Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Asante Ila huja nitag...bwasheee najua baadae ikianza kulipiwa kwa pesa money nitatoa tu baba
 
SEHEMU YA 13



“Unahakika kuwa nitakuwa salama?”
“Harishi hatakuja leo. Ameshakuja asubuhi ni mpaka kesho”
“Ngoja niwaage wenzangu”
Tukatoka ukumbini. Wenzangu walikuwa wameketi wakizungumza. Nikawambia kwa namsindikiza Yasmin.
“Ninakwenda kupika, nitampa chakula awaletee” Yasmin akawambia.
“Yaani utasubiri chakula huko huko?” Mmoja akaniuliza lakini uso wake haukuonesha furaha.
“Ndio atakisubiri” Yasmin akamjibu.
Masudi akawatazama wenzake kabla ya kuniambia.
“Sawa. Sisi tutasubiri”
Jina lake lilikuwa Masudi. Katika sisi watu wanne tuliobaki, yeye alikuwa ndiye mkubwa kwetu kiumri.
SASA ENDELEA
Wakati mimi na Yasmin tunatoka kwenye ile nyumba tukirudi nyumbani kwa Yasmin, Yasmin aliniambia. “Yule kaka uliyezungumza naye anaitwa nani?’
“Anaitwa Masudi”
“Naona kama hakufurahi ulivyomwambia tunatoka mimi na wewe”
“Inawezekana, ni binaadamu. Labda ameona tumewabagua”
“Mbona wengine hawakusema kitu?”
“Kila mtu ana mawazo yake. Yule amezoea kutuamrisha kwa sababu kwenye kundi letu yeye ndiye mkubwa kiumri na amekuwa kama kiongozi wetu”
“Kwa hiyo alitaka anisindikize yeye”
Yasmin aliposema hivyo nilicheka, na yeye akacheka.
“Unafikiri nakutania?” aliponiuliza hivyo alitaja jina langu.
“Hunitanii, unaniambia ukweli. Najua Masudi hakufurahi” nikamwambia.
Pakapita kimya kifupi kabla ya Yasmin kuniambia.
“Kisiwa chote hilki kilikuwa kina watu”
“Wewe uliwakuta hao watu?” nikamuuliza.
“Wakati Harishi ananileta hapa alikuwa ameshamaliza watu wote. Wengine walihama wenyewe kukimbia kifo”
“Na kama leo anakuja na kutukuta hivi itakuwaje?”
“Atakukamata wewe. Atakufyonza damu na ndio ataniuliza wewe ni nani na ulifuata nini hapa”
“Ina maana wewe hatakuadhibu?”
“Ananitisha tu pale ninapomuudhi lakini kama atanikuta na mwanaume nadhani ataniadhibu”
“Lakini hatakufyonza damu?”
“Hapo siwezi kujua”
“Inatisha. Ni kwa vile tu umenihakikishia kwamba hatarudi tena leo”
Tulipofika katika jumba la Yasmin. Tulikaa katika ule ukumbi tukaanza kuzungumza.
Yasmin akanieleza wazi kuwa alikuwa amenipenda.
“Wewe ndio ungefaa uwe mume wangu” akaniambia kiudhati.
“Tayari umeshakuwa mke wa jini, huwezi tena kuwa mke wangu”
“Jini amenioa wapi? Si ananibaka tu!”
“Lakini ndio mume wako na amekuleta huku kusudi aweze kukudhibiti”
“Hakuna kisichokuwa na mwisho. Mwisho wake utafika tu”
“Inshaallah!”
“Mimi na wewe tutakwenda kuoana Comoro!”
Nikatikisa kichwa changu. Niliona Yasmin alikuwa anaota ndoto ya mchana.
“Yasmin huoni kuwa tuko jela! Unawazia kwenda kuoana Comoro, hapa tutatoka vipi?”
“Tutatoka tu iko siku. Kila siku mimi naswali kuomba”
“Angekuwa ni mwanaadamu aliyekuweka hapa tungepambana naye. Lakini jini aliyemaliza kisiwa kizima ni hatari”
“Usikate tama, usinivunje moyo. Wewe mwanaume!” Yasmin aliposema hivyo alinyanyuka.
“Ngoja nikapike sasa” akaniambia na kuelekea jikoni.
Wakati anatembea nilimtazama kwa nyuma. Nguo alizokuwa amevaa zilimpendeza. Kama alivyotueleza mwenyewe nguo hizo alikuwa naletewa na Harishi ambaye huziiba kwnye maduka ya miji mikuwa.
Yasmin alipofika kwenye mlango wa kuingilia ndani aligeuka na kunitazama. Alipoona nilikuwa namuangalia akatabasamu kabla ya kuingia ndani.
Nilikaa peke yangu nikiwaza hili na lile. Nilijiambia Yasmin alikuwa msichana mzuri, kikwazo kilikuwa ni lile jini. Kama nafanikiwa kumuoa binti wa rais ni heshima kubwa.
Baada ya muda kidogo niliondoka nikamfuata Yasmin jikoni.
“Umenifuata huku?” Yasmin akaniambia.
“Nataka tusaidiane kupika” nikamwambia kwa mzaha.
“Si ungekaa tu nikakupikia mume wangu mtarajiwa”
Nilijua Yasmin alikuwa anajifariji kuniita “mume wangu mtarajiwa” Na mimi sikutaka kumvunja moyo. Kwa upande mwingine mimi pia nilihitaji faraja kutoka kwa Yasmin.
“Hapana nataka nikusaidie mtarajiwa wangu”
“Haya nisaidie”
Nikamsaidia Yasmin kupika huku mizaha na dhihaka zikipita. Kwa mara ya kwanza niligundua Yasmin alikuwa mchangamfu na aliyependa mzaha. Alikuwa akicheka hadi sauti yake ilisikika nje. Alikuwa amesahau kabisa mateso yaliyokuwa yanatukabili sisina yeye.
“Yasmin unacheka sana, sauti yako inasikika nje” nikamwambia.
“Kwani nani atatusikia, si tuko peke yetu?”
“Najua tukompeke yetu lakini usicheke sana”
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 12


