Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

SEHEMU YA 04


ILIPOISHIA
Yasmin akajifuta machozi yake kwa shuka aliyokuwa amejifunga kisha akainua uso wake na kututazama. Sasa macho yake yalikuwa mekundu na uso wake ulikuwa umeiva.
“Wiki moja kabla ya harusi yangu huko Comoro nilikiota hiki kisiwa. Nikamuota kichaa mmoja akiniambia siku zako zimekaribia za kuja kukaa katika kisiwa hiki” Yasmin akaanza kutueleza. Tukawa tunamsikiliza kwa makini.
Akaendelea. “Nikamwambia yule kichaa, siwezi kuja kukaa hapa, mimi natarajia kufunga ndoa hivi karibuni. Nitakwenda kukaa Ufaransa si hapa
“Yule kichaa akaniambia, ndoa yangu nitafunga na yeye kwani yeye alinichunuka tangu nilipokuwa ninasoma na hatakubali niolewe na mtu mwingine.
“Nilipoamka asubuhi nilipuuza ile ndoto. Sikumuelezea mtu yeyote na kwa kweli nilifanya kosa kuipuuza, pengine nisingekuwa hapa leo hii. Yaani mpaka leo hii ninajuta”
Msichana huyo akaendelea kutuelea. “Ile siku ya harusi yangu ilipofika saa mbili usiku niliona kizunguzungu. Macho yangu yakafunga kiza. Nikaona kama moyo wangu unanisokota na ghafla nikapiga ukelele na kuanguka chini. Baada ya hapo sikujijua tena
“Nilizinduka asubuhi na kujikuta nomo ndani ya jumba hili katika kisiwa hiki. Mbele yangu nikamuona yule kichaa niliyemuota akiniambia kuwa nitakuja kukaa hapa”
SASA ENDELEA
“Yule mtu niliyemuota hakuwa binaadamu bali alikuwa jinni aliyekuwa amenichunuka. Siku ile nilipomuota nilimuona katika sura ya kibinaadamu kichaa lakini nilipozinduka nikiwa katika jumba hili alikuwa katika sura na umbile la kijini” Yasmin aliendelea kutueleza. Kisa chake kilikuwa kimetushangaza na kutuogopesha.
Akaendelea. “Huyo jinni aliponiona nimeshituka aliniambia Yasmin usiogope umeshafika nyumbani kwako, mimi ndio nitakuwa mume wako. Utaishi katika jumba hili na hutarudi tena kwenu.
“Akaniambia kwamba yeye ni jini wa ukoo wa kisubiani makata. Jina lake ni Harishi wa Harishn. Chakula chake ni damu ya binaadamu. Ameniambia wazi kuwa yeye ni jini mbaya aliyelaaniwa na ameshaua watu wengi.
“Akanihadithia kisa cha kisiwa hiki. Aliniambia kilikuwa kinaishi watu zamani na mfalme wao alikuwa akiishi katika jumba hili. Lakini yeye harishi ndiye aliyewaua mmoja mmoja kwa kuwafyonza damu hadi kukimaliza kisiwa chote.
“Watu wachache waliobaki waliondoka na kikiacha kisiwa kikiwa kitupu. Ndiyo sababu mlikuta magofu matupu na mifupa ya watu waliouliwa na Harishi. Siku za mwanzo mwannzo mji huu ulikuwa haukaliki kwa harufu zilizotokana na maiti za watu. Kunguru wa Zanzibar walihamia hapa kujipatia riziki zao. Sasa hivi iliyobaki ni mifupa mitupu.
“Kwa sasa kisiwa hiki kinajulikana kama kisiwa cha mauti. Wavuvi ambao hawajui habari za kisiwa hiki wakifika hapa kushona nyavu zao Harishi aliwaua mmoja mmoja kwa kuwafyonza damu”
Maelezo ya Yasmin yalitufanya tutazamane mara kwa mara huku nyuso zetu zikiwa zimepigwa na butwaa. Hatukuwahi kusikia kisa cha ajabu kama kile.
“Mimi nilikuwa nikilia peke yangu hadi sasa silii tena. Ni kama nimeshazoea kuishi na yule jinni” Yasmin aliendelea kutueleza.
“Kila wiki ankuja mara moja. Au kama nina dharura ninamuita, anakuja. Humu ndani mna kila kitu. Mna kila aina ya vyakula. Huwa najipikia mwenyewe chakula ninachotaka. Vyakula vikipungua ananilete vingine.
