Mke kuthamini ndugu zake kuliko Mume

Mke kuthamini ndugu zake kuliko Mume

Wakuu inakuaje Mke anathamini na kusikiliza ndugu zake kuliko mumewe? Mfano, nilihamishiwa kikazi Namanga miaka 5 iliyopita (Mke akabaki Dar lakini Mke hajawahi kuja kunitembelea hata mara 1 japo mm najitahid kila mwezi naenda kusalimia Dar. Nikiuliza anadai yupo bize. La ajabu mara kadhaa anasafiri kwenda Mwanza kumuuguza mjomba (mwenye Mke na watoto). Nimeduwaa, nimeamua kuwa mpole kwa muda ili kupisha hasira hii
Mpe pesa. Tatizo humpi pesa mke wako. Tafuta pesa ujenge heshima kwa mkeo. Mpe milion 3 kama hatakuja huko ulipo? Usikwepe majukumu pesa haya yote yatakwisha.
 
Miaka mitano unaacha mwanamke mjini na wala hajigusi kuja kukusalimia ndo unatafuta ushauri saa hizi? Kunae mwenzie huku mjini anammalizia shida zake. Kalagabaho
Haaaa wakati wenziwe mwezi tu mtihani huyo ndiye kichwa cha familia
 
Mara kadhaa nimeacha nauli na wakati wa Pasaka nilikata mpaka tiketi ya fastjet atue KIA kisha apande shuttle mpaka Arusha mjini baadae Namanga. Pesa ile ilienda bure na hakuja.
Duu pole na hapo unasema unamke? Wengine me akisafiri kikazi mwezi tu lazima kwenda kuchungulia hata wiki1 tunakaba mpaka penalty
 
. Huyu labda miguu ya familia
Haaaa yaani jamani vitu vingine mpaka aibu kuviongelea itakuwa yeye huko yupo na michepuko ndiyo maana hamfuatilii mkewe naye kuona hivyo anajisasambua tu kama jogoo
 
Back
Top Bottom