Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

16831207_1899205690105785_140789355008334865_n.jpg

MTUNZI : FAKI A FAKI


Sikuwahi kuona sherehe kubwa ya harusi kama ile niliyoiona katika visiwa vya Ngazija nchini Comoro mwaka mmoja uliopita.
Ilikuwa harusi ya binti wa Rais wa Moroco Yasmini binti Sharif Abdilatif aliyekuwa akolewa na mwana wa mkuu wa majeshi ya ulinzi wa Comoro
Abubakar Mustafa Al- Shiraz aliyekuwa akiishi Ufaransa.
Sisi tulikuwa tumetoka Zanzibar. Mke wa mkuu wa majeshi ya Comoro Kulthum alikuwa Mzanzibari tena Mkojani wa Pemba, ndiye aliyetoa mwaliko kwa ndugu zake walioko Zanzibar.
Zilitolewa kadi kumi za mwaliko kwa watu kumi. Kwa vile na mimi nilikuwa na nasaba na Kulthum nikapata kadi moja na tiketi ya ndege ya kwenda Ngazija.
Wakati ule nilikuwa na umri wa miaka ishirini na minne(24). Nilikuwa bado kijana na shughuli zangu zilikuwa ni uvuvi. Nilikuwa sijaoa bado lakini nilikuwa katika maandalizi ya kutafuta mchumba.
Ndege tuliyosafiri nayo ilifika Comoro saa kumi jioni. Ndoa ilikuwa inafungwa saa mbili usiku baada ya swala ya Inshaa katika msikiti wa Riadha, msikiti mkuu wa Ijumaa nchini humo.
Nyumbani kwa bwana harusi kulikuwa kumejaa shamra shamra. Kadhalika nyumbani kwa Rais Sharif Abdulatif nako kulikuwa hakutoshi.
Kulikuwa na hoteli mbili kubwa zilizokodishwa siku ile kwa ajili ya sherehe za harusi. Na kulikuwa na hoteli nyingine kadhaa zilizokodiwa kwa ajili ya wageni walioalikwa kutoka nchi mbalimbali.
Sisi tulifikia katika hoteli ya Zaharani. Jina la hoteli hiyo lilifanana na jina langu. Jina langu ni Zaharani Shazume. Hoteli hiyo ilikuwa jirani na msikiti wa Riadha mahali ambapo ndoa ya Yasmin na Abubakar ingefungwa usiku ule.
Kwa kawaida msikiti wa ijumaa hujaa watu siku za ijumaa lakini siku ile kwa mara ya kwanza ulijaa watu katika swala ya Inshaa.
Kulikuwa na ulinzi mkali wa polisi na maafisa usalama waliokuwa na kazi ya kuhakikisha usalama unakuwepo katika eneo hilo.
Nilijitahidi sana nipate safu ya mbele lakini sikuweza. Safu hiyo ilikuwa imejaa masheikh na maafisa usalama. Nilibahatika kupata safu ya tatu yake.
Baadaya swala ya isha Rais wa Comoro Sharif Abdulatif alitakiwa kutoa idhini ya kumuozesha mwanawe.
Wakati anatoa idhini alipokea simu hapo hapo iliyomtambulisha kuwa binti yake Yasmin alikuwa ameanguka nyumbani na alikuwa akitokwa na povu mdomoni.
Shughuli ya ufungishaji ndoa ikasimama. Hapo hapo Rais Abdulatif na wasaidizi wake pamoja na maafisa usalama walitoka kwenda nyumbani.
Habari iliyopatikana baadaye ilieleza kuwa Yasmini alikuwa ameanguka na kupoteza fahamu huku akitokwa na povu midomoni. Baba yake alipofika na kumuona aliamrisha apelekwe hospitali haraka.