“Pia ananiletea nguo za kifalme pamoja na dhahabu. Huwa anaiba nguo hizo katika kasri za wafalme na marais. Kila kitu ninachotaka ananiletea lakini hainisaidii. Maisha ya upweke yananifanya nijione kama nimo ndani ya kaburi”
Wakati Yasmin anatuhadithia kile kisa, nilimuuliza. “Umetuambia huyo jini anafyonza damu za watu na kuwaua, je wewe utaendelea kuwa salama kweli”
“Mimi nimeshakuwa mke wake. Ameniambia damu yangu ni haramu kwake. Hawezi kuniua ila hatanirudisha tena kwetu. Nitaendelea kuishi hapa hadi mauti yanikute” Yasmin alituambia.
Kwa kweli hayakuwa maneno ya kuogopesha tu bali pia yalikuwa yanasikitisha sana.
Maisha ya Yasmin yalikuwa yanasikitisha. Alionesha wazi kukata tama na pia niliona kwa vyovyote itakavyokuwa maish yake yatakuwa mafupi.
“Kwa hiyo sisi hatutapona?” Mwenzetu mmoja akamuuliza Yasmin
“Sipendi niwafiche, nawaeleza ukweli ili mujue kuwasaa zenu zimekaribia sana”
“Je kama tutaondoka ndani ya jumba hili na kwenda kujificha mahali pengine?”
“Mtajificha wapi ambapo hafiki. Kisiwa chote hiki amekimiliki yeye. Halafu yeye ni jini, lazima atawagundua tu”
“Sisi tuko watu saba. Kweli ataweza kutuua sisi sote kwa pamoja?”
“Nyinyi atawaua mmoaja mmoja. Leo akiua mmoja, kesho anarudi tena kuua mwingine hadi mtamalizika nyote. Akishaua mtu anamtupa nje aliwe na kunguru”
Msichana akatikisa kichwa peke yake kabla ya kuendelea.
“Halafu hataki kuona mtu humu ndani. Wivu wake ni mkali sana. Siku nyingine anakuja na hasira, anasema anasikia harufu ya mtu humu ndani, basi hunipiga hadi nazimia kisha huenda zake”
Kila mmoja wetu aliguna na kumtazama mwenzake.
“Unadhani atakuja lini tena?” nikamuuliza.
Usipitwe na Uhondo huu
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 04


ILIPOISHIA
Yasmin akajifuta machozi yake kwa shuka aliyokuwa amejifunga kisha akainua uso wake na kututazama. Sasa macho yake yalikuwa mekundu na uso wake ulikuwa umeiva.
“Wiki moja kabla ya harusi yangu huko Comoro nilikiota hiki kisiwa. Nikamuota kichaa mmoja akiniambia siku zako zimekaribia za kuja kukaa katika kisiwa hiki” Yasmin akaanza kutueleza. Tukawa tunamsikiliza kwa makini.
Akaendelea. “Nikamwambia yule kichaa, siwezi kuja kukaa hapa, mimi natarajia kufunga ndoa hivi karibuni. Nitakwenda kukaa Ufaransa si hapa
“Yule kichaa akaniambia, ndoa yangu nitafunga na yeye kwani yeye alinichunuka tangu nilipokuwa ninasoma na hatakubali niolewe na mtu mwingine.
“Nilipoamka asubuhi nilipuuza ile ndoto. Sikumuelezea mtu yeyote na kwa kweli nilifanya kosa kuipuuza, pengine nisingekuwa hapa leo hii. Yaani mpaka leo hii ninajuta”
Msichana huyo akaendelea kutuelea. “Ile siku ya harusi yangu ilipofika saa mbili usiku niliona kizunguzungu. Macho yangu yakafunga kiza. Nikaona kama moyo wangu unanisokota na ghafla nikapiga ukelele na kuanguka chini. Baada ya hapo sikujijua tena
“Nilizinduka asubuhi na kujikuta nomo ndani ya jumba hili katika kisiwa hiki. Mbele yangu nikamuona yule kichaa niliyemuota akiniambia kuwa nitakuja kukaa hapa”
SASA ENDELEA
“Yule mtu niliyemuota hakuwa binaadamu bali alikuwa jinni aliyekuwa amenichunuka. Siku ile nilipomuota nilimuona katika sura ya kibinaadamu kichaa lakini nilipozinduka nikiwa katika jumba hili alikuwa katika sura na umbile la kijini” Yasmin aliendelea kutueleza. Kisa chake kilikuwa kimetushangaza na kutuogopesha.
