Mke wa mtu ni sumu

Mke wa mtu ni sumu

Mwanaume ya yoyote anaetembea na mke wa mtu siku nisimkamate au nisiuziwe hiyo kesi. Mwanaume kamili hagombani na mkewe ila anamtafuta na kuweka mitego anayetafuna wake za watu.

Ukibahatika umeingia kwenye mikono yangu kwa kesi ya kutembea na mke wa mtu basi umekwisha!!
 
Kumekuwa na kauli itumikayo ktk jamii kwamba "mke wa mtu ni sumu" ikimaanisha kuwa kujihusisha "KIMAPENZI" na mke wa mtu ni HATARI sawa kama mtu "alobwia" sumu ....

SWALI: Kwani "mume wa mtu" si sumu?
Mkuu huyo mke wa mtu ana Bango mgongoni? Mm nitamjuaje jamani ? Wakati yeye mwenyewe amekana kwamba hana MTU ?
 
Mkuu huyo mke wa mtu ana Bango mgongoni? Mm nitamjuaje jamani ? Wakati yeye mwenyewe amekana kwamba hana MTU ?
Sasa ndo utakuwa umeuziwa mbuzi ktk gunia bwashee .... afu mwenye mke wake yeye hiyo "verse" wala haijui .... ni majanga tu ktk mji wa SEPUKA
 
Kwa sababu mwanaume karuhusiwa kumiliki mwanamke zaidi ya mmoja... ila wasiwe wake za watu...
Wake za watu sumu ....afu maziwa ya cku hizi ni ya MWENDOKASI maji kibao hayaondoi sumu
 
Kwenda zako huko umenichomesha mahindi weekend nzima nikijua naenda dubai yani hufai kabisaaaa
Mrembo kua mpole,nilikula ban baby,uwe standby maana ili kukupoza trip imebadilika,nakupeleka Thailand,Pattaya dream village ukapoze roho yako baby.
 
Mijini hali inazidi kuwa mbaya zaidi, wamama wengi hawana hata chembe ya uoga, anakupa makavu tuu kama vile si mwanandoa, mbaya zaidi wanaambizana~kuna kijana mmoja aliajiriwa kazini kwetu pale, ndani ya muda mfupi kawapitia kina dada/mama karibia wote (sababu ya msingi=ana dushe la kufa mtu) w.t.f.....!?, kapoteza kazi kizembe kbs
kala vya "watu" hadi kazi ikayeyuka
 
utamaduni uliopo mwanaume anaweza kuwa na mwanamke zaidi ya mmoja na jamii ikamsifia ila mwanamke akiwa na mwanaume zaidi ya mmoja jamii itamuita malaya
Waambie kwamba, kufuli inayofunguka kila ufunguo ni ya hovyo lakini funguo inayofungua kila kufuli huitwa master.
 
Mume wa mtu sisumu maana hafumaniwi, anakutwa ila hafukuziki na familia inasonga mbele jopo kutakuwa na kutokuaminiwa tena na upendo utapungua kwa couple, ila mke akifumaniwa mara nyingi familia inaparanganyika coz mama anafukuzwa na maisha yanabadilika ktk familia.
 
Aisee umenikumbusha mbali.
Kuna mwanaume alitembezwa uchi mtaani huku akila kichapo kisa mke wa mtu baada ya kufumwa nae.
Chaajabu mwanamke hakupewa adhabu yeyote.
Yaani yule kaka alitia huruma kwa kutembezwa uchi mtaa mzima na baadhi ya watu walilaani sana kile kitendo.
Toka hapo nikajua kuna wanaume wanaroho za ajabu likija suala la kuibiwa wake zao.
Sijui yule kaka kama atakaa arudie tena maisha yake yote
 
Back
Top Bottom