Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

SEHEMU YA 21



Yasmin naye akaomba dua.
Kwa muda wa nusu saa hivi mahali hapo pakawa kama madarasa kutokana na kurindima visomo vyetu vya dua.
“Pia tungekuwa tunaswali” Shazume akatukumbusha.
Sikuzote binaadamu humkumbuka sana mola wake pale anapofikwa na matatizo. Siku zote hizo tulikuwa hatukumbuki kuswali ila ni kwa siku ile ambayo tuliona tutamalizika.
“Pia ilitakiwa leo tufunge” na mimi nikawakumbusha.
“Ni kweli” Shazume akanikubalia na kuongeza “Lakini tumeshakunywa uji”
“Kama tutanusurika leo tutafunga kesho. Umesikia Yasmin?”
“Nimesikia” Yasmin akanijibu.
“Sasa sisi hatuko tohara, tutaswali vipi?’ nikawauliza wenzangu.
“Twendeni tukaoge baharini tujitoharishe” Shazume akasema.
“Hizi nguo zetu pia hazina tohara”
“Tuoge na nguo zetu ziweze kutoharika, zikikauka tutaswali”
Tukakubaliana.
SASA ENDELEA
Tukaamua sasa twende baharini tukaoge. Tukaenda sote watatu, mimi, Shazume na Yasmin. Yasmin alipotuona sisi tunajitosa kwenye maji na yeye akajitosa. Tukawa tunaoga na kuogelea pamoja.
Tuliendelea kukaa kwenye maji kwa muda kidogo ili kujisahaulisha matatizo yaliyokuwa yanatukabili.
Asubuhi ile maji yalikuwa matamu kwa mtu ambaye alikusudia aogelee kwa starehe ila kwa sisi ilikuwa starehe ya kujilazimisha. Mawazo mabaya yalituepuka kwa muda yakitusubiri tumalize kuogelea.
Tulitamani tusitoke ndani ya maji lakini nilipomuona Yasmin aliyekuwa akiogelea karibu yangu anarudi ufukweni na mimi nikaamua kurudi.
Tukakaa ufukweni na kumsubiri Shazume. Naye alipotuona tumerudi ufukweni akatufuata.
Tukakaa kuota jua. Nguo zetu zilikuwa zimetota. Kitendo cha kuogelea na nguo zetu hakikuwa cha maana sana kwani mzizimo ungeweza kutuletea madhara ya kiafya lakini hatukuwa na la kufanya.
Yasmin ambaye alikuwa na nguo za kubadili alizokuwa akiletewa na Harishi alikuwa akifuata mkumbo tu, haikumpasaaloweshe nguo zake ila alipotuona sisi tunaoga na yeye akajitosa.
Tulikaa kwa muda kwenye ufukwe tukiangalia bahri na ndege waliokuwa wakiruka ruka. Ili miiliyetu isisinyae tuliamua kufanya mazoezi ya kukimbizana.
Tulikimbizana mpaka tulipochoka tukarudi kwenye ile nyumba. Tukapanga kwamba itakapofika sa saba tuanze kuswali swala ya adhuhuri. Yasmin alituaga akatuambia kuwa anakwenda kupika chakula cha mchana.
Kwa mustakabali wetu tatizo la chakula halikuwepo. Chakula kilikuwepo kwa Yasmin. Tatizo lilikuwa ni la kuuliwa na Harishi. Kama si tatizo hilo mahali pale pangekuwa ni pazuri pa kuishi. Sikuvutika na kisiwa hicho pekee bali pia nilivutika na Yasmin. Nilifarijika sana kuona jinsi alivyokuwa akitupa moyo na matumaini japokuwa hali ilikuwa tete.
Baada ya Yasmin kuondoka tuliendelea kukaa, hatimaye tukapitiwa na usingizi.
Tulipokuja kuamka yalikuwa majira ya saa nane. Tukaenda kutawadha kwenye maji ya bahari na kuswali swala ya adhuhuri.
Yasmin alikuja saa tisa akiwa amechukua kapu la chakula. Alikuwa amebadili nguo zake na kuvaa mavazi mengine.
