Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

SEHEMU YA 08



Mara kwa mara nilikuwa nikitupa macho kila upande wa chumba hicho kwa hisia kwamba Harishi angeweza kutokea mle chumbani.
Asubuhi kulipokucha Yasmin alikuja kutugongea mlango.
“Amkeni. Kumeshakucha” Alikuwa akituambia wakati akigonga. Tukatambua kuwa alikuwa ni yeye.
Tukafungua mlango.
“Mmeamkaje?” akatuuliza.
“Tunashukuru tumeamka salama” nilimjibu kwa niaba ya wenzangu.
Wenzetu waliolala chumba kingine walikuwa hawana habari ya tukio lililotokea usiku. Nikawaeleza mbele ya Yasmin. Wakasikitika sana na kupata hofu.
“Sasa nendeni mkaoge halafu niwaandalie chai” Yasmin akatuambia.
Tukaenda kuoga. Kwanza waliingia watu wanne kwa vile vyoo vilikuwa vine. Walipotoka nikaingia mimi na mwenzangu.
Yasmin akatuandalia chai pale sebuleni. Ilikuwa chai iliyotengezwa kwa maziwa ya unga na iliyoungwa kwa iliki, tangawizi na bdalasini. Pia alitupa mikate iliyotengezwa kwa mayai.
SASA ENDELEA
Yeye mwenyewe alikunywa chai pamoja na sisi. Nikamuona amefurahi na kuchangamka licha ya kwamba usiku wa jana yake tu tulishuhudia machungu ya kuuawa mwenzetu.
“Ningekuwa nakula na wageni kila siku namna hii ningechangamka, lakini mh!” Yasmin alisema kama aliyekuwa akisema pek yake.
“Ni kweli Yasmin lakini tutafanyaje? Tunapenda kukusaidia lakini hatuna uwezo. Kama hivyo umeona mwenzetu ameshauawa na sisi hatujui maish yetu yatakuwaje!” nikamwambia Yasmin kwa huzuni.
“Kusema ukweli napenda niendelee kuwa na nyinyi hapaili nipate wenzangu wa kuzungumza nao. Lakini haitawezekana nyinyi muwepo hapa mkiwa hai.”
“Na pia hatuna mahali pengine pa kwenda” nikamwambia Yasmin.
“Huu ni mtihani. Sijui mtatumia mbinu gani muwe salama”
“Labda tuendelee kujifichaficha humu ndani” Mwenzetu mmoja akaingilia yale mazungumzo.
“Humu ndani atawagundua tu” Yasmin akamjibu.
“Sasa tutakwenda wapi jamani!”
“Mimi sijui niwambie nini ndugu zangu!” Yasmin akatuambai.
Tulipomaliza kunywa chai Yasmin aliondoa vyombo. Alituacha tumekaa tukiendelea kujadiliana. Baadaye kidogo alirudi akiwa na karata.
“Hizi karata ziko siku zote. Huyu mwendawazimu ananiletea. Lakini sina mwenzangu wa kucheza naye”
Tulipoona karata tukazunguka duara. Yasmin akakaa na kutugawia.
“Tunacheza mchezo gani?” nikamuuliza Yasmin.
“Tunacheza mchezo wa arbasitini”
Mchezo huo ulikywa maarufu kule Zanzibara na Comoro.
Tukaanza kucheza karata. Tukasahau kabisa habari ya Harishi. Mchezo ulinoga sana. Kelele zetu zikawa zinasikika hadi nje.
Ilipofika saa tano Yasmin akavunja mchezo na kutuambia tukatembee tembee. Tukiona jua la saa saba ndio turudi kula chakula. Mda ule alitaka kwenda kupika chakula.
“Niwapikie nini?” akatuuliza.
“Tupikiechochote tu utakachopenda” nikamwambia.
“Basi nitawapikia pilau”
“Tutashukuru sana”
“Sasa mtakapokuja, kwanza mchungulie na kusikiliza. Mkimuona Harishi msiingie ndani, rudini huko huko mtakakotoka. Anaweza kuja ghafla”
“Tumekuelewa” nilimjibu.
Baada ya hapo tulitoka tukarudi kule kwenye boti letu.
Ni tabia ya maumbile ya binaadamu kutokata tama na kujaribu kubahatisha kila mara hasa kwa watu kama sisi ambao tulikuwa katika hatari. Kwa mara nyingine tulijaribu tena kuliwasha lile boti. Kila mmoja wetu alijaribu kuliwasha bila mafanikio.
Tukakaa chini ya mti na kuanza kujadiliana. Hata hivyo mjadala wetu ulikuwa kama usio na maana yoyote kwani haukutupa ufumbuzi wa jinsi ya kusalimisha maisha yetu.
