Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

SEHEMU YA 08



Mara kwa mara nilikuwa nikitupa macho kila upande wa chumba hicho kwa hisia kwamba Harishi angeweza kutokea mle chumbani.
Asubuhi kulipokucha Yasmin alikuja kutugongea mlango.
“Amkeni. Kumeshakucha” Alikuwa akituambia wakati akigonga. Tukatambua kuwa alikuwa ni yeye.
Tukafungua mlango.
“Mmeamkaje?” akatuuliza.
“Tunashukuru tumeamka salama” nilimjibu kwa niaba ya wenzangu.
Wenzetu waliolala chumba kingine walikuwa hawana habari ya tukio lililotokea usiku. Nikawaeleza mbele ya Yasmin. Wakasikitika sana na kupata hofu.
“Sasa nendeni mkaoge halafu niwaandalie chai” Yasmin akatuambia.
Tukaenda kuoga. Kwanza waliingia watu wanne kwa vile vyoo vilikuwa vine. Walipotoka nikaingia mimi na mwenzangu.
Yasmin akatuandalia chai pale sebuleni. Ilikuwa chai iliyotengezwa kwa maziwa ya unga na iliyoungwa kwa iliki, tangawizi na bdalasini. Pia alitupa mikate iliyotengezwa kwa mayai.
SASA ENDELEA
Yeye mwenyewe alikunywa chai pamoja na sisi. Nikamuona amefurahi na kuchangamka licha ya kwamba usiku wa jana yake tu tulishuhudia machungu ya kuuawa mwenzetu.
“Ningekuwa nakula na wageni kila siku namna hii ningechangamka, lakini mh!” Yasmin alisema kama aliyekuwa akisema pek yake.
“Ni kweli Yasmin lakini tutafanyaje? Tunapenda kukusaidia lakini hatuna uwezo. Kama hivyo umeona mwenzetu ameshauawa na sisi hatujui maish yetu yatakuwaje!” nikamwambia Yasmin kwa huzuni.
“Kusema ukweli napenda niendelee kuwa na nyinyi hapaili nipate wenzangu wa kuzungumza nao. Lakini haitawezekana nyinyi muwepo hapa mkiwa hai.”
“Na pia hatuna mahali pengine pa kwenda” nikamwambia Yasmin.
“Huu ni mtihani. Sijui mtatumia mbinu gani muwe salama”
“Labda tuendelee kujifichaficha humu ndani” Mwenzetu mmoja akaingilia yale mazungumzo.
“Humu ndani atawagundua tu” Yasmin akamjibu.
“Sasa tutakwenda wapi jamani!”
“Mimi sijui niwambie nini ndugu zangu!” Yasmin akatuambai.
Tulipomaliza kunywa chai Yasmin aliondoa vyombo. Alituacha tumekaa tukiendelea kujadiliana. Baadaye kidogo alirudi akiwa na karata.
“Hizi karata ziko siku zote. Huyu mwendawazimu ananiletea. Lakini sina mwenzangu wa kucheza naye”
Tulipoona karata tukazunguka duara. Yasmin akakaa na kutugawia.
“Tunacheza mchezo gani?” nikamuuliza Yasmin.
“Tunacheza mchezo wa arbasitini”
Mchezo huo ulikywa maarufu kule Zanzibara na Comoro.
Tukaanza kucheza karata. Tukasahau kabisa habari ya Harishi. Mchezo ulinoga sana. Kelele zetu zikawa zinasikika hadi nje.
Ilipofika saa tano Yasmin akavunja mchezo na kutuambia tukatembee tembee. Tukiona jua la saa saba ndio turudi kula chakula. Mda ule alitaka kwenda kupika chakula.
“Niwapikie nini?” akatuuliza.
“Tupikiechochote tu utakachopenda” nikamwambia.
“Basi nitawapikia pilau”
“Tutashukuru sana”
“Sasa mtakapokuja, kwanza mchungulie na kusikiliza. Mkimuona Harishi msiingie ndani, rudini huko huko mtakakotoka. Anaweza kuja ghafla”
“Tumekuelewa” nilimjibu.
Baada ya hapo tulitoka tukarudi kule kwenye boti letu.
Ni tabia ya maumbile ya binaadamu kutokata tama na kujaribu kubahatisha kila mara hasa kwa watu kama sisi ambao tulikuwa katika hatari. Kwa mara nyingine tulijaribu tena kuliwasha lile boti. Kila mmoja wetu alijaribu kuliwasha bila mafanikio.
Tukakaa chini ya mti na kuanza kujadiliana. Hata hivyo mjadala wetu ulikuwa kama usio na maana yoyote kwani haukutupa ufumbuzi wa jinsi ya kusalimisha maisha yetu.
Kikubwa tulichokizingatia ni kujaribu kumkwepa Harish kadiri itakavyowezekana. Tuliona kama tutafanikiwa kumkwepa tunaweza kuendelea kuishi.
Tuliendelea kukaa pale chini ya mti hadi saa saba tulipoamua kurudi kwa Yasmin. Tulimtuma mmoja wetu aingie akachunguze kama Harishi yuko ndani aje atuambie.
Mwenzetu huyo akaingia ndani. Sisi tukawa tunamchungulia kwenye dirisha. Alinyata hadi ndani. Tukawa hatumuoni tena. Tukahamia kwenye dirisha jingine. Tukamuona amesimama pembeni mwa ukumbi akiangalia huku na huku. Akaenda jikoni kuchungulia kisha akatoka.
Alipotoka jikoni alikwenda moja kwa moja kwenye mlango wa chumba cha Yasmin na kutega masikio yake kwenye mlango. Alisikiliza kwa muda kidogo kisha akaanza kugonga mlango taratibu.
Mlango ukafunguliwa ghafla. Aliyetoka alikuwa Yasmin. Alitoka haraka haraka akaufunga mlango kisha akamuashiria yule jamaa aondoke. Nikajua kuwa hapakuwa salama.
“Moshi unajaa kwenye chupa, Harishi anakuja!” Yasmin alimwambia.
Yule mwenzetu aliposikia vile aligeuka ili aondoke lakini ghafla tena mlango ukafunguliwa. Harish akaibuka mbele ya yule mtu. Alikuwa ameshika upanga wake. Akamshika yule jamaa kwa mkono mmoja.
“Unataka ukimbie wapi wewe?” akamuuliza akiwa amemtolea macho.
ITAENDELEA
hahaaa mamaee " hizo nguvu za kucheza karata wamezitoa wapi hao"... huyo waliyemtoa chambo kwenda kumuangalia huyo so called harish ni zwazwa wa kiwango cha SGR .. mimi nisingekubali Aisee
 