Hakukuwa na aliyemjibu. Sote tulikuwa tumeshikwa na fadhaa.
“Si niliwambia mtoke alfajiri, mmelala hadi saa hizi wakati niliwambia kuwa Harishi atakuja leo”
“Ni kweli ulituambia” nikamkubalia.
“Sasa mbona hamkutoka alfajiri?’
“Tumepitiwa”
“Mtanilaumumimi bure jamani!”
Hatutakulaumu hata kidogo. Umetufanyia wema sana”
“Harishi alikuja mapema sana akaniambia anasikia harufu ya kimtumtu. Nikamwambia mtu ni mimi. Akaniambia hebu ngoja. Akatoka kuja kuwatafuta”
“Siku hizi atakuwa anakuja kila siku kwa sababu ameona anapata mlo anaoutaka. Ni lazima mjihadhari”
“Mimi naona tuondoke tu humu ndani” Mwenzangu akasema kwa woga.
“Lakini amekwishakwenda zake. Kwa leo hatarudi tena” Yasmin akatuambia.
“Itabidi tuondoke tu” Mwenzangu alizidi kusisitiza.
“Kwani wenzenu wengine wako wapi?”
ITAENDELEA
“Bado wamelala hadi sasa?” Yasmin akauliza kwa mshangao.
“Naona bado wamelala” nikamjibu.
“Kumbe nyinyi hamuwezi kuamka alfajiri?”
“Tatizo ni kuwa usingizi wenyewe unakuja wakati wa alfajiri” nikamwambia Yasmin.
“Basi ni balaa. Sasa itabidi usiku mwende mkalale sehemu nyingine, mjaribu bahati yenu”
“Tutafanya hivyo”
“Kuna nyumba nyingi hazina watu. Mnaweza kutafuta nyumba nzuri yenye vitanda mfanye makazi yenu. Hapamtakuwa mnakuja mchana tu, muda ambao nitawambia mimi”
“Tumekue;lewa, ngoja niwaamshe hawa mabwana”
Tukatoka pamoja mle chumbani. Tulipotoka tukawaona wenzetu nao wametoka.
“Hivi ndio mnaamka jamani?” Yasmin akawauliza.
“Dadayetu si unajua usingizi hautabiriki?” Mtu mmoja akamjibu.
“Hamkumbuki jana niliwambiaje? Si niliwambia muamke alfajiri muondoke?” Yasmin akawauliza.
“Ni kweli ulituambia lakini ndio tumepitiwa”
“Shakiri ameuliwa leo na Harishi!” nikawambia.
“Unasema kweli?” wakaniuliza kwa pamoja kwa mshituko.
“Ni kwa sababu ya kuchelewa kuamka. Sisis tumeponea chupuchupu baada ya kuingia mvunguni mwa kitanda”
“Basi utakwisha!”
“Yasmin ametupa wazo. Badala ya kulala hapa tutafute nyumba nyingine tuweke makazi yetu. Hapa tutakuwa tunakuja kula chakula mchana katika muda atakaotuambia Yasmin”
“Hivyo itakuwa vizuri” Mmoja wa wenzetu hao akasema.
“Sasa mjitayarishe, ninaenda kuwaandalia chai” Yasmin akatuambia.
Wakati Yasmin anakwenda jikoni, wenzetu wawili waliokuwa wamelala chumba cha pili ilivyokuwa hadi mwenzetu akauliwa.Tukawaeleza.
Kwa kweli walipata hofu.
“Sasa tukishakunywa chai tutoke tukatafute hiyo nyumba” nikawambia wenzangu.
