Mke kachoma moto vyeti vya ndoa

Mke kachoma moto vyeti vya ndoa

Dada samahani ety ukumbi wa mawela sinza uko wapi naelekea harusini nadhani nimepotea njia,
 
Eebwana eeh ndoa hizi ni nbaya kweli, huwa nahisi na naamini mapepo yote na majini yasiyo na makazi huwa yanakimbilia kuishi kwemye hizi pete zinazoitwa za ndoa.

Nilifunga ndoa ya kanisani kabisa kanisa la TAG, ila kwa sababu kadhaa ikiwemo maelewano mabovu na mwenzangu ndoa ikawa shimo la mateso kwa kila mmoja.

Tukabahatika kupata mtoto miaka ana miaka 5 sasa ila mwisho wa siku baaada ya taabu na mateso mengi mke akaamua kuondoka, na mimi nikakaza roho sikumfata ni mwaka wa 3 huu.

Sasa majuzi hapa nikasema ngoja nimtafute mwenzangu hatukuwa na mawadiliano ya maana kabla, cha kwanza akajibu vema na kwa adabu za kutosha nikamwambia sasa nadhani kila mmoja ashagundua kila kitu walp tulikuwa tunafeli.

Binafis natamani urudi ila kama utakuwa na mipango mingine huko sio mbaya tukapeana nafasi jumla, na kwa kuwa uliondoka na vyeti vya ndoa kama huna mpango wa kurudi shughulikia suala la taraka au kama huna muda nipatie mimi nishughulikie ili kila mmoja awe huru na kwa amani.

Jibu alilonipa ni kuwa heye kwa sasa hana kumbukumbu zozote kuhusu ndoa alichoma moto kila kitu vyeti na picha, sasa hapo kisheria imekaaje maana nataka kuivunjilia mbali hii ndoa ili nianze upya?
Hatari sana ndoa ndoano.
 
Usisikilize huo upuuzi wa kuwa alichoma cheti.

Ole wako upate hela, atarudi na utashangaa cheti cha ndoa anacho au nakala yake. Kila unachokipata sasa mtagawana.
Hawajui wanawake huyu.

Cheti amechoma, ila scanned copy zake anazo. Anasubiri utajirike tu aanze seke seke. Ama ufariki aje kudai mirathi yako kwamba ni mke halali
 
Mimi naolewa siwezi acha kisa wajinga wanaolewa wanaacha ndoa zao kwa ajili ya umalaya wanawake wengi nimalaya sasa wakishaona mahali wamepazoea wanaenda kwingine ukiacha filamu za jua kali na huba wanandoa wanaongoza kwa ngono zembee il kwa ukweli hadi mitaani wao ndio malaya hawajali ndoa ni heshima .

Nakujitolea na uvumilivu na kuwa na kifua .
umesema vema
 
Pole. Wanawake ni waoga sana wa kuvunja ndoa halafu mume afanikiwe kifedha. We fanikiwa tu habari zimfikie atarudi na vyeti hata kama keshavichoma.

Ila kama unataka kuvunja ndoa anzia kanisani kwako.
 
Ili ndoa ibatilishwe/ivunjwe mahakamani itahitajika cheti, nenda kwa msajili wa ndoa ukapewe cheti tena kwa kuwa ushahidi upo huko kwa msajili wa ndoa. Kama hilo zoezi ni gumu ndoa haitatambuliwa na huyo mwanamke kapoteza haki zake za kugawana mali, kwako ni faida akidai unamruka futi mia na kielelezo hana kisheria hiyo ndoa haitambuliki bila cheti
 
Mnahangaikaga bure na ndoa nyie watu. Siku hizi mwanamke akizingua hataki ndoa unamuacha aende zake kwa amani, akidai mgao wa mali unampa tu bila kuvutana mahakamani. Ndoa ni hiari mtu anaweza kuingia na kutoka kama hana maadili ya ndoa na imani
 
Nadhani angechoma vya chuo ungenena kwa lugha
Aisee hii ilikaribia kunitokea, nilienda mkoa kikazi nikamuacha mama watoto wangu mjamzito pia. Siku moja si tukakorofishana, akasema nachoma kila kitu chako na vyeti vyako vyote nachoma hukuti kitu. Nilichanganyikia ikabidi niombe msaada kwa mama mkwe amsihi mwanae asichime vyeti.
Nashukuru alichoma nguo tu na baadhi ya viti havikiwa na umuhimu sana, hatari sana.
 
Fata ushauri ukaivunje hiyo ndoa kisheria. Mwanamke akisema hakutaki ujue amejitafakari vya kutosha na wewe mwanaume unatakiwa ukubali hilo na uendelee na maisha yako. Mwanaume anaweza akamwambia mwanamke hamtaki lakini akawa haamanishi lakini sio kwa mwanamke.
Wanaume tutafute amani na furaha ya mioyo yetu ili tuwe na siku nyingi za kuishi.
 
Aisee hii ilikaribia kunitokea, nilienda mkoa kikazi nikamuacha mama watoto wangu mjamzito pia. Siku moja si tukakorofishana, akasema nachoma kila kitu chako na vyeti vyako vyote nachoma hukuti kitu. Nilichanganyikia ikabidi niombe msaada kwa mama mkwe amsihi mwanae asichime vyeti.
Nashukuru alichoma nguo tu na baadhi ya viti havikiwa na umuhimu sana, hatari sana.
We mwenyewe unamuendekeza ndio maana anakupanda kichwani,angekuwa anajua kunakutenguliwa kiuno asingethubutu
 
Back
Top Bottom