Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

SEHEMU YA 28



“Wametueleza habari ya kusisimua sana. Huyu msichana ni binti wa Rais wa Comoro. Aliletwa katika kisiwa hiki katika mazingira ya kutatanisha,mwe
nyewe akiwa hajifahamu. Na ameishi hapa kwa zaidi ya mwaka mmoja akiwa peke yake”
Watu hao watatu waliotoka kwenye helikopta walipatwa na mshangao waliposikia habari ile.
“Eti ni kweli?” Yule polisi akaniuliza.
“Ni kweli” Yasmin akamjibu.
“Wewe ni binti wa Rais wa Comoro?”
“Ndiyo”
“Ulifikaje katika kisiwa hiki kisichokuwa na watu na ulikuwa unaishije?”
Yasmin akaeleza kisa chake kuanzia alivyokumbwa na Harishi katika siku ya harusi yake hadi kuletwa katika kisiwa kile.
Akeleza jinsi alivyokuwa anaishi.
“Wageni wangu wa kwanza kufika katika kisiwa hiki ni huyu kaka na wenzake”
Alinionesha mimi.
SASA ENDELEA...
“Wenzake wote waliuawa na Harishi na kubaki yeye peke yake. Siku yake ya kuuawa ilikuwa ni leo lakini Mungu mkubwa, amenusurika” Yasmin akaeleza.
Alilieleza tukio zima la kumfungia Harishi kwenye chupa lililotokea usiku uliopita.
“Hatukudhani kuwa ungekuwa mwisho wake. Sisi sote tulikuwa tumeshapanga kufa”
“Sasa ikawaje?” Polisi aliendelea kumuuliza kwa shauku.
“Harishi alishindwa kutoka ndani ya chupa na leo asubuhi tukaenda kuizamisha baharini”
“Ni habari kubwa nay a kushangaza kwa kweli. Unaweza kwenda kutuonesha nyumba uliyokuwa unaishi?”
“Ninaweza. Twendeni”
Yasmin akaliongoza kundi hilo la watu kuelekea katika lile jumba alilokuwa anakaa.
Watu hao waliingia ndani na kujionea jumba hilo lilivyokuwa. Yasmin aliwatembeza sehemu zote za jumba hilo hadi katika chumba alichokuwa analala.
Watu hao walimpa pole na kumsifu kuwa alikuwa msichana jasiri aliyeweza kuishi katika mazingira kama yale.
“Leo imekuwa ni siku yako ya uokozi, wewe na mwenzako” polisi aliyetoka kwenye helikopta alimwambia na kuongeza.
“Washukuru hawa watalii ambao chombo chao kilizama kwani wao ndio sababu ya sisi kufika hapa na kuwagundua nyinyi”
“Nawashukuru nyote kwa jumla, hawa watalii na nyinyi mliokuja kutuokoa” Yasmin akawambia watu hao huku akitabasamu.
“Sasa twendeni tukajipakie tuondoke” Polisi huyo akatuambia.
Yasmin akanitazama.
“Hatutakula tena?” akaniuliza.
“Hata njaa yenyewe siioni, kwaniwewe unahitaji tena kula?”
‘Basi ningojeni nibadili hizi nguo zangu”
Yasmin akaingia chumbani kwake haraka. Yule polisi akawambia wenzake.
“Unaona kama alikuwa anaishi maisha ya kawaida kumbe alikuwa katika mazingira magumu”
“Ameyazoea” Yule Mzanzibari akasema.
“Na pia ni jasiri sana” na mimi nikati akauli. “Mimi nimekaa hapa kwa siku chache tu lakini nimeshachoka. Inakuwaje kwa yeye aliyekaa kwa zaidi ya mwaka?”
Wote wakatikisa vichwa.
Baadaya robo saa hivi Yasmin alitoka. Alikuwa amebadili nguo na kuvaa vazi jingine lililokuwa limempendeza na kufanya aonekane kama malkia. Vazi hilo lilikuwa ni moja ya mavazi aliyokuwa akiletewa na Harishi. Alikuwa amejitia manukato yaliyokuwa yakinukia vizuri na nywele zake aliziweka katika mtindo wa Kikomoro.
Alikuwa ameshika mkoba wa kike mkono mmoja na mkono mwingine alishika begi kama msafiri.
“Hili vazi umelipata wapi?” Yule polisi akamuuliza.
“Nililipata kutoka kwa huyo jini. Alikuwa akiniletea nguo”
“Na hilo begi na huo mkoba?”
“Vyote”
Watu wote wakatazamana kwa mshangao.
Tulitoka katika lile jumba. Wakati tunatoka Yasmin aligeuka juma akalitazama jumba hilo kwa mara ya mwisho. Sikujua alikuwa akiwaza nini. Baada ya kulitazama kwa sekunde chache aligeuka mbele na kuendelea na safari.
“Lete begi nikusaidie” nikamwambia.
Nilimpokea begi. Lilikuwa zito kiasi.
“Umetia nini?” nikamuuliza.
“Mna vitu vyangu”
“Umeamua kuondoka navyo”
“Nataka wazazi wangu wakavione”
“Naamini watafurahi kukuona”
“Na mimi nitafurahi kuwaona”
“Tulifika mahali ilipoachwa helikopta. Rubani akatufundisha jinsi ya kujipakia kwenye helikopta.
“Mnapotaka kupanda helikopta mnainama namna hii ili kukwepa mapangaboi na hata wakati wa kushuka mnainama” akatuambia huku akituonesha jinsi ya kuinama.
