Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

hii kitu haiishi hamu kuitia ubongoni, ahsante sana mr kanungila kwa kutuletea hii kitu
 
SEHEMU YA 11



Akagawa karata, tukacheza hadi usiku mwingi. Wenzangu wengine walikuwa wameshaanza kusinzia. Tukavunja mchezo na kwenda kulala.
Tuliingia katika vyumba viwili. Chumba kimoja waliingia watu wawili na chumba kingine waliingia watu watatu. Mmoja aliweka godoro chini. Mimi nilikuwemo katika kile chumba walichongia watu watatu. Nililala kitandani. Na mwenzetu mmoja ndio alilala chini.
Licha ya Yasmin kututoa wasiwasi kuwa Harishi hatatokea usiku ule, hatukulala kwa raha. Mara kwa mara nilikabiliwa na hofu. Nilipolala kidogo nilijikuta ninagutuka na kutupa macho huku na huku.
Wakati inakaribia kuwa alfajiri ndipo nilipopata usingizi wa uhakika. Nikalala moja kwa moja. Sikuzinduka mpaka kumekucha. Kilichonizindua ni hisia zangu. Niliona kama mlango wa mle chumbani unafunguliwa na mtu aliyekuwa nje.
Nilipofumbua macho niliona kweli mlango unafunguliwa na kulikuwa kumeshakucha ingawa Yasmin alituambia tuamke alfajiri na kuondoka.
Nikajiuliza ni nani anayefungua mlango. Nikaona kanzu yenye madoa ya damu ikiingia ndani.
Alikuwa harishi!
SASA ENDELEA
Nilishituka sana nilipogundua kuwa aliyefungua ule mlango alikuwa ni jini Harishi. Tulipaswa kujilaumu kwa uzembe wetu wa kulala hadi muda ule wakati Yasmin alituambia tuondoke kabla hakujapambazuka.
Na kwa kweli haukuwa uzembe bali tulipitiwa na usingizi, tena wakati mimi nazinduka wenzangu wote walikuwa bado wamelala.
Harishi aliingia ndani ya kile chumba. Sasa niliweza kuuona vizuri uso wake. Alikuwa na macho makubwa yenye makengeza.
Nikajifanya kama nimelala lakini nilikuwa nikimuangalia kwa pembeni na kwa makengeza huku mwili wangu ukitetemeka kwa hofu.
Pengine ni kutokana na ale makengeza yake, Harishi alipoingia mle chumbani macho yake yalikwenda kwa yule mtu aliyelala chini.
Mara moja aliinama na kumshika shingo yake kisha akamuinua na kutoka naye ukumbini.
Nikaisikia sauti ya Harishi akiuliza.
“Hii nyumba ni yako?”
Sikusikia jibu bali nilimsikia mwenzetu akipiga ukulele mmoj tu.
“Jamani nakufa!”
Halafu sikusikia kitu tena.
Hapo nilijua mwenzetu huyo alikuwa ameshatoolewa utosi na alikuwa akifyonzwa damu.
Ule ukulele aliopiga ulimuamsha mwenzangu niliyelala naye. Akainuka na kuketi kitandani.
“Kitu gani?” akaniuliza.
Nikaweka kidole changu cha shahada kwenye midomo yangu kumkataza asitoe sauti.
“Nini kwani?” Sasa sauti yake ilikuwa ya chini. Uso wake ulikuwa umeanza kushituka.
Nilishuka kitandani nikamnong’oneza “Harishi!”
Akagutuka. Uso wake ukabadilika na kuvamiwa na hofu.
“Yuko wapi?” akauliza kipumbavu
Sikumjibu. Nikamwambia “Tuingie mvunguni mwa kitanda”
Akakurupuka na kujiingiza kwenye mvungu huku akiburuza shuka aliyokuwa amejifinika. Tulipoingia kwenye mvungu huo tukanyamaza kimya.
Tuliamua kujificha humo japokuwa hatukuwa na uhakika kuwa tutapona. Bada ya muda kidogo tuliona mlango unafunguliwa tena.
Nilimuona mwenzangu anatikisa kichwa kwa hofu. Tuliona miguu ya Harishi ikiingia. Ilikuwa miguu mikubwa iliyochafuka na yenye vidole vyenye kucha ndefu. Ilikuwa pekupeku.
“Kumbe alikuwa ni yule peke yake!” Tukamsikia akisema Peke yake.
Ile shuka ya mwenzangu aliyokuwa akiiburuza ilitokeza nje ya mvungu wa kitanda. Harishi akaiona!
Tukaona mkono wake ukishika ncha ya shuka na kuivuta. Jamaa akaiachia. Shuka yote ikavutwa na kuchukuliwa na Harishi.
“Hizi ni shuka zangu ninazoziiba kwa Wahindi. Imewekwa na nani huku mvunguni?’ akajiuliza mwenyewe kisha akaitupa chini.
Tukaona miguu inageuka na kutoka. Alipotoka tulishukuru. Mimi nilitambaa hadi kwenye mlango, nikaufungua na kumchungulia.
Nilimuona akiinama na kuushika mguu wa mwenzetu aliyemuua, akamburuza kuelekea kwenye mlango wa kutokea.
Mwenzangu alikuwa amebaki mvunguni akinitazama. Nikaufunga mlango taratibu kisha nikarudi mle mvunguni.
“Mwenzetu ameuawa” nikamwambia mwenzangu. “Harishi amemburuza na kutoka naye”
“Alimuona wapi?”
“Mara ya kwanza aliingia ndani, wewe ulikuwa umelala, Akamsomba pale kwenye godoro na kutoka naye kwenda kumuua. Ndio pale ulipoamka”
“Kumbe Yasmin alitaka tufe alipotuambia tulalae humu?”
“Ni makosa yetu sisi. Yasmin alituambia tutoke Alfajiri, sisi tumelala hadi saa hizi kumekucha”
“Lakini ni kweli”
Wakati tunazungumza kwenye mvungu, Yasmin akaingia.
Tulipoona miguu yake tulitoka mvunguni.
“Jamani niliwambia nini?” akatuuliza kwa kutaharuki.
ITAENDELEA
 