Wewe jamaa kwani haujamjulia harishi shuaitwain???
Muda wankutupia stori ni baada ya saa ngapi.....Kuna kijisehemu nilicheka lkn inauma....jamaa mazembe Sana....unaogopa mvua kuliko harishi..etu tungeloa
Yaani mijinga kweli kweli " halafu seems like ni mi-limbukeni na kauli ya mwanamke " Anacho washauri ndio wanachokifuata" pasipo kuangalia usalama wa maisha yao ... Jinga sana
 
Yaani mijinga kweli kweli " halafu seems like ni mi-limbukeni na kauli ya mwanamke " Anacho washauri ndio wanachokifuata" pasipo kuangalia usalama wa maisha yao ... Jinga sana
Mkuu tulikuwa tunaogopa kulowa na mvua
 
SEHEMU YA 16


“Kaka Masudi ana matatizo sana. Kwanza hatuelewi ni kitu kilichomfanya amsindikize yule msichana” Shazume akasema.
“Tusiwe na wasiwasi naye sana. Huenda mwenyewe ameamua kubaki” nikawambia wenzangu.
“Atabakije kule wakati anajua kuwa lazima Harishi atakuja?” Haji akauliza.
“Kila mtu ana akili yake jamani tusimuhukumu” nikawambia Shazume na Haji.
“Atajua mwenyewe, shauri yake” ilikuwa sauti ya kukata tamaa ya Haji.
Baada ya kujadiliana kwa kirefu tuliamua kwenda kulala. Kila mtu aliingia kwenye chumba chake.
Unapofika wakati wa kulala mawazo hubadilika. Fikira zote huondoka na kichwa kujaa mawazo ya Harishi.
Nilikuwa na hakika kuwa sikuwa mimi peke yangu bali wenzangu wote walikuwa na mawazo kama yangu. Likini hatukuwa na lolote la kufanya zaidi ya kukubali matokeo yatakayotokea usiku huo kwa Masudi.
SASA ENDELEA
Usiku ule tulilala na kuamka salama ingawa tulilala kwa mashaka.
Lakini Masudi hakuwa miongoni mwetu. Tukadhani kwamba atatokea wakati ule wa asubuhi baada ya kushindwa kurudi usiku. Lakini tulikaa hadi majira ya saa bila kumuona yeye wala Yasmin.
“Wenzangu mnaonaje twende tukamuangalie Masudi au tuendelee kumsubiri?” nikawauliza wenzangu.
“Kwenda kumuangalia ni jambo zuri lakini tunaweza kukutana na Harishi” Haji akasema.
“Nina wasiwasi kwa sababu Yasmin pia amekaa kimya. Kwa kawaida muda huu angekuwa ameshakuja” nikawambia wenzangu.
“Hatuwezi kujua lolote linaweza kuwa limetokea” Shazume naye akasema.
“Basi tusiende, tuendelee kusubiri hapa hapa hadi atakapokuja Masudi au Yasmin” nikawambia.
Wakati tunaendelea kujadiliana tulimuona Yasmin akiingia. Sote tukageuka na kumtazama. Kitu kilichotushitua si tu alikuwa peke yake bali macho yake yalikuwa mekundu yaliyoonesha alikuwa analia.
Akatusalimia na kutuambia kuwa amepatwa na fadhaa.
“Kwanini?” akatuuliza.
“Kaka yenu Masudi hakutumia busara hata kidogo” Masudi alituambia huku akitikisa kichwa kusikitika.
“Kwanini hakutumia busara?” nikamuuliza huku nikifikiria mengine. Nilifikiria ama Masudi alitaka kumbaka Yasmin au alimbaka kwani ile hali niliyowakuta nayo usiku uliopita haikuwa ya kawaida.
