Wakili Mwita kaandika utaratibu wa kikatiba unaotakiwa kufuatwa pale Rais akiugua kimwili au kiakili

Mathanzua

JF-Expert Member
Jan 4, 2017
15,859
20,714
1711133944251.png

UTARATIBU WA KIKATIBA RAIS ANAPOUGUA KIMWILI AU AKILI

Wakili Mwita ameandika maoni yake juu ya Kifo cha Hayati John Magufuli baada ya kauli ya CDF Mstaafu Mabeyo siku ya kuadhimisha miaka mitatu ya Rais Samia.

"Kikatiba, rais wa nchi anapougua na kushindwa kabisa kutekeleza majukumu yake, Baraza la Mawaziri linapaswa kupewa taarifa. #Fact 1

Baraza la Mawaziri limepewa uwezo Kikatiba chini ya Ibara 37 kupeleka AZIMIO kwa Jaji Mkuu ili aunde jopo la madaktari wasiopungua 3 wanaotambulika na sheria ya matabibu nchini ili kuchunguza afya ya rais ya AKILI au/na MWILI. Ripoti ya madaktari ikitoka, ikithibitisha rais ni mgonjwa na hawezi tekeleza majukumu kabisa & hakuna dalili ya yeye kupona, ripoti hiyo hupelekwa kwa Jaji Mkuu ambaye hutakiwa kuiwasilisha kwa Spika wa Bunge kama AZIMIO la kumwondoa rais madarakani.

Jaji Mkuu asipofuta AZIMIO hilo ndani ya SIKU SABA, rais anahesabika amepoteza madaraka yake. Sheria inaelekeza taarifa za rais kuugua zipelekwe Bungeni kwa sababu rais ni mtumishi wa Umma & taarifa za kuugua kwake hazitakiwi kuwa siri. #Fact 2

Endapo ripoti itathibitisha kuwa rais ni mgonjwa na ameshindwa kabisa kutekeleza majukumu yake, sharti ya Kikatiba ni kwamba Makamu wa rais anatakiwa kuapishwa na kushika madaraka ya urais haraka iwezekanavyo & kumalizia kipindi kilichobaki kabla ya uchaguzi unaofuata. #Fact 3

Hivyo, kwa msimamo huu wa Kikatiba, Baraza la Mawaziri lilitakiwa kuwa na taarifa ya afya ya rais pale tu JPM alipoanza kuugua na kushindwa kutekeleza majukumu yake, hii ni kabla ya kuwa MAHUTUTI. Samia alitakiwa kuapishwa KABLA hata JPM hajafariki!

Pia, kutokana na alichokisema CDF mstaafu Mabeyo, ni wazi kwamba kuna kikundi cha watu KIMEVUNJA Katiba ya nchi kwa kutofuata taratibu zilizotajwa pale ambapo rais anaugua, taratibu ambazo zimewekwa ili kuepuka mambo ya UHAINI.

MASWALI

1. Kwanini utaratibu wa Kikatiba uvunjwe na hawa wavunja Katiba wako wapi na wanachukuliwa hatua gani & kuna uhakika gani hili halitajirudia?

Katika hili pia nakumbushia tu kumficha mtu mhaini ni kosa kubwa kisheria.

2. CDF Mabeyo ametuambia wakati rais JPM anafariki, akiwa MAHUTUTI sana, mbele yake alikuwa yeye (CDF), Mkurugenzi Mkuu TISS & IGP. Hawa ni wakuu wa vyombo vya ulinzi & usalama tu, ilikuwaje hakukuwa na kiongozi yeyote wa Kiserikali toka Baraza la Mawaziri akiwemo VP, PM au Waziri wa Afya?

3. Mnafahamu nguvu ya kisheria ya mwenza (mke) wa mgonjwa? Kwahiyo Mama Janet hakuwepo au mwanafamilia yeyote wakati mpendwa wao anaaga duniani?

