Jocasta
JF-Expert Member
- Aug 28, 2014
- 474
- 588
Amefanyiwa operation ya kwanza kichwani wiki iliyopita na jana alifanyiwa operation ya pili, inauma na inaumiza sana kijana mdogo sana ambaye hata miaka 20 hajafikisha. Jamani mke wa mtu sumu.
Iko hivi, jamaa alipopata taarifa ya kwamba "msela nondo" anatoka kimapenzi na mke wake alimtafuta na kumuonya na alimtamkia kabisa ya kwamba usipoacha siku nikikufumania ntakumaliza,"msela nondo"alikataa katakata.
Siku ya siku ikafika, mida ya jioni jamaaa akamuaga mkewe ya kwamba anaenda kuangalia mifugo huko bondeni inakochungwa, ambapo kama kawaida ilitegemewa angelala huko. hawakujua kuwa siku hiyo ilikuwa mtego.
Mkewe bila hiyana akamtaarifu "msela nondo" kuwa jamaa hatakuwepo usiku hivyo aje, ni kweli "msela nondo" akatinga na moja kwa moja wakaanza mchezo.
Muda si mrefu mwenye mke akatinga(walikuwa wanamuita boya), kugonga mlango ukaitika moja kwa moja chumbani, uso kwa uso na "msela nondo". Katika hali ya kujitetea apate nafasi ya kuchomoka "msela nondo" akamchoma kisu tumboni jamaa mwenye mke(kosa Lingine kubwa alilofanya).
Mwenye mke akashika kiti na kumpiga nacho "msela nondo" kichwani, "msela nondo" akazima. Mwenye mke akaanza kutumia panga kumkata kata "msela nondo" kila sehemu mwilini, hasa kichwani ambako alikata panga za kutosha.
Mpaka alipohisi ya kuwa amemmaliza kabisa, akambeba juu juu na kumpeleka kwao, bahati yake.
Tumuombee msela nondo apone, huenda akapata nafasi ya kujifunza. Narudia kusema mke wa mtu sumu, inauma sana tena sana, naamini akipona hatarudia alichokifanya.
Iko hivi, jamaa alipopata taarifa ya kwamba "msela nondo" anatoka kimapenzi na mke wake alimtafuta na kumuonya na alimtamkia kabisa ya kwamba usipoacha siku nikikufumania ntakumaliza,"msela nondo"alikataa katakata.
Siku ya siku ikafika, mida ya jioni jamaaa akamuaga mkewe ya kwamba anaenda kuangalia mifugo huko bondeni inakochungwa, ambapo kama kawaida ilitegemewa angelala huko. hawakujua kuwa siku hiyo ilikuwa mtego.
Mkewe bila hiyana akamtaarifu "msela nondo" kuwa jamaa hatakuwepo usiku hivyo aje, ni kweli "msela nondo" akatinga na moja kwa moja wakaanza mchezo.
Muda si mrefu mwenye mke akatinga(walikuwa wanamuita boya), kugonga mlango ukaitika moja kwa moja chumbani, uso kwa uso na "msela nondo". Katika hali ya kujitetea apate nafasi ya kuchomoka "msela nondo" akamchoma kisu tumboni jamaa mwenye mke(kosa Lingine kubwa alilofanya).
Mwenye mke akashika kiti na kumpiga nacho "msela nondo" kichwani, "msela nondo" akazima. Mwenye mke akaanza kutumia panga kumkata kata "msela nondo" kila sehemu mwilini, hasa kichwani ambako alikata panga za kutosha.
Mpaka alipohisi ya kuwa amemmaliza kabisa, akambeba juu juu na kumpeleka kwao, bahati yake.
Tumuombee msela nondo apone, huenda akapata nafasi ya kujifunza. Narudia kusema mke wa mtu sumu, inauma sana tena sana, naamini akipona hatarudia alichokifanya.