“Kama yeye amenipenda mimi kama alivyoniambia mwenyewe ni sawa lakini kitendo alichokifanya si kizuri kwa sababu anajua mimi nimemilikiwa na Harishi”
Hapo nilijua moja kwa moja kuwa Masudi amembaka Yasmin na ndio sababu alikuwa analia.
“Kwani amefanya nini?” nikamuuliza.
“Ungetueleza alichofanya” Haji naye akamwambia.
“Jana usiku nilimwambia arudi huku, ulikuwa ni usiku. Lakini alikataa kurudi, akataka kulala na mimi. Nilimsihi sana arudi lakini aligoma kabisa, tena alitaka alale na mimi chumba kimoja. Aliniambia ananipenda” Yasmin akatueleza.
“Masudi ni kaka yetu lakini ana matatizo sana” Shazume akadakia.
“Sasa ikawaje?” na mimi nikauliza kwa pupa.
“Nilimuachia alale. Yule ni mwanaume nisingeweza kumzuia”
“Ulilala naye chumba kimoja?” nikamuuliza.
“Nilimuomba sana akalale chumba kingine kwa usalama wake. Nilimwambia Harishi akija na kukukuta atakuua. Akakubali kwenda kulala chumba kingine”
“Sasa nini kimetokea?” Shazume akauliza.
“Harishi alikuja muda ule ule akamkuta ukumbini anazungukazunguka, akashikwa”
Alipofikia hapo Yasmin alianza kulia.
“Sasa ameuliwa?’ nikamuuliza.
“Harishi aliacha mtu siku gani?” Yasmin akaniuliza.
Mimi na Haji na Shazume tulitazamana tukiwa tumeacha midomo wazi.
“Aliyataka mwenyewe!” Yasmin akasema.
“Ni kweli aliyataka mwenyewe, kifo kilikuwa kinamuita” nikamuunga mkono.
“Angekuja kulala na wenzake pengine angenusurika” Yasmin aliendelea kutuambia.
“Mbona hukuja mapema kutuambia?” nikamuuliza.
“Harishi ameondoka sasa hivi. Jana usiku alipokuja alikuwa amelewa na alipomuua Masudi hakuondoka tena hadi hii asubuhi”
“Kumbe majini pia wanalewa?”
“Wanalewa kama watu. Harishi analewa sana”
“Hiyo pombe anaipata wapi?”
“Sijui mwenyewe”
“Na anapokuta mtu mle ndani anakuuliza ni nani?”
“Anaua kwanza halafu ndio anauliza. Mimi humwambia kwamba ni wavuvi wameingia kwa bahati mbaya. Lakini kama angenikuta nimelala naye angejua ni mwanaume wangu”
“Angekuua?”
“Sijui ingekuwaje?”
Pakapita kimya cha sekunde kadhaa. Sote tulikuwa tunamkumbuka kaka yetu Masidi.
“Mtanisamehe sikuwaletea chai. Nilikuwa nimetaharuki sana” Yasmin akatuambia baadaye.
“Misiba kama hii. Kila siku anakufa mtu. Hamu ya kula pia inapotea” nikamwambia.
“Nyinyi mtabaki huku huku mjaribu bahati zenu. Mnaweza kusalimika”
ITAENDELEA
 
Subra itakusaidia..usije ukamzini binti wa Rais...

Haya Mambo yapo Sana...Mimi nasumbuliwa na jini simjui.anaonekana anapenda nipige Punyeto....yawezekana anapenda shahawa....I just knew it... someone will reject it but it is....Dua zinanisaidia...ananimaliza nguvu za kiume but ninazo bado napambana nae...tangu zaman.... Nina miaka 27 sasa...na nimeoa 4 yrs katika ndoa.....

Nilikuwa nikipiga bao 4 ndani kwa ndani...saa hii...hata nikiwa na mke nakosa nguvu japo hamu ninayo na muda wa alfajir nikipiga mzigo....napiga kweli...kwa nn nguv Sina????