“Mmepauka kwa chumvi. Mnasikitisha sana kaka zangu” akatuambia.
“Ndiyo hivyo, tutafanyaje sasa” nikamwambia huku nikimpokea lile kapu.
“Mmeshaswali?” akatuuliza.
“Tumeswali na wewe umeswali?” Na mimi nikamuuliza.
“Mimi naswali kila siku kuomba nusura na kuwaombea na nyinyi. Sijui kama nyinyi mmekumbuka kuniombea”
“Tumekuombea” nikamdanganya. Tulikuwa tumemsahau.
“Mngesema mmesahau kuniombea ningejua hamnipendi”
“Tunakupenda sana. Umetuletea chakula gani?”
“Wali”
“Roho zetu zimekinai, hatutamani hata kula” Shazume akasema.
“Shazume unaanza maneno yako!” Yasmin akamwambia Shazume.
“Unafikiri nakudanganya, mimi sina hamu ya kula kabisa”
“Mbona juzi na jana ulikuwa unakula?”
“Nilikuwa na matumaini”
“Si vizuri hivyo. kuleni japokuwa kidogo mpate nguvu. Mkiacha kula mtakuwa mnajitesa wenyewe. Mimi pia sikula. Nimekuja huku nile na nyinyi”
Yasmin alitoa kile chakula akakiweka chini. Akatoa tasa la maji tukaosha mikono kisha tukaanza kula.
Mimi pia sikuwa na hamu ya kula lakini nilikula kumridhisha Yasmin.
Tuliendelea kula kidogo kidogo hadi Shazume alipomuuliza Yasmin.
“Yasmin ukibaki peke yako itakuwaje?”
“Hatuombei hivyo, tuombee tubaki sote. Ukiomba dua uweke matumaini, isiwe unakata tama”
“Ni kweli Yasmin huwezi kuomba kitu bila kukiwekea matumaini. Kama huna matumaini na kitu hicho kwanini unakiomba?” nikasema.
Shazume akaguna.
“Pamoja na kuomba kwetu bado naona wakati wetu umekaribia sana” Shazume akasema kwa hali ile ile ya kukata tama.
“Shazume usiseme hivyo, mnaweza kunusurika. Harishi ni kiumbe kama nyinyi”
“Lakini mwenzetu amepewa uwezo”
yasmin naye akaguna. Pakawa kimya. Yasmin ndiye aliyeutanzua ukimya huo alipotuambia. “ Jamani tukinusurika nitawachukua Comoro. Nitamwambia baba yangu nyinyi ni ndugu zangu wa damu. Mtaenziwa kama watoto wa rais”
ITAENDELEA
 
Tunashukuru kwa hadithi nzuri mkuu. Kwanini usingetuletea yote kwa mara moja na ikaisha?. Maana ni hadithi iliyowahi kusimuliwa kabla.

Shukran
SEHEMU YA 21



Yasmin naye akaomba dua.
Kwa muda wa nusu saa hivi mahali hapo pakawa kama madarasa kutokana na kurindima visomo vyetu vya dua.
“Pia tungekuwa tunaswali” Shazume akatukumbusha.
Sikuzote binaadamu humkumbuka sana mola wake pale anapofikwa na matatizo. Siku zote hizo tulikuwa hatukumbuki kuswali ila ni kwa siku ile ambayo tuliona tutamalizika.
“Pia ilitakiwa leo tufunge” na mimi nikawakumbusha.
“Ni kweli” Shazume akanikubalia na kuongeza “Lakini tumeshakunywa uji”
“Kama tutanusurika leo tutafunga kesho. Umesikia Yasmin?”
“Nimesikia” Yasmin akanijibu.
“Sasa sisi hatuko tohara, tutaswali vipi?’ nikawauliza wenzangu.
“Twendeni tukaoge baharini tujitoharishe” Shazume akasema.
“Hizi nguo zetu pia hazina tohara”
“Tuoge na nguo zetu ziweze kutoharika, zikikauka tutaswali”
Tukakubaliana.
