Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Hii simulizi inanikumbusha Unguja kulikua na mvuvi amepotea yy na wenzake.
Baadhi ya wenziwe wamepatikana wameshakufa na wengine hawajapatikana pamoja na yeye basi familia ikachukulia kama ameshakufa taratibu zote za mazishi pamoja na arubaini zikafanyika.
Baada ya miezi mitatu akarejea kwake watu wakawa wanamuogopa ni mkewe tu ndie aliyemuelewa alikuwa yupo kipindi cha eda mpaka leo hii mkewe jina lake limekufa anajuulikana kama kizuka tu.
 
16831207_1899205690105785_140789355008334865_n.jpg

MTUNZI : FAKI A FAKI


Sikuwahi kuona sherehe kubwa ya harusi kama ile niliyoiona katika visiwa vya Ngazija nchini Comoro mwaka mmoja uliopita.
Ilikuwa harusi ya binti wa Rais wa Moroco Yasmini binti Sharif Abdilatif aliyekuwa akolewa na mwana wa mkuu wa majeshi ya ulinzi wa Comoro
Abubakar Mustafa Al- Shiraz aliyekuwa akiishi Ufaransa.
Sisi tulikuwa tumetoka Zanzibar. Mke wa mkuu wa majeshi ya Comoro Kulthum alikuwa Mzanzibari tena Mkojani wa Pemba, ndiye aliyetoa mwaliko kwa ndugu zake walioko Zanzibar.
Zilitolewa kadi kumi za mwaliko kwa watu kumi. Kwa vile na mimi nilikuwa na nasaba na Kulthum nikapata kadi moja na tiketi ya ndege ya kwenda Ngazija.
Wakati ule nilikuwa na umri wa miaka ishirini na minne(24). Nilikuwa bado kijana na shughuli zangu zilikuwa ni uvuvi. Nilikuwa sijaoa bado lakini nilikuwa katika maandalizi ya kutafuta mchumba.
Ndege tuliyosafiri nayo ilifika Comoro saa kumi jioni. Ndoa ilikuwa inafungwa saa mbili usiku baada ya swala ya Inshaa katika msikiti wa Riadha, msikiti mkuu wa Ijumaa nchini humo.
Nyumbani kwa bwana harusi kulikuwa kumejaa shamra shamra. Kadhalika nyumbani kwa Rais Sharif Abdulatif nako kulikuwa hakutoshi.
Kulikuwa na hoteli mbili kubwa zilizokodishwa siku ile kwa ajili ya sherehe za harusi. Na kulikuwa na hoteli nyingine kadhaa zilizokodiwa kwa ajili ya wageni walioalikwa kutoka nchi mbalimbali.
Sisi tulifikia katika hoteli ya Zaharani. Jina la hoteli hiyo lilifanana na jina langu. Jina langu ni Zaharani Shazume. Hoteli hiyo ilikuwa jirani na msikiti wa Riadha mahali ambapo ndoa ya Yasmin na Abubakar ingefungwa usiku ule.
Kwa kawaida msikiti wa ijumaa hujaa watu siku za ijumaa lakini siku ile kwa mara ya kwanza ulijaa watu katika swala ya Inshaa.
Kulikuwa na ulinzi mkali wa polisi na maafisa usalama waliokuwa na kazi ya kuhakikisha usalama unakuwepo katika eneo hilo.
Nilijitahidi sana nipate safu ya mbele lakini sikuweza. Safu hiyo ilikuwa imejaa masheikh na maafisa usalama. Nilibahatika kupata safu ya tatu yake.
Baadaya swala ya isha Rais wa Comoro Sharif Abdulatif alitakiwa kutoa idhini ya kumuozesha mwanawe.
Wakati anatoa idhini alipokea simu hapo hapo iliyomtambulisha kuwa binti yake Yasmin alikuwa ameanguka nyumbani na alikuwa akitokwa na povu mdomoni.
Shughuli ya ufungishaji ndoa ikasimama. Hapo hapo Rais Abdulatif na wasaidizi wake pamoja na maafisa usalama walitoka kwenda nyumbani.