4. Inakuwaje rais wa nchi ni mgonjwa halafu makamu wa rais afanye ziara Mkoa mwingine wa mbali huku rais yuko MAHUTUTI (fighting for his life), na ndiyo siku ambayo alifariki? Hiyo ziara ilikuwa na ulazima gani?

5. Kwanini Waziri Mkuu auambie umma kuwa rais ni mzima wakati alikuwa MAHUTUTI?

Ningepata nafasi ya kumfanyia CROSS-EXAMINATION mstaafu CDF ningeitumia taaluma yangu vyema. NINA MASWALI 50, HAYO NI YA UTANGULIZI TU" Wakili Mwita.

Mwanzo TV Plus
 
Ni wakati gani itaamuliwa kwamba kiongozi hawezi tena kutekeleza majukumu yake?

Izingatiwe kwamba ni kama desturi kwa nchi yetu kuficha hali ya afya za viongozi.

Kiongozi anaweza kufariki hata msijue, zikapita hata wiki kadhaa ndipo raia wanatangaziwa ni mgonjwa au ameaga dunia.

Kwa usiri huu hivi kuna uhalisia wowote wa kile isemacho katiba?
 
Kujitokeza kukumbushia sio dhambi,kwa kuwa tayari amesema isije kujitokeza.Hata hivyo ni muhimu kufahamu taratibu muhimu kama zipo.
Lakini pia kwanini Wakili kazungumza sasa? Ina maana hapo kabla hakuwa Wakili kulisemea hili...?
Bila CDF kuzungumza tusingejua kilichotokea.

But imagine kulingana na alichosema wakili.

1. Baraza la mawaziri lilikaa kujadili afya ya Rais?
2. Jaji mkuu aliuunda hilo jopo la madaktari?
3. Bunge lilikaa, au hakukuwa na haja?
4. Je Nani alithibitisha ugonjwa wa Rais?

Ni kweli Makamu ndiye mrithi wa Rais endapo kutatokea la kutokea, Ila utaratibu unasemaje?

Huoni tusipokuwa makini Wapinzani wa Samia wanaweza kutumia hoja ya utaratibu wa kikatiba na kumfanya Samia onekane aliingia kwa mapinduzi?

Naamini sio kila inabidi tuwe watu wa utaratibu sheria zinaachiwaga mwanya kimkakati
 
Mambo ya Tanzania katiba inamuogopa Rais hata kama inatamka bayana nini kifanyike, pia Mwanasheria mkuu wa serikali atasitatita kusema katiba inatamka kipi kifanyike na hata jaji Mkuu au wa mahakama za juu wote watafuata utashi wa rais anataka iwe vipi huku wakiogopa kumuambia mheshimiwa katika katiba inatamka kuwa .....
 
Bila CDF kuzungumza tusingejua kilichotokea.

But imagine kulingana na alichosema wakili.

1. Baraza la mawaziri lilikaa kujadili afya ya Rais?
2. Jaji mkuu aliuunda hilo jopo la madaktari?
3. Bunge lilikaa, au hakukuwa na haja?
4. Je Nani alithibitisha ugonjwa wa Rais?

Ni kweli Makamu ndiye mrithi wa Rais endapo kutatokea la kutokea, Ila utaratibu unasemaje?

Huoni tusipokuwa makini Wapinzani wa Samia wanaweza kutumia hoja ya utaratibu wa kikatiba na kumfanya Samia onekane aliingia kwa mapinduzi?

Naamini sio kila inabidi tuwe watu wa utaratibu sheria zinaachiwaga mwanya kimkakati
Kwa hiyo unataka kusema kuna uhaini ilitokea na Kwa sababu zipi...
Ina maana CDF Mstaafu ni sehemu ya njama na uzandiki....
Binafsi sioni tatizo lolote kwa kuwa kipindi kile kilikuwa ni kipindi kigumu Kwa Nchi na Dunia kutokuhoji kwanini fulani kafariki ...rejea janga la COVID-19.
Anyway nadhani ujumbe umefika lakini usimwonee MTU yeyote eti ndio sababu.
 