Gari la hospitali lilikuwa limeshafika. Yasmin alipakiwa na kukimbizwa hospitali. Gari hilo la hospitali lilifuatana na gari la maafisa usalama na gari la rais mwenyewe.
Lakini gari alilopakiwa Yasmin likapata ajali kabla ya kufika hospitali. Tairi lake la mbele la upande wa kulia lilipasuka na kusababisha gari hilo kuyumba na kuligonga gari jingine kabla ya kupindukia kwenye mtaro uliokuwa kando ya barabara.
Heka heka ikawa kubwa!. Magari ya maafisa usalama yakasimama. Maafisa hao wakashuka na kukimbilia kutoa msaada. Dereva wa gari la hospitali alipotolewa alikutwa akiwa ameshakufa. Yasmin mwenyewe hakuonekana. Wauguzi wawili waliokuwa naye walikutwa wamezirai. Tukio hilo lilizua taharuki kubwa.
Rais Abdulatif hakuamini macho yake, akawa anauliza kwa ukali “Binti yangu yuko wapi?”
Lakini hakukuwa na aliyejua. Yasmin alikuwa ametoweka ghafla. Kila aliyeshuhudia alishangaa.
Harusi ikavunjika. Badala ya furaha sasa ikawa huzuni. Bwana harusi na mke wa Rais Sharif Abdullatif Bi Kulthum
walikuwa wanalia kutokana na muujiza huo.
Usiku ule ule Rais Abdullatif aliita masheikh Ikulu na kuwauliza kama walikuwa wanajua kilichomtokea binti yake.
Kila sheikh alisema lake. Wako waliomwambia kuwa binti yake alikuwa amechukuliwa na wachawi. Wako waliomwambia kuwa haikuwa muafaka kwa binti yake kuolewa na Abubakar ndiyo sababu tukio hilo limetokea. Na wako waliomwambia kuwa Yasmin alikuwa amechukuliwa na jini aliyekuwa amemchunuka.
Rais Abdullatif hakujua ashike kauli ya sheikh yupi. Kwa vile lilikuwa limeshamfika alikubaliana na masheikh wote na kuwataka masheikh hao kutumia elimu zao kumrudisha binti yake. Aliahidi mamilioni ya shilingi za ki Comoro kwa sheikh yeyote atakayefanikiwa kumrudisha Yasmin.
Licha ya Rais Abdullatif kusubiri kwa zaidi ya miezi mitatu. Hakukuwa na sheikh yeyote aliyefanikiwa kumrudisha Yasmin! Yasmin akabaki kuwa historia kwani hakupatikana tena. Ulikuwa msiba ambao kila mkazi wa Comro alihisi kuwa hautasahaulika.
Hivi sasa mwaka mmoja umeshapita tangu tukio hilo la kuhuzunisha litokee. Tangu wakati ule sikuwahi tena kurudi Moroco. Nilikuwa Unguja nikiendelea na shughuli zangu za uvuvi.
Sasa siku moja ambayo sitaisahau maishani mwangu tulikuwa kwenye boti letu tukielekea maji makuu kuvua samaki. Ndani ya boti hilo tulikuwa wavuvi saba.
Ilipofika saa nne asubuhi tulikuwa mbali sana. Boti yetu ilipigwa na dharuba kali. Mashine ya boti ikazima ghafla. Tilijaribu kuiwasha lakini boti haikuwaka. Ikawa inakokotwa na maji.
Tulipumzika kidogo kisha tulijaribu kuiwasha tena na tena lakini hatukufanikiwa kuiwasha Mashine ilitugomea kabisa. Hatukujua ilikuwa imepatwa na hitilafu gani.
Je nini kitawatokea wavuvi hao?
Wavuci hao ni wajinga sana, walikosaje backup ss hata ya kutumia tanga km hawakuweza kua na machine nyingine, pumbavu zao
 