Habari iliyopatikana baadaye ilieleza kuwa Yasmini alikuwa ameanguka na kupoteza fahamu huku akitokwa na povu midomoni. Baba yake alipofika na kumuona aliamrisha apelekwe hospitali haraka.
Gari la hospitali lilikuwa limeshafika. Yasmin alipakiwa na kukimbizwa hospitali. Gari hilo la hospitali lilifuatana na gari la maafisa usalama na gari la rais mwenyewe.
Lakini gari alilopakiwa Yasmin likapata ajali kabla ya kufika hospitali. Tairi lake la mbele la upande wa kulia lilipasuka na kusababisha gari hilo kuyumba na kuligonga gari jingine kabla ya kupindukia kwenye mtaro uliokuwa kando ya barabara.
Heka heka ikawa kubwa!. Magari ya maafisa usalama yakasimama. Maafisa hao wakashuka na kukimbilia kutoa msaada. Dereva wa gari la hospitali alipotolewa alikutwa akiwa ameshakufa. Yasmin mwenyewe hakuonekana. Wauguzi wawili waliokuwa naye walikutwa wamezirai. Tukio hilo lilizua taharuki kubwa.
Rais Abdulatif hakuamini macho yake, akawa anauliza kwa ukali “Binti yangu yuko wapi?”
Lakini hakukuwa na aliyejua. Yasmin alikuwa ametoweka ghafla. Kila aliyeshuhudia alishangaa.
Harusi ikavunjika. Badala ya furaha sasa ikawa huzuni. Bwana harusi na mke wa Rais Sharif Abdullatif Bi Kulthum
walikuwa wanalia kutokana na muujiza huo.
Usiku ule ule Rais Abdullatif aliita masheikh Ikulu na kuwauliza kama walikuwa wanajua kilichomtokea binti yake.
Kila sheikh alisema lake. Wako waliomwambia kuwa binti yake alikuwa amechukuliwa na wachawi. Wako waliomwambia kuwa haikuwa muafaka kwa binti yake kuolewa na Abubakar ndiyo sababu tukio hilo limetokea. Na wako waliomwambia kuwa Yasmin alikuwa amechukuliwa na jini aliyekuwa amemchunuka.
Rais Abdullatif hakujua ashike kauli ya sheikh yupi. Kwa vile lilikuwa limeshamfika alikubaliana na masheikh wote na kuwataka masheikh hao kutumia elimu zao kumrudisha binti yake. Aliahidi mamilioni ya shilingi za ki Comoro kwa sheikh yeyote atakayefanikiwa kumrudisha Yasmin.
Licha ya Rais Abdullatif kusubiri kwa zaidi ya miezi mitatu. Hakukuwa na sheikh yeyote aliyefanikiwa kumrudisha Yasmin! Yasmin akabaki kuwa historia kwani hakupatikana tena. Ulikuwa msiba ambao kila mkazi wa Comro alihisi kuwa hautasahaulika.
Hivi sasa mwaka mmoja umeshapita tangu tukio hilo la kuhuzunisha litokee. Tangu wakati ule sikuwahi tena kurudi Moroco. Nilikuwa Unguja nikiendelea na shughuli zangu za uvuvi.
Sasa siku moja ambayo sitaisahau maishani mwangu tulikuwa kwenye boti letu tukielekea maji makuu kuvua samaki. Ndani ya boti hilo tulikuwa wavuvi saba.
Ilipofika saa nne asubuhi tulikuwa mbali sana. Boti yetu ilipigwa na dharuba kali. Mashine ya boti ikazima ghafla. Tilijaribu kuiwasha lakini boti haikuwaka. Ikawa inakokotwa na maji.
Tulipumzika kidogo kisha tulijaribu kuiwasha tena na tena lakini hatukufanikiwa kuiwasha Mashine ilitugomea kabisa. Hatukujua ilikuwa imepatwa na hitilafu gani.
Je nini kitawatokea wavuvi hao?
Hua nakukubali sana
 
