Frumence M Kyauke
JF-Expert Member
- Aug 30, 2021
- 630
- 1,245
Rafiki yangu tuliyesoma wote yeye yupo kwenye mahusiano na mwanamke kutoka Arusha ingawa bado hawaja tambulishana kwa ndugu na wazazi mpaka sasa.
Rafiki yangu amekuwa akiniomba ushauri sijui namsaidiaje, anadai kuwa anampenda sana huyo binti nae binti halikadhalika, tatizo kubwa ni kwamba huyo binti anapenda kuvaa nguo za kiume ikiwemo pensi, track, mashati ya kiume na kofia za kiume.
Kipindi chote huyu kaka amfahamu huyu binti hajawahi kuona nguo ya kike tangu waishi wote isipokuwa chupi tu za kike lakini nguo zote na viatu ni vya kiume.
Huyu kaka amekua akimshauri binti kuwa avae mavazi ya kike lakini binti amekaidi na kumjibu mwanaume kwani ni lazima! na wala hana mpango huo.
Sasa huyu kaka anawaza je atampelekaje kwao?
Je atamtambulishaje kwa rafiki zake?
Je, jamii kwa ujumla itamwelewaje huyo kaka itakapomuona huyu binti?
Je, watoto watakaozaliwa watamuonaje mama yao kwa tabia za yeye kuvaa mavazi ya kiume?
Rafiki yangu amekuwa akiniomba ushauri sijui namsaidiaje, anadai kuwa anampenda sana huyo binti nae binti halikadhalika, tatizo kubwa ni kwamba huyo binti anapenda kuvaa nguo za kiume ikiwemo pensi, track, mashati ya kiume na kofia za kiume.
Kipindi chote huyu kaka amfahamu huyu binti hajawahi kuona nguo ya kike tangu waishi wote isipokuwa chupi tu za kike lakini nguo zote na viatu ni vya kiume.
Huyu kaka amekua akimshauri binti kuwa avae mavazi ya kike lakini binti amekaidi na kumjibu mwanaume kwani ni lazima! na wala hana mpango huo.
Sasa huyu kaka anawaza je atampelekaje kwao?
Je atamtambulishaje kwa rafiki zake?
Je, jamii kwa ujumla itamwelewaje huyo kaka itakapomuona huyu binti?
Je, watoto watakaozaliwa watamuonaje mama yao kwa tabia za yeye kuvaa mavazi ya kiume?