Kikubwa tulichokizingatia ni kujaribu kumkwepa Harish kadiri itakavyowezekana. Tuliona kama tutafanikiwa kumkwepa tunaweza kuendelea kuishi.
Tuliendelea kukaa pale chini ya mti hadi saa saba tulipoamua kurudi kwa Yasmin. Tulimtuma mmoja wetu aingie akachunguze kama Harishi yuko ndani aje atuambie.
Mwenzetu huyo akaingia ndani. Sisi tukawa tunamchungulia kwenye dirisha. Alinyata hadi ndani. Tukawa hatumuoni tena. Tukahamia kwenye dirisha jingine. Tukamuona amesimama pembeni mwa ukumbi akiangalia huku na huku. Akaenda jikoni kuchungulia kisha akatoka.
Alipotoka jikoni alikwenda moja kwa moja kwenye mlango wa chumba cha Yasmin na kutega masikio yake kwenye mlango. Alisikiliza kwa muda kidogo kisha akaanza kugonga mlango taratibu.
Mlango ukafunguliwa ghafla. Aliyetoka alikuwa Yasmin. Alitoka haraka haraka akaufunga mlango kisha akamuashiria yule jamaa aondoke. Nikajua kuwa hapakuwa salama.
“Moshi unajaa kwenye chupa, Harishi anakuja!” Yasmin alimwambia.
Yule mwenzetu aliposikia vile aligeuka ili aondoke lakini ghafla tena mlango ukafunguliwa. Harish akaibuka mbele ya yule mtu. Alikuwa ameshika upanga wake. Akamshika yule jamaa kwa mkono mmoja.
“Unataka ukimbie wapi wewe?” akamuuliza akiwa amemtolea macho.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 09



Mwenzetu aliishiwa na nguvu kabisa. Akawa amemkodolea macho Harishi.
“Mimi nasikia harufu zenu tangu jana”
Mwenzetu kimya. Sasa mwili wake ulikuwa ukitetemeka waziwazi.
“Sheikh nisamehe sana…” Sauti yake ikasikika kwa mbali ikiomba.
“Chombo chetu kiliharibika jana”
Harisha alikuwa akimtazama kama vile alikuwa hamuelewi.
“Wasemaje?”
“Nisamehe sana…nakuomba” jamaa alikuwa analia.
“Kwani wewe huna damu?. Ngoja nione”
Hapo hapo Harishi akamuinua juu mwenzetu huyo kwa mkono mmoja tu. Akamgeuza kichwa chini.
Kiasi cha kufumba na kufumbua tu alishamtoboa utosi kwa ncha ya upanga wake.
Yasmin alipoona hivyo alikimbilia nje. Akatuona tumeinamia dirisha.
“Jamani balaa gani hili?” akajisemea peke yake.
SASA ENDELEA
Idadi yetu sasa tulikuwa watu watano, wenzetu wawili walikuwa wameshauawa. Na sisi pia hatukuwa na matumaini kuwa tungebaki.
Tulijua kuwa kama hatutakufa kwa njaa, tutauliwa na lile jini la Yasmin. Kila mmoja wetu alikuwa ameshikwa na hofu na fadhaa. Tulitamani angalau kipite chombo kituokoe kuliko vile tulivyokuwa matumatu tukisubiri kufa.
Tulitamani tusifike tena katika lile jumba la Yasmin lakini tungekula nini, wakati kwa Yasmin ndiko tunakotarajia kupata riziki yetu. Kusema kweli tulichanganyikiwa na hatukujua la kufanya.
Tulikaa pale chini ya mti kwa karibu saa mbili. Ghafla tuliona mwanamke akiambaa na ufukwe wa bahari akija upande wetu. Mkono mmoja alikuwa ameshika kapu.
“Jamani ni nani yule?” Mwenzetu mmoja akauliza.
“Naona ni kama Yasmin” nikajibu.
Mjadala ukaanza.
“Ni Yasmin kweli!”
“Amefuata nini huku?”
“Labda anatutafuta sisi”
“Mmoja wetu atokeze ili atuone au aende akampokee lile kapu. Labda anatuletea chakula”
“Hatujui Harishi yuko wapi. Unaweza kujitokeza ukajikuta unakamatwa!”
“Bila shaka Harishi ameshaondoka, Yasmin asingeweza kuja huku. Ngoja nimfuate” Mimi ndiye niliyesema hivyo. Nikanyanyuka na kuanza mwendo kuelekea upande ule aliotokea Yasmin.
Yasmin akaniona.