Yaani wanakaribia kufa na bado wanapatwa na muda wa kutongozana na kutiana nyege... hao wavuvi mawhack kweli.
 
SEHEMU YA 15


Wenzangu wote walikuwa na wake zao isipokuwa mimi lakini Masudi alisema alioa kisha aliachana na mke wake. Nilichokuwa nakijua mimi ni kuwa Masudi alikuwa na mke wake.
Sikujua ni kwanini Yasmin alituuliza vile.
“Kwa hiyo wewe na Masudi ndio hamna wake?” Yasmin akaniuliza.
“Ninachojua mimi Masudi anaye mke” nilimwambia Yasmin.
Kauli ile ilimkera Masudi.
“Nina mke mimi?” Masudi akaniuliza kwa ukali kidogo.
“Unaye!” nikamwambia kwa mkazo.
“Mke si nilishamuacha?. Au wewe ulikuwa hujui?”
“Mimi najua watania tu lakini mke bado unaye”
“Basi na yaishe. Mimi niliuliza tu kutaka kujua. Kama unaye mke au huna hakuna tatizo” Yasmin akaingilia kati.
“Huyu bwana mdogo anapenda sana kuniingilia!” Masudi akaunguruma.
Nikaamua kunyamaza.
“Nimesema yaishe jamani. Ngoja tulete karata tucheze”
SASA ENDELEA
Yasmin alitumia hekima kuyageuza yale mazungumzo akaenda kuleta karata, tukawa tunacheza.
“Hivi hizi karata ulikuwa unacheza na nani?” nikamuuliza Yasmin wakati tunacheza.
“Ninacheza na huyo aliyezileta”
“Harishi?”
“Ndiye huyo huyo. Anapoona nimepooza ananiambia kalete karata”
“Anajua kucheza karata?” akaulizwa na Masudi.
“Anajua. Hawa majini ni kama watu tu. Tofauti yetu ni ndogo sana. Wanafanya mambo mengi wanayofanya binaadamu”
Mazungumzo ya Harishi yalitufanya tukose amani. Yalitukumbusha wenzetu waliouawa. Mwenzetu mmoja lakini si Masudi akatuambia.
“Tuondoke twende kule tulikohamia”
“Chukueni hizo karata mwende nazo. Mtakwenda kucheza huko huko” Yasmin akatuambia.
Ilibidi tuondoke twende katika ile nyumba lakini Yasmin tulimuacha.
Tulipofika tuliendelea kucheza karata. Baadaye sote tulipitiwa na usingizi tukalala.
Tuliamshana jioni tukaamua tutoke twende tukatembee tembee. Tulizunguka sana katika kile kisiwa. Tulienda pia kuliangalia jahazi letu. Tuliporudi jua lilikuwalimeshakuchwa.
Tulimkuta Yasmin akitusubiri. Alikuwa ametuletea chakula cha jioni.
“Mnatoka wapi?” akatuuliza.
“Tulikwenda kutembea tembea kidogo” Masudi akamjibu na kuongeza “Kukaa tu kunachosha”
“Umetuletea chakula?” nikamuuliza Yasmin.
“Nimewaletea kabisa. Ikifika usiku sitaweza kuja huku. Harishi anaweza kuja wakati wowowte” Yasmin alituambia na kutuwekea chakula hicho juu ya meza.
“Ngoja nikusindikize” Masudi akawahi kumwambia Yasmin. Nilijua alitaka kunipiku mimi kwani alijua mimi ndiye ningemsindikiza.
Yasmin akakubali kuondoka na Masudi. Kwa upande wangi kitendo kile cha Masudi nilikiona kama ulimbukeni uliopitiliza na kutaka kujipendekeza kwa Yasmin.
Walipoondoka sisi tulikaa barazani mwa ile nyumba hadi giza likaingia.
“Mbona masudi harudi?” Tukawa tunaulizana.
Kusema kweli kitendo chake cha kuchelewa kurudi kilinikera. Nikaamua nimfuate peke yangu nijua alikuwa anafanya nini muda wote huo.
Nikaenda huku nikiwa na hasira. Nilipofika sikuingia ndani. Niliamua kufanya upelelezi kwa kuchungulia kwenye madirisha.
Wakati nachungulia niliana kusikia sautiya Yasmin ikiwa katika dhihaka, mwenyewe sikumuon. Nilibadilisha dirisha na ndipo nilipowaona wote wawili. Masudi alikuwa akikimbizana na Yasmin mle ndani kam waliokuwa wakicheza. Wakati mwingine Masudi alimkamata Yasmin na kuanguka naye chini akiwa amemshika kiuno.
“Kumbe wana mchezo huu, ndio maana amesahau kurudi” nikajisemea kimoyo moyo.
Licha ya moyo wangu kuuma nilijiambia chaguo la Yasmin ni mimi, Masudi alikuwa akijipendekeza tu.
Macho yangu yaliwashuhudia wakiwa wamelala chini. Masudi alikuwa kama akibembeleza kitu kwa Yasmin. Yasmin alikuwa ametulia akimsikiliza.
Sikuweza kufikiria chochote zaidi ya kuhisi kuwa Masudi alikuwa akimtongoza Yasmin na alikuwa akinifitini mimi.
Sikutaka tena kuuona upumbvu wake. Nikaamua kuondoka kwani usiku ulikuwa unazidi kushamiri.
Yasmin haweza kumkubali Masudi, Yasmin amenipenda mimi, nilijiambia kujifariji wakati naondoka.
Nilirudi kwa wenzangu huku nikiuzuia moyo wangu usitaharuki kutokana na kitendo kile nilichokiona kwa Masudi kumkumbatia Yasmin.
“Umemkuta?” Wenzangu wakaniuliza.
“Sikufika” nkawadanganya. “Nimeamua kurudi njiani, naona usiku mwingi huu”
“Au twendeni sote?” Mmoja akaniuliza.
“Tumsubirini tu hapa hapa”
Sikutaka kuwambia ukweli kuwa nilimkuta akifanya vitendo vya kipuuzi. Nilihisi wangeweza kuja kumwambia mwenyewe halafu kwa akili za Masudi tunaweza kugombana bure.
Tukakaa kumsubiri hadi saa tatu. Tulipoona hatokeai tuliamua kula chakula na kumbakishia chake.
Nilikuwa nimebaki na wenzangu wawili Shazume na Haji. Kwa upande wangu nilishakijua kilichokuwa kinamchelewesha Masudi lakini wenzangu walikuwa na wasiwasi kwamba huenda Masudi amepata matatizo.
Walikuwa wakisisitiza kuwa twende tukamuangalie.
“Kutoka usiku huu si vizuri” nikawambia. “Acheni tungoje kesho asubuhi tutakwenda kumuangalia”
ITAENDELEA
 