Yasmin ndiye aliyetakiwa ajipakie kwanza. Baada ya Yasmin kujipakia tulifuatia sisi.
Sote tulipokuwa ndani ya helikopta, helikopta ikapaa juu na kuanza safari. Nilimuona Yasmin akitazama chini kupitia kwenye vioo. Bila shaka macho yake yalikuwa yanaagana na kisiwa hicho alichokikaa kwa zaidi ya mwaka mmoja akiwa peke yake na asiye na matumaini ya kunusurika.
Kwa upande wangu nilikuwa siamini kuwa tunaondoka. Niliona kama niko kwenye ndoto.
Nasaha za Yasmin zilikuwa zimetimia siku ile. Nilikumbuka kuwa aliwahi kuniambia kuwa aliota ninamuua Harishi na kumuokoa yeye. Wakati huo niliona kama maneno ya mzaha lakini kweli yametimia. Bila kutegemea nimemzamisha Harishi chini ya bahari na hatukutegemea kama angeweza kutoka tena.
Pia nilikumbuka jinsi Yasmin alivyokuwa akinipa moyo kuwa tutaokoka. Na siku ile tukaokoka kweli.
Wakati helikopta ikizidi kuyoyoma na Yasminakiendele
a kukiangalia kisiwa hicho, pengine akikumbuka enzi zake na Harishi, nilikumbuka jambo moja tena jambo muhimu.
Niliikumbuka ahadi yetu ya kumuoa Yasmin pindi tutakaponusurika na kurudi makwetu.
Sikudhani kuwa Yasmin alikuwa angali akiikumbuka ahadi ile japokuwa alinipa siku chache tu zilizopita
Niliamini kuwa kwa vile tulikuwa tumeshaokolewa mawazo ya Yasmin yanaweza kuwa yamebadilika. Kule aliniona kama mwenza wake kwa vile tulikuwa kwenye kifungo. Sote tulikuwa sawa. Lakini tukifika huko tunakokwenda yeye atakuwa binti wa rais mwenye hadhi na heshima, na mimi nitakuwa mvuvi nisiye na thamani yoyote. Sikudhni kama nitakuwa na maana tena kwake.
Helikopta sasa ilikuwa ikipita juu ya Bahari ya Hindi. Yasmin aliacha kutazama chini, sasa akawa anatazama mbele. Kwa vile viti vyetu vilikuwa vinapakana aligeuza uso akanitazama mimi. Nilidhani alitaka kuniambia kitu. Na mimi nikamtazama. Lakini hakuniambia kitu. Nikauona uso wake ukichanua tabasamu. Na mimi nikatabasamu. Baada ya hapo aliugeuza uso wake mbele.
Sikuweza kujua alikuwa akiwaza nini au aliwazia nini aliponitazama na kutabasamu lakini vyovyote ambavyo aliwaza alikuwa ameniwazia vizuri.
Wakati helikopta ikiendelea kupasua bahari niligeuka nyuma kuangalia kwenye vioo vilivyokuwa vimeizunguka helikopta nzima. Nilikuwa naangalia kile kisiwa tulichokuwa tumekiacha kwa mbali. Tuliendelea kukiacha kadiri helikopta ilivyozidi kusonga mbele.
Hatimaye tulikuwa katikati ya bahari. Hatukuona nchi tena. Baadaye tuliona mitumbwi ya wavuvi wakivua samaki. Baada ya muda ambao sikuweza kuukadiria tuliona nchi kwa mbali. Ilianza kutokea mbele yetu kama chuguu ya rangi ya kijani iliyochukua eneo kubwa. Kadiri tulivyozidi kwenda chuguu hiyo ilizidi kuonekana kubwa.
Sasa tuliweza kuona miti kwa mbali. Kijani tulichokuwa tunakiona ilikuwa miti iliyokuwa imeenea katika ardhi. Majumba ya ghorofa na barabara sasa vilionekana waziwazi. Nikajiambia kwamba tulikuwa tumekitokea kisiwa cha Unguja.
Muda si muda tukawa tumeivuka bahari. Sasa tulikuwa tunapita juu ya kisiwa cha kwetu baada ya kukitoka kile kisiwa cha kifo. Nilishukuru sana.
Tuliona vespa, bajaji na magari yanayokokotwa na punda yakipita chini yetu. Nikawa natabasamu peke yangu.
“Yasmin unakuona kwetu?” nikamwambia Yasmin.
“Ahaa ndio hapa!” Yasmin akaniuliza.
“Hapa ni Zanzibar. Kisiwa hiki kinaitwa Unguja”
“Uliniambia wewe unatoka Pemba”
“Pemba ni kwetu na Unguja pia kwetu. Yote ni Zanzibar moja”
Yasmin akatabasamu.
“Nimefurahi kufika kwenu. Nitawaona wazazi wako na ndugu
zako”
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 29


Tuliona vespa, bajaji na magari yanayokokotwa na punda yakipita chini yetu. Nikawa natabasamu peke yangu.
“Yasmin unakuona kwetu?” nikamwambia Yasmin.
“Ahaa ndio hapa!” Yasmin akaniuliza.
“Hapa ni Zanzibar. Kisiwa hiki kinaitwa Unguja”
“Uliniambia wewe unatoka Pemba”
“Pemba ni kwetu na Unguja pia kwetu. Yote ni Zanzibar moja”
Yasmin akatabasamu.
“Nimefurahi kufika kwenu. Nitawaona wazazi wako na ndugu
zako”
SASA ENDELEA...
