Midumare Ngatuni Iwato
JF-Expert Member
- Jul 13, 2016
- 1,653
- 2,052
Hadithi zake kama za kiuajemi zuri sana Hadithi za Uajemi au Iran ndio Hadithi zuri kuliko zote duniani
ewaaa mambo sindio haya sasa "... weekend kama hii inapaswa kusukumwa barabara na kuisha salama kwa ma hekaya kama haya "..
Leta burudaniiii wekend hiiSEHEMU YA 04
ILIPOISHIA
Yasmin akajifuta machozi yake kwa shuka aliyokuwa amejifunga kisha akainua uso wake na kututazama. Sasa macho yake yalikuwa mekundu na uso wake ulikuwa umeiva.
“Wiki moja kabla ya harusi yangu huko Comoro nilikiota hiki kisiwa. Nikamuota kichaa mmoja akiniambia siku zako zimekaribia za kuja kukaa katika kisiwa hiki” Yasmin akaanza kutueleza. Tukawa tunamsikiliza kwa makini.
Akaendelea. “Nikamwambia yule kichaa, siwezi kuja kukaa hapa, mimi natarajia kufunga ndoa hivi karibuni. Nitakwenda kukaa Ufaransa si hapa
“Yule kichaa akaniambia, ndoa yangu nitafunga na yeye kwani yeye alinichunuka tangu nilipokuwa ninasoma na hatakubali niolewe na mtu mwingine.
“Nilipoamka asubuhi nilipuuza ile ndoto. Sikumuelezea mtu yeyote na kwa kweli nilifanya kosa kuipuuza, pengine nisingekuwa hapa leo hii. Yaani mpaka leo hii ninajuta”
Msichana huyo akaendelea kutuelea. “Ile siku ya harusi yangu ilipofika saa mbili usiku niliona kizunguzungu. Macho yangu yakafunga kiza. Nikaona kama moyo wangu unanisokota na ghafla nikapiga ukelele na kuanguka chini. Baada ya hapo sikujijua tena
“Nilizinduka asubuhi na kujikuta nomo ndani ya jumba hili katika kisiwa hiki. Mbele yangu nikamuona yule kichaa niliyemuota akiniambia kuwa nitakuja kukaa hapa”
SASA ENDELEA
“Yule mtu niliyemuota hakuwa binaadamu bali alikuwa jinni aliyekuwa amenichunuka. Siku ile nilipomuota nilimuona katika sura ya kibinaadamu kichaa lakini nilipozinduka nikiwa katika jumba hili alikuwa katika sura na umbile la kijini” Yasmin aliendelea kutueleza. Kisa chake kilikuwa kimetushangaza na kutuogopesha.
Akaendelea. “Huyo jinni aliponiona nimeshituka aliniambia Yasmin usiogope umeshafika nyumbani kwako, mimi ndio nitakuwa mume wako. Utaishi katika jumba hili na hutarudi tena kwenu.
“Akaniambia kwamba yeye ni jini wa ukoo wa kisubiani makata. Jina lake ni Harishi wa Harishn. Chakula chake ni damu ya binaadamu. Ameniambia wazi kuwa yeye ni jini mbaya aliyelaaniwa na ameshaua watu wengi.
“Akanihadithia kisa cha kisiwa hiki. Aliniambia kilikuwa kinaishi watu zamani na mfalme wao alikuwa akiishi katika jumba hili. Lakini yeye harishi ndiye aliyewaua mmoja mmoja kwa kuwafyonza damu hadi kukimaliza kisiwa chote.
“Watu wachache waliobaki waliondoka na kikiacha kisiwa kikiwa kitupu. Ndiyo sababu mlikuta magofu matupu na mifupa ya watu waliouliwa na Harishi. Siku za mwanzo mwannzo mji huu ulikuwa haukaliki kwa harufu zilizotokana na maiti za watu. Kunguru wa Zanzibar walihamia hapa kujipatia riziki zao. Sasa hivi iliyobaki ni mifupa mitupu.