Vijistori vy a kukopi bana
Fanya kama utani tu ndugu mimi siku hizi nipo diriaz sichekagi kifalafala shauri yako.Hata yule lofa mwenzako anayejiita Mikwara Ya Andunje anichekeshi kwa lolote.
Mtu ambaye anaweza kunichekesha ni @chaliifransisko na Mr Miller pekee nyie wengine malofa tu
 
Afadhali mimi mkuu hivi ulishawahi kusimuliwa story na bibi yako au na masela wako halafu ukawa unakaa nayo tu kichwani bila kuwasimulia watu wengine?
Weee mwenyewe habari nyingi unazitafsiri kwa masaada wa Wikipedia
Mara nyingi natumia Wikipedia coz ndio inataarifa ya vitu vingi "dhambi kutumia Wikipedia? Sio nazitafsiri Bali nazipata kwa msaada Wa Wikipedia
 
Mara nyingi natumia Wikipedia coz ndio inataarifa ya vitu vingi "dhambi kutumia Wikipedia? Sio nazitafsiri Bali nazipata kwa msaada Wa Wikipedia
Fanya kama utani tu ndugu mimi siku hizi nipo diriaz sichekagi kifalafala shauri yako.Hata yule lofa mwenzako anayejiita Mikwara Ya Andunje anichekeshi kwa lolote.
Mtu ambaye anaweza kunichekesha ni @chaliifransisko na Mr Miller pekee nyie wengine malofa tu
 
Fanya kama utani tu ndugu mimi siku hizi nipo diriaz sichekagi kifalafala shauri yako.Hata yule lofa mwenzako anayejiita Mikwara Ya Andunje anichekeshi kwa lolote.
Mtu ambaye anaweza kunichekesha ni @chaliifransisko na Mr Miller pekee nyie wengine malofa tu
Hahaaa kwahiyo una wary wajo special Wa kukuchekesha?
 
