Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Hii movie imeisha kizembe sana, memshindwa kumfungilia Harishi hata mara moja? Na hao wazungu wamekuja mapema mno, mngekula utamu hapo hata kawiki kazima nyoooo mtungaji atakuwa kalewa
 
Subra itakusaidia..usije ukamzini binti wa Rais...

Haya Mambo yapo Sana...Mimi nasumbuliwa na jini simjui.anaonekana anapenda nipige Punyeto....yawezekana anapenda shahawa....I just knew it... someone will reject it but it is....Dua zinanisaidia...ananimaliza nguvu za kiume but ninazo bado napambana nae...tangu zaman.... Nina miaka 27 sasa...na nimeoa 4 yrs katika ndoa.....

Nilikuwa nikipiga bao 4 ndani kwa ndani...saa hii...hata nikiwa na mke nakosa nguvu japo hamu ninayo na muda wa alfajir nikipiga mzigo....napiga kweli...kwa nn nguv Sina????


Huyu jini aliisha wahi kuninajisi.siku moja..nilikuwa nimelala nikahisi nalawitiwa...kitu kama maji baridii vikiingia mk.unduni pale pa kunyea aka hajakubwa. Nilisikitika sana

Hawa jamaa wapo na niwasumbufu, sijajua Kama ni sababu siku moja alinijia msichana mzur Sana....akaniambia wenzio wanakuacha...niliingia hotel flan kubwa Kula.. kweli nikaona gari inazunguka, nikanawa nlmikono nikatoka, nikawaulizlja jamaa kwa nn mnaniacha wakadai muda umeisha tuondoke, nikahoji ndio msiniambie?! Hapakuwa na jawabu la maana.....

Huyu msichana mrembo ndio uhusiano ukaanzia hapo..ni mzur kuliko kawaida...
Bado namhusisha na jini....hajaolewa yupo tu.
Alikupiga mashine mkuu? Duuh sasa mwanamke anakulawiti vipi? Hii habari ni ya kweli?
 
Hapo naona wazungu wakifanikiwa kutengeneza boti ya ya wale jamaa wa mwanzo,,safari ianze
 
Hii movie imeisha kizembe sana, memshindwa kumfungilia Harishi hata mara moja? Na hao wazungu wamekuja mapema mno, mngekula utamu hapo hata kawiki kazima nyoooo mtungaji atakuwa kalewa
Jamaa kajitahidi hadi leo hajaomba mzigo
 
wavuvi wajinga hawa.. Ningekuwa mimi ile chupa ya moshi ningeifunga kifuniko chake. Ili moshi ukijaa mchizi ashindwe kutokea mbona kazi rahisi tu hiyo.
hahaha teh teh mze baba hapo juu kasema et umepeleka utam mbele teh teh
 
Alikupiga mashine mkuu? Duuh sasa mwanamke anakulawiti vipi? Hii habari ni ya kweli?
hahaa sio mwanamke" kapigwa mashine na mwanaume ..then baadae ndio akajakumpata huyo mwanamke"... daaahh alinichekesha sana jamaa
 