“Nawatafuta nyinyi, mko wapi?” akaniuliza tangu akiwa mbali.
“Tuko huku chini ya mti. Tumekuona tangu ukiwa mbali”
“Nimewaletea chakula”
Nilikuwa nimeshamfikia. Nikampokea lile kapu.
Tukawa tunatembea pamoja kuelekea kule waliko wenzetu
“Lile shetani limeshaondoka, ndio maana nimeweza kutoka” Yasmin akaniambia’
“Halitarudi tena kwa leo?”
“Halitarudi labda kwa kesho”
“Yule mwenzetu ndio ameuawa?”
“Ndio aliuawa. Si mliona wenyewe akikamatwa”
Nikatikisa kichwa changu kusikitika.
“Wakati anabisha mlango niliona ile chupa ya Harishi inajaa moshi. Nikajua kuwa Harishi anakuja. Nikawahi kutoka ili niwambie muondoke. Wakati nasemeshana na yule mwenzenu, Harishi akasikia akawahi kutoka na kumkamata” Yasmin aliendelea kunieleza.
“Sasa yule jinni atatumaliza sote. Tulikuwa watu saba sasa tumebaki watano tu”
“Basi msije kule”
“Sasa tusipokuja utatuletea chakula?”
“Nitawaletea. Na leo ameshakula mtu mmoja harudi tena hadi kesho”
Tukawa tumefika walipokuwa wenzetu.
“Leo tumepata msiba mwingine” Mtu mooja akamwambia Yasmin.
“Nilishawambia tangu mapema kuwa usalama hapa ni mdogo sana kwa sababu ya Harishi. Sasa mnaona wenyewe, na ijui mtafanya nini ndugu zangu”
“Jamani kwanza tuleni chakula. Yasmin ametuletea chakula. Tukanawe mikono kwa maji ya chumvi. Mazungumzo baadaye” nikawambia wenzangu.
Tukaenda kunawa maji ya bahari kisha tukarudi pale chini ya mti, tukaketi. Yasmin naye akaketi.na sisi. Tukaanza kula.
“Kwani Harish ameshaenda zake?” Mtu mmoja akamuuliza Yasmin.
“Ameshaondoka” nikamjibu mimi. “Angekuwepo Yasmin asingeweza kuja huku”
Fuatiliakisahiki hapo na usikose
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 10




Tulikula pilau ikiwa ndani ya kapu. Tukashiba na kupata nguvu.
“Nimesahau kuwachukulia maji ya kunywa” Yasmin akatuambia.
“Na maji tuliyokuwa nayo yamekwisha” nikasema.
“Lakini kwa leo Harishi hatarudi, mnaweza kuja nyumbani” Yasmin akatuambia.
“Mh!. Nyumbani kwako kunaogopesha” nikamwambia Yasmin.
“Tunaweza kwenda mnywe maji halafu mtarudi huku huku”
Tukajadiliana na Yasmin, mwisho tukaamua turudi katika lile jumba. Tukarudi.
Tulipofika alitupatia maji ya kunywa. Tukamshukuru kwa wema wake.
“Bado mna wasiwasi?” Yasmin akatuuliza.
“Kuwa na wasiwasi ni lazima” nikamjibu na kuongeza. “Tunajiona kama tuko kwenye vita”
“ Kwa leo msiwe na wasiwasi. Yule jini hatarudi tena. Kama ni kurudi ni kesho. Tunaweza kukaa tukaongea hadi usiku mkaenda zenu”
Tukashauriana na kukubaliana tukae hadi usiku kwa vile mwenyeji wetu ameshatuhakikishia kuwa tutakuwa salama. Pia tulikuwa tunamuhurumia Yasmin aliyekuwa mpweke katika jumba lile. Tukaona tukae tumchangamshe.
Tukakaa kwenye ule ukumbi pamoja na Yasmin na kuanza kuzungumza.
“Yasmin alitupa hadithi ya jinsi alivyofikishwa katika jumba lile na jinsi alivyokuwa akilia katika siku za mwanzo mwanzo.
ITAENDELEA
.
“Lile jini hata ukilia, halijali. Linakwambia utazoea tu. Na ni kweli kadiri siku zilivyokwenda nilijikuta nikizoea” Yasmin aliendelea kutuhadithia.
“Sasa mnaishije, wakati wewe ni mtu na yule ni jini?” Mwenzetu mmoja akamuuliza.
“Tunaishi kama mke na mume ingawa mwenzangu ni jini lakini ndio nimeshamzoea. Ameshaniambia kwamba nitaishi naye hadi kufa kwangu”
“Je kama akifa yeye?” nikamuuliza.