Akaendelea. “Huyo jinni aliponiona nimeshituka aliniambia Yasmin usiogope umeshafika nyumbani kwako, mimi ndio nitakuwa mume wako. Utaishi katika jumba hili na hutarudi tena kwenu.
“Akaniambia kwamba yeye ni jini wa ukoo wa kisubiani makata. Jina lake ni Harishi wa Harishn. Chakula chake ni damu ya binaadamu. Ameniambia wazi kuwa yeye ni jini mbaya aliyelaaniwa na ameshaua watu wengi.
“Akanihadithia kisa cha kisiwa hiki. Aliniambia kilikuwa kinaishi watu zamani na mfalme wao alikuwa akiishi katika jumba hili. Lakini yeye harishi ndiye aliyewaua mmoja mmoja kwa kuwafyonza damu hadi kukimaliza kisiwa chote.
“Watu wachache waliobaki waliondoka na kikiacha kisiwa kikiwa kitupu. Ndiyo sababu mlikuta magofu matupu na mifupa ya watu waliouliwa na Harishi. Siku za mwanzo mwannzo mji huu ulikuwa haukaliki kwa harufu zilizotokana na maiti za watu. Kunguru wa Zanzibar walihamia hapa kujipatia riziki zao. Sasa hivi iliyobaki ni mifupa mitupu.
“Kwa sasa kisiwa hiki kinajulikana kama kisiwa cha mauti. Wavuvi ambao hawajui habari za kisiwa hiki wakifika hapa kushona nyavu zao Harishi aliwaua mmoja mmoja kwa kuwafyonza damu”
Maelezo ya Yasmin yalitufanya tutazamane mara kwa mara huku nyuso zetu zikiwa zimepigwa na butwaa. Hatukuwahi kusikia kisa cha ajabu kama kile.
“Mimi nilikuwa nikilia peke yangu hadi sasa silii tena. Ni kama nimeshazoea kuishi na yule jinni” Yasmin aliendelea kutueleza.
“Kila wiki ankuja mara moja. Au kama nina dharura ninamuita, anakuja. Humu ndani mna kila kitu. Mna kila aina ya vyakula. Huwa najipikia mwenyewe chakula ninachotaka. Vyakula vikipungua ananilete vingine.
“Pia ananiletea nguo za kifalme pamoja na dhahabu. Huwa anaiba nguo hizo katika kasri za wafalme na marais. Kila kitu ninachotaka ananiletea lakini hainisaidii. Maisha ya upweke yananifanya nijione kama nimo ndani ya kaburi”
Wakati Yasmin anatuhadithia kile kisa, nilimuuliza. “Umetuambia huyo jini anafyonza damu za watu na kuwaua, je wewe utaendelea kuwa salama kweli”
“Mimi nimeshakuwa mke wake. Ameniambia damu yangu ni haramu kwake. Hawezi kuniua ila hatanirudisha tena kwetu. Nitaendelea kuishi hapa hadi mauti yanikute” Yasmin alituambia.
Kwa kweli hayakuwa maneno ya kuogopesha tu bali pia yalikuwa yanasikitisha sana.
Maisha ya Yasmin yalikuwa yanasikitisha. Alionesha wazi kukata tama na pia niliona kwa vyovyote itakavyokuwa maish yake yatakuwa mafupi.
“Kwa hiyo sisi hatutapona?” Mwenzetu mmoja akamuuliza Yasmin
“Sipendi niwafiche, nawaeleza ukweli ili mujue kuwasaa zenu zimekaribia sana”
“Je kama tutaondoka ndani ya jumba hili na kwenda kujificha mahali pengine?”
“Mtajificha wapi ambapo hafiki. Kisiwa chote hiki amekimiliki yeye. Halafu yeye ni jini, lazima atawagundua tu”
“Sisi tuko watu saba. Kweli ataweza kutuua sisi sote kwa pamoja?”
“Nyinyi atawaua mmoaja mmoja. Leo akiua mmoja, kesho anarudi tena kuua mwingine hadi mtamalizika nyote. Akishaua mtu anamtupa nje aliwe na kunguru”
Msichana akatikisa kichwa peke yake kabla ya kuendelea.