Wakati nazungumza na yasmin helikopta ilikuwa inatua kwenye kiwanja cha ndege. Tukaacha mazungumzo na kuchungulia kwenye madirisha. Tuliona jingo la kiwanja cha ndege kwa mbele. Pia tuliona ndege kadhaa zikiwa zimeegeshwa huku wafanyakazi wakienda huku na huko.
Helikopta ilipotua tulishuka
Kwa vile rubani alikuwa akifanya mawasiliano tangu tukiwa juu. Tulikuta maofisa wanne wa polisi wakitusubiri. Polisi tuliyekuwa naye aliwapa maelezo ya zoezi lililofanyika. Akawaeleza pia tulivyopatikana katika kile kisiwa.
Polisi hao walituchukua katika chumba kimoja wakaanza kuwahoji wale wazungu pamoja na mwendesha boti waliyekuwa naye. Baada ya wao kutoa maelezo lilikuja gari likawachukua. Tukaanza kuhojiwa mimi na Yasmin. Maelezo yetu ndio yaliyowaacha hoi maofisa hao.
“Unasema wewe ni bini wa rais wa Comoro na ulikumbwa na jinni aliyekupeleka katika hicho kisiwa mwaka mmoja uliopita?” Afisa mmoja akamuuliza Yasmin.
“Ndiyo”
Niliposema “ndiyo” maofisa hao walitazamana kwa mshangao.
“Hebu tueleze ulivyofikishwa katika kisiwa hicho kutoka Comoro?” Afisa huyo akaendelea kumuuliza.
“Sijui. Ninachokumbuka ni kwamba nilikuwa kwenye sherehe ya harusi yangu nikaanguka na kupoteza fahamu. Nilipozinduka nikajikuta niko katika kile kisiwa ndani ya lile jumba nililokuwa ninaishi” Yasmin aliendelea kueleza.
“Ulijuaje kuwa ulikumbwa na jinni?’
“Wakati nazinduka nilimuona jinni mwenyewe. Aliniambia anaitwa Harishi na kwamba yeye ndiye aliyenikumba na kunileta pale”
“Alikuwa anataka nini kwako?”
“Alikuwa anataka niishi naye kama mke wake”
“Na ukawa unaishi naye?”
“Sikuwa na la kufanya zaidi ya kukubali”
“Ulikuwa unapata wapi chakula na mahitaji mengine?”
“Alikuwa ananiletea yeye chakula na nguo”
“Anavipata wapi?”
“Aliniambia kuwa anaiba kwenye maduka”
“Wapi?”
“Alikuwa anazunguka sehemu nyingi za Afrika Mashariki pamoja na Comoro”
Tumeambiwa kwamba kisiwa ulichokuwa unaishi wewe hakina watu isipokuwa nyumba tupu, ni kwanini?”
“Harishi alinieleza kuwa watu waliokuwa wakiishi katika kisiwa kile aliwaua yeye kwa kuwafyonza damu na kula bongo zao. chakula chake kilikuwa damu na ubongo”
Maafisa hao wakatazamana tena kwa mshangao.
“Chakula chake kilikuwa damu na ubongo wa binaadamu?” Afisa huyo akamuuliza tena Yasmin.
“Ndiyo” Yasmin alimjibu.
“Kwanini wewe hakukula?”
“Mimi alinichukulia kama mke wake”
“Na tuliambiwa kwamba kuna watu saba ambao chombo chao kiliharibika baharini na walifikakatika kile kisiwa, ni kina nani?”
“Mmojawapo ni huyu hapa” Yasmin alinionesha mimi na kuongeza.
“Walifikapale wakiwa watu saba wakauawa na Harishi akabaki yeye peke yake”
“Kwanini yeye hakuuawa?”
“Kuna kisa kirefu kimepita”
“Tunataka tukisikie”
Yasmin akawaeleza yaliyotokea hadi tukaweza kumzamisha Harishi chini ya bahari akiwa ndani ya chupa.
Baada ya Yasmin kuhojiwa nilihojiwa mimi. Nilijieleza kuwa nilikuwa Mzanzibari na kazi yangu ilikuwa uvuvi. Nikaeleza jinsi nilivyofika katika kisiwa kile na kumkuta Yasmin ndani ya lile jumba.
Nilipomaliza maelezo yangu simu zilipigwa sehemu mbalimbali. Haukupita muda mrefu maofisa usalama wa ikulu pamoja na waziri wa nchi ofisi ya raisi walifika kiwanja cha ndege.
Baada ya kupata maelezo yetu, waziri wan chi alimuuliza Yasmin kama kweli alikuwa binti wa rais wa Comoro.
Yasmin akasisitiza kuwa alikuwa binti wa rais huyo na akaomba aunganishwe naye kwenye simu.
Taarifa za Yasmin zilipofika ikulu, Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi iliwasiliana na Wizara ya mambo ya nje ya Comoro.
Mpaka inafika saa kumi na moja jioni ndege ya serikali iliyotoka Comoro ikiwa imempakia kaka wa Yasmin ambaye alikuwa kanali wa jeshi pamoja na maofisa usalama wa ikulu ya Comoro ilitua kiwanja cha ndege cha Unguja.
Watu hao walipokewa na mkurugenzi wa usalama na kupelekwa kukutanishwa na Yasmin ambaye mpaka wakati huo nilikuwa pamoja naye.
Kaka wa Yasmin Kanali Umar Sharif Abdilatif alipomuona Yasmin alishituka. Na Yasmin naye alishituka. Walitazamana kwa sekunde kadhaa kabla ya kukimbiliana na kukumbatiana kwa furaha na majonzi.