Huyu jini aliisha wahi kuninajisi.siku moja..nilikuwa nimelala nikahisi nalawitiwa...kitu kama maji baridii vikiingia mk.unduni pale pa kunyea aka hajakubwa. Nilisikitika sana

Hawa jamaa wapo na niwasumbufu, sijajua Kama ni sababu siku moja alinijia msichana mzur Sana....akaniambia wenzio wanakuacha...niliingia hotel flan kubwa Kula.. kweli nikaona gari inazunguka, nikanawa nlmikono nikatoka, nikawaulizlja jamaa kwa nn mnaniacha wakadai muda umeisha tuondoke, nikahoji ndio msiniambie?! Hapakuwa na jawabu la maana.....

Huyu msichana mrembo ndio uhusiano ukaanzia hapo..ni mzur kuliko kawaida...
Bado namhusisha na jini....hajaolewa yupo tu.
Hahaaa ameota anafanywa nini ""......?? daaahhh
 
Subra itakusaidia..usije ukamzini binti wa Rais...

Haya Mambo yapo Sana...Mimi nasumbuliwa na jini simjui.anaonekana anapenda nipige Punyeto....yawezekana anapenda shahawa....I just knew it... someone will reject it but it is....Dua zinanisaidia...ananimaliza nguvu za kiume but ninazo bado napambana nae...tangu zaman.... Nina miaka 27 sasa...na nimeoa 4 yrs katika ndoa.....

Nilikuwa nikipiga bao 4 ndani kwa ndani...saa hii...hata nikiwa na mke nakosa nguvu japo hamu ninayo na muda wa alfajir nikipiga mzigo....napiga kweli...kwa nn nguv Sina????


Huyu jini aliisha wahi kuninajisi.siku moja..nilikuwa nimelala nikahisi nalawitiwa...kitu kama maji baridii vikiingia mk.unduni pale pa kunyea aka hajakubwa. Nilisikitika sana

Hawa jamaa wapo na niwasumbufu, sijajua Kama ni sababu siku moja alinijia msichana mzur Sana....akaniambia wenzio wanakuacha...niliingia hotel flan kubwa Kula.. kweli nikaona gari inazunguka, nikanawa nlmikono nikatoka, nikawaulizlja jamaa kwa nn mnaniacha wakadai muda umeisha tuondoke, nikahoji ndio msiniambie?! Hapakuwa na jawabu la maana.....

Huyu msichana mrembo ndio uhusiano ukaanzia hapo..ni mzur kuliko kawaida...
Bado namhusisha na jini....hajaolewa yupo tu.
kwahiyo mkuu Jini amekula 0713 ... hahaaa daahh bado siamini aisee
 
Subra itakusaidia..usije ukamzini binti wa Rais...

Haya Mambo yapo Sana...Mimi nasumbuliwa na jini simjui.anaonekana anapenda nipige Punyeto....yawezekana anapenda shahawa....I just knew it... someone will reject it but it is....Dua zinanisaidia...ananimaliza nguvu za kiume but ninazo bado napambana nae...tangu zaman.... Nina miaka 27 sasa...na nimeoa 4 yrs katika ndoa.....

Nilikuwa nikipiga bao 4 ndani kwa ndani...saa hii...hata nikiwa na mke nakosa nguvu japo hamu ninayo na muda wa alfajir nikipiga mzigo....napiga kweli...kwa nn nguv Sina????


Huyu jini aliisha wahi kuninajisi.siku moja..nilikuwa nimelala nikahisi nalawitiwa...kitu kama maji baridii vikiingia mk.unduni pale pa kunyea aka hajakubwa. Nilisikitika sana

Hawa jamaa wapo na niwasumbufu, sijajua Kama ni sababu siku moja alinijia msichana mzur Sana....akaniambia wenzio wanakuacha...niliingia hotel flan kubwa Kula.. kweli nikaona gari inazunguka, nikanawa nlmikono nikatoka, nikawaulizlja jamaa kwa nn mnaniacha wakadai muda umeisha tuondoke, nikahoji ndio msiniambie?! Hapakuwa na jawabu la maana.....

Huyu msichana mrembo ndio uhusiano ukaanzia hapo..ni mzur kuliko kawaida...
Bado namhusisha na jini....hajaolewa yupo tu.
Mkuu umeoa miaka 23 au uliteleza?
 
Mkuu tulikuwa tunaogopa kulowa na mvua
hahaa mkuu Yaani mkiahidiwa pilau tu " Akili zina waruka " Mnapenda kula kula kama panya road ... haya ona huyo mwingine nae papuchi imemponza mwisho wa siku amekufa"... Hivi kwenye mazingira kama hayo Hata dushe lina simama kweli .. duh!!!! kuna watu wana vipaji
 
Back
Top Bottom