Mkasa wa kweli: Kazi za ndani nchini Oman zilivyonikutanisha na kifo

SEHEMU YA 12

Nilishukuru japo kwa hilo kwani niliona angalau sasa ndugu zangu watapata fursa ya kuona maiti yangu na kuzikwa kwenye ardhi ya nchi yangu, nafsi yangu haikuogopa kufa, ila kilichoniumiza ni kufa nikiwa na mtoto tumboni, hilo liliniliza machozi.
“Usilie Agripina ndivyo maisha yalivyo, hujafa hujaumbika” mtu mmoja mwenyeji wa Kigoma alinipa moyo.
“Silii kwa sababu ya hukumu, namlilia mwanangu aliye tumboni”
“Una mtoto tumboni?”
“Ndio.”
“Nafikiri huwezi kutumikia adhabu ya kifo hadi pale utakapokuwa umejifungua mtoto.”
“Labda ngoja tusubiri,” nilisema kinyonge huku matone ya machozi yakijikusanya kwenye macho yangu.
Siku, wiki na miezi ikayoyoma, niliendelea kuishi ndani ya gereza kama mfungwa ninayesubiri siku ya kutumikia adhabu yangu ya kifo. Wakati nikingoja siku ya hukumu pia tumbo langu lilizidi kuwa kubwa.
Siku moja nikafuatwa na askari magereza walikuwa kama sita, mikononi mwao walibeba bunduki. Walinizunguka huku wakionekana kuwa makini na mimi, mmoja miongoni mwao akanisogelea na kunieleza ilibaki wiki moja tu kabla ya kutumikia adhabu yangu ya kifo.
Nilihisi mate mepesi yakijaa mdomoni, pamoja na kwamba nilikuwa sina hofu dhidi ya kifo lakini kwa mara ya kwanza nikahisi mwili ukinisisimka, hofu ikanisambaa kifuani mwangu, taswira ya tukio la mtu kunyongwa likajitengenza kwenye akili yangu, kwa kweli niliogopa mno.
Walipoondoka wale askari, wafungwa wenzangu walinifuata na kuniuliza nilikuwa naambiwa nini. Niliwaeleza yote nilioambiwa na wale askari wa kiarabu, simanzi na hofu ilienea katika nyuso za wafungwa hasa Watanzania wenzangu ambao pia walihukumiwa kifo.
“Ndiyo maana wameanza kuwa makini na wewe, kuanzia leo unaweza usiwe na sisi tena ndani ya selo. Siku za mfungwa kunyongwa zikikaribia huwa anawekwa mbali na watu kwa imani kwamba anaweza kufanya lolote dhidi ya mtu yeyote ili mradi asife peke yake,” alisema mfungwa mmoja miongoni mwa waliokuja kunipa pole.
Saa kumi na mbili jioni nilijiwa tena na wale askari wenye bunduki, kama alivyonieleza yule mfungwa mwezangu nilihamishwa na kupelekwa katika selo ya peke yangu. Niliingizwa kwenye chumba kimoja kizuri ambacho kilikuwa na kila kitu cha thamani, chumba hicho kilikuwa ndani ya jela hiyo.
Sikujua mantiki ya kuingizwa kwenye chumba nadhifu ingawa wakati mwingine nilihisi hizo ni itifaki za kumkirimu mtu ambaye hukumu yake ya kifo ipo jirani, hata hivyo wakati mwingine nilipingana na fikra hizo kwa kuwa mwanzoni nilipohukumiwa kifo, sikufanyiwa ikhisani ya mambo haya.
Niliishi ndani ya chumba kile nadhifu, kila siku nikiletewa vyakula vizuri ambavyo nafikiri vingine sijawahi kuvila hadi leo ninaposimulia mkasa huu. Wiki ile moja ilienda harakaharaka, hatimaye siku ya hukumu ikafika.
Walikuja askari wenye bunduki na kunitoa nje ya chumba kile, nilifungwa minyororo miguuni, mnyororo huo ukaunganishwa na shingo yangu ukapita hadi mikononi, kisha nikavikwa soksi nyeusi usoni.
Nilishikwa bega kwa nguvu na askari mmoja miongoni mwa waliokuwa wamenizunguka huku mkono mmoja wa askari yule ukiwa umekamata silaha yake vizuri.
Akawa ananiongoza na kunipeleka mahali nisikokujua, mapigo yangu ya moyo yakawa yananidunda “duk duk duk” nikaanza kutokwa jasho mwilini, hofu ya kifo ikawa kubwa, hatimaye nikaanza kulia, machozi na kamasi vilinitoka ndani ya ile soksi nyeusi iliyofunika uso wangu. Hata hivyo hakuna aliyejali hilo..
Nilifikishwa ndani ya chumba kimoja ambacho kilikuwa na baridi kali kisha nikaondolewa ile soksi usoni, nikashangaa nilipojikuta nipo ndani ya mochwari, moyo wangu ukalipuka “paaa” niliogopa.
Ndugu msomaji hapa ngoja niseme kitu. Hakuna hukumu mbaya ambayo inavuruga saikorojia ya mtu kama hukumu ya kifo, kama wadau wa sheria watapata bahati ya kusoma maandishi haya ni vema wakafanyia marekebisho sheria hii katika taifa letu, kwani sheria hii inamtafuna binadamu kisaikolojia kabla ya kuitumikia.