SASA ENDELEA
Tukaamua sasa twende baharini tukaoge. Tukaenda sote watatu, mimi, Shazume na Yasmin. Yasmin alipotuona sisi tunajitosa kwenye maji na yeye akajitosa. Tukawa tunaoga na kuogelea pamoja.
Tuliendelea kukaa kwenye maji kwa muda kidogo ili kujisahaulisha matatizo yaliyokuwa yanatukabili.
Asubuhi ile maji yalikuwa matamu kwa mtu ambaye alikusudia aogelee kwa starehe ila kwa sisi ilikuwa starehe ya kujilazimisha. Mawazo mabaya yalituepuka kwa muda yakitusubiri tumalize kuogelea.
Tulitamani tusitoke ndani ya maji lakini nilipomuona Yasmin aliyekuwa akiogelea karibu yangu anarudi ufukweni na mimi nikaamua kurudi.
Tukakaa ufukweni na kumsubiri Shazume. Naye alipotuona tumerudi ufukweni akatufuata.
Tukakaa kuota jua. Nguo zetu zilikuwa zimetota. Kitendo cha kuogelea na nguo zetu hakikuwa cha maana sana kwani mzizimo ungeweza kutuletea madhara ya kiafya lakini hatukuwa na la kufanya.
Yasmin ambaye alikuwa na nguo za kubadili alizokuwa akiletewa na Harishi alikuwa akifuata mkumbo tu, haikumpasaaloweshe nguo zake ila alipotuona sisi tunaoga na yeye akajitosa.
Tulikaa kwa muda kwenye ufukwe tukiangalia bahri na ndege waliokuwa wakiruka ruka. Ili miiliyetu isisinyae tuliamua kufanya mazoezi ya kukimbizana.
Tulikimbizana mpaka tulipochoka tukarudi kwenye ile nyumba. Tukapanga kwamba itakapofika sa saba tuanze kuswali swala ya adhuhuri. Yasmin alituaga akatuambia kuwa anakwenda kupika chakula cha mchana.
Kwa mustakabali wetu tatizo la chakula halikuwepo. Chakula kilikuwepo kwa Yasmin. Tatizo lilikuwa ni la kuuliwa na Harishi. Kama si tatizo hilo mahali pale pangekuwa ni pazuri pa kuishi. Sikuvutika na kisiwa hicho pekee bali pia nilivutika na Yasmin. Nilifarijika sana kuona jinsi alivyokuwa akitupa moyo na matumaini japokuwa hali ilikuwa tete.
Baada ya Yasmin kuondoka tuliendelea kukaa, hatimaye tukapitiwa na usingizi.
Tulipokuja kuamka yalikuwa majira ya saa nane. Tukaenda kutawadha kwenye maji ya bahari na kuswali swala ya adhuhuri.
Yasmin alikuja saa tisa akiwa amechukua kapu la chakula. Alikuwa amebadili nguo zake na kuvaa mavazi mengine.
“Mmepauka kwa chumvi. Mnasikitisha sana kaka zangu” akatuambia.
“Ndiyo hivyo, tutafanyaje sasa” nikamwambia huku nikimpokea lile kapu.
“Mmeshaswali?” akatuuliza.
“Tumeswali na wewe umeswali?” Na mimi nikamuuliza.
“Mimi naswali kila siku kuomba nusura na kuwaombea na nyinyi. Sijui kama nyinyi mmekumbuka kuniombea”
“Tumekuombea” nikamdanganya. Tulikuwa tumemsahau.
“Mngesema mmesahau kuniombea ningejua hamnipendi”
“Tunakupenda sana. Umetuletea chakula gani?”
“Wali”
“Roho zetu zimekinai, hatutamani hata kula” Shazume akasema.
“Shazume unaanza maneno yako!” Yasmin akamwambia Shazume.
“Unafikiri nakudanganya, mimi sina hamu ya kula kabisa”
“Mbona juzi na jana ulikuwa unakula?”
“Nilikuwa na matumaini”
“Si vizuri hivyo. kuleni japokuwa kidogo mpate nguvu. Mkiacha kula mtakuwa mnajitesa wenyewe. Mimi pia sikula. Nimekuja huku nile na nyinyi”
Yasmin alitoa kile chakula akakiweka chini. Akatoa tasa la maji tukaosha mikono kisha tukaanza kula.