Maofisa usalama waliotoka ikulu ya Comoro ambao walikuwa wakimfahamu Yasmin nao walishangaa walipomuona kwani taarifa zilizokuwa nchini mwao zilionesha kuwa Yasmin alipotea katika mazingira ya kutatanisha wakati wa harusi yake zaidi ya mwaka mmoja uliopita.
Baada ya maofisa hao kumsalimia Yasmin walithibitisha kwamba alikuwa binti wa Rais Sharif Abdulatif aliyepotea nchini mwao katika mazingira ya kutatanisha.
Wakati huo Yasmin alikuwa akitiriikwa na machozi kwa kumuona kaka yake.
Yasmin aliwaeleza masahibu yaliyokuwa yamemtokea, maelezo ambayo yalimshitua kaka yake pamoja na maofisa hao.
Baada ya kuthibitishwa kwamba Yasmin alikuwa binti wa Rais wa Comoro aliitwa ikulu pamoja na kaka yake. Yasmin aliomba na mimi niwemo kwenye msafara huo. Ombi lake lilikubaliwa. Nilipatiwa mavazi mengine tukapakiwa kwenye gari kupelekwa ikulu ambako tulikutana na rais wa Zanzibar.
Rais wa Zanzibar alimsikiliza Yasmin na kushangazwa na maelezo ya binti huyo wakati akimsimulia masahibu aliyokutana nayo.
“Hata hivyo wewe ni shujaa kwa sababu hukukata tama” Rais alimwambia Yasmin. Pia alinipongeza mimi kwa kunusurika kufa.
“Mkasa uliowakuta ni historia kubwa ya visiwa vyetu” Rais aliendelea kutuambia.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 29


Tuliona vespa, bajaji na magari yanayokokotwa na punda yakipita chini yetu. Nikawa natabasamu peke yangu.
“Yasmin unakuona kwetu?” nikamwambia Yasmin.
“Ahaa ndio hapa!” Yasmin akaniuliza.
“Hapa ni Zanzibar. Kisiwa hiki kinaitwa Unguja”
“Uliniambia wewe unatoka Pemba”
“Pemba ni kwetu na Unguja pia kwetu. Yote ni Zanzibar moja”
Yasmin akatabasamu.
“Nimefurahi kufika kwenu. Nitawaona wazazi wako na ndugu
zako”
SASA ENDELEA...
Wakati nazungumza na yasmin helikopta ilikuwa inatua kwenye kiwanja cha ndege. Tukaacha mazungumzo na kuchungulia kwenye madirisha. Tuliona jingo la kiwanja cha ndege kwa mbele. Pia tuliona ndege kadhaa zikiwa zimeegeshwa huku wafanyakazi wakienda huku na huko.
Helikopta ilipotua tulishuka
Kwa vile rubani alikuwa akifanya mawasiliano tangu tukiwa juu. Tulikuta maofisa wanne wa polisi wakitusubiri. Polisi tuliyekuwa naye aliwapa maelezo ya zoezi lililofanyika. Akawaeleza pia tulivyopatikana katika kile kisiwa.
Polisi hao walituchukua katika chumba kimoja wakaanza kuwahoji wale wazungu pamoja na mwendesha boti waliyekuwa naye. Baada ya wao kutoa maelezo lilikuja gari likawachukua. Tukaanza kuhojiwa mimi na Yasmin. Maelezo yetu ndio yaliyowaacha hoi maofisa hao.
“Unasema wewe ni bini wa rais wa Comoro na ulikumbwa na jinni aliyekupeleka katika hicho kisiwa mwaka mmoja uliopita?” Afisa mmoja akamuuliza Yasmin.
“Ndiyo”
Niliposema “ndiyo” maofisa hao walitazamana kwa mshangao.
“Hebu tueleze ulivyofikishwa katika kisiwa hicho kutoka Comoro?” Afisa huyo akaendelea kumuuliza.
“Sijui. Ninachokumbuka ni kwamba nilikuwa kwenye sherehe ya harusi yangu nikaanguka na kupoteza fahamu. Nilipozinduka nikajikuta niko katika kile kisiwa ndani ya lile jumba nililokuwa ninaishi” Yasmin aliendelea kueleza.
“Ulijuaje kuwa ulikumbwa na jinni?’
“Wakati nazinduka nilimuona jinni mwenyewe. Aliniambia anaitwa Harishi na kwamba yeye ndiye aliyenikumba na kunileta pale”
“Alikuwa anataka nini kwako?”
“Alikuwa anataka niishi naye kama mke wake”
“Na ukawa unaishi naye?”
“Sikuwa na la kufanya zaidi ya kukubali”
“Ulikuwa unapata wapi chakula na mahitaji mengine?”
“Alikuwa ananiletea yeye chakula na nguo”
“Anavipata wapi?”
“Aliniambia kuwa anaiba kwenye maduka”
“Wapi?”
“Alikuwa anazunguka sehemu nyingi za Afrika Mashariki pamoja na Comoro”
Tumeambiwa kwamba kisiwa ulichokuwa unaishi wewe hakina watu isipokuwa nyumba tupu, ni kwanini?”
“Harishi alinieleza kuwa watu waliokuwa wakiishi katika kisiwa kile aliwaua yeye kwa kuwafyonza damu na kula bongo zao. chakula chake kilikuwa damu na ubongo”
Maafisa hao wakatazamana tena kwa mshangao.
