Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

SEHEMU YA 19



Nilijikuta nikiwa na furaha na mwenye matumaini kutokana na maneno ya Yasmin. Upendo aliouonesha kwangu ulitosha kunipa hamasa ingawa tulikuwa katika hali ngumu.
ENDELEA....
Nilipofika katika ile nyumba niliwakuta wenzangu tayari wameshaanza kupata wasiwasi.
“Ilibaki kidogo tu tukufuate kwa maana tuliona unachelewa” Haji akaniambia.
“Mlijua na mimi nimeshakwenda na maji?” nikawatania.
“Si ajabu. Haa tunahesabiana siku na saa tu”
“Tusikate tama kiasi hicho. sisi ni wanaume. Mmeshakula?”
“Tulikuwa tunakusubiri wewe” Shazume akaniambia.
“Mimi nimeshakuja. Toeni chakula tule”
Chakula kikatolewa. Tukakaa chini na kuanza kula.
Tulipomaliza kula tulikaa uani tukawasha moto na kuuzunguka. Kiza kilikuwa kimeshaingia na kulikuwa na baridi.
Tuliota moto hadi majira ya saa mbili usiku. Tukaingia vyumbani kulala. Usiku ule haukuwa wa mawazo sana. Nilipitiwa na usingizi mara moja.
Nilipoamka asubuhi nilishituka nilipoona mlango wa nje ulikuwa umeng’olewa mzima mzima. Palibaki uwazi mtupu. Mlango wa chumba alicholala Haji pia ulikuwa umeng’olewa. Mlango wa chumba cha Shazume ulikuwa mefungwa.
Nikaenda katika ule mlango wa chumba cha Haji na kuchungulia. Nilimkuta Haji akiwa amelala chini amekufa. Kichwa chake kilikuwa kimetobolewa kwenye utosi. Damu iliyoganda ilionekana kwenye nywele zake.
Hapo nilijua kuwa tulikuwa tumeingiliwa. Bila shaka Harishi alikuwa amekuja usiku akang’oa milango na kumuua Haji.
SASA ENDELEA
Lilikuwa tukio ambalo sikulitegemea. Katika kundi letu Haji ndiye aliyekuwa mdogo kuliko sote. Kifo chake kilinisikitisha na kunikatisha tamaa kabisa.
Nilijiambia kama Harishi ameweza kutufuata huku na kumuua Haji na sisi hatutabaki. Tilichokuwa tunasubiri ni siku na saa zetu ziwadie.
Baada ya kushangaa kwenye mlango kwa sekunde kadhaa nilikwenda kumgongea Shazume. Shazume akaamka na kufungua mlango.
“Una habari gani?” nikamuuliza nikiwa nimetaharuki.
“Sina habari yoyote” Shazume akanijibu huku akionesha kupata hofu.
“Haji ameuawa!” nikamwambia.
Shazume akagutuka.
“Haa! Haji naye ameuawa? Si tulilala naye humu ndani jana usiku?”
“Tazama ule mlango wa nje”
Nilimuonesha Haji ule mlango uliong’olewa kisha nikamwambia. “Harishi ameung’oa usiku”
Shazume aliutazama huku akitikisa kichwa.
“Ameng’oa na mlango wa chumba cha Haji” nikaendelea kumwambia.
Shazume akasogea kwenye mlango wa kilichokuwa chumba cha Haji. Alipoiona maiti ya Haji alishituka sana.
“Mimi naona hatutapona”
“Kupona tusitegemee ndugu yangu. Harishi ameshajua tupo hapa, usishangae kesho tukiamka mmoja wetu akawa hayupo!”
“Hapa nyumbani hapafai tena kukaa. Tutafute sehemu nyingine ya kujificha”
“Tutajificha wapi Shazume?”
“Popote tu, nyumba ziko nyingi”
“Sawa. Tumngoje Yasmin aje tumueleze kuwa mwenzetu ameuawa”
“Pia tumueleze kuwa tunaondoka hapa. Harishi akija tena asitukute”
“Sawa, tutamueleza”
Tukaenda kunawa uso na kusukutua maji bila kupiga mswaki. Tulikuwa tumeshachanganyikiwa. Tulipomaliza tulikaa kumsubiri Yasmin.
Yasmin alikuja majira ya saa tatu hivi. Hakuwa amechukua kitu.
Akatusalimia na kutuuliza kwanini tumeng’oa milango.
“Hebu chungulia kwenye hicho chumba” nikamwambia.
Yasmin akachungulia na kugutuka.
“Haji amepatwa na nini?”
“Haji ameuawa usiku na Harishi” nikamwambia.
“Mama yangu!” Yasmin alimaka huku akijishika kichwa. “Kumbe Harishi alipotoka usiku alikuja huku?”
“Sisi tumeona asubuhi Harishi ameuawa na milango imeng’olewa”
“Sasa tumepanga tuondoke hapa” Shazume akamwambia Yasmin.
“Muondoke muende wapi?”
“Twende mahali pengine. Tukiendelea kukaa hapa Harishi atakuja tena usiku”
“Sasa mmepanga muende wapi?’
“Mimi naona kama tunajisumbua, kama ni kufa tutakufa tu” nikasema.
“Hata kama tutakufa lakini hapa tuondoke” Shazume akasisitiza.
“Ni sawa. Sasa tufikirie hapo pa kwenda. Tutakwenda wapi?”
“Nyumba ziko nyingi”
“Yasmin unatushauri nini?”
Machozi yalikuwa yanamtoka Yasmin. Bila shaka yalimtoka kutokana na ukweli kwamba sote tutakufa. Hakunijibu.
“Yasmin usilie. Tunaomba ushauri wako” nikamwambia.
Yasmin alijifuta machozi kisha akatuambia. “Niwapeleke katika nyumba nyingine”
“Huko utakakotupeleka Harish hatafika?” nikamuuliza.
Yasmin akaguna kisha akajibu. Hatafika”
Nilijua alitujibu hivyo kututia moyo tu lakini mawazo ya Shazume yalikuwa tofauti.
“Ni mahali gani?” Shazume akamuuliza haraka.
“Kwanza twendeni mkanywe uji”
“Turudi kule tena?” Shazume akamaka.
“Mnakunywa uji tu halafu tunaondoka”
Shazume akanitazama.
“Mimi sitakwenda”
“Si tunakwenda kunywa uji tu” nikamwambia.
“Kwanza Harishi hatakuja muda huu” Yasmin akasema.
“Mimi sitaki uji”
“Utashinda hivyo hivyo na njaa?” Yasmin akamuuliza.
“Sioni njaa na ile hamu ya kula pia sina”
“Kama tumeandikiwa kuuawa tutauawa tu Shazume hata kama hutakula, ni bora ule tu” nikamwambia Shazume.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 19