16831207_1899205690105785_140789355008334865_n.jpg

MTUNZI : FAKI A FAKI


Sikuwahi kuona sherehe kubwa ya harusi kama ile niliyoiona katika visiwa vya Ngazija nchini Comoro mwaka mmoja uliopita.
Ilikuwa harusi ya binti wa Rais wa Moroco Yasmini binti Sharif Abdilatif aliyekuwa akolewa na mwana wa mkuu wa majeshi ya ulinzi wa Comoro
Abubakar Mustafa Al- Shiraz aliyekuwa akiishi Ufaransa.
Sisi tulikuwa tumetoka Zanzibar. Mke wa mkuu wa majeshi ya Comoro Kulthum alikuwa Mzanzibari tena Mkojani wa Pemba, ndiye aliyetoa mwaliko kwa ndugu zake walioko Zanzibar.
Zilitolewa kadi kumi za mwaliko kwa watu kumi. Kwa vile na mimi nilikuwa na nasaba na Kulthum nikapata kadi moja na tiketi ya ndege ya kwenda Ngazija.
Wakati ule nilikuwa na umri wa miaka ishirini na minne(24). Nilikuwa bado kijana na shughuli zangu zilikuwa ni uvuvi. Nilikuwa sijaoa bado lakini nilikuwa katika maandalizi ya kutafuta mchumba.
Ndege tuliyosafiri nayo ilifika Comoro saa kumi jioni. Ndoa ilikuwa inafungwa saa mbili usiku baada ya swala ya Inshaa katika msikiti wa Riadha, msikiti mkuu wa Ijumaa nchini humo.
Nyumbani kwa bwana harusi kulikuwa kumejaa shamra shamra. Kadhalika nyumbani kwa Rais Sharif Abdulatif nako kulikuwa hakutoshi.
Kulikuwa na hoteli mbili kubwa zilizokodishwa siku ile kwa ajili ya sherehe za harusi. Na kulikuwa na hoteli nyingine kadhaa zilizokodiwa kwa ajili ya wageni walioalikwa kutoka nchi mbalimbali.
Sisi tulifikia katika hoteli ya Zaharani. Jina la hoteli hiyo lilifanana na jina langu. Jina langu ni Zaharani Shazume. Hoteli hiyo ilikuwa jirani na msikiti wa Riadha mahali ambapo ndoa ya Yasmin na Abubakar ingefungwa usiku ule.
Kwa kawaida msikiti wa ijumaa hujaa watu siku za ijumaa lakini siku ile kwa mara ya kwanza ulijaa watu katika swala ya Inshaa.
Kulikuwa na ulinzi mkali wa polisi na maafisa usalama waliokuwa na kazi ya kuhakikisha usalama unakuwepo katika eneo hilo.
Nilijitahidi sana nipate safu ya mbele lakini sikuweza. Safu hiyo ilikuwa imejaa masheikh na maafisa usalama. Nilibahatika kupata safu ya tatu yake.
Baadaya swala ya isha Rais wa Comoro Sharif Abdulatif alitakiwa kutoa idhini ya kumuozesha mwanawe.
Wakati anatoa idhini alipokea simu hapo hapo iliyomtambulisha kuwa binti yake Yasmin alikuwa ameanguka nyumbani na alikuwa akitokwa na povu mdomoni.
Shughuli ya ufungishaji ndoa ikasimama. Hapo hapo Rais Abdulatif na wasaidizi wake pamoja na maafisa usalama walitoka kwenda nyumbani.
Habari iliyopatikana baadaye ilieleza kuwa Yasmini alikuwa ameanguka na kupoteza fahamu huku akitokwa na povu midomoni. Baba yake alipofika na kumuona aliamrisha apelekwe hospitali haraka.