“Halafu hataki kuona mtu humu ndani. Wivu wake ni mkali sana. Siku nyingine anakuja na hasira, anasema anasikia harufu ya mtu humu ndani, basi hunipiga hadi nazimia kisha huenda zake”
Kila mmoja wetu aliguna na kumtazama mwenzake.
“Unadhani atakuja lini tena?” nikamuuliza.
Usipitwe na Uhondo huu kila siku na Kumekucha blog nitaendelea kukupa habari na mambo kemkem
ITAENDELEA
Leta burudaniiii wekend hii
 
SEHEMU YA 05



“Sasa unamuitaje?”
“Alinipa chupa. Mnaiona ile chupa iliyopo juu ya kabati? Chupa ile iko wazi. Kifiniko chake kipo pembeni. Ameniambia nisiifunge. Anapotaka kuja ile chupa inajaa moshi halafu inavuma. Ule moshi ukishajaa unatoka kwenye mdomo wa ile chupa na kuundaumbile la jinni halafu anakuwa jinni kabisa.
“Sasa nikitaka kumuita nachukua ile chupa naiweka naiweka karibu na mdomo wangu kisha nataja jina lake mara tatu, hazitapita dakika mbili chupa itajaa moshi. Moshi ule utatoka kwenye mdomo wa chupa na kugeuka Harishi”
“Sasa kama anakuja kila wiki tutapata muda wa kuishi na pengine tunaweza kupata msaada kwani tutakwenda kukaa fukweni kusubiri vyombo vinavyopita” nikamwambia Yasmin
“Jaribuni hahati yenu. Nawaombe Mungu awasalimishe” Yasmin alituambia kwa ungonge.
Nikawambia wenzangu. “Jamani maneno mmeyasikia. Hapa hapakaliki”
“Sasa tuondoke” Mtu mmoja akauliza.
“Inabidi tuondoke tusalimishe maisha yetu”
“Sasa tutakwenda wapi?” Mwingine akauliza.
“Twende ufukweni tuangalie vyombo vinavyopita, tunaweza kupata msaada”
“Sasa huyu msichana naye
tumchukue?” Mtu mwingine naye akauliza.
SASA ENDELEA
“Itakuwa ni jambo zuri tukimchukua kama mwenyewe atakubali” nikawambia wenzangu kish nikamtazama Yasmin.
“Bibie unaonaje kama tutakuchukua ili tukunusuru?” nikamuuliza yasmin.
“Kunichukua mimi hakutakuwa nusura kwangu wala kwenu kwa sababu mpaka sasa hamna uhakika wa usalama wenu hata kama mtakwenda ufukweni mwa bahari kusuiri vyombo vinavyopita” Yasmin akatuambia.
“Kwanini unatuambia hivyo?” nikamuuliza.
“Kwa sababu Harishi anaweza kututoke hapa hapa na kutuua sote kwa hasira’
Sote tukagunana kutazamana. Yasmin aliendelea kutuambia.
“kwanza akija hapa nyumbani hata kama mtakuwa mmeshaondoka atasema anasikia harufu ya binaadamu na atataka kujua ni nani aliyeingia humu na itakuwa ni balaa kubwa”
“Sasa unatushauri nini?” nikamuuliza Yasmin katika hali ya kukata tama.
“Nawashauri muondoke ndani ya jumba hili. Mwende popote mtakapoona mtaweza kujiokoa. Mimi niacheni hapa hapa”
“Sawa. Basi sisi tunondoka”
Yule msichana kwa kuonesha wema na ukarimu alituambia tumpishe mle chumbani avae nguo. Tukatoka ukumbini. Yasmin alipovaa alitoka akaenda jikoni. Akachukua vyakula na kututilia ndani ya mfuko.
“Sasa nendeni, msikae karibu kabisa” akatuambia.
Tukamuaga na kutoka. Tukaanza kutembea haraka haraka kwa kufuata ile njia tuliokwendea.
Kisiwa kilikuwa kimya na kilichokuwa kinatisha. Kelele zilizosikika zilikuwa ni za kunguru waliokuwa wakilialia na kurukaruka kwenye miti kama waliokuwa wakiambizana “Hao! Hao! Hao!”