Nilijikuta nikiwa na furaha na mwenye matumaini kutokana na maneno ya Yasmin. Upendo aliouonesha kwangu ulitosha kunipa hamasa ingawa tulikuwa katika hali ngumu.
ENDELEA....
Nilipofika katika ile nyumba niliwakuta wenzangu tayari wameshaanza kupata wasiwasi.
“Ilibaki kidogo tu tukufuate kwa maana tuliona unachelewa” Haji akaniambia.
“Mlijua na mimi nimeshakwenda na maji?” nikawatania.
“Si ajabu. Haa tunahesabiana siku na saa tu”
“Tusikate tama kiasi hicho. sisi ni wanaume. Mmeshakula?”
“Tulikuwa tunakusubiri wewe” Shazume akaniambia.
“Mimi nimeshakuja. Toeni chakula tule”
Chakula kikatolewa. Tukakaa chini na kuanza kula.
Tulipomaliza kula tulikaa uani tukawasha moto na kuuzunguka. Kiza kilikuwa kimeshaingia na kulikuwa na baridi.
Tuliota moto hadi majira ya saa mbili usiku. Tukaingia vyumbani kulala. Usiku ule haukuwa wa mawazo sana. Nilipitiwa na usingizi mara moja.
Nilipoamka asubuhi nilishituka nilipoona mlango wa nje ulikuwa umeng’olewa mzima mzima. Palibaki uwazi mtupu. Mlango wa chumba alicholala Haji pia ulikuwa umeng’olewa. Mlango wa chumba cha Shazume ulikuwa mefungwa.
Nikaenda katika ule mlango wa chumba cha Haji na kuchungulia. Nilimkuta Haji akiwa amelala chini amekufa. Kichwa chake kilikuwa kimetobolewa kwenye utosi. Damu iliyoganda ilionekana kwenye nywele zake.
Hapo nilijua kuwa tulikuwa tumeingiliwa. Bila shaka Harishi alikuwa amekuja usiku akang’oa milango na kumuua Haji.
SASA ENDELEA
Lilikuwa tukio ambalo sikulitegemea. Katika kundi letu Haji ndiye aliyekuwa mdogo kuliko sote. Kifo chake kilinisikitisha na kunikatisha tamaa kabisa.
Nilijiambia kama Harishi ameweza kutufuata huku na kumuua Haji na sisi hatutabaki. Tilichokuwa tunasubiri ni siku na saa zetu ziwadie.
Baada ya kushangaa kwenye mlango kwa sekunde kadhaa nilikwenda kumgongea Shazume. Shazume akaamka na kufungua mlango.
“Una habari gani?” nikamuuliza nikiwa nimetaharuki.
“Sina habari yoyote” Shazume akanijibu huku akionesha kupata hofu.
“Haji ameuawa!” nikamwambia.
Shazume akagutuka.
“Haa! Haji naye ameuawa? Si tulilala naye humu ndani jana usiku?”
“Tazama ule mlango wa nje”
Nilimuonesha Haji ule mlango uliong’olewa kisha nikamwambia. “Harishi ameung’oa usiku”
Shazume aliutazama huku akitikisa kichwa.
“Ameng’oa na mlango wa chumba cha Haji” nikaendelea kumwambia.
Shazume akasogea kwenye mlango wa kilichokuwa chumba cha Haji. Alipoiona maiti ya Haji alishituka sana.