Gari la hospitali lilikuwa limeshafika. Yasmin alipakiwa na kukimbizwa hospitali. Gari hilo la hospitali lilifuatana na gari la maafisa usalama na gari la rais mwenyewe.
Lakini gari alilopakiwa Yasmin likapata ajali kabla ya kufika hospitali. Tairi lake la mbele la upande wa kulia lilipasuka na kusababisha gari hilo kuyumba na kuligonga gari jingine kabla ya kupindukia kwenye mtaro uliokuwa kando ya barabara.
Heka heka ikawa kubwa!. Magari ya maafisa usalama yakasimama. Maafisa hao wakashuka na kukimbilia kutoa msaada. Dereva wa gari la hospitali alipotolewa alikutwa akiwa ameshakufa. Yasmin mwenyewe hakuonekana. Wauguzi wawili waliokuwa naye walikutwa wamezirai. Tukio hilo lilizua taharuki kubwa.
Rais Abdulatif hakuamini macho yake, akawa anauliza kwa ukali “Binti yangu yuko wapi?”
Lakini hakukuwa na aliyejua. Yasmin alikuwa ametoweka ghafla. Kila aliyeshuhudia alishangaa.
Harusi ikavunjika. Badala ya furaha sasa ikawa huzuni. Bwana harusi na mke wa Rais Sharif Abdullatif Bi Kulthum
walikuwa wanalia kutokana na muujiza huo.
Usiku ule ule Rais Abdullatif aliita masheikh Ikulu na kuwauliza kama walikuwa wanajua kilichomtokea binti yake.
Kila sheikh alisema lake. Wako waliomwambia kuwa binti yake alikuwa amechukuliwa na wachawi. Wako waliomwambia kuwa haikuwa muafaka kwa binti yake kuolewa na Abubakar ndiyo sababu tukio hilo limetokea. Na wako waliomwambia kuwa Yasmin alikuwa amechukuliwa na jini aliyekuwa amemchunuka.
Rais Abdullatif hakujua ashike kauli ya sheikh yupi. Kwa vile lilikuwa limeshamfika alikubaliana na masheikh wote na kuwataka masheikh hao kutumia elimu zao kumrudisha binti yake. Aliahidi mamilioni ya shilingi za ki Comoro kwa sheikh yeyote atakayefanikiwa kumrudisha Yasmin.
Licha ya Rais Abdullatif kusubiri kwa zaidi ya miezi mitatu. Hakukuwa na sheikh yeyote aliyefanikiwa kumrudisha Yasmin! Yasmin akabaki kuwa historia kwani hakupatikana tena. Ulikuwa msiba ambao kila mkazi wa Comro alihisi kuwa hautasahaulika.
Hivi sasa mwaka mmoja umeshapita tangu tukio hilo la kuhuzunisha litokee. Tangu wakati ule sikuwahi tena kurudi Moroco. Nilikuwa Unguja nikiendelea na shughuli zangu za uvuvi.
Sasa siku moja ambayo sitaisahau maishani mwangu tulikuwa kwenye boti letu tukielekea maji makuu kuvua samaki. Ndani ya boti hilo tulikuwa wavuvi saba.
Ilipofika saa nne asubuhi tulikuwa mbali sana. Boti yetu ilipigwa na dharuba kali. Mashine ya boti ikazima ghafla. Tilijaribu kuiwasha lakini boti haikuwaka. Ikawa inakokotwa na maji.
Tulipumzika kidogo kisha tulijaribu kuiwasha tena na tena lakini hatukufanikiwa kuiwasha Mashine ilitugomea kabisa. Hatukujua ilikuwa imepatwa na hitilafu gani.
Je nini kitawatokea wavuvi hao?
Umezungumzia Comoro hapo mwisho unasema hurudi tena Moroco!Hapo ndo umeniacha sasa!
 
Back
Top Bottom