Mimi pia sikuwa na hamu ya kula lakini nilikula kumridhisha Yasmin.
Tuliendelea kula kidogo kidogo hadi Shazume alipomuuliza Yasmin.
“Yasmin ukibaki peke yako itakuwaje?”
“Hatuombei hivyo, tuombee tubaki sote. Ukiomba dua uweke matumaini, isiwe unakata tama”
“Ni kweli Yasmin huwezi kuomba kitu bila kukiwekea matumaini. Kama huna matumaini na kitu hicho kwanini unakiomba?” nikasema.
Shazume akaguna.
“Pamoja na kuomba kwetu bado naona wakati wetu umekaribia sana” Shazume akasema kwa hali ile ile ya kukata tama.
“Shazume usiseme hivyo, mnaweza kunusurika. Harishi ni kiumbe kama nyinyi”
“Lakini mwenzetu amepewa uwezo”
yasmin naye akaguna. Pakawa kimya. Yasmin ndiye aliyeutanzua ukimya huo alipotuambia. “ Jamani tukinusurika nitawachukua Comoro. Nitamwambia baba yangu nyinyi ni ndugu zangu wa damu. Mtaenziwa kama watoto wa rais”
ITAENDELEA
 
Itakuwa vyema ukiimaliza hii weekend maana baada ya hapa wiki ya kazi na mishe mishe inaanza
 
SEHEMU YA 22


“Sidhani kama hapa ni karibu na kwenu Comoro. Mimi nadhani kama tutapata msaada wa kuokolewa tutapelekwa kwanza Zanzibar” nikasema.
“Si vibaya Zanzibar pia ni nyumbani lakini baba akipata habari atatuma ndege siku hiyo hiyo ituchukue pamoja na nyinyi”
“Itakuwa raha sana tukienda Comoro na kupokewa na rais” nikasema.
Shazume alikuwa kimya akitusikiliza. Bila shaka alikuwa anaona tunajidanganya kujifariji. Kwa mawazo yake sisi tulikuwa ni wa kufa tu.
“Si unajua mzazi aliyekwishamkatia tamaa mwanawe halafu anaambiwa amepatikana, atafurahije?” Yasmin akaniuiza.
“Atafurahi sana”
Iliwezekana tulikuwa tulikuwa tunajidanganya kweli kama alivyowaza Shazume lakini tulifarijika. Saa zikapita.
Tulipomaliza kula Yasmin alileta storitofauti tofauti kutuondoa katika mawazo mabaya. Tukawa tunazungumza.
Aliondoka jioni sana. Tukamsindikizakwa pamoja hadi nusu ya njia, tukarudi. Tukakaa kwenye kile kisehemu chetu kusubiri usiku. Hatukujua nini kitatokea kati yetu usiku huo.
SASA ENDELEA
Usiku ule tulikesha macho kwa sababu ya hofu. Tulikuwa tumejilaza chini kila mmoja upande wake lakini hakukuwa na aliyelala usingizi. Mara kwa mara nilimuona Shazume akijigeuza kila upande.
Ilikuwa kati kati ya usiku Shazume aliposhika mguu wangu. Sikujua kama alikuwa anataka kuniamsha au alitaka kujua nilikuwa macho lakini aliponishika nilishituka nikarusha mguu wangu.
“Nini?” nikamuuliza nikiizuia sauti yangu isisikike sana.
“Nimebanwa na haja ndogo” akaniambia.
“Sasa?” nikamuuliza.
“Tunaweza kutoka nikajisaidie”
“Haya tutoke” nikamwambia.
Shazume akainuka na mimi nikainuka. Akatangulia kutoka kwenye mlango. Kulikuwa giza sana. Hatukuweza kuona kwa mbali.
“Twende nje au uani?” Shazume akaniuliza.
“Naona tutoke uani” nikamjibu.