“Chakula chake kilikuwa damu na ubongo wa binaadamu?” Afisa huyo akamuuliza tena Yasmin.
“Ndiyo” Yasmin alimjibu.
“Kwanini wewe hakukula?”
“Mimi alinichukulia kama mke wake”
“Na tuliambiwa kwamba kuna watu saba ambao chombo chao kiliharibika baharini na walifikakatika kile kisiwa, ni kina nani?”
“Mmojawapo ni huyu hapa” Yasmin alinionesha mimi na kuongeza.
“Walifikapale wakiwa watu saba wakauawa na Harishi akabaki yeye peke yake”
“Kwanini yeye hakuuawa?”
“Kuna kisa kirefu kimepita”
“Tunataka tukisikie”
Yasmin akawaeleza yaliyotokea hadi tukaweza kumzamisha Harishi chini ya bahari akiwa ndani ya chupa.
Baada ya Yasmin kuhojiwa nilihojiwa mimi. Nilijieleza kuwa nilikuwa Mzanzibari na kazi yangu ilikuwa uvuvi. Nikaeleza jinsi nilivyofika katika kisiwa kile na kumkuta Yasmin ndani ya lile jumba.
Nilipomaliza maelezo yangu simu zilipigwa sehemu mbalimbali. Haukupita muda mrefu maofisa usalama wa ikulu pamoja na waziri wa nchi ofisi ya raisi walifika kiwanja cha ndege.
Baada ya kupata maelezo yetu, waziri wan chi alimuuliza Yasmin kama kweli alikuwa binti wa rais wa Comoro.
Yasmin akasisitiza kuwa alikuwa binti wa rais huyo na akaomba aunganishwe naye kwenye simu.
Taarifa za Yasmin zilipofika ikulu, Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi iliwasiliana na Wizara ya mambo ya nje ya Comoro.
Mpaka inafika saa kumi na moja jioni ndege ya serikali iliyotoka Comoro ikiwa imempakia kaka wa Yasmin ambaye alikuwa kanali wa jeshi pamoja na maofisa usalama wa ikulu ya Comoro ilitua kiwanja cha ndege cha Unguja.
Watu hao walipokewa na mkurugenzi wa usalama na kupelekwa kukutanishwa na Yasmin ambaye mpaka wakati huo nilikuwa pamoja naye.
Kaka wa Yasmin Kanali Umar Sharif Abdilatif alipomuona Yasmin alishituka. Na Yasmin naye alishituka. Walitazamana kwa sekunde kadhaa kabla ya kukimbiliana na kukumbatiana kwa furaha na majonzi.
Maofisa usalama waliotoka ikulu ya Comoro ambao walikuwa wakimfahamu Yasmin nao walishangaa walipomuona kwani taarifa zilizokuwa nchini mwao zilionesha kuwa Yasmin alipotea katika mazingira ya kutatanisha wakati wa harusi yake zaidi ya mwaka mmoja uliopita.
Baada ya maofisa hao kumsalimia Yasmin walithibitisha kwamba alikuwa binti wa Rais Sharif Abdulatif aliyepotea nchini mwao katika mazingira ya kutatanisha.
Wakati huo Yasmin alikuwa akitiriikwa na machozi kwa kumuona kaka yake.
Yasmin aliwaeleza masahibu yaliyokuwa yamemtokea, maelezo ambayo yalimshitua kaka yake pamoja na maofisa hao.
Baada ya kuthibitishwa kwamba Yasmin alikuwa binti wa Rais wa Comoro aliitwa ikulu pamoja na kaka yake. Yasmin aliomba na mimi niwemo kwenye msafara huo. Ombi lake lilikubaliwa. Nilipatiwa mavazi mengine tukapakiwa kwenye gari kupelekwa ikulu ambako tulikutana na rais wa Zanzibar.
Rais wa Zanzibar alimsikiliza Yasmin na kushangazwa na maelezo ya binti huyo wakati akimsimulia masahibu aliyokutana nayo.
“Hata hivyo wewe ni shujaa kwa sababu hukukata tama” Rais alimwambia Yasmin. Pia alinipongeza mimi kwa kunusurika kufa.
“Mkasa uliowakuta ni historia kubwa ya visiwa vyetu” Rais aliendelea kutuambia.
ITAENDELEA
Rais wa Zenji kipindi hiko alikuwa nani?
 
SEHEMU YA 30



Rais wa Zanzibar alimsikiliza Yasmin na kushangazwa na maelezo ya binti huyo wakati akimsimulia masahibu aliyokutana nayo.
“Hata hivyo wewe ni shujaa kwa sababu hukukata tama” Rais alimwambia Yasmin. Pia alinipongeza mimi kwa kunusurika kufa.
“Mkasa uliowakuta ni historia kubwa ya visiwa vyetu” Rais aliendelea kutuambia.
SASA ENDELEA...
Rais wa Zanzibar akawasiliana na Rais mwenzake wa Comoro na kuzungumza naye.
“Binti yako Yasmin ninaye hapa” Rais wa Zanzibar alimwambia Rais wa Comoro.
“Nimepata habari zake na nimeshukuru sana kusikia kwamba mwanangu bado yuko hai. Sisi tulidhani ameshakufa” Rais wa Comoro alisema kwenye simu.
“Ni kweli kwamba alipotea siku ya harusi yake mwaka mmoja uliopita?”
“Nikweli. Lilikuwa tukio la kushangaza sana!”