Hii simulizi inanikumbusha Unguja kulikua na mvuvi amepotea yy na wenzake.
Baadhi ya wenziwe wamepatikana wameshakufa na wengine hawajapatikana pamoja na yeye basi familia ikachukulia kama ameshakufa taratibu zote za mazishi pamoja na arubaini zikafanyika.
Baada ya miezi mitatu akarejea kwake watu wakawa wanamuogopa ni mkewe tu ndie aliyemuelewa alikuwa yupo kipindi cha eda mpaka leo hii mkewe jina lake limekufa anajuulikana kama kizuka tu.
...nimeweka notification ON ukirudi nitag Mkuu
 
SEHEMU YA 03



Tulitoka katika kile chumba tukaingia katika chumba kingine. Pia tulikuta kitanda na makabati. Tukawa tunatazamana kwa mshangao. Kutoka hapo tulichangukana. Kila mmoja akawa anafungua chumba alichotaka na kuangalia ndani.
Mimi niliingia katika vyumba viwili. Nilipoingia chumba cha tatu nilishituka nilipomuona msichana mzuri amelala kitandani. Alikuwa amelala usingizi kabisa huku amejifinika shuka kuanzia miguuni hadi shingoni. Uso wake uliokuwa wazi ulikuwa umeelekea upande wangu.
Nilipomuona nilisita kwenye mlango na kujiuliza msichana huyo ni nani na kwanini alikuwa peke yake katika jumba hilo.
Baada ya kusita kidogo niliingia ndani. Nilikuwa nataka kuhakikisha kama alikuwa hai kweli au amekufa.
Nilipofika karibu yake, msichana huyo alifumbua macho ghafla. Akashituka aliponiona.
“Wewe nani?” akaniuliza kwa mshangao akitumia lugha ya kingazija ambayo nilikuwa siijui vizuri. Lakini nilimjibu kwa Kiswahili.
“Mimi ni mgeni katika kisiwa hiki na katika jumba hili, je wewe ni nani?”
Alikuwa anajua Kiswahili. Akanijibu kwa Kiswahili cha kipemba.
“Miye ni Yasmin, binti wa Rais Shariff Abdilatif wa Comoro!”
SASA ENDELEA
Nilishituka sana aliponiambia yeye ni binti wa Sharif Abdulatif wa Comoro.
Papo hapo nikakumbuka ile harusi iliyovunjika kati ya binti wa rais wa Comoro na mwana wa mkuu wa majeshi ya ulinzi nchini humo.
Mimi nilikuwa mmoja wa waalikwa kutoka Zanzibar na nikashuhudia maajabu. Yasmin alitoweka katika mazingira ya kutatanisha baada ya gari iliyokuwa inampeleka hospitali kupasuka tairi na kuingia kwenyenye mtaro. Yasmin alikuwa anakimbizwa hospitali baada ya kuanguka ghafla wakati baba yake Rais Sharif Abdulatif anataka kutoa idhini ya kumuozesha binti yake.
Baada ya kutoweka ghafla kwenye gari, Yasmin hakupatikana tena na sasa mwaka ulikuwa umeshapita.
Ingawa sikuwahi kuonana naye uso kwa uso lakini niliona picha zake katika magazeti na televisheni wakati habari zake zilipokuwa zinaandikwa na kutangazwa.
Alikuwa ndiye Yasmin kweli binti wa Rais Sharif Abdulatif wa Comoro.
Kwa kweli tukio la kumkuta ndani ya jumba hilo na katika kisiwa kile kisicho na watu, mbali ya kunishitua, liliniongezea hofu mara dufu.
“Wewe ni binti wa Rais wa Comoro” nikamuuliza kwa mshangao.
Huku akinyanyuka kwenye kitanda na kuketi msichana huyo alinijibu.
“Ndiye mimi. Rais Sharif Abdulatif ni baba yangu”