Shazume akaelekea upande wa uani. Mimi nilikuwa nikimfuata nyuma. Alifungua mlango akachungulia uani. Mwezi ulikuwa unaangaza, ua ulikuwa mweupe. Baada ya kuchungulia kwa tahadhari Shazume alivuka kizingiti cha mlango akatoka uani na mimi nikatoka.
Yeye alikwenda upande wake na miminilikwenda upande wangu tukachutama na kujisaidia. Mimi sikuwa na haja ndogo lakini baada ya mwenzangu kuniambiana mimi nikaisikia.
Tulipomaliza haja zetu tulirudi ndani tukajilaza tena. Safari hii tulipojilaza tu usingizi ulitupitia tukalala.
Wakati nipo usingizini niliota Harishi anatufukuza baada ya kutufuma tukiwa na Yasmin kwenye lile jumba lake. Tukaingia katika chumba kimoja kujificha chini ya mvungu wa kitanda. Muda si muda Harishi akafungua mlango na kuingia mle chumbani kututafuta.
Akaona mguu wa Shazume umetokeza chini ya mvungu. Akaushika na kuuvuta. Shazume akawa anapiga kelele kuniita.
Kelele hizo ndizo zilizoniamsha. Nikaamka na kuangaza macho. Nikasikia Shazume akiendelea kupiga kelele kuniita lakini sauti yake ilitokea kwa juu, sio pale chini tulipolala. Nikashituka sana kwa kujua kuwa haikuwa ndoto.
Nikatazama juu. Kwanza niliona kanzu nyeupe halafu nikaona upanga uking’aa. Nilipoona hivyo nilijisogeza zaidi ndani ya makorokoro na kuendelea kuchungulia.
Nilimuona Shazume ameinuliwa juu juu na Harishi. Nikajiambia kumbe ile ndoto ilikuwa ni kweli. Shazume alitolewa mle chumbani. Sikuweza kujua Harishi aliwasili muda gani na kumkamata Shazume.
Bila shaka kilichokuwa kimeninusuru mimi, ni kuwa nililala nyuma ya mlango. Harishi alipoingia alimuona Shazume na kumkamata yeye.
Ile ndoto niliyoota ilikuwa ya kweli. Harishi alikuwa ametuingilia!
Jitihada zetu za kujaribu kumkwepa zilikuwa za bure kwani Harishi alikuwa akitugundua kila tulipokwenda kujificha na sababu ni kuwa alikuwa akifuata harufu zetu kama vile m’bwa.
Harishi alipomtoa Shazume ukumbini, nilimsikia Shazume akipiga ukulele mmoja tu “Nakufa!”. Halafu sikusikia kitu tena.
Moyo ulikuwa ukinienda mbio na nilikuwa nikihema kwa nguvu kama niliyekuwa nafukuzwa. Tukio hilo lilikuwa la ghafla sana kiasi kwamba nililazimika kujiuliza, kama bado nilikuwa kwenye ile ndoto au kilichokuwa kinatokea kilikuwa kweli.
Hofu yangu sasa ilikuwa kwangu. Nilijiua Harishi akimaliza kumuua Shazume ataniingilia na mimi kwani alipoingia humo chumbani alituona tukiwa wawili.
Wazo hilo likanifanya nizidi kujisogeza kwenye makorokoro ili Harishi akiingia tena asinione. Lakini muda ulipita. Sikumuona tena Harishi.
Nikaendelea kukaa hapo hapo hadi nikaona kunakucha. Nikahisi kwa muda ule Harishi atakuwa ameshaondoka. Nikajiburuza kujitoa kwenye yale makorokoro nilikojiingiza.
Nilinyata hadi kwenye mlango nikaufungua na kuchungulia ukumbini. Nilichungulia upande wa mbele na upande wa uani. Niliiona maiti ya Shazume imelala chini kando ya mlango wa chumba tulichokuwemo. Harishi mwenyewe hakuwepo.
Nikatoka nje na kuangalia kila upande. Sikuona kitu. Kando ya ile nyumba palikuwa na mti. Nikapata wazo kuwa nipande juu ya ule mti kujificha. Nikaenda kwenye mti huo nikaupanda na kukaa kwenye tawi mahali ambapo nisingeweza kuonekana.