“Ameniambia alikuwa akiishi katika kisiwa kimoja kisicho na watu na hajui alifikaje katika kisiwa hicho”
“Binti yangu alipata masahibu makubwa lakini nashukuru kuwa amenusurika”
“Huyu hapa, ongea naye”
Rais alimpa Yasmin mkono wa simu ili azungumze na baba yake.
“Asalam alaykum baba!” Yasmin alimwamkia baba yake.
“Wa alaykum salam warahmatulahi wabarakat. Hujambo mwanangu?”
“Sijambo baba. Matatizo yaliyonitokea ni kama ulivyoyasikia”
“Nimeyasikia na nimemtuma kaka yako Umar na maofisa wangu kuja kukuona. Nimeambiwa kuwa mmeshakutana”
“Tumekutana na kaka ninaye hapa”
“Nimefurahi kwamba uko naye kwa rais mwenzangu. Je wewe afya yako ikoje?”
“Afya yangu si nzuri lakini pia si mbaya sana. Nikija huko mtaniona”
“Ulikuwa unaishi vipi huko kisiwani ulikokuwa?”
“Nimeishi kwa taabu tu baba. Nikija nitawaeleza vizuri”
“Ningependa uzungumze na mama yako ili umtoe wasiwasi lakini hatapatikana kwa sasa kwa sababu mimi bado niko ikulu”
“Hakuna wasiwasi baba. Mwambie mama mimi ni mzima. Ni masahibu tu yamenikuta na ishallah nitakutana naye”
”Si mtakuja hii leo?”
“”Kama tutaruhisiwa kuondoka tutakuja leo”
“Sawa. Sasa mpe simu mheshimiwa rais”
Yasmin akampa samu rais wa Zanzibar.
“Umeshazungumza na mwanao?” Rais wa Zanzibara akamuuliza rais wa Comoro kimzaha.
“Tumezungumza kidogo. Unatarajia wataweza kuondoka leo hii kurudi Comoro”
“Kwa vile ndege iko tayari sioni cha kuwazuia kuondoka leo”
“Basi ningependa uwaruhusu kuondoka na mtupatie taarifa muda ambao wanaondoka”
Baada ya maraisi hao kumaliza kuzungumza, rais wa Zanzibar alizungumza na maofisa wake.
“Nataka mhakikishe kuwa ugeni huu unaondoka leo kurudi Comoro. Na kwa upande wa huyu binti apatiwe mahitaji yote ya kibinaadamu kwa gharama ya serikali wakati akiwa hapa nchini kwetu bila kumsahau kijana Zahrani aliyekuwa naye kule kisiwani”
Baada ya rais kutoa agizo hilo aliagana na sisi na kuwatakia safari njema akina Yasmin.
Yasmin alimuahidi rais wa Zanzibar kuwa hataisahau Zanzibar na atarudi kuitembelea tena atakapojaliwa.
Tulipotoka ikulu tulipelekwa katika hoteli ya Bwawani ambako tulipatiwa huduma mbalimbali kama vile chakula, nguo na mahali pa kupumzika. Hapo tulikutana na watu mbali mbali waliopata habari zetu na kututembelea. Walikuja maofisa wa serikali na pia mawaziri.
Kusema kweli nilipata umaarufu mkubwa kutokana na Yasmin. Kwa vile mwenzangu alikuwa binti wa rais na alikuwa akieleza mara kwa mara kuwa kama si mimi na yeye angeangamia, watu waliotutembelea walikuwa wakitupa pole pamoja na kunipongeza.
Maelezo yetu yalionekana kama kioja kikubwa kwa vile yalimuhusisha jini anayeitwa Harishi ambaye alimteka Yasmin nchini Comoro na kumpeleka katika kile kisiwa cha mauti.
Taarifa zilipowafikia waandishi nao walianza kumiminika katika hoteli ya Bwawani kutuhoji na kutupiga picha.
Baadhi ya waandishi hao baada ya kupata maelezo kutoka kwangu na kwa Yasmin, walimuhoji Yasmin kutaka kujua jinsi tulivyoishi katika kisiwa hicho tukiwa peke yetu.
Mwandishi: “Mliishije na Zaharani mkiwa watu wawili wa jinsia tofauti katika kisiwa hicho?”
Yasmin: “Tuliishi kama marafiki”
Mwandishi: “Mlitarajia kuwa mngeokoka?”
Yasmin: “Kusema kweli hatukutarajia ingawa tulikuwa tunaomba sana”
Mwandishi: “Mlikuwa mnalalaje usiku?”
Yasmin: “Usiku wa jana ndio tulilala pamoja lakini pia hatukulala usingizi kwa sababu tulijua kuwa tungeuawa”
Mwandishi: “Sasa umeshaokoka. Unadhani utaendelea kuwa karibu na Zahrani?”
Yasmin: “Bila shaka. Tulipokuwa kule kisiwani nilimpa ahadi Zahrani kuwa kama tutasalimika atanioa”
Mwandishi: “Una maana kwamba umempenda Zahrani?”
Yasmin akacheka kabla ya kujibu. “Nimempenda sana”
Mwandishi: Je sasa unadhani utatimiza ahadi uliyomuahidi?”
Yasmin: “Ndiyo nitaitimiza”
Mwandishi: “Kwa hiyo una mpango wa kuoana na Zahrani?”
Yasmin: “Mpango bado, ni mawazo tu ambayo naamini hayatabadilika”
Mwandishi: “Umetuambia kuwa kabla ya kupotelea katika kisiwa mlichokua mnaishi ulikuwa unaolewa na mwana wa mkuu wa jeshi la ulinzi la Comoro, je kijana huyo akitaka muoane tena itakuwaje wakati umeshamuahidi Zahrani kuwa mtaoana?”