“Mimi naona hatutapona”
“Kupona tusitegemee ndugu yangu. Harishi ameshajua tupo hapa, usishangae kesho tukiamka mmoja wetu akawa hayupo!”
“Hapa nyumbani hapafai tena kukaa. Tutafute sehemu nyingine ya kujificha”
“Tutajificha wapi Shazume?”
“Popote tu, nyumba ziko nyingi”
“Sawa. Tumngoje Yasmin aje tumueleze kuwa mwenzetu ameuawa”
“Pia tumueleze kuwa tunaondoka hapa. Harishi akija tena asitukute”
“Sawa, tutamueleza”
Tukaenda kunawa uso na kusukutua maji bila kupiga mswaki. Tulikuwa tumeshachanganyikiwa. Tulipomaliza tulikaa kumsubiri Yasmin.
Yasmin alikuja majira ya saa tatu hivi. Hakuwa amechukua kitu.
Akatusalimia na kutuuliza kwanini tumeng’oa milango.
“Hebu chungulia kwenye hicho chumba” nikamwambia.
Yasmin akachungulia na kugutuka.
“Haji amepatwa na nini?”
“Haji ameuawa usiku na Harishi” nikamwambia.
“Mama yangu!” Yasmin alimaka huku akijishika kichwa. “Kumbe Harishi alipotoka usiku alikuja huku?”
“Sisi tumeona asubuhi Harishi ameuawa na milango imeng’olewa”
“Sasa tumepanga tuondoke hapa” Shazume akamwambia Yasmin.
“Muondoke muende wapi?”
“Twende mahali pengine. Tukiendelea kukaa hapa Harishi atakuja tena usiku”
“Sasa mmepanga muende wapi?’
“Mimi naona kama tunajisumbua, kama ni kufa tutakufa tu” nikasema.
“Hata kama tutakufa lakini hapa tuondoke” Shazume akasisitiza.
“Ni sawa. Sasa tufikirie hapo pa kwenda. Tutakwenda wapi?”
“Nyumba ziko nyingi”
“Yasmin unatushauri nini?”
Machozi yalikuwa yanamtoka Yasmin. Bila shaka yalimtoka kutokana na ukweli kwamba sote tutakufa. Hakunijibu.
“Yasmin usilie. Tunaomba ushauri wako” nikamwambia.
Yasmin alijifuta machozi kisha akatuambia. “Niwapeleke katika nyumba nyingine”
“Huko utakakotupeleka Harish hatafika?” nikamuuliza.
Yasmin akaguna kisha akajibu. Hatafika”
Nilijua alitujibu hivyo kututia moyo tu lakini mawazo ya Shazume yalikuwa tofauti.
“Ni mahali gani?” Shazume akamuuliza haraka.
“Kwanza twendeni mkanywe uji”
“Turudi kule tena?” Shazume akamaka.
“Mnakunywa uji tu halafu tunaondoka”
Shazume akanitazama.
“Mimi sitakwenda”
“Si tunakwenda kunywa uji tu” nikamwambia.
“Kwanza Harishi hatakuja muda huu” Yasmin akasema.
“Mimi sitaki uji”
“Utashinda hivyo hivyo na njaa?” Yasmin akamuuliza.
“Sioni njaa na ile hamu ya kula pia sina”
“Kama tumeandikiwa kuuawa tutauawa tu Shazume hata kama hutakula, ni bora ule tu” nikamwambia Shazume.
ITAENDELEA
Shazume Is the Next target...
 