Baadhi ya nchi za ulaya na Marekani, sheria ya hukumu ya kifo haipo kidogo na baadhi ya nchi za Afrika, lakini kwa bara la Asia bado sheria hii inaendelea kutesa saikolojia ya binadamu kwa kiwango kibaya sana.
Baada ya kujiona nipo ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti nilianza kuhisi kizunguzungu, maiti nyingi zilikuwa zimetapakaa chini huku zikiwa zimefunikwa kwa mashuka meupe, kulikuwa na harufu kama ya jiki (ile dawa ya kuondoa madoa), nikatambua hiyo ni dawa ambazo maiti zile zimedungwa kwenye miili yao ili pengine zisiharibike.
Nafsi yangu ikazidi kuzongwa na jinamzi la hofu baada ya kubaini kuwa kumbe na mimi dakika chache nitakuwa maiti kama zile zilizolazwa pale chini kisha nitachomwa sindano yenye dawa ambayo ina harufu ya jiki kisha nitalazwa chini na kufunikwa shuka jeupe nikingoja kuzikwa.
“Mlazeni juu ya kitanda” alisema daktari huku akivuta sumu kwa kutumia sindano kwenye kichupa kidogo.
Nilishikwa na askari wawili nikalazwa juu ya kitanda, nikawa nimelala chali, mtoto wangu aliyekuwa tumboni nikamsikia akichezacheza. Machozi yalinitoka.
“Tutaonana mbinguni kwa baba mwanangu, samahani kwa kutumikia adhabu yangu, Labda pengine ni sahihi tu kufa na mama yako. Kama usipokufa sasa utakufa baadae kwa Ukimwi ambao naamini tayari nimekwisha kuambukiza.”
Nilinong’ona huku nikisubiri kudungwa sindano yenye sumu hadi kufa. Nilimwona daktari yule akiinyanyua sindano iliyokuwa imejazwa dawa ya Tetrodotoxin ambayo ni sumu maalumu kwa kuulia watu waliohukumiwa kifo, akaibonyeza kidogo ile sindano, matone madogo ya sumu yakaruka angani, kisha akanisogelea pale kitandani nilipolazwa tayari mkononi akiwa amekamata sindano ya SUMU.
“Nina mimba jamani, msiniue,” nilisema huku nikilia, macho yangu yakimtizama mtu yule kwa huruma.
“Nina mtoto tumboni baba yangu niache tafadhali, usinichome sindano ya sumu,” niliendela kulalama, hakuna kilicho badilika. Mtu huyo hakuwa na muda na mimi, alionekana alikwisha zoea huruma zile. Kwahiyo jambo lile mbele yake ilikuwa ni kitu cha kawaida. Hakunijali kabisa hata usoni hakuniangalia.
Alitizama saa yake ya mkononi nikaona ameganda kwenye saa hiyo. Ni kama alikuwa akingoja muda fulani uwadie ndipo afanye kazi yake. Naam! hisia zangu zilikuwa sahihi, baada ya sekunde kadhaa akanigeukia tena na kunikabili:
“Mfungeni mikanda,” alitoa amri. Askari wenye bunduki wakaanza kufanya kazi hiyo. Pamoja na kwamba nilifumgwa minyororo kwenye mikono na miguu lakini nilifungwa tena mikanda.
Nikawa siwezi kufurukuta. Daktari yule alinisogelea tena akiwa na sindano mkononi, akanijia usawa wa shingo yangu kisha akaniinamia na kunidunga sindano ile ya sumu kwenye shingo yangu.
Nilifumba macho wakati tendo hilo linafanyika ingawa niliusikia uchungu wa sindano ile hasa wakati daktari anaibinya sumu ya Tetrodotoxin kuingia ndani ya mishipa ya mwili wangu.
Sekunde tatu zilitosha kunifanya nianze kuona maluweluwe, nikajiona napatwa na maumivu makali mwili wote, yalikuwa ni maumivu kama vile nababuliwa na moto, nikataka kupiga kelele mdomo nao ukawa mzito, mara povu zito likaanza kunitoka modomoni, damu ikanitoka puani .
Giza la ajabu likazikumba mboni zangu, muda mfupi badaye sikujua tena kilicho endelea duniani.
Toba!!
Nimekufa!!!.


Je mwanamke huyo alikufa? Usikose sehemu ya MWISHO ya mkasa huu wa kweli.
Sehemu ya mwisho ni lini??
 
Pole kwa huu mkasa, tena pole mno, ila tunarudia tena na tena, hata yaandikwe maovu mengi kiasi gani jinsi wenzetu mnavyonyanyaswa huko inakuwa haisaidii wenzenu toka ukanda wa pwani, pemba na unguja kwenda huko, tena kuna wengi huja humu na kuyakana kabisa hayo maovu mnayofanyiwa, kuanzia kushindishwa njaa. kupigwa, kulawitiwa, kubakwa, kufungiwa ndani bila kutoka nje ya nyumba n.k. n.k.
Tunachojiuliza kwanini hizi kesi bado zinaendelea na hatuoni mwisho wake?