Yasmin: “Nadhani atakuwa ameshaoa”
Kaka wa Yasmin Umar Sharif Abdulatif ambaye alikuwepo wakati Yasmin anahojiwa alithibitisha kuwa aliyekuwa anamuoa Yasmin kabla ya Yasmin kupotea Comoro alishaoa mke mwingine na walikuwa wanaishi Ufaransa. Visiwa vya Comoro vilikuwa koloni la Ufaransa.
Mwandishi: “Kwa hiyo unatarajia kwenda Comoro na Zaharani?”
Yasmin: “Natarajia hivyo”
Mwandishi: “Ndoa yenu itafanyika lini?’
Yasmin: “Siku yoyote wazazi wetu watakaponiidhin
isha kuolewa na Zaharani”
Mwandishi aliyekuwa akimuhoji Yasmin alinigeukia mimi.
Mwandishi: “Je umeyachukuliaje maelezo ya Yasmin?”
Zahrani: “Yamenifurahisha sana”
Mwandishi: “Uko tayari kuoana na msichana ambaye baba yake ni rais wa nchi?”
“Zahrani: “Kama wazazi wake watakubali niko tayari”
Mwandishi: “Mtakuwa mnaishi wapi
mtakapooana, Zanzibar au Comoro?’
Zahrani : “Popote tu tutakapokubaliana”
Mara tu baada ya waandishi wa habari kuondoka maofisa usalama kutoka ikulu ya Zanzibar walinitambulisha kwamba umefika wakati ambapo nitaachana na Yasmin kwa vile muda wa safari yao ya kurudi Comoro ulikuwa umefika.
Kauli ile ilinivunja moyo hasa kwa vile nilitegemea kuondoka na Yasmin. Yasmin akawaomba maofisa hao waniache niende naye Comoro.
“Hatumzuii mtu yeyote kwenda mahali popote anapotaka ila Zahrani hana hati ya kusafiria” Afisa mmoja alimwambia Yasmin.
Itaendelea.
 
SEHEMU YA 31


Mwandishi: “Mtakuwa mnaishi wapi
mtakapooana, Zanzibar au Comoro?’
Zahrani : “Popote tu tutakapokubaliana”
Mara tu baada ya waandishi wa habari kuondoka maofisa usalama kutoka ikulu ya Zanzibar walinitambulisha kwamba umefika wakati ambapo nitaachana na Yasmin kwa vile muda wa safari yao ya kurudi Comoro ulikuwa umefika.
Kauli ile ilinivunja moyo hasa kwa vile nilitegemea kuondoka na Yasmin. Yasmin akawaomba maofisa hao waniache niende naye Comoro.
“Hatumzuii mtu yeyote kwenda mahali popote anapotaka ila Zahrani hana hati ya kusafiria” Afisa mmoja alimwambia Yasmin.
sasa endelea...
Ilikuwa kweli sikuwa na hati ya kusafiria na hata Yasmin hakuwa nayo lakini kwa vile aliingia Zanzibar kidharura alilazimika pia kuondoka kidharura.
Yasmin akanitazama kwa butwaa.
“Hivi huna hati ya kusafiria?” akaniuliza.
“Sina” nikamjibu huku nikitikisa kichwa.
“Kuna kipindi ulikuja Comoro, ulifikaje bila ya hati?”
“Sina maana kwamba sina kabisa. Hati yangu ya kusafiria iko pemba”
“Kumbe unayo. Sasa tutafanyaje?”
“Amua wewe”
“Sasa sikiliza” Yasmin alitaka kusema kitu lakini akasita na kumtazama kaka yake. “Kaka kama una dola mia tano mpatie Zahrani zimuwezeshe kuja Comoro”
Umar alitoa dola mia tano hapo hapo na kunipa.
“Hizo zitakuwezesha kwenda Pemba kuonana na ndugu zako na kujiandaa kwa safari ya kuja Comoro siku yoyote utakayopenda” Yasmin akaniambia.
Umar akanipa namba za simu za kuwatambulisha wakati nitakapokwenda Comoro.
Nilikubaliana na Yasmin kwa shingo upande. Mwenyewe alijua kuwa sikuridhika kuniacha Zanzibar ingawa nilipatiwa nauli ya kwenda Comoro siku nitakayopenda kuondoka.
Baada ya Yasmin kuniambia hivyo aliishia kunitolea tabasamu lenye mchanganyiko wa furaha na majonzi.
Mimi sikuweza kutabasamu. Kwa siku chache nilizokuwanaye nilikuwa nimeshamzoea Yasmin. Kitu muhimu ambacho nitakikosa kwake ni ile hewa ya mwili wake. Alikuwa na hewa tamu nay a kusisimua ambayo huisikia kila ninapokuwa karibu naye.
Hewa ile ilikuwa inaniliwaza kuliko manukato ambayo hujitia mwilini mwake.
“Nitasubiri. Sina la kufanya” nikamwambia kwa sauti nzito ya huzuni.
“Tutakutana mahabuba wangu. Sitakuacha” Yasmin akaniambia kwa sauti ya chini. Hakutaka isikiwe na wengine.
Sasa msafara ulikuwa unakwenda kiwanja cha ndege. Na mimi nililazimika kuwasindikiza nikiwa pamoja na maofisa usalama.