@wastendi umemuona mwanaume mwenzetu huyu anatumia ID ya kike ili anaingize watu mkenge?
We nae hebu acha kujiona kisa unaleta hadithi watu wanafatilia kua na kauli nzuri na si lazima umjibu kila mtu.... huyo MADAME ni mwanamke unless uwe mgeni wa JF.... ndio maana The Bold anakua juu kwenu sababu ya vitu hivi huwezi kumkuta anabishana na wasomaji wake.

Sorry ila hua nachukia kuona Mtoto wa kiume anajibizana na Mwanamke.
 
Nashangaa mpaka wanabaki wawili wanashindwa kumvizia anapokuja waifunge chupa. Anyways, ndo watakachofanya.
 
We nae hebu acha kujiona kisa unaleta hadithi watu wanafatilia kua na kauli nzuri na si lazima umjibu kila mtu.... huyo MADAME ni mwanamke unless uwe mgeni wa JF.... ndio maana The Bold anakua juu kwenu sababu ya vitu hivi huwezi kumkuta anabishana na wasomaji wake.

Sorry ila hua nachukia kuona Mtoto wa kiume anajibizana na Mwanamke.
wee tulia hauhusiki na hili battle naongea na Madame S
wee haikuhusu
 
SEHEMU YA 20



Shazume akatikisa kichwa bila kusema lolote.
“Kakangu najua umepatwa na fadhaa lakini tumbo lako likipata riziki ndio akili itakuja” Yasmin akamwambia Shazume.
“Tulikuwa watu saba sasa tumebaki wawili tu bado nile? Sitakula!”
“Wewe ni mwanaume Shazume usiogope kula. Unatakiwa upambane mpaka dakika ya mwisho. Mnaweza kuokoka ndugu zangu. Msikate tama kiasi hicho. Twende ukanywe uji japo kidogo!” Yasmin alimwambia.
Shazume akakubali kwenda. Tukaondoka sote kwenda kwa Yasmin. Ile maiti ya Haji tuliiacha pale pale. Tangu wenzetu walivyoanza kuuawa hatukuzika maiti yoyote. Zote tuliziacha ziliwe na kunguru.
Kwa hisia zetu tulikuwa kama watu tuliokuwa vitani. Akifa mtu hakuna kuzika. Kuzika kuna utaratibu wake ambao kutokana na hali tuliyokuwa nayo tusingeuweza.
Tulipofika kwa Yasmin alituandalia uji tukanywa. Mimi nilikunywa vikombe viwili, Shazume alikunywa kikombe kimoja.
Wakati tumepumzika Shazume akawa anahimiza tuondoke.
“Tumeshakunywa uji sasa tunaweza kwenda”
“Tusubiri kidogo nifikirie pa kuwapeleka” Yasmin akamwambia.
SAS ENDELEA
Baada ya kusubiri kwa muda kidogo Yasmin akatuambia. “Haya twendeni tukatafute nyumba nyingine”
Tukatoka na Yasmin. Niliona wazi kuwa Yasmin alikuwa na wasiwasi. Alikuwa akitupeleka katika nyumba nyingine lakini hakuwa mtu aliyeonesha matumaini.
Tulizunguka sana kutafuta nyumba nyingine ambayo ingeweza kutufaa kumkwepa Harishi. Tulikuta nyumba moja iliyokuwa ufukweni mwa bahari iliyokuwa na hali nzuri kidogo.
“Mnaionaje nyumba hii?” Yasmin akatuuliza huku akituonesha nyumba hiyo.
“Hii inafaa” nikamwambia kisha nikamtazama Shazume ili nipate mawazo yake.
“Unaionaje Shazume?”
“Hapa pamejificha kidogo, panafaa” akaniambia ingawa sauti yake haikuwa na nguvu.
Tukaingia katika ile nyumba. Humo ndani ilikuwa kama stoo iliyosahauliwa. Vitu vilikuwa vimerundikwa ovyo. Ubuibui na vumbi vilikuwa vimetanda pande zote.
