Faana
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 31,824
- 33,210
Kuna uzi humu unasema kuolewa bongo ni kama ajira ...sikuelewa ila sasa nimeelewaNina rafiki yangu dam dam kaoa mwaka huu mwezi wa pili,ndoa ya mkeka ya kiislam,kabla ya kuoana walikuwa kwenye mahusiano kwa miaka miwili.
Sasa jana umetokea ugomvi mdogo kisa mke alitaka jioni wale nyama na jamaa hakuagiza boda kupeleka iyo nyama ili ipikwe jioni.maisha yetu ni haya ya uswahilini katika hili jiji la Amos.
Sasa jamaa angu kabla ya haya mambo kutokea asubuh alikuwa amemwachia elf tano kwa ajili ya mboga tu maana kila kitu kipo ndani.sasa jamaa alimwambia kuwa nyama nimegairi tumia hiyo efu tano nilokwachia asubuh ununue mboga yoyote tule jioni mke hakumjibu chochote akakata simu.kufika usiku jamaa alirudi sa nne ana njaa ya atar kakuta mke kalala hajapika chochote jamaa akamaindi akamchapa kofi tatu tu.