Giza lilikuwa limeshaanza kuingia na taa za mji wa Unguja zilikuwa zimewashwa. Tulikuwa katika basi dogo ambalo liliweza kutupakia sote. Gari la maofisa usalama lilikuwa limetutangulia.
Tilipofika kiwanja cha ndege niliagana na kaka wa Yasmin kisha nikaagana na Yasmin mwenyewe. Kwa mara ya kwanza Yasmin hakuona aibu kunikumbatia mbele ya macho ya kaka yake.
Kwa mujibu wa tamaduni za Wangazija wa Comoro, kitendo hicho kwa watu wa jinsia tofauti ambao si ndugu kilikuwa ni cha faragha sana. Lakini Yasmin alikifanya kuonesha mapenzi yake kwangu.
Wakati ananiachia aliupeleka haraka mkono wake kwenye macho yake kufuta machozi yaliyoanza kumtiririka.
Kwaheri, tutaonana” akaniambia na kunisisitizia “Nitakusubiri Comoro. Usichelewa kuja. Usiwe na majonzi, tutaonana”
Yasmin alijaribu kutabasamu licha ya uso wake kujaa huzuni. Tabasamu lake lilinifariji sana.
Maofisa usalama walikuwa wakimtazama Yasmin alivyokuwa ananiaga kabla ya kugeuka na kuungana na wenzake’
Sikuondoka hapo kiwanjani hadi ndege waliyosafiri kina Yasmin iliporuka na kuanza safari.
Nilijisikia mwenye majonzi sana lakini nilijikaza.
“Wewe hujui kama yule ni binti wa rais?” Afisa usalama mmoja aliniuliza wakati tunaondoka kiwanjani hapo.
“Ninajua” nikamjibu.
“Sasa mbona unataka kututia aibu. Unataka kwenda naye wapi?”
Swali hilo lilinikera sana. Nikamtazama yule afisa usalama aliyetaka kunishushua.
“Yeye ndiye aliyeomba aondoke na mimi” nikamwambia.
“Wewe pia si ulikuwa unataka kwenda?”
Nilijua kuwa yule afisa alikua ameona donge. Nilitaka kumuuliza “Sasa kinakuuma nini?” lakini nilimstahi. Nikamwambia. “Ni baada ya yeye kutaka aondoke na mimi”
“Sasa yule ni binti wa rais, wewe huwezi kufuatana naye. Ukifika huko utasema nini?”
Niliona nisijibizane naye. Nikaamua kubaki kimya.
Maofisa hao walinipakia kwenye gari na kunirudisha kule hoteli. Wakaniambia nitalala pale na asubuhi nirudi Pemba.
“Tutakufuata asubuhi tukupeleke bandarini” Afisa mmoja akaniambia.
Nikamjibu “Sawa”
Nililala pale hoteli. Usiku kucha nilikuwa namuwaza Yasmin. Asubuhi simu iliyokuwa mle chumbani ikaita. Nilipoipokea niliambiwa nipokee simu yangu kutoka Comoro.
Hapo hapo nilisikia sauti niliyoitambua kuwa ni Yasmin ikinisalimia.
“Subalheri muadhamu (asubuhi njema mpendwa)”
“Subalnuur azizi (asubuhi yenye nuru mremo)” Kwa kutaka kuhakikisha kuwa alikuwa Yasmin nikamuuliza “Wewe ni Yasmin?”
“Naam, ndiye mimi. Nilitaka kukujulia hali”
“Nashukuru, mie sijambo. Je mlifika salama?”
“Alhamdulilahi. Tulifika salama. Nimekutana na wazazi wangu na ndugu zangu na pia wananchi wenzangu. Wamefurahi kuniona na mimi nimefurahi kuwaona. Kumbe bado uko hapo hoteli?”
“Ninaondoka hii asubuhi kwenda Pemba na mimi nikaonane na wazazi wangu pamoja na ndugu zangu. Najua wameshanikatia tama”
“Ni kweli. Basi ukifika unaweza kunipigia kwa kutumia zile namba ulizopewa na kaka”
“Sawa, nitakupigia”
“Ongea na mama yangu”
Mara nikasikia sauti nyingine ikiniuliza. “Hujambo mwanangu?”
“Sijambo mama. Habari za huko?’
“Huku ni salama. Unajisikiaje hali yako?”
“Hali yangu ni nzuri. Nashukuru”
“Pole sana kwa masahibu yaliyowafiaka”
“Tumeshapoa mama”
“Tunakusubiri kwa hamu huku. Utakuja lini?”
“Siku ya kuja nitawambia. Kwanza nataka nifike Pemba nikawaone wazazi na ndugu”
“Basi utatujulisha siku utakayokuja tukupokee”
“Asante mama. Nitawajulisha”
“Nampa simu Yasmin”
“Haya mpe”
“Hallo Zahran!” Sauti ya Yasmin ikasikika.
“Ndiyo Yasmin”
“Usijali kuwa mbali nami, ishallah tutakuwa pamoja. Nimeshamueleza mama yangu kilicho ndani ya moyo wangu kuhusu wewe”
Aliponiambia hivyo, mwili wangu ulisisimka.
“Hakuna tatizo Yasmin. Wewe pia usijali”
“I miss you” Yasmin akaniambia kwa kingreza.
“Sikujua jinsi ya kujibu, nikabaki kucheka. Yasmin naye akacheka.
“Bye bye (baibai): akaniaga.
“Bye…”
Simu ikakatwa.
Je Zahrani ambaye ni mvuvi na masikini asiye na elimu atamuoa Yasmin binti wa rais?
 
Back
Top Bottom