha huduma za jamii wakati rais anafanya shughuli nyingine.Tatizo labda, kama lipo, MOJA ni gharama na umuhimu wa safari kutowiana katika "cost benefit analysis" na la pili ni kuingilia sana katika kazi za kisera za watendaji wa serikali.

Siyo kwa sababu Kikwete tu au CCM tu basi kila kitu tuwe tunaponda bila msingi.
 
Nilishasema nikapigwa vita hapo nyuma. Mke wa raisi kuchukuwa ndege na kwenda South Africa kushuhudia sherehe za mfalme anayeoa mke kila mwaka ni aibu na inaonyesha uswahili wa hali ya juu. Mama ni mwalimu lakini kashajiingiza kwenye siasa za mikoa badala ya ku focus kwenye shughuli za Afya na Elimu. Wakati wa Mkapa tuliambiwa hivihivi kwamba mahusiano ya kimapenzi hayapo na sasa ni yale yale. Haja mambo ya mapenzi hayatuhusu lakini Mke wa raisi anatakiwa kutulia Ikulu na kufanya shughuli za muhimu na si kujionyesha na mfungo tofauti ya vitenge kila siku. Vilevile kunatakiwa kuwe na vazi maalumu la Kitaifa kwa first lady, Mama kijana lakini anavaa kama mama wa miaka 60.
 
.......Mke Wa Rais Ni Chumbani Na Njiani Akiwa Na Mumewe Na Sio Vinginevyo.

Wacheni machismo dunia ya sasa wote ni sawa....na kama anafanya vitu vya maendeleo basi ni kheri lakini mtindo wa kutusimamisha barabarani yeye apite NOOOOOOOOO
 
Mkuu,

Katiba ya US inamtambuaje mke wa rais na wetu haimtambui vipi? Unaweza kutoa vifungu vya reference?

Mimi nafikiri kama kuna mjadala uwe ni juu ya umuhimu wa safari na kama haingiliii kazi za kiutendaji ambazo zingetakiwa kuwa a strict domain ya watendaji wa serikali na siyo juu ya kwamba First Lady anasafiri mwenyewe.Kusema kuwa First Lady hawezi kusafiri mwenyewe kutakuwa ni hatua ya kwanza kuelekea kusema kwamba dada zetu hawatakiwi kutoka nje ya nyumba bila kusindikizwa na kaka, mume au ndugu wa kiume. First Lady anaweza kutumika vizuri sana katika "ceremonial duties" kama kufungua Zahanati na ku officiate mashindano ya uzuri.Siafiki First Lady kuwa na nafasi katika ushauri wa sera.

Sioni tatizo la First Lady kusafiri kivyake, anaweza kutumika vizuri kuhamasisha huduma za jamii wakati rais anafanya shughuli nyingine.tatizo labda, kama lipo, ni gharama na umuhimu wa safari kutowiana katika "cost benefit analysis"

Siyo kwa sababu Kikwete tu au CCM tu basi kila kitu tuwe tunaponda bila msingi.

hatuongeleai mambo ya haki za wanawake sijui haki sawa hapa...wat pipo ongelea ni kuwa hw come she is even using ndege ya raisi kwenda kwenye misafara sehemu mbali mbali kwa kutumia kodi za wananchi....she is moving here and there kwa kutumia vingora msafara mreeefu wenye mashushu kibaoo wanaolipwa kwa jasho letu while she aint even the first lady she is jus among the first ladies Tanzania has got!!!!
even if she is among them,but its too much!!
 
hatuongeleai mambo ya haki za wanawake sijui haki sawa hapa...wat pipo ongelea ni kuwa hw come she is even using ndege ya raisi kwenda kwenye misafara sehemu mbali mbali kwa kutumia kodi za wananchi....she is moving here and there kwa kutumia vingora msafara mreeefu wenye mashushu kibaoo wanaolipwa kwa jasho letu while she aint even the first lady she is jus among the first ladies Tanzania has got!!!!
even if she is among them,but its too much!!

Mtaalam,

Ukiangalia bandiko la kwanza utaona First Lady "kutembea mwenyewe" imekuwa raised as an issue.

Tunajiuliza na kushangaa kuona kwamba mke wa Rais sasa naye anafanya ziara nchi nzima bila mumewe.

Katiba yetu haimtambui mke wa Rais kama ilivyo kwa US. Inakuwaje huyu mama sasa anahangaika kuliko Makamu wa Rais? Anaweza akasikika kama atakuwa akiandamana na mumewe.

JK yabidi amu-kontroo mukewe bwana sisi hatukumchagua.

Naelewa kuhusu accountability na matumizi mabaya ya kodi za wananchi ndiyo maana nikasema swala la "cost benefit analysis", siyo First Lady akitaka kusuka nywele Fifth Ave au Champs-Elysees anachukua dege la rais na kwenda kivyake tu.Hilo siafiki.

Nisichoafiki kingine ni kumzuia First Lady kwenda kutazama wagonjwa, kufungua zahanati, kufariji wahanga wa ukimwi, kusafisha miji, kupanda miti na mambo mengine kama hayo just because hajaandamana na rais.

Hiyo original post inaweza kutafsiriwa kwamba First Lady hatakiwi kwenda kwenye shughuli hizi peke yake kwa sababu si kiongozi na ni lazima aambatane na mumewe.Utaona kuwa hapa mtu akiingiza mambo ya haki za wanawake na usawa wa binadamu atakuwa hajakosea kwa maana wazo hili la kwamba First Lady ashikwe mkono kila anapoenda linatupeleka Saudia sasa.
 
na afanye vitu vya maendeleo .....lakini gharama za first lady ni nyingi. kuna kulipiwa ma body gurd, pesa za madereva wa misafara, posho ya madereva n.k.
tukiambiwa vyote hivyo vinatoka kwenye mfuko wake na si kwenye pesa ya wananchi, nobody will be bothered......
 