Wewe jamaa kwani haujamjulia harishi shuaitwain???
Muda wankutupia stori ni baada ya saa ngapi.....Kuna kijisehemu nilicheka lkn inauma....jamaa mazembe Sana....unaogopa mvua kuliko harishi..etu tungeloa
 
Wewe jamaa kwani haujamjulia harishi shuaitwain???
Muda wankutupia stori ni baada ya saa ngapi

Hii ndio moda yenyewe sasa.

Yaani picha ya huyu jini niliyonayo kichwani nikiiprinti katika karatasi mleta mada ataahirisha kusimulia kwa uoga.
 
Duh, imeisha? itaendelea lini? hrf watunzi bwana, mnakatiaga story kwenye utamu
 
SEHEMU YA 12


Hakukuwa na aliyemjibu. Sote tulikuwa tumeshikwa na fadhaa.
“Si niliwambia mtoke alfajiri, mmelala hadi saa hizi wakati niliwambia kuwa Harishi atakuja leo”
“Ni kweli ulituambia” nikamkubalia.
“Sasa mbona hamkutoka alfajiri?’
“Tumepitiwa”
“Mtanilaumumimi bure jamani!”
Hatutakulaumu hata kidogo. Umetufanyia wema sana”
“Harishi alikuja mapema sana akaniambia anasikia harufu ya kimtumtu. Nikamwambia mtu ni mimi. Akaniambia hebu ngoja. Akatoka kuja kuwatafuta”
“Siku hizi atakuwa anakuja kila siku kwa sababu ameona anapata mlo anaoutaka. Ni lazima mjihadhari”
“Mimi naona tuondoke tu humu ndani” Mwenzangu akasema kwa woga.
“Lakini amekwishakwenda zake. Kwa leo hatarudi tena” Yasmin akatuambia.
“Itabidi tuondoke tu” Mwenzangu alizidi kusisitiza.
“Kwani wenzenu wengine wako wapi?”
ITAENDELEA
“Bado wamelala hadi sasa?” Yasmin akauliza kwa mshangao.
“Naona bado wamelala” nikamjibu.
“Kumbe nyinyi hamuwezi kuamka alfajiri?”
“Tatizo ni kuwa usingizi wenyewe unakuja wakati wa alfajiri” nikamwambia Yasmin.
“Basi ni balaa. Sasa itabidi usiku mwende mkalale sehemu nyingine, mjaribu bahati yenu”
“Tutafanya hivyo”
“Kuna nyumba nyingi hazina watu. Mnaweza kutafuta nyumba nzuri yenye vitanda mfanye makazi yenu. Hapamtakuwa mnakuja mchana tu, muda ambao nitawambia mimi”
“Tumekue;lewa, ngoja niwaamshe hawa mabwana”
Tukatoka pamoja mle chumbani. Tulipotoka tukawaona wenzetu nao wametoka.
“Hivi ndio mnaamka jamani?” Yasmin akawauliza.
“Dadayetu si unajua usingizi hautabiriki?” Mtu mmoja akamjibu.
“Hamkumbuki jana niliwambiaje? Si niliwambia muamke alfajiri muondoke?” Yasmin akawauliza.
“Ni kweli ulituambia lakini ndio tumepitiwa”
“Shakiri ameuliwa leo na Harishi!” nikawambia.
“Unasema kweli?” wakaniuliza kwa pamoja kwa mshituko.
“Ni kwa sababu ya kuchelewa kuamka. Sisis tumeponea chupuchupu baada ya kuingia mvunguni mwa kitanda”
“Basi utakwisha!”
“Yasmin ametupa wazo. Badala ya kulala hapa tutafute nyumba nyingine tuweke makazi yetu. Hapa tutakuwa tunakuja kula chakula mchana katika muda atakaotuambia Yasmin”