“Kwa sasa kisiwa hiki kinajulikana kama kisiwa cha mauti. Wavuvi ambao hawajui habari za kisiwa hiki wakifika hapa kushona nyavu zao Harishi aliwaua mmoja mmoja kwa kuwafyonza damu”
Maelezo ya Yasmin yalitufanya tutazamane mara kwa mara huku nyuso zetu zikiwa zimepigwa na butwaa. Hatukuwahi kusikia kisa cha ajabu kama kile.
“Mimi nilikuwa nikilia peke yangu hadi sasa silii tena. Ni kama nimeshazoea kuishi na yule jinni” Yasmin aliendelea kutueleza.
“Kila wiki ankuja mara moja. Au kama nina dharura ninamuita, anakuja. Humu ndani mna kila kitu. Mna kila aina ya vyakula. Huwa najipikia mwenyewe chakula ninachotaka. Vyakula vikipungua ananilete vingine.
“Pia ananiletea nguo za kifalme pamoja na dhahabu. Huwa anaiba nguo hizo katika kasri za wafalme na marais. Kila kitu ninachotaka ananiletea lakini hainisaidii. Maisha ya upweke yananifanya nijione kama nimo ndani ya kaburi”
Wakati Yasmin anatuhadithia kile kisa, nilimuuliza. “Umetuambia huyo jini anafyonza damu za watu na kuwaua, je wewe utaendelea kuwa salama kweli”
“Mimi nimeshakuwa mke wake. Ameniambia damu yangu ni haramu kwake. Hawezi kuniua ila hatanirudisha tena kwetu. Nitaendelea kuishi hapa hadi mauti yanikute” Yasmin alituambia.
Kwa kweli hayakuwa maneno ya kuogopesha tu bali pia yalikuwa yanasikitisha sana.
Maisha ya Yasmin yalikuwa yanasikitisha. Alionesha wazi kukata tama na pia niliona kwa vyovyote itakavyokuwa maish yake yatakuwa mafupi.
“Kwa hiyo sisi hatutapona?” Mwenzetu mmoja akamuuliza Yasmin
“Sipendi niwafiche, nawaeleza ukweli ili mujue kuwasaa zenu zimekaribia sana”
“Je kama tutaondoka ndani ya jumba hili na kwenda kujificha mahali pengine?”
“Mtajificha wapi ambapo hafiki. Kisiwa chote hiki amekimiliki yeye. Halafu yeye ni jini, lazima atawagundua tu”
“Sisi tuko watu saba. Kweli ataweza kutuua sisi sote kwa pamoja?”
“Nyinyi atawaua mmoaja mmoja. Leo akiua mmoja, kesho anarudi tena kuua mwingine hadi mtamalizika nyote. Akishaua mtu anamtupa nje aliwe na kunguru”
Msichana akatikisa kichwa peke yake kabla ya kuendelea.
“Halafu hataki kuona mtu humu ndani. Wivu wake ni mkali sana. Siku nyingine anakuja na hasira, anasema anasikia harufu ya mtu humu ndani, basi hunipiga hadi nazimia kisha huenda zake”
Kila mmoja wetu aliguna na kumtazama mwenzake.
“Unadhani atakuja lini tena?” nikamuuliza.
Usipitwe na Uhondo huu kila siku na Kumekucha blog nitaendelea kukupa habari na mambo kemkem
ITAENDELEA
mbona unaquote uzi mzima mkuu?Leta burudaniiii wekend hii
Meyyadah Madame B Midumare Ngatuni Iwato hearly mkumbwa junior maji ya moto kawombe geesten66 madindigwa Frega Bao zipompa Kiporo kipya tasia mmari URBAN MONKEY Source07 Jeceel Mshana Jr Afrospear hydarybairu bato Dindira Madame S KingY kichaa msafi Mkushi Mbishi Trimmer Nelson nely mkuzi Slow pancha zipompa
Mnyongeni Mnyonge Rubawa
Mbona mimi sina ugomvi aidha na serikali,ndugu zangu wala marafiki zangu.Kanungila Karim umetekwa?
Uje huku ulete sehemu ya 4.
Umekosea njia nini?Kwamba hatapatikana mo