Wakati nipo juu ya ule mti nilimuona Yasmin kwa mbali akija. Nikajiambia tuliobaki katika kisiwa kile tulikuwa watu wawili tu, mimi na Yasmin.
Sikupenda kujisifu kuwa nilikuwa nina bahati kwa sababu nimenusurika. Nilijua kuwa wakati wangu ulikuwa haujafika. Pengine niliandikiwa niwe wa mwisho kufa.
Historia ya kisiwa hicho tangu tulipofika kila siku alikufa mtu. Leo nimeishuhudia maiti ya Shazume, huenda kesho Yasmin ataishuhudia maiti yangu.
Yasmin alipofika pale nilimuacha aingie mle ndani. Mara moja nikamuona ametoka akiwa amechanganyikiwa. Bila shaka alikuwa ameshitushwa na maiti ya Shazume.
ITAENDELEA
 
SEHEMU YA 23



Kile kitendo cha kutoniona mimi inawezekana kilimpa hisia kuwa na mimi nilikuwa nimeuawa kama Shazume. Tatizo ni kuwa mwili wangu hakuuona. Bila shaka alitoka nje kuutafuta mwili wangu.
Alisimama mbele ya ile nyumba akaangalia kila upande kisha akarudi tena mle ndani. Mimi nikashuka kwenye ule mti.
Yasmin alipotoka tena akanikuta nimesimama mbele ya mlango. Akashituka na kuniuliza. “Ulikuwa wapi?”
“Nilikuwa nimepanda juu ya huu mti” nikamjibu.
Akaja kunikumbatia kifuani kwangu. Kumbe alikuwa analia. Nilipoona analia na mimi nikaanza kulia. Kama Yasmin alikuwa anaona uchungu jinsi tulivyokuwa tunauliwa na Harishi, mimi niliona uchungu nilipowaza nitakavyouliwa na Harishi hapo kesho.
“Buriani Yasmin, ndio tunaagana. Kesho hatutakuwa pamoja tena. Shazume ametutangulia leo” nikamwambia Yasmin.
Yasmin akajifuta machozi yake na kunitazama.
“Wewe hutaniacha, kama ni kufa tutakufa sote. Mwili wangu utalala juu ya mwili wako” Yasmin akaniambia kwa sauti nzito lakini ya kijasiri.
Akaongeza. “Ili uamini kuwa wewe utakufa na mimi turudi kule kule kwenye lile jumba,hatuna sababu yoyote ya kujificha. Akija Harishi nitamwambia atuue sote, Anitangulize mimi kisha wewe”
SASA ENDELEA
“Twende!” nikamwambia Yasmin bila kusita.
Yasmin akanishika mkono tukatembea kuelekea katikalile jumba. Hatukuzungumza kitu tena mpaka tulipofika katika jumba hilo Yasmin aliniuliza.
“Utakunywa uji?”
“Sitakunywa” nikamjibu kwa mkato
“Kwanini?”
“Roho yangu imefadhaika sana”
“Hata roho yangu imefadhaika lakini kama wanipenda tunywe kidogo”
Ilikumridhisha Yasmin nilimkubalia. Yasmin aliniacha ukumbini akaenda jikoni. Baaada ya muda kidogo alikuja na vikombe viwili vilivyojaa uji wa ngano uliotiwa asali.
Alinipa kikombe kimoja kisha aliketi nami.
“Yasmin kweli tumeshindwa kuondoka kwenye kisiwa hiki cha mauti” nikamuuliza Yasmin
“Tutaondokaje wakati tumezungukwa na bahari na hatuna chombo!”
“Nashangaa kwamba hakuna wavuvi wanaokuja katika kisiwa hiki!”
“Hiki kisiwa kiko mbali na pia kinajulikana. Hakuna wavuvi wanaoweza kufika hapa”
“Chombo chetu kilipotuharibikia tulipokiona kisiwa hiki tulidhani tumeokoka kumbe tumekuja kuangamia”
“Hata kama msingekiona hiki kisiwa pia mngeangamia. Mngekula nini? Mngekufa kwa njaa”
“Mimi naona bora kufa kwa njaa kwa sababu njaa itakuwa imekulevya, hutajijua. Kuliko kusubiri….” sikumalizia sentensi yangu.