Nikiwa kwenye mshangao niliendelea kumtazama msichana huyo bila kummaliza. Alikuwa amevaa shumizi inayoonya. Alipoketi alijifunga ile shuka kwenye mwili wake kama mtu aliyekuwa anaona baridi. Lakini nilijua alikuwa anajisitiri kwa sababu sumizi aliyovaa ilikuwa inaonya.
Kwa tamaduni za kiislamu na za kule Comoro mwanamke hatakiwi kuonekana mwili wake pamoja na kichwa chake.
Lakini Yasmin kwa sababu ya kutaharuki alisahau kujifinika kichwa. Nywele zake za mawimbi zilizokuwa ndefu zilikuwa zimeshuka na kumfikia mabegani.
“Yasmin umefikaje huku?” nikamuuliza.
Yasmin akanitazama. Macho yake makubwa yenye mboni za rangi ya kahawia yalinifanya nikiri kimoyomoyo kuwa Yasmin alikuwa mzuri.
Badala ya Yasmin kunijibu, na yeye akaniuliza.
“Kwani wewe umefikaje hapa?”
“Mimi siko peke yangu, nina wenzangu na tumefika hapa kwa bahati mbaya. Sisi ni wavuvi kutoka Zanzibar. Chombo chetu kilipigwa na dharuba kikapata hitilafu. Kwa siku nne kilikuwa kinaelea kwenye maji, hatujui tunakokwenda. Leo siku ya tano ndio tumetokea kwenye kisiwa hiki”
“Huko ulikopita hadi umetokea hapa, umeona nini?”
“Tumekuta nyumba hazina watu. Pia tumekuta mafuvu na mifupa ya watu kila mahali”
“Basin a nyinyi ndio mtakuwa hivyo hivyo, hamtapona”
Yale maneno yalinitisha na kunifadhaisha.
“Yasmini kwanini unaniambia hivyo. Mimi ni ndugu yako wa Zanzibar. Hata katika harusi yako na mwana wa mkuu wa majeshi ya ulinzi wa Moroco nilialikwa na nilikuja Comoro lakini wewe ulitoweka katika mazingira ya ajabu. Na leo ndio nakuona hapa” nikamwambia Yasmin kwa hofu.
“Nashukuru kwamba leo nimetembelewa na ndugu yangu wa Zanzibar na nashukuru kwamba umenijua lakini naona uchungu kuwa nitayashuhudia mauti yako muda si mrefu”
>Kwanini unaniambia hivyo Yasmin?. Niambie”
Yasmin bdala ya kunijibu aliangua kilio.
Wenzangu mmoja mmoja wakaanza kuingia mle chumbani na kushangaa kumuona yule msichana akilia.
“Je ni nani huyu?” Mmoja wa wale wenzangu akaniuliza wakati wenzetu wengine walikuwa wamepigwa na butwaa.
“Ni msichana nimemkuta amelala humu chumbani. Nilipoingia alizinduka na kuniambia anaitwa Yasmin. Ni binti wa Rais wa Comoro” nikawaeleza.
“Ni binti wa Rais wa Comoro?” Baadhi ya wenzangu wakaniuliza kwa mshangao. Walidhani labda nilikosea kusema.
“Ndiyo, mwenyewe ameniambia hivyo na mimi pia namfahamu. Nilihudhuria katika harusi yake nchini Comoro mwaka uliopita.
“Si ilisemekana kuwa yule binti alitoweka?” Mmoja wa wenzangu akauliza.
“Ni kweli. Mimi pia nimeshangaa kumkuta katika kisiwa hiki, tena akiwa peke yake. Na amenieleza kitu cha kutisha”
“Kitu gani?”
“Mh! Ameniambia anaona uchungu kuwa atayashuhudia mauti yetu muda si mrefu!”
Wenzangu wote wakashituka, ndipo nilipojua kuwa hakuna mtu anayependa kufa.
“Kwanini amekwambia hivyo?” Sautu za kuuliza zilisikika kutoka kwa wenzangu.
“Ndio nilikuwa namuuliza, naona analia”
“Asilie, atueleze ili tujue…”
“Usilie dada yangu, nyamaza utueleze ili tujue jinsi ya kujihami” nikamwambia msichan huyo.
“Pia atueleze jinsi alivyofika katika kisiwa hiki cha ajabu” Mtu mwingine akasema.
Leta sehemu ya nne mkuu
 
Back
Top Bottom