Tulikuwa tukiangalia huku na huku kwa hofu ya kutokewa na Harishi. Kuwa na silaha katika mazingira yale ilikuwa muhimu. Mimi nilikuwa na sime niliyokuwa nimeichomeka kiunoni. Wenzangu wawili walikuwa na mapanga. Wenzetu wengine walikuwa mikono mitupu.
Kwa sababu ya hofu iliyosababishwa na kelele za wale kunguru nilitoa sime yangu na kuishika mkononi. Sasa nikawa tayari kukabiliana na chochote kitakachotokea.
Mpaka tunatokea kule ufukweni mwa bahari tulizungukazunguka sana kwani tulikuwa tunapotea njia mara kwa mara. Kulikuwa na mti mkubwa ulioota kando ya bahari. Tukakaa chini ya ule mti.
Tulitoa vyakula tulivyopewa na Yasmin na kuanza kula. Vilikuwa vhyakula vizuri vikiwa mchanganyiko wa mikate ya mayai, keki, sambusa na biriani.
Wakati tunakula mawazo yangu yalikuwa kwa yule msichana. Kwa kweli nilimuhurumia sana kwa kuishi maisha ya peke yake katika kisiwa kile cha kutisha. Laiti ningekuwa na uwezo wa kumuokoa ningemuokoa lakini ndio hivyo hatukuwa na uwezo na bado sisi wenyewe pia hatukuwa na uhakika wa maisha yetu.
Hata hivyo nilimsifu kwa kuwa na moyo wa kijasiri na wa kiume kwani asingeweza kuishi na kuendelea kuwa hai hadi leo wakati yuko kwenye jinamizi la mauti. Kuishi na jini anayeua watu peke yake lilikuwa ni jinamizi la mauti mbali ya kule kuishi peke yake katika kisiwa kile kinachotisha!.
Nikajiambia kama chombo chetu kingekuwa kizima tungeondoka naye hata kama angekataa.
Baada ya kula kile chakula tulipata akili tukaanza kujadiliana.
“Sasa tufanye nini jamani?” Mwenzetu mmoja akauliza.
“Tuijaribu tena ile boti, inaweza kukubali” nikatoa wazo ambalo lilikubaliwa na wenzangu.
Tukaenda kwenye chombo chetu tukajaribu kukiwasha lakini chombo hakikuwaka. Kila mmoja wetu alijaribu kukiwasha kwa mkono wake. Hakukuwa na yeyote aliyefanikiwa.
Tukaamua kujitia ufundi kuanza kuichokoresha mashine ya boti. Kila mmoja alitia ufundi wake lakini pia hatukufanikiwa. Mimi nilijitupa chini kwenye mchanga nikawaacha wenzangu wakiendelea kushindana nayo.
Yalipita karibu masaa mawili. Hatimaye niliona wenzangu mmoja mmoja akiondoka kwenye boti na kutafuta mahali pa kukaa. Wote walikuwa wamekata tama kama nilivyokata mimi.
Mawazo yangu yakarudi kwa Harishi. Kama alivyotwambia Yasmin Harishi anaweza kutokea na kutumaliza kama alivyowamaliza watu wa kisiwa hicho.
Kwa muda sote tulikuwa kimya. Kila mmoja alikuwa akiwaza lake. Tulipokitokea kisiwa kile tuliona tuliona tumeokoka tukafurahi. Kumbe tumeepuka kufa maji, tumekwenda kwa muuaji mwingine anayefyonza damu.
Tuliendelea kukaa pale tukiangalia baharini hadi jua likaanza kuchwa. Hatukuona chombo chochote kilichopita karibu. Tulichokiona ni mawingu yaliyoonekana kama yanazama upeoni mwa macho yetu.
Wakati giza linaingia hatukujua tungejisitiri mahali gani usiku huo kwani kwa vyovyote vile tusingeweza kuupitisha usiku mahali hapo kutokana na baridi. Pia usalama wetu ulikuwa mdogo. Lolote lingeweza kutokea wakati wa usiku. Kuna vitu kama majoka na wanyama wakali ambao hujificha wakati wa mchana na kujitokeza wakati wa usiku.
Baada ya kuufikiria usalama wetu tulishauriana turudi tena katika lile jumba la yule msichana. Kuna waliopinga wakataka tupande juu ya mti ule tuupitishe usiku.