Niliona nilikuwa najikumbusha kifo kibaya cha kutobolewa utosi kwa ncha ya upanga na kufyonzwa damu na ubongo1.
Siku zote tulizokaa hapa kisiwani niliweza kujikaza na kuondoa hofu licha ya wenzangu kuendelea kuuawa lakini kwa siku ile ambayo nilibakimimi na Yasmin peke yetu, sikuweza kuzuia hofu yangu.
Mawazo ya kifo cha kutobolewa utosi kwa ncha ya upanga na kufyonzwa damu na ubongo yalikuwa yametawala akili yangu.
“Harishi ni kiumbe na sisi ni viumbe. Huwezi kujua Mungu amepanga nini” Yasmin akaniambia.
“Namuamini Mungu na simkatii tamaa”
“Hapo umezungumza kitu cha maana sana. Haifai kukata tama. Nimeshakwambia kama ni kufa leo tutakufa sote. Na mimi ndio nitakufa kwanza”
“Unataka tuendelee kukaa humu hadi usiku”
“Ndiyo. Unafikiri utakwenda wapi?”
“Sioni pa kwenda”
“Basi tukae tu humu”
“Harishi akija atukute pamoja?”
“Ndiyo”
“Aniue mbele yako!”
“Hapana. Ataniua mimi kwanza”
“Mimi sipendi nikusababishie kifo, niache nife mwenyewe”
“Na mimi sitapenda nikusababishie kifo”
“Wewe hutanisababishia kifo, ni Harishi”
“Sikiliza kaka yangu. Sisi tukae hapa hadi usiku.Litakalotokea lolote na litokee lakini kama ni kufa nitatangulia mimi”
Nilimuangalia tu Yasmin, sikumjibu kitu tena. Nikaendelea kunywa uji huku nikiwaza kama ni kweli alikuwa amejitolea nafsi yake kwa ajili yangu.
Maneno yake yalionesha alichokuwa akisema kilikuwa na udhati.
Hata hivyo niliwaza kuwa msimamo wa Yasmin haukuwa na msaada wowote kwangu zaidi ya kuonesha upendo. Ulikuwa msimamo wa kukata tamaa na haukuwana maana.
Atangulie yeye kufa halafu nifuatie mimi? Maana yake ni kuwa sote tutafikwa na mauti. Jambo hilo kwangu lilikuwa tishio ingawa yeye aliona lilikuwa la kijasiri.
Jambo la maana lilikuwa kupata wazo la kutunusuru sote na sio tufe sote.
Tulibaki kimya tukinywa uji. Uji huo niliunywa kwa kujilazimisha ili kumridhisha Yasmin. Kama ningekuwa peke yangu ningebaki na njaa hadi mauti yatakaponikuta.
Nilipomaliza kikombe changu cha uji Yasmin aliniuliza.
“Nikutilie tena?”
“Umetosha’ nikamjibu.
Yeye pia alikuwa amemaliza uji wake akaniambia.
“Basi nenda ukaoge, umeshatia nguvu kidogo”
Pamoja na kukabiliwa na tishio hilo la kifo kusema kweli nilihitajika sana kuusafisha mwili wangu. Nilikuwa nimechafuka sana na nilikuwa sijaoga kwa siku tatu.
Niliona aibu kumwambia Yasmin kuwa sitaoga. Nikainuka.
Yasmin akanipeleka bafuni kisha akaondoka. Nilioga haraka haraka. Nilipomaliza niliondoka bafuni na kumbishia Yasmin mlango.
Yasmin alinifungulia mlango na kuniambia.
“Karibu”
Niliingia mle chumbani alimokuwa. Hamkuwa na kiti. Akaniambia.
Kaa kitandani”
Nikakaa.
“Unajisikia vizuri kidogo?” akaniuliza.
Nilijaribu kutabasamu bila kufanikiwa. Niliishia kubenua midomo tu, uso haukukunjuka.
ITAENDELEA
 
Back
Top Bottom