SEHEMU YA 27


“Sasa kule nyumbani Comoro wanajua uko wapi?” Yule Mzanzibari alendelea kumuuliza Yasmin.
“Wao hawajui niko wapi na kwa sasa wanaamini kuwa nimeshakufa”
“Je wakikuona tena itakuwaje?”
“Itakuwa mshangao mkubwa. Wazazi wangu hawataamini”
“Ni mkasa wa kutisha kweli na unastahili kuandikwa katika historia ya Comoro”
“Hapo ni kama tutanusurika na nitarudi kwetu kwani kama niivyowambia mwanzo hapa hatutarajii kupata msaada wowote. Hatima yetu tumemwachia Mwenyezi Mungu”
SASA ENDELEA....
Wakati tunazungumza tulikuwa tumeshaondoka katika ile nyumba aliyouawa Shazume na tulikuwa tunaelekea ufukweni mwa bahari. Tulipofika ufukweni Yasmin akataka tukae kidogo tupumzike kwani tulikuwa tumetembea mwendo mrefu.
“Tangu niletwe katika kisiwa hiki, nyinyi ni wageni wangu wa pili kufika hapa” Yasmin aliwambia wale watu wakati tumeketi.
“Wa kwanza walikuwa kina nani” Mzanzibari akamuuliza.
“Wa kwanza walikuwa ni hao watu saba ambao waliuawa na Harishi na kubaki mtu mmoja mliyenikuta naye”
Yasmin alinionesha mimi.
“Ulikuwa unakula nini?”
“Harishi alikuwa akiniletea chakula”
“yeye alikuwa anakipata wapi?”
“Anaiba kwenye masoko. Harishi ni mwizi na anatembea sehemu nyingi kuanzia kwetu Comoro hadi Afrika Mashariki”
Tulikaa pale ufukweni tukazungumza na wale wageni hadi Yasmin aliposema kuwa anhitaji kurudi nyumbani.
Wakati tunarudi yule Mzanzibari aliyekuwa pamoja na wale wazungu alituambia kuwa boti waliyokuwa wakitalii nayo ilipopigwa na dharuba waliweza kupiga simu Zanzibar kuomba msaada lakini baadaye mawasiliano yalikatika.
“Boti ya polisi wanamaji inaweza kuwa inatutafuta baharini” akatuambia.
“Lakini haitawapata, mmeshafika huku” Yasmin akamwambia.
“Ni vizuri kama tungeendelea kukaa ufukweni ili tuangalie vyombo vinavyopita. Tunaweza kuwaona”
“Sawa. Mnaweza kwenda kukaa. Tutawafuata baadaye”
Mzanzibari huyo alizungumza na wale wazungu na kukubaliana kuwa wabaki kule kule ufukweni. Tukawaacha na kurudi kwenye lile jumba.
“Unajua ni kwanini nimetaka turudi?” Yasmin akaniuliza.
“Sijui”
“Ninataka kupika”
“Ukipika tutawapelekea chakula na wale jamaa?”
“Tutawapelekea. Wameshakuwa wageni wetu”
“Nilitaka kujua hilo tu”
“Jibu umeshalipata?”
“Nimelipata”
“Sawa” Yasmin akaanza kushughulika. Baada ya masaa mawili akawa ameshaivisha wali na mboga ya uyoga.
“Unaonaje ukaenda kuwaita tuje tule nao hapa?” Yasmi akaniuliza.
“Ni sawa. Ngoja nikawaite”
Nikatoka. Wakati nachanganya mwendo kuelekea ufukweni nilisikia mlio wa helikopta. Ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kusikia mlio kama huo tangu tulipofika katika kisiwa hicho. Nikashituka na kutazama juu. Niliona helikopta ikipita chini chini. Ilinipita ikaendelea kwenda na kupote mbele yangu.
Laiti ningekuwa na uwezo wa kuisimamisha, ningeisimamisha lakini sikujua ningeisimamishaje. Nikabaki kuikodolea macho huku nikisikitika.
Mlio wa helikopta hiyo ulikuwa bado ukisikika masikioni mwangu. Ilikuwa kama inayozunguka kwenye hicho kisiwa. Ghafla nikausikia tena mlio huo ukitokea kwa nyuma yangu. Nikageuka na kuitazama. Ilinipita tena na kuendelea kuzunguka.
Ghafla kwa mbele yangu nikasikia kelele za watu zikitokea kwenye miti. Baadaye kidogo nikawaona wale wazungu pamoja na yule mswahili wamevua mashati wakiifukuza ile helikopta huku wakiipungia mashati yao.
Ile helikopta ilirudi tena upande niliokuwa mimi. Sasa mwendo wake ulikuwa wa taratibu na ilikuwa chini chini sana. Ilitafuta sehemu iliyokuwa wazi ikatua. Kitendo cha kutua kwa helikopta hiyo kilinipa furaha na kunirudishia matumaini. Nikajua msada umeshapatikana. Nilitaka nirudi mbio nikamchukue Yasmin lakini naye alishausikia mlio wa helikopta hiyo. Alitoka na kuja mbio.
Ndani ya ile helikopta walishuka watu watatu. Moja alikuwa na mavazi ya kipolisi lakini sikuweza kujua alikuwa polisi wa wapi na pia sikuweza kujua ile helikopta ilitokea wapi na ilikuwa inatafuta nini kwenye kile kisiwa.
Watu hao waliposhuka walitutazama.Yule polisi akauliza.
“Yinyi ndio ambao mliripoti kuwa chombo chenu kinazama?” Alikuwa akimtazama yule Mzanzibar aliyevua shati pamoja na wale wazungu.
“Ndiyo sisi” Mzanzibari huyo akajibu haraka.
“Na hao wataliiwa Kifaransa ndio hawa mabwana?”
Aliwaonesha wale wazungu.
“Ndio hawa niliokuwa nao kwenye boti. Tuliogelea hadi kwenye kisiwa hiki”
“Tumezunguka sana baharini kuwatafuta bila mafanikio. Huku tulikuja kubahatisha tu, ndio tunaona watu wanatupungia. Poleni sana”
“Tunashukurusana kwa msaada wenu”
“Tuliambiwa mlikuwa watu watatu, na hawa watu wengine ni kina nani?”
“Ndio wenyeji wetu tuliowakuta hapa kisiwani, hakuna watu wengine”
“Ninachofahamu mimi ni kuwa hiki kisiwa kilihamwa na watu. Sasa hawa wametokea wapi?”
“Wametueleza habari ya kusisimua sana. Huyu msichana ni binti wa Rais wa Comoro. Aliletwa katika kisiwa hiki katika mazingira ya kutatanisha,mwe
nyewe akiwa hajifahamu. Na ameishi hapa kwa zaidi ya mwaka mmoja akiwa peke yake”
Watu hao watatu waliotoka kwenye helikopta walipatwa na mshangao waliposikia habari ile.
“Eti ni kweli?” Yule polisi akaniuliza.
“Ni kweli” Yasmin akamjibu.
“Wewe ni binti wa Rais wa Comoro?”
“Ndiyo”
“Ulifikaje katika kisiwa hiki kisichokuwa na watu na ulikuwa unaishije?”
Yasmin akaeleza kisa chake kuanzia alivyokumbwa na Harishi katika siku ya harusi yake hadi kuletwa katika kisiwa kile.
Akeleza jinsi alivyokuwa anaishi.
“Wageni wangu wa kwanza kufika katika kisiwa hiki ni huyu kaka na wenzake”
Alinionesha mimi.
ITAENDELEA
 
Yaani wanakaribia kufa na bado wanapatwa na muda wa kutongozana na kutiana nyege... hao wavuvi mawhack kweli.
Halafu pia nilitaka kujua zile maiti za wenzao walikuwa wanaziona asubuhi palipokucha au kunguru walikula ile miili usiku usiku!!?
 
Shida yako kanungila story zako huishia kati kati tu wakati watu tuna shauku ya kujua ending kama "Jini mweusi"- ulituishia penye uhondo..
 
Back
Top Bottom