Wakuu inakuaje Mke anathamini na kusikiliza ndugu zake kuliko mumewe? Mfano, tumefunga ndoa miaka 10 iliyopita (2008) kama tunavyoonekana pichani. Peter''s RC church Dar baadae nilihamishiwa kikazi Namanga miaka 5 iliyopita (Mke akabaki Dar lakini Mke hajawahi kuja kunitembelea hata mara 1 japo mm najitahid kila mwezi naenda kusalimia Dar. Nikiuliza anadai yupo bize. La ajabu mara kadhaa anasafiri kwenda Mwanza kumuuguza mjomba (mwenye Mke na watoto). Nimeduwaa, nimeamua kuwa mpole kwa muda ili kupisha hasira hii.