Huyu mama sasa anamfunika makamu wa Rais,yawezekana kuna posho naye analipwa anakozunguka asingeweza kuzunguka bure.Lakini gharama tujue zinaongezeka kwani itabidi kuwe na msafara posho kwa walinzi n.k.
kuna uwezekano huyu mama anauwezo mkubwa wa kuiwakilisha Tanzania na kupata mafanikio kuliko huyo uliye mlinganisha nae hivi kwani makamo wa Rais anatokea upande gani wa Tanzania?
 
kuna uwezekano huyu mama anauwezo mkubwa wa kuiwakilisha Tanzania na kupata mafanikio kuliko huyo uliye mlinganisha nae hivi kwani makamo wa Rais anatokea upande gani wa Tanzania?

Unless you are utterly and primarily predisposed to prescription potent and purely prejudiced propositions, why is this question even remotely relevant to the reigning rhetoric rouses reservations of repugnantly rotten ramifications.
 
Unless you are utterly and primarily predisposed to prescription potent and purely prejudiced propositions, why is this question even remotely relevant to the reigning rhetoric rouses reservations of rotten ramifications.

Blame the authors of the articles!
 
Tunajiuliza na kushangaa kuona kwamba mke wa Rais sasa naye anafanya ziara nchi nzima bila mumewe.

Katiba yetu haimtambui mke wa Rais kama ilivyo kwa US. Inakuwaje huyu mama sasa anahangaika kuliko Makamu wa Rais? Anaweza akasikika kama atakuwa akiandamana na mumewe.

JK yabidi amu-kontroo mukewe bwana sisi hatukumchagua.

akikaa ikulu na kuanza kunenepeana na ndugu zake, mtasema mke wa rais mvivu ! na mtasema ndo maana wafrica hatuendelei, leo hii mama wa watu wanachakarika mnaanza kulalama na kusema jk amcontrol mke wake, HIVI NYINYI WATANZANIA MNATAKA NINI ???????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????????
 
Hata Kikwete anachakarika lakini hajui anachokifanya.

Hatutaki kuchakarika kunako tulostisha!
 
The authors of the article are a bigger mystery than the Knight Templars and The Shroud of Turin combined!

In fact it's a model cited the world over.

Hey, how come the other guy didn't get a copy?

They say no one has seen the article since it was written. I always wonder where is a copy the other signatory was given.
 
Mkuu,

Katiba ya US inamtambuaje mke wa rais na yetu haimtambui vipi? Unaweza kutoa vifungu vya reference?

Mimi nafikiri kama kuna mjadala uwe ni juu ya umuhimu wa safari na kama haingiliii kazi za kiutendaji ambazo zingetakiwa kuwa a strict domain ya watendaji wa serikali na siyo juu ya kwamba First Lady anasafiri mwenyewe.Kusema kuwa First Lady hawezi kusafiri mwenyewe kutakuwa ni hatua ya kwanza kuelekea kusema kwamba dada zetu hawatakiwi kutoka nje ya nyumba bila kusindikizwa na kaka, mume au ndugu wa kiume. First Lady anaweza kutumika vizuri sana katika "ceremonial duties" kama kufungua Zahanati na ku officiate mashindano ya uzuri.Siafiki First Lady kuwa na nafasi katika ushauri wa sera.

Sioni tatizo la First Lady kusafiri kivyake, anaweza kutumika vizuri kuhamasisha huduma za jamii wakati rais anafanya shughuli nyingine.Tatizo labda, kama lipo, MOJA ni gharama na umuhimu wa safari kutowiana katika "cost benefit analysis" na la pili ni kuingilia sana katika kazi za kisera za watendaji wa serikali.

Siyo kwa sababu Kikwete tu au CCM tu basi kila kitu tuwe tunaponda bila msingi.
hapo napenda kupingana nawe kabisa ndugu, ktk nchi yetu mke wa raisi ni mke wa raisi tuu na kila kitu kinaishia hapo, kama mmoja alivyosema hapo juu katiba yetu haimtambui mke wa raisi kama kiongozi au mwakilishi wa kitu chechote cha kiserikali zaidi ya kuwa mke wa raisi... kuhusu marekani au nchi nyingine yeyote ile sitambui katiba zao zinasema nini ktk hilo...
kwa hiyo unaposema kwamba mke wa raisi atumike kuhamasisha jamii nakuwa sielewi una maana gani kwani kwa kawaida kuna mtu ambaye ameajiliwa ktk kufanya yoote hayo uliyoyasema na analipwa mshahara...
sasa unaposema kwamba "tatizo kama lipo, moja ni gharama" sielewei unamaanisha nini.....kwani lawama zetu zote juu yake zimesimama hapo, kama angekuwa anafanya yote haya kwa gharama zake bila kugusa mfuko wa serikali yetu, basi sidhani kama kuna mtu angethubutu kulalamika hapa, tatizo letu sisi kubwa ni pesa inayotumika bila sababu... ni kwanini mafuta yachomwe kwa ajili ya mke wa raisi kwenda kufungua shule? au hospitali au kitu chechote wakati kuna watu wanalipwa kwa hilo....kwani kuna ulazima gani wa hivi vitu kufunguliwa rasmi? mbona ni vitu vya kawaida tuu... kama ni shule kuna wizara husika kufungua, hospiatali hali kadhalika...
 
Back
Top Bottom