Lakini upepo mkali ulioanza kuvuma pamoja na ngurumo za radi ndio uliofanya tukubaliane kwa pamoja kurudi katika lile jumba kwani tulijua muda si mrefu mvua kali ingenyesha na kututosa.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 06


Si tu tuliona tungeweza kujisitiri katika lile jumba pia tungeweza kufanya uchunguzi wetu na kujua kama huyo Harishi tuliyeambiwa ameshakuja au bado.
Tukaanza tena safari ya kurudi katika lile jumba. Mvua ilikuwa imeshaanza kunyesha kidogo dogo huku upepo mkali ukiendelea kuvuma pamoja na radi.
Tulitembea kwa mashaka mashaka tukikwepa kuwa karibu na miti kwa kuhofia kupigwa na radi.
Kulikuwa giza na hatukuweza kupata mwanga ila pale radi ilipopiga ndipo tulipoona tulikokuwa tunaelekea. Kutokana na giza hilo tulihangaika katika pori kwa muda kabla ya kufanikiwa kutokea katikati ya ule mji uliohamwa.
Tulikuwa tunaendelea kutota na mvua na huku tukiendelea kwenda. Tukawa tunalitafuta lile jumba. Tulidhani tusingeliona kwa urahisi lakini lilikuwa linawaka taa. Tukaliona kwa mbali. Tukalifuata.
Kwanza tulinyata kwenye madirisha. Tukawa tunachungulia na kutega masikio kusikiliza. Hatukusikia sauti yoyote. Kulikuwa kimya. Ndipo tukaamua tuingie.
SASA ENDELEA
Tukaingia ndani ya jumba hilo lililokuwa linawaka taa ndani. Lakini tuliingia kwa kunyata ili hatua zetu zisisikike. Jumba hilo lilikuwa kimya kama vile tulivyoliacha mchana.
Kila tulipofikia kona tulichungulia kwanza kabla ya kuendelea kwenda. Tukaenda hadi katika kile chumba tulichomkuta Yasmin binti wa rais wa Comoro.
Mlango wa chumba hicho ulikuwa umefungwa. Tukaenda jikoni tukapekua pekua na kukuta vyakula vilivyokuwa vimebaki. Tukakaa chini na kuanza kula kwani njaa ilikuwa inatuuma na hatukutarajia kupata chakula usiku huo.
Baada ya kula tulitoka humo jikoni tukaamua kutafuta mahali pa kulala ndani ya jumba hilo hilo. Karibu vyumba vyote tulivyofungua ukiacha kile cha Yasmin vilikuwa na vitanda. Kila kitanda kilikuwa na chumba kimoja kilichowezesha kulala watu wawili.
Tukaamua tulale kila chumba watu wawili. Tulikuwa tupo saba. Mmoja wetu akaamua kuchukua godoro kutoka chumba kingine na kuliingiza katika chumba tulichokuwemo mimi na mwenzangu. Akalilaza chini. Kwa vile yeye hakuwa na mwenzake wa kulala naye na asingeweza kulala peke yake, ndipo aliamua kuja kulala na sisi.
Mvua likuwa inaendelea kunyesha na radi ilikuwa inapiga. Kama tungekuwa tuko kwenye boti yetu tungejuta.
Mimi nilisoma aya zangu kisha nikajifunika shuka. Naamini na wenzangu kila mmoja alisoma dua yake kabla ya kulala.
Tulikuwa tumepanga tuamke alfajiri tutoke kwenye hilo jumba bila hata kumshitua Yasmin.
Hata hivyo usingizi hatukuupata kirahisi kwa sababu ya hofu. Tuliendelea kukaa macho hadi usiku mwingi. Wenzangu walipata usingizi lakini mimi sikulala.
Kulikuwa na wakati usingizi ulikuwa umeanza kunijia nikaamshwa na mwenzetu aliyekuwa amelala chini.
“Unasemaje?” nikamuuliza.
“Mkojo umenibana nisindikize chooni” akaniambia.
Vyoo vilikuwa nje.
Nikatenga shuka na kunyanyuka. Mwenzangu niliyelala naye alikuwa anakoroma.
“Twende!” nikamwambia yule aliyeniamsha.
Tukatoka pamoja. Vyoo vilikuwa ukumbini karibu na mlango wa kutokea.
Tulikwenda hadi karibu na milango ya vyoo. Kulikuwa na vyoo vinne. Mwenzangu alishaingia choo kimojawapo. Mimi nikasikia hatua za mtu nyuma yangu nikageuka. Alikuwa ni yule mwenzetu tuliyemuacha amelala, naye aliamka na kutufuata.