Ilipofika saa nne tayari tulikuwa tumeoga na kunywa chai. Tukamwambia Yasmin tunataka kwenda kutafuta nyumba ya kukaa kwa maana tayari tulishakuwa wakazi wa kisiwa kile na hatukuwa na mategemeo ya kuondoka.
“Kwani mpaka mwende nyote”Yasmin akaniuliza.
“Unataka twende wangapi?” nikamuuliza.
“Mnaweza kwenda wawili, wawili mkabaki”
Mimi na wenzangu tukatazamana lakini sote tulionekana kutoliafikiwazo la Yasmin.
“Acha tu twende sote” nikamwambia Yasmin.
“Basi ngoja niwasindikize, msiniache peke yangu”
“Tukizunguka na wewe itakuwa vizuri” nikamwambia.
“Kwanini?’
“Kwa sababu wewe ndiye mwenyeji wetu, utaweza kutuongoza vizuri”
“Haya basi twendeni”
Tukatoka na Yasmin. Yasmin alikuwa akikijua vyema kisiwa hicho. Alituzungusha mitaa mbalimbali tukiangalia nyumba. Mwisho alitupeleka katiaka nyumba moja ambayo alituambia ilikuwa ya mtu mmoja tajiri wa kisiwa kile.ambaye naye naye aliuawa na Harishi.
Ilikuwa nyumba nzuri lakini ilikuwa imechakaa kwa vile ilikuwa haiishi watu. Tulipoingia ndani tulikuta mavumbi yalikuwa yameenea nyumba nzima.
Tukaanza kazi ya kuisafisha nyumba. Yasmin alitusaidia kufanya usafi. Ilikuwa kazi iliyotuchukua saa kadhaa.
Tulipomaliza tulichota maji kwenye kisima tukaoga kisha tukapumzika. Hapo ndipo tulipoanza kugawana vymba
Nyumba yenyewe ilikuwa ya vyumba vine na sisi wenyewe tulikuwa wanne. Kila mmoja alijichagulia chumba chake alichokipenda. Tulifungua makabati tukatoa mashuka na kutandika vitanda tulivyovikuta humo ndani.
Wakati ninatandika kitanda Yasmin aliniambia nimpe shuka atandike yeye. Nikampa.
“Natamani sana ningekuwa hapa pamoja na nyinyi” Yasmin akaniambia wakati anatandika.
“Ukiwa hapa utatuponzea sote”
“Ninasema tu lakini najua haitawezekana. Unajua katika nyinyi nyote nimekupenda wewe zaidi. Ninatamani ungekuwa mume wangu”
“Hata mimi natamani ungekuwa mke wangu lakini ndio tupo jela. Uhai wetu unahisabika”
“Ni kweli. Usikumbushiie hayo. Tuswali tuombe nusura itufikie”
“Wewe unaswali?” nikamuuliza Yasmin.
“Ninaswali lakini kwa siri sana. Harishi hataki niswali. Swala ndiyo inayonipa matumaini ya kuishi”
“Umenikumbusha jambo zuri sana na sisi tutaanza kuswali”
“Kila mara ninaota kunamtu atakuja kumuangamiza Harish na mtu huyo atakuwa mume wangu”
ITAENDELEA
Kwa kuwa umesema ni KISA CHA KWELI, Mkipata nafasi mwambieni Yasmini na wenzako kuwa yuko mwanaume mmoja ambaye ni Simba wa kabila la Yuda! Jina lake ni YESU KRISTO. Amekuja kuwaganga walovunjika moyo na kuwatangazia mateka uhuru wao.. huyo Harishi atakalishwa chini ghafla!
 