Endapo wanasiasa wa nchi hii wangeiheshimu, kuitii na kuiogopa hii Katiba tuliyonayo. Nchi hii ingekuwa mbali sana kimaendeleo na kiustaarabu
 
Upuuzi tu unapost hapa. Una uhakika gani rais alikuwa mahututi sana ?

Kama ni hivyo angewezaje kumuita paroko na kadinali waje kumpa sacrament ya mwisho?

Kwa mujibu wa CDF baada ya kupata mpako mtakatifu wa wagonjwa ilivyofika saa 8 hali yake ndio ilibadilika/kuzidiwa !

Punguza ujuaji, sio kila kitu unaokota huko bila kukifanyia upembuzi yakinifu unakileta hapa
 
Tukumbuke Mwafrika bado hajafanikiwa kuwa mtu wa kufuata utaratibu. Sisi bado tupo kwenye Primitive era.!

Kwahiyo yote hayo yaliyoandikwa kuhusu huo utaratibu si rahisi kufuatwa na sisi Waafrika. Hayo mambo tuwaachie Wazungu. Japo na wao wanachangamoto zao.
 
Bila CDF kuzungumza tusingejua kilichotokea.

But imagine kulingana na alichosema wakili.

1. Baraza la mawaziri lilikaa kujadili afya ya Rais?
2. Jaji mkuu aliuunda hilo jopo la madaktari?
3. Bunge lilikaa, au hakukuwa na haja?
4. Je Nani alithibitisha ugonjwa wa Rais?

Ni kweli Makamu ndiye mrithi wa Rais endapo kutatokea la kutokea, Ila utaratibu unasemaje?

Huoni tusipokuwa makini Wapinzani wa Samia wanaweza kutumia hoja ya utaratibu wa kikatiba na kumfanya Samia onekane aliingia kwa mapinduzi?

Naamini sio kila inabidi tuwe watu wa utaratibu sheria zinaachiwaga mwanya kimkakati
Usijali hata.

Rais wa Tanzania ni zaidi ya Katiba
 
Upuuzi tu unapost hapa ,,,, una uhakika gani rais alikuwa mahuti sana ?

Kama ni hivyo angewezaje kumuita paroko na kadinali waje kumpa sacrament ya mwisho ?

Kwa mujibu wa CDF baada ya kupata mpako mtakatifu wa wagonjwa ilivyofika saa 8 hali yake ndo ilibadilika/kuzidiwa !

Punguza ujuaji ,,,,sio kila kitu unaokota huko bila kukifanyia upembuzi yakinifu unakileta hapa
Hawa watu ndugu zetu wanasheria watakuja kuipeleka hii nchi pabaya...

Watu wanaweza kugeuka na kusema Rais hakuwa Mahututi, kuna mambo yalitokea
 
Upuuzi tu unapost hapa ,,,, una uhakika gani rais alikuwa mahuti sana ?

Kama ni hivyo angewezaje kumuita paroko na kadinali waje kumpa sacrament ya mwisho ?

Kwa mujibu wa CDF baada ya kupata mpako mtakatifu wa wagonjwa ilivyofika saa 8 hali yake ndo ilibadilika/kuzidiwa !

Punguza ujuaji ,,,,sio kila kitu unaokota huko bila kukifanyia upembuzi yakinifu unakileta hapa
Ila kwa kweli, hapo kwenye bold ink, ni uthibitisho kuwa katika hili, wewe ndiye mpuuzi halisi..!!

Rais Magufuli si alikufa baadaye? Sasa wewe unashindwaje kufikiri hata kwa kutumia miguu yako tu na kisha ukaelewa kuwa ni kweli na ni lazima "hayati" aliipitia hali ya umahututi..??

Please, don't be sarcastic..!
 
Back
Top Bottom