Mke kuthamini ndugu zake kuliko Mume

Mke kuthamini ndugu zake kuliko Mume

Wakuu inakuaje Mke anathamini na kusikiliza ndugu zake kuliko mumewe? Mfano, nilihamishiwa kikazi Namanga miaka 5 iliyopita (Mke akabaki Dar lakini Mke hajawahi kuja kunitembelea hata mara 1 japo mm najitahid kila mwezi naenda kusalimia Dar. Nikiuliza anadai yupo bize. La ajabu mara kadhaa anasafiri kwenda Mwanza kumuuguza mjomba (mwenye Mke na watoto). Nimeduwaa, nimeamua kuwa mpole kwa muda ili kupisha hasira hii
Uyo mke atakua amepata ndugu wa Faida, jitaidi uachane nae hamna dawa nyingine.

Usipoteze mda kusubiri, "kuku hawezi kua bata kamwe"
 
Polee mkuu, nawe jaribu kujiuguza labda atakuja Namanga...
Miaka 5 bado unalalamika???
 
"Hata mimea/miti ikiona hamna mwanga inakata kona kufwata huo mwanga".. Mzee baba miaka mitano mingi
(Urais huu jaman)
 
Naweza kuonekana mjinga kwa sasa lakini ukimya wangu umenilipa good time
 
Mara kadhaa nimeacha nauli na wakati wa Pasaka nilikata mpaka tiketi ya fastjet atue KIA kisha apande shuttle mpaka Arusha mjini baadae Namanga. Pesa ile ilienda bure na hakuja.
Kweli binadamu tuko tofauti ila hapo unachapiwa mchana kweupe tena kwenye makutano ya barabarani kabisa jiongeze Ndugu.
 
Kiukweli mawazo na rasilimali zangu karibu zote nimeelekeza kwa watoto
 
Wakuu inakuaje Mke anathamini na kusikiliza ndugu zake kuliko mumewe? Mfano, nilihamishiwa kikazi Namanga miaka 5 iliyopita (Mke akabaki Dar lakini Mke hajawahi kuja kunitembelea hata mara 1 japo mm najitahid kila mwezi naenda kusalimia Dar. Nikiuliza anadai yupo bize. La ajabu mara kadhaa anasafiri kwenda Mwanza kumuuguza mjomba (mwenye Mke na watoto). Nimeduwaa, nimeamua kuwa mpole kwa muda ili kupisha hasira hii
Naona Shetani anakukaria. Mkemee, vinginevyo Jela inakuita.
 
Aatakuja kukutembelea na kukupa pale atakapopata mimba, ili uwe uwe baba mzazi mlezi.
 
Back
Top Bottom