“Hivyo itakuwa vizuri” Mmoja wa wenzetu hao akasema.
“Sasa mjitayarishe, ninaenda kuwaandalia chai” Yasmin akatuambia.
Wakati Yasmin anakwenda jikoni, wenzetu wawili waliokuwa wamelala chumba cha pili ilivyokuwa hadi mwenzetu akauliwa.Tukawaeleza.
Kwa kweli walipata hofu.
“Sasa tukishakunywa chai tutoke tukatafute hiyo nyumba” nikawambia wenzangu.
Ilipofika saa nne tayari tulikuwa tumeoga na kunywa chai. Tukamwambia Yasmin tunataka kwenda kutafuta nyumba ya kukaa kwa maana tayari tulishakuwa wakazi wa kisiwa kile na hatukuwa na mategemeo ya kuondoka.
“Kwani mpaka mwende nyote”Yasmin akaniuliza.
“Unataka twende wangapi?” nikamuuliza.
“Mnaweza kwenda wawili, wawili mkabaki”
Mimi na wenzangu tukatazamana lakini sote tulionekana kutoliafikiwazo la Yasmin.
“Acha tu twende sote” nikamwambia Yasmin.
“Basi ngoja niwasindikize, msiniache peke yangu”
“Tukizunguka na wewe itakuwa vizuri” nikamwambia.
“Kwanini?’
“Kwa sababu wewe ndiye mwenyeji wetu, utaweza kutuongoza vizuri”
“Haya basi twendeni”
Tukatoka na Yasmin. Yasmin alikuwa akikijua vyema kisiwa hicho. Alituzungusha mitaa mbalimbali tukiangalia nyumba. Mwisho alitupeleka katiaka nyumba moja ambayo alituambia ilikuwa ya mtu mmoja tajiri wa kisiwa kile.ambaye naye naye aliuawa na Harishi.
Ilikuwa nyumba nzuri lakini ilikuwa imechakaa kwa vile ilikuwa haiishi watu. Tulipoingia ndani tulikuta mavumbi yalikuwa yameenea nyumba nzima.
Tukaanza kazi ya kuisafisha nyumba. Yasmin alitusaidia kufanya usafi. Ilikuwa kazi iliyotuchukua saa kadhaa.
Tulipomaliza tulichota maji kwenye kisima tukaoga kisha tukapumzika. Hapo ndipo tulipoanza kugawana vymba
Nyumba yenyewe ilikuwa ya vyumba vine na sisi wenyewe tulikuwa wanne. Kila mmoja alijichagulia chumba chake alichokipenda. Tulifungua makabati tukatoa mashuka na kutandika vitanda tulivyovikuta humo ndani.
Wakati ninatandika kitanda Yasmin aliniambia nimpe shuka atandike yeye. Nikampa.
“Natamani sana ningekuwa hapa pamoja na nyinyi” Yasmin akaniambia wakati anatandika.
“Ukiwa hapa utatuponzea sote”
“Ninasema tu lakini najua haitawezekana. Unajua katika nyinyi nyote nimekupenda wewe zaidi. Ninatamani ungekuwa mume wangu”
“Hata mimi natamani ungekuwa mke wangu lakini ndio tupo jela. Uhai wetu unahisabika”
“Ni kweli. Usikumbushiie hayo. Tuswali tuombe nusura itufikie”
“Wewe unaswali?” nikamuuliza Yasmin.
“Ninaswali lakini kwa siri sana. Harishi hataki niswali. Swala ndiyo inayonipa matumaini ya kuishi”
“Umenikumbusha jambo zuri sana na sisi tutaanza kuswali”
“Kila mara ninaota kunamtu atakuja kumuangamiza Harish na mtu huyo atakuwa mume wangu”
ITAENDELEA
 
Back
Top Bottom