Alikuwa anakuja harakaharaka kutukimbizia. Nilijua ni sababu ya uoga. Wakati huo huo nikaona mlango wa chumba cha Yasmin unafunguliwa. Nikaingia chooni haraka ili niweze kumchungulia aliyekuwa anatoka bila yeye kuniona.
Ghafla nikaliona jitu likitoka katika kile chumba. Lilikuwa jitu la kutisha lililojifunga kilemba kikubwa. Lilikuwa na msitu wa nywele zilizotokeza nje ya kilemba chake. Lilivaa kanzu nyeupe iliyochafuka kwa madoa ya damu na iliyokatwa mikono.
Mikono yake minene iliyoota manyoya marefu ilikuwa imeshupaa. Mkono mmoja alishika upanga mrefu.
Uso wake ulikuwa na ndevu nyingi na sharafa kiasi kwamba sura yake haikuweza kutambulika. Kilichoonekana kwenye uso wake ni pua yake iliyofura kamailiyopachikwa na macho yake makubwa yenye makengeza.
Miguu yake ilikuwa pekupeku. Alikuwa na vidole virefu na vinene vya miguu, tena vilikuwa na kucha ndefu kama kucha za mnyama.
Hapo hapo nikahisi kwamba yule alikuwa ndiye Harushi. Alikuwa ametufuma vizuri ndani ya hilo jumba.
Uso wake ukiwa na hasira kali, macho yake ya makengeza yalielekea kwa yule mwenzetu aliyekuwa anatufuata. Alikuwa ameshafika karibu yake kiasi kwamba jitu hilo lilinyoosha mkono wake wa kushoto na kumshika shati.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 07



“Mimi nasikia harufu ya binaadamu humu ndani. Kumbe ni wewe!” akamwambia yule mwenzetu aliyemshika shati. Suati yake ilikuwa ya kuunguruma kama gari bovu.
Wakati anasema meno yake yalitoka nje. Yalikuwa meno marefu kama ya nyani!
Alipomshika mwenzetu shati alimvuta karibu yake.
“Umeingiaje humu ndani na umefuata nini….kwanza umetoka wapi?” akamuuliza kwa hasira.
Ghafla Yasmin akatoka.
“Ni nani?” akauliza huku akimtazama yule mtu ambaye alikuwa akitetemeka.
Yasmin alipomuona alimgundua.
“Itakuwa ni wavuvi walioharibikiwa na chombo chao, wameona nyumba wameingia wakidhani watapata msaada” Yasmin akaliambia lile jitu.
“Anaingia humu anamfuata nani. Huyu simuachi ng’o!” jitu hilo lilisema na kumshika yule mwenzetu kwenye kiuno kisha likamuinua juu kwa mkono mmoja na kumgeuza kichwa chini. KIchwa cha mwenzetu kikawa chini ya kichwa cha jitu lile jitu.
Ndipo jitu hilo lilipokita utosi wa yule mtu kwa ncha ya upanga wake. Mwenzetu huyo alipiga ukulele mmoja tu “Nakufaaa!” kisha akawa kimya. Damu ikaanza kuchuruzika kutoka kwenye utosi wakei jitu hilo likakinga mdomo wake na kuanza kuifyonza!.
SASA ENDELEA
Aliendelea kuinywa ile damu iliyokuwa ikitoka kama maji ya bomba. Mwisho alibandika mdomo wake pale kwenye utosi na kuanza kufyonza.
Nilikuwa nikitetemeka kwa hofu kama niliyepatwa na homa ya baridi ya ghafla. Nilijua akimalizwa yule mwenzetu itaanza zamu yetu sisi kwani sote tulikuwa ndani ya lile jumba.
Midomo ya Harishi ilitapakaa damu. Damu nyingine ilikuwa inavuja midomoni mwake na kuingia kwenye ndevu zake na kisha kutiririka hadi kwenye kanzu yake.
Yasmin alikuwa ameshika kichwa chake kwa huzuni na alikuwa amekiinamisha kichwa chake chini ili asiangalie lile tukio.
Pamoja na huzuni na uchungu vilivyompata Yasmin bila shaka alikuwa akijiambia “Wameyataka wenyewe. Nilishawambia waondoke, kumbe wamerudi tena”
Nikaona mafunda ya Harish yanafutuka huku akitafuna kwa haraka haraka na kumeza. Kumbe alikuwa alikuwa anafyonza ubongo wa mwenzetu na kuula. Aliula kwa ulafi. Mwingine ulimvuja midomoni na kuingia kwenye ndevu zake.