“Amesema yeye hatakufa haraka. Umri wa majini ni mrefu sana. Pale alipo ana miaka mia tatu na anaweza kuishi hadi miaka mia tano”
“Loh!. Wewe utakufa, yeye ataendelea kuishi kwa miaka mingi sana” Mtu mmoja akamwambia Yasmin.
“Lakini mimi ningependa kujua hisia zako. Unajisikiaje unapohisi kuwa utaishi ndani a jumba hili hadi ufe wakati bado ni msichana mdogo” Mimi nilimuuliza Yasmin swali hilo.
Yasmin akabetua mabega.
“Nasikia vibaya lakini nitafanyaje sasa. Nimelia nimechoka, sasa silii tena”
“Kwa hiyo ndio unaishi ukisubiri kifo chako kitokee humu humu ndani?” Mtu mwingine alimuuliza. Lilikuwa si swali zuri. Sikulipenda. Lakini Yasmin alimjibu.
“Wakati mwingine najidanganya kwamba iko siku yaweza kutokea miujiza nikaokolewa kwa namna nisiyoijua.
“Na tangu uishi humu hakujatokea watu kama sisi wakaingia katika jumba hili?” nikamuuliza.
“Nyinyi ndio watu wa kwanza kuwaona tangu nianze kuishi katika jumba hili”
Tukaendelea kuzungumza na Yasmin hadi alipotuambia kuwa anakwenda kupika chakula cha usiku.
Tukabaki sisi peke yetu na kuendelea kuzungumza na kujadiliana kuhusu maisha ya Yasmin na maisha yetu wenyewe.
Jua lilipokuwa limekuchwa nilimfuata Yasmin jikoni nikamwambia kwamba tunaondoka.
“Kwanini…subirini mle chakula. Nimepika chakula kingi kwa ajili yenu” Yasmin akaniambia
“Giza linaingia. Tuna hofu yule jini anaweza kutokea. Acha tuondoke tu”
“Jamani mkiwepo mnanichangamsha na mimi. Sasa mnataka kwenda wapi?”
“Tunarudi kule kule ulikotukuta”
“Kwanini jamani? Nimewambia Harishi hawezi kurudi leo labda kwa kesho. Mnaweza hata kulala hapa na mkawa salama. Muhimu ni kuamka kabla hakujapambazuka mwende zenu”
“Unajua tuna hofu na wasiwasi, wenzetu wawili wameshauawa humu humu ndani”
“Sasa kule mtakaaje usiku huu na baridi? Je mvua ikinyesha usiku huu mtafanyaje. Si bora mlale hapa hapa”
“Ngoja nikawashauri wenzangu” nikamwambia Yasmin na kurudi kule ukumbini. Yasmin naye akanifuata.
“Yasmin amesema tusubiri chakula na pia tunaweza kulala hapa hapa” nikawambia wenzangu.
“Tulale hapa hapa?” Mtu mmoja akaniuliza kwa mshituko.
“Hakuna neno. Mnaweza kulala tu ilimradi muamke alfajiri kabla ya kupambazuka mwende zenu” Yasmin akawambia.
“Una hakika kwamba Harish hatakuja usiku huu?’
“Hatakuja tena kwa leo ila kesho anaweza kuja. Sasa kwa vile sijui atakuja saa ngapi ndio maana nninawambia muondoke alfajiri”
Yasmin alipoona wenzangu wameduwaa wakitazamana kutafakari yale maneno yake akatuambia.
“Jamani kuweni na mimi. Hivi nashukuru kupata wenzangu wa kunichangamsha. Harish hatakuja tena leo”
“Mimi naona tumsikilize mwenyeji wetu, acha tukae” Nikawambia wenzangu kwa kumuonea huruma Yasmin.
Pia huko tulikotaka kwenda hakukuwa salama. Tungeweza kushambuliwa na wanyama usiku ule au kunyeshewa na mvua.
Tukakubaliana kuwa tubaki na Yasmin.
“Hakuna lolote litakalotokea, kaeni kwa roho moja. Mimi ndiye ninayejua kawaida na nyendo za Harishi. Mnachotakiwa ni kujihimu wakati wa alfajiri muondoke humu ndani ili kama kesho atatokea asiwakute” Yasmin akatusisitizia kabla ya kurudi jikoni.
Baada ya muda kidogo alituletea chakula, tukala pamoja na yeye.
Tulipomaliza kula Yasmin aliondoa vyombo. Aliporudi tena alikuwa ameshika karata. Akaketi na kutuambia. “Sasa tuchezeni karata, tukichoka tunakwenda kulala”
ITAENDELEA
 
Back
Top Bottom