Binaadamu mwenye akili zake timamu asingeweza kukaa ndani ya nyumba ile labda waduu kama vile nyoka na matandu. Lakini sisi hatukuwa timamu. Tulikuwa tumetingwa. Tungeweza kukaa.
Kama tungehitaji kufanya usafi ili nyumba hiyo iweze kukalika tungelazimika kutoa nje vitu vyote vilivyokuwa ndani na kuanza kufagia, kupiga deki na kusafisha kuta. Ingekuwa kazi kubwa. Ingetuchukua hata kwa siku mbili.
Tuliingia katika chumba kimoja tukatenga vitu na kupata upenyu mdogo ambao tuliusafisha na kuamua kukaa hapo.
Kusema kweli siku ile sisi sote hatukuwa na furaha. Tulikaa chini pamoja na Yasmin. Tukawa kimya. Kila mtu akiwaza lake.
Mimi nilkuwa nikiomba usiku usifike kwani karibu wenzetu wote waliuawa usiku.
Sikujua Yasmin na Shazume walikuwa wakiwaza nini. Lakini kila nilivyomuangalia Shazume niliona mawazo yake yalikuwa mbali sana. Nilikisia kwamba alikuwa akikumbuka kwao Pemba, akiwakumbuka wazazi wake na ndugu zake. Pengine hakuwa na matumaini ya kuwaona tena.
Bila shaka Yasmin alikuwa akiwaza kama tutauawa atakosa wenzake wa kuzungumza nao na ataendelea kuwa mkiwa.
Mimi licha ya kuwa na hofu nlishajitolea kufa kupona. Sikupenda kujipa tama moja kwa moja kuwa nitapona na sikutaka kujikatia tama.
Ghafla Shazume akaanza kuimba kwa sauti ya huzuni. Ulikuwa wimbo maarufu uliokuwa unaimbwa na vikundi vya ngoma za kiasili.
“We Yauledi we niletee mashua twende Unguja!. We Yauledi niletee mashua twende Unguja!”
Na mimi nikamuitikia. “Ukipamba mke nawe ujipambe ndio suna. Usipojipamba watu hukwambia umtumwa! We Yauledi niletee mashua twende Unguja!”
Shazume aliendelea kuimba ubeti wake kwa kughani huku na mimi nikimuitikia.
Sauti ya wimbo huo ilikuwa ya huzuni lakini ilituchangamsha. Yasmin alikuwa akitutazama. Wakati ninamuitikia Shazume, Yasmin alikuwa akinifuatisha ninavyoimba.
Pengine tulikuwa tunajifariji kwa siku yetu ya mwisho kwani tangu tufike katika kisiwa kile, kila siku mwenzetu mmoja aliuawa na Harishi. Hakukuwa na siku yoyote ambayo hakukutokea kifo.
Kwa hiyo hatukujua usiku wa siku ile atakufa nani kati yangu na Shazume.
Shazume aliendelea kuimba kwa huzuni. Mimi nilikuwa nimenyamaza. Yasmin akawa anamuitikia.
Shazume alipoona mimi nimenyamaza na yeye akaacha kuimba tukawa kimya. Baada ya muda kidogo nilipata wazo.
“Tuombeni dua” nikawambia wenzangu.
“Tulikuwa tumejisahau kidogo” Shazume akasema
Nikasoma dua ndefu. Shazume na Yasmin wakawa wanaitikia “Amin”
Nilipomaliza nilimwambia Shazume aombe na yeye. Shazume akaomba dua ndefu, sisi tukamuitikia “Amin”
Alipomaliza nikamwambia Yasmin. “Omba na wewe”
ITAENDELEA
 
We nae hebu acha kujiona kisa unaleta hadithi watu wanafatilia kua na kauli nzuri na si lazima umjibu kila mtu.... huyo MADAME ni mwanamke unless uwe mgeni wa JF.... ndio maana The Bold anakua juu kwenu sababu ya vitu hivi huwezi kumkuta anabishana na wasomaji wake.

Sorry ila hua nachukia kuona Mtoto wa kiume anajibizana na Mwanamke.
achana naye tu mwenyew nimempotezea
 
Back
Top Bottom