Alipotosheka alitupa chini ile maiti akaanza kujirambaramba midomo na kujifuta kwa mkono. Alipomaliza aliinama akaushika mguu wa yule mtu aliyemuua.
“Sasa nimeshiba vizuri, ngoja niondoke” alijisemea peke yake akiuinua ule mguun na kuuburuza kuutoa ule mwili nje. Aliuburuza huku akiendelea kujirambaramba. Alipofika kwenye mlango aliufungua na kutoka na ile maiti nje.
Yasmin alikuwa bado amesimama akimtazama.
“Lakini mimi niliwambia ila hawakunisikia” akajisemea peke yake huku akitikisa kichwa.
Kwa sababu ya kuzidiwa na hofu na kujua kuwa sote tutakufa nilijitokeza pale nilipokuwa nimejificha. Nikamfuata Yasmin.
Yasmin alishituka aliponiona.
“Na wewe umetokea wapi?” akaniuliza kwa kutaharuki.
“Nilikuwa nimejificha chooni” nikamjibu kwa sauti ya kutetemeka.
“Unaiona damu hii ya mwenzenu?”
Yasmin akanionesha damu iliyokuwa imedondoka chini.
“Nimeiona na nimeona pia alivyouawa”
“Si niliwambia mwendezenu?”
“Tulirudi huu usiku tulipoona kuna mvua na hatukuwa na mahali pa kujisitiri”
“Sasa mmerudi na Harishi ametokea. Mwenzenu ameonekana”
“Kwani atarudi tena usiku huu?”
“Usiku huu hatarudi tena lakini kama ameshasikia harufu zenu anaweza kurudi hata kesho akijua atapata mlo mwingine. Yule hali kitu isipokuwa damu na ubongo. Watu wa kisiwa chote hiki amewamaliza yeye na ana nguvu zisizo za kawaida. Yule mtu amemuinua juu kwa mkono mmoja tu”
“Na amempeleka wapi?”
“Amekwenda kumtupa nje ili asubuhi aliwe na kunguru”
“Sasa sijui sisi tutakimbilia wapi kwani chombo chetu kimekataa kabisa kuwaka”
“Mimi sina la kuwambia kwani popote mtakapokwenda ndani ya kisiwa hiki atawagundua na atawamaliza mmoja mmoja”
Nilibaki kuduwaa na kutikisa kchwa. Kwa mara ya kwanza niliona kazi ya uvuvi ilikuwa mbaya. Laiti kama ningejua kuwa chombo chetu kingeharibika baharini nisingeshiriki katika safari ile.
“Wenzako wengine wako wapi?” Yasmin akaniuliza.
“Nikwambie ukweli Yasmin, sisi tulirudi mapema huu usiku tukaigia jikoni na kula chakula chako kwa sababu tulikuwa na njaa. Tukaingia vyumbani kulala. Sasa tulitoka watu wawili kuja kujisaidia. Huku nyuma mwenzetu mmoja naye alitoka peke yake, Ndiye yule aliyekamatwa na kuuawa”
“Wenzako wengine wako wapi?”
“Mmoja amejificha chooni na wenzetu wengine wako vyumbani”
“Sasa na nyinyi nendeni mkalale, asubuhi mtafanya maarifa. Yule jini hatarudi kwa leo, ameshashiba”
Yule mwenzangu aliyekuwa chooni aliposikia maneno yale alitoka haraka. Yasmin akamtazama.
“Nyinyi mna bahati sana. Angeweza kushikwa mmojawenu”
“Ni kweli kwa sababu sisi ndio tuliotoka kwanza” nikamwambia Yasmin.
“Basi nendeni mkalale”
Tukarudi kwenye vile vyumba. Yasmin alikuwa bado amesimama akituangalia hadi tulipofungua mlango na kuingia chumbani’
Wala hatukulala kamwe. Mimi nilikaa macho usiku kucha nikimuwaza yule mwenzetu aliyeuawa kikatili.
“Nyinyi mna bahati sana. Angeweza kushikwa mmojawenu…” nikawa nayakumbuka maneno ya Yasmin huku mwili ukinisisimka kwa hofu.
ITAENDELEA
 
Back
Top Bottom