SEHEMU YA 02


Hapo ndipo tulipoanza kufadhaika. Hatukuwa na la kufanya, tukawa tunatazamana!.
Tulikuwa tumepelekwa mbali sana kiasi kwamba hatukuweza kuona vyombo vyovyote ambavyo vingeweza kutusaidia. Tukakata tama kabisa.
Injini ya boti inapozima boti inakuwa kwenye hatari ya kupigwa na dharuba na kupinduka. Kama hilo lingetokea ungekuwa ndio mwisho wetu!
Hata hivyo bahari ilikuwa tulivu. Tatizo letu ni kuwa safari yetu haikuwa na mwisho wala muelekeo maalumu. Boti yetu ilikuwa inakokotwa kufuata upepo unakokwenda.
Mpaka jua linakuchwa hatukuwa tumetokea kwenye nchi yoyote wala kisiwa chochote. Ndani ya boti tulikuwa na vyakula vya akiba lakini hakukuwa na yeyote miongoni mwetu aliyesikia njaa.
Usiku ukapita kwa taabu huku tukiendelea kupelekwa. Asubuhi tuliendelea tena na jitihada ya kuiwasha injini lakini injini ilikataa katakata kuwaka. Tukaendelea kukokotwa hadi jioni. Hapo tukatoa vyakula vyetu na maji tukala kidogo tu.
Tulilala tena kwenye boti hadi siku ya tatu na ya nne. Vyakula vikatuishia licha ya kwamba tulikuwa hatuli sana. Tulibakisha maji kidogo tu.
Sasa tukahisi kwamba kama hatutakufa maji tutakufa kwa njaa kwani kwa siku hizo nne tulizokuwa baharini tulikuwa tumekonda.
Alfajiri ya kuamkia siku ya tano ndipo tulipotokea kwenye kisiwa. Sote tukashukuru ingawa hatukujua kilikuwa kisiwa gani na kilikuwa katika eneo gani.
Kilikuwa kisiwa kikubwa ingawa hakikuwa kikubwa sana. Kwa vile tulikitokea wakati wa usiku hatukukiona kwa sababu ya giza. Tulikiona kulipoanza kucha. Wakati tunakiona tulikuwa tumekikaribia sana. Sote tukapata furaha na matumaini ya kuokoka.
Mawimbi yaliendelea kutusukuma kidogodogo na kutufikisha kwenye maji madogo kabisa.
Suala kwamba kisiwa hicho kilikuwa kisiwa gani na kipo wapi halikuwa na umuhimu kwetu. Kilichokuwa muhimu ni kuwa tumefika mahali ambapo tungeweza kuyasalimisha maisha yetu nap engine kupata msaada wa kutuwezesha kurudi kwetu.
Tulishusha nanga na kushuka kwenye boti. Maji yalikuwa yakitufikia kwenye magoti. Tukaliacha boti na kutembea kwa miguu kwa kuyasukuma maji hadi tukafika ufukweni mwa bahari. Mahali tulipotokea hapakuwa na muinuko mkubwa. Tukapanda kwenye nchi kavu na kuanza kutembea kwemye vichaka huku tukiangaza macho huku na huku.
Kulikuwa na kunguru wengi waliokuwa wakiruka ruka kwenye miti. Jinsi walivyokuwa wakipiga kelele walikuwa kama wanaotukaribisha katika kisiwa hicho kilichokuwa kimya.
Tukaendelea kutembea tukiingia ndani zaidi ya kisiwa. Mtarajio yetu yalikuwa kupata mji au kijiji kilichokuwa kinakaa watu ili tuweze kusaidiwa.
Baada ya mwendo wa kama nusu saa tulianza kuona vibanda vilivyokuwa vimebomoka. Tukapata matumaini kuwa kulikuwa na watu waliokuwa wanaishi katika kisiwa hicho. Pia tulikuta visima viwili vya maji ambavyo vilikuwa vimekauka.
Wakati tunaendelea kwenda ghafla tuliona tumetokea kwenye barabara pana ya changarawe. Tukaifuata ile barabara mpaka tukatokea katikati ya mji. Ulikuwa mji mzuri uliokuwa na barabara na majumba. Lakini nyumba zote zilikuwa zimechakaa na kubomoka. Baadhi yake zilionekana kama mahame.
Jambo ambalo lilitushangaza ni kuwa hatukuona mtu hata mmoja. Mji wote ulikuwa kimya kabisa. Tulikuwa ni sisi peke yetu tu. Tulikatiza mtaa hadi mtaa kutafuta wenyeji wa kisiwa hicho lakini hatukuona mtu.
Udadisi ukatufanya tuanze kuingia katika zile nyumba. Tuliingia katika
nyumba ya kwanza. Tukakuta vitu vya ndani vilivyochakaa na kukongoroka. Vilikuwa kama vitu vya zamani visivyotumika tena. Katika kutafiti tafiti tulishituka tulipokuta mafumvu na mifupa ya binaadamu. Kuna iliyokuwa imelala kwenye kitanda na mengine ilisambaa ovyo.
Tukatoka haraka katika nyumba ile na kuingia katika nyumba nyingine, nako tulikuta vitu mbalimbali vya ndani ya nyumba vilivyokuwa vimechakaa na mifupa ya binaadamu.
Tukawa tunatazamana kwa hofu. Kila mmoja wetu alikuwa akijiuliza moyoni mwake, kulikoni? Lakini hatukupata jibu.
Katika mitaa mengine tulikuta mafuvu na mifupa ya binaadamu ikiwa barazani mwa nyumba na kando kando ya barabara. Tulivyozidi tena kwenda mbele tulikuta mifupa ya mikono nay a miguu ya binaadamu ikining’nia kwenye miti. Tukawa tunazidi kuitazama ile mifupa huku tunazidi kwenda.
Ghafla tukatokea kwenye jumba moja kubwa. Jumba hilo ndilo lililokuwa kubwa na zuri kuliko jumba lolote katika kisiwa hicho.
Mbele ya jumba hilo kulikuwa na bustani ya maua na miti ya vivuli. Kutokana na uzuri wa jumba hilo tukaona tuingie ndani ili tuangalie lilivyo.
Tulipoingia tu pua zetu zilikaribishwa na harufu nzuri ya manukato yaliyokuwa yananukia humo ndani. Tulitembea katika sakafu ya marumaru iliyonakishiwa maua ya kupendeza.
Tulikuwa tumeingia katika ukumbi mpana uliokuwa na madirisha na mapazia ya hariri. Tulikuta meza, viti na makabati. Zilikuwa fanicha za kifahari sana.
Baada ya kuupita ukumbi huo tulitokea katika kumbi nyingine ndogondogo zilizokuwa na vyumba vipana. Tukawa tunaingia kila chumba kuchunguza.
Katika chumba cha kwanza tulikuta kitanda kilichotandikwa vizurii. Pia tulikuta makabati ya vioo yaliyokuwa yanapendeza.
“Inaelekea kuna watu wanaoishi ndani ya jumba hili” Mwenzetu mmoja akasema.
“Lakini mbona hatuwaoni hao watu?” Mwingine akauliza.
“Ndiyo hatuelewi sasa” aliyesema mwanzo akamjibu.
Je wavuvi hao wametokea kwenye kisiwa gani hicho na ni kitu gani kitakachowatokea?
Iletee[emoji119][emoji119][emoji119]
 
Subra itakusaidia..usije ukamzini binti wa Rais...

Haya Mambo yapo Sana...Mimi nasumbuliwa na jini simjui.anaonekana anapenda nipige Puli...yawezekana anapenda shahawa....I just knew it... someone will reject it but it is....Dua zinasaidia...ananimaliza nguvu za kiume but ninazo bado napmbana nae...tangu Raman.... Nina miaka 27 na nimeoa 4 yrs katika ndoa.....

Nilikuwa nikipiga bao 4 ndani kwa ndani...saa hii...hata Niko na mke nakosa nguvu hamu ninayo na alfajir nikipiga mzigo....napiga kweli...kwa nn nguv Sina????


Huyu jini Alisha wahi kuninajisi...nilikuwa nimelala nikahisi nalawitiwa...

Hawa jamaa wapo na niwasumbufu, sijajua Kama ni sababu siku moja alinijia msichana mzur Sana....akaniambia wenzio wanakuacha...niliingia hotel flan kubwa Kula.. kweli nikaona gari inazunguka, nikanawa nlmikono nikatoka, nikawaulizlja jamaa kwa nn mnaniacha wakadai muda umeisha tuondoke, nikahoji ndio msiniambie?! Hapakuwa na jawabu la maana.....

Huyu msichana mrembo ndio uhusiano ukaanzia hapo..ni mzur kuliko kawaida...
Bado namhusisha na jini....hajaolewa yupo tu.
Namba ya simu yake tafadhali
 
SEHEMU YA 14



“Acha nifurahishe moyo wangu nisife na kinyongo”
“Sikuwa nikijua kuwa umchangamfu kiasi hicho”
“Mimi ni mchangamfu sana, sema hili jinni ndilo limeniharibia maisha yangu. Ningeweza kuliua ningeliua”
“Hata ukiliua utaondoka vipi hapa kisiwani?”
“Hayo yatakuwa masuala mengine, bora nimeshaliua”
“Kama boti yetu ingekuwa nzima tungekutorosha tukaenda Zanzibar”
“Halafu ungenioa huko huko”
“Upendavyo”
“Mimi ningependa unioe Zanzibar. Gharama zote angetoa baba yangu”
“Mimi nisingekuwa na amri zaidi ya kukusikiliza wewe”
Nilipomwambia hivyo Yasmin alifurahi sana. Chakula kilipokuwa tayari alikipekua sehemu mbili. Sehemu moja ilikuwa yetu mimi nay eye. Sehemu ya pili ilikuwa ya wenzetu.
“Sasa wapelekee halafu urudi tuje tule” Yasmin akaniambia.
Alinitilia chakula kwenye kapu nikaondoka. Wakati nakaribia kufka kwenye mlango wa kutokea, nikawaona wenzangu wamenifuata.
“Tumeona unachelewa, tukapata wasiwasi” Masudi akaniambia.
SASA ENDELEA
“Nilikuwa nasubiri chakula na ndicho hiki ninawaletea” nikamwambia Masudi.
“Sasa na sisi tumeshakuja. Kuna haja ya kwenda tena kule”
“Tunaweza kula hapa hapa”
Masudi akawatazama wenzake.
“Jamani tuleni hapa hapa, au mnasemaje?’ akawauliza.
“Popote tu tunaweza kula”
Nikarudi ndani na kuliweka lile kapu la chakula.
Yasmin alikuwa amesikia sauti zetu akatufuata.
“Jamani mmekuja huku huku?” akawauliza.
“Tuliona mwenzetu anachelewa tukapata wasiwasi. Tulidhani labda ameshikwa na Harishi” Masudi akamjibu.
“Hapana. Alikuwa anasubiri chakula, lakini mnaweza kula hapa hapa”
Yasmin akaandaa kile chakula kwenye mswala. Kwa vile wenzetu walikuwa wamekuja, tuliona tule pamoja. Yasmin akaleta na kile chakula kingine.
Tulipomaliza kula tuliendelea kuzungumza pale pale tukiwa pamoja na Yasmin.
Masudi alikuwa akimtania sana Yasmin huku akimsifia kwa uzuri. Yasmin alikuwa akichekacheka tu na kuficha uso wake uliokuwa umejaa aibu.
Masudi akaeleza kisa ambacho nilihisi kilikuwa cha uongo kwamba zamani alipokuwa anakaa Mombasa alipendana na msichana mmoja wa Kilamu.
“Msichana. Alikuwa mzuri huyo. Alinipenda na mimi nilimpenda lakini wanawake wa Mombasa hawaoleki bwana!”
“Kwanini?” nikamuuliza.
Wana gharama sana. Huyo msichana wangu alikuwa anaitwa Nargisi. Kila siku alikuwa amechorwa piku, utadhania mwari wa harusi”
“Sasa huyo atapata kweli muda wa kupika ukimuoa?” nikamuuliza.
“Ndio maana nilishindwa kumuoa. Nilikuwa nikijiambia huyu msichana sijamuoa yuko hivi, je nikimuoa atakuwaje, piku kila siku…safari haziishi”
“Mapenzi ya kweli yana gharama” Yasmin akamwambia.
“Ni kweli lakini gharama ya mwanamke wa Mombasa ni kubwa. Kwanza kunai le gharama ya miraa. Kila siku ni lazima umnunulie kilo moja ya miraa, tena ile miraa safi ya bei ghali”
“Wacha we!” Yasmin alimwambia kumtia jazba.
“Halafu wkati wa kula ile miraa ni lazima apate kokakola na chupa ya maji safi pamoja na mfuko mzima wa Big G. Zote ni pesa” Masudi aliendelea kueleza.
“Na wewe ulikuwa unakula?” nikamuuliza.
“Mimi nilikuwa nakula lakini si sana. Simalizi hata nusu lakini mwenzangu anaua kilo nzima. Akianza saa tisa hadi saa nne usiku hakuna kitu”
“Sasa akishakula hiyo miraa itamsaidia nini?” Yasmin akauliza.
“Anapata handasi” Masudi akamjibu.
“Handasi ni kitu gani?”
“Handasi ni kileo cha miraa. Wengine wanakiongezea na kungumanga. Wanasaga kungumanga, ule unga wake wanachanganya na kahawa. Ashiki yake ni hatari!”
Sote tukacheka. Yasmin ndio alicheka sana.
“Yaani mwanamke akitoka hapo ni lazima apate bwana!” Masudi aliendelea.
“Asipopata bwana inakuwaje?” Yasmin akamuuliza.
“Yaani anapokula miraa na kuchanganya na kahawa ya kungumanga tayari anakuwa na ahadi ya bwana”
“Kwa hiyo huyo mpenzi wako akishakula ndio mnakutana?’ Yasmin aliendelea kumuuliza. Maneno yalikuwa yamemkolea.
“Ndiyo maana yake”
“Unaonaje mapenzi yake?”
“Ni mapenzi adhimu. Sijapata kuona na sitamsahau yule msichana” Masudi kwa kutaka sifa aliongeza. “Na yeye pia hatanisahau kwani nilikuwa…mh!...hata havisemeki”
“Sema tu ulikuwaje?” Yasmin akamsisitizia.
“Mwenyewe alikuwa akiniambia penzi nililokuwa nikimpa hajalipata kwa mwanaume yeyote”
Hapo tulicheka tena. Lakini mimi nilicheka kwa kujua kuwa Masudi alikuwa akisema uongo kumfurahisha Yasmin. Na kwa kweli nilihisi alitaka kujipependekeza naye ili apendwe yeye.
“Sasa ilikuwaje mkaachana?’ nikamuuliza.
“Tuliachana baada ya mimi kurudi Unguja. Mama yangu aliniambia nirudi kwa sababu alikuwa akiishi peke yake”
“Baba yako alikuwa yuko wapi?” Yasmin akamuuliza.
“Alikuwa ameshakufa”
“Nani ambaye hajaoa katika nyinyi?”
ITAENDELEA
 
Mkali tupia hata moja tu nipate kulala mkuu"

Nasubiria kiongozi.
 
Back
Top Bottom