Mke wa mtu aning’ang’ania

Mke wa mtu aning’ang’ania

Anaitwa kichenchede
Ahaaa haaaa haaaa, Mzee ndio maana ndoa ilikushinda aseeee ... nikukumbushe tu, ukioa alafu ukaachika hautwi bachela arif, nafikiri lazima kuna jina lenu jingine mtakuwa mmepewa.

Bachelor - A man who is not and has never been married.
 
Habari zenu humu ndani,bila shaka wote humu wazima.Mimi ni kijana mwenye umri 36,ni mfanyakazi wa taasisi ya uma.Ndoa yangu ilinishinda muda mrefu sana kutokana na makwazo ya wanawake zetu.nilishindwa kuvumilia na nikaachana na mke wangu.Hivyobasi katika kuishi maisha ya u bachelor nikiwa kazini nikawa karibu sana na mdada ambaye alikua ananielezea shida anazozipata kwenye ndoa yake.Mwisho wa siku nilimfariji na tukawa marafiki wakubwa mpaka leo natoka naye.Ananipenda kupita maelezo.na mimi kwa kweli nampenda jinsi anavyo care.ameniahidi yuko tayari aachane na mme wake ili tuishi wote.naombeni ushauri wenu wadau,nifanyaje ili niishi na huyu mke wa mtu.
Mke wako ulimuacha kutokana na makwazo ya wanawake na huyo mke wa mtu nae tayari anamakwazo na mume wake unafikiri ukimchukua wewe hayo makwazo atayaacha,think twice before you make that silly decision...
 
kila mla cha mwenziwe mihuu humwelekea, hakunamkate mgumu mbele ya chai kaka, huyo sio mwanamke kwani mwanamke hasa aliyefundishwa maadili ya ndoa hawezi kueleza changamoto za ndoa yake nje hata siku moja. Na wala usijione kidume kwa kula mke wa mwenzio kumbuka na mkeo naye atakuja liwa hata kama baada ya miaka mia ukijakuoa. Huyo mwanamke ni wakumkwepa kama ukoma
 
Kuna watu wa kula ban pacha wng kpnz. Sasa nashanga hata wewe ikawaje ati...?

Pole mwaya...!
Tuyaache tu Pacha mana naeza pata ban ingine bure. 😀😀😀

Ahsante pacha.
 
Habari zenu humu ndani,bila shaka wote humu wazima.Mimi ni kijana mwenye umri 36,ni mfanyakazi wa taasisi ya uma.Ndoa yangu ilinishinda muda mrefu sana kutokana na makwazo ya wanawake zetu.nilishindwa kuvumilia na nikaachana na mke wangu.Hivyobasi katika kuishi maisha ya u bachelor nikiwa kazini nikawa karibu sana na mdada ambaye alikua ananielezea shida anazozipata kwenye ndoa yake.Mwisho wa siku nilimfariji na tukawa marafiki wakubwa mpaka leo natoka naye.Ananipenda kupita maelezo.na mimi kwa kweli nampenda jinsi anavyo care.ameniahidi yuko tayari aachane na mme wake ili tuishi wote.naombeni ushauri wenu wadau,nifanyaje ili niishi na huyu mke wa mtu.
nunua mafuta kabisa maana
 
bro huyo ni mke wa mtu....futa delete.....sawa ana mgogoro na mumewe.....but wewe ndio umekoleza waachane....jipange upya.....mbona toto's zuri wapo wengi tuu........
 
kila mla cha mwenziwe mihuu humwelekea, hakunamkate mgumu mbele ya chai kaka, huyo sio mwanamke kwani mwanamke hasa aliyefundishwa maadili ya ndoa hawezi kueleza changamoto za ndoa yake nje hata siku moja. Na wala usijione kidume kwa kula mke wa mwenzio kumbuka na mkeo naye atakuja liwa hata kama baada ya miaka mia ukijakuoa. Huyo mwanamke ni wakumkwepa kama ukoma

nilishaoa na niliachana na mke wangu.Ni muda mrefu siishi nae na haitaniuma hata kidogo kama nikija kujua ana danga.Huyu nilyempata naona kitachoweza kututenganisha ni kifo tu peke yake. asanteni kwa ushauri wenu.
 
Kijana wa miaka 36 halaf huna akili kiasi hicho? Ni akili hizo hizo ndogo ndio zimekufanya ukaishindwa ndoa na bila aibu tena unataka kuvunja ndoa ya mtu asiyekuwa na hatia eti kwa kisingizio mke wa mtu anakupenda na wewe unampenda.
Baada ya kufanikiwa kuvunja hiyo ndoa ya mwenzako utapata adhabu hutaisahau mpaka unaingia kaburini, malipo ni hapa hapa. Na kama utazinduka kiakili kimbia hiyo kitu tafuta wanawake waliokwisha achika tena sio kwasababu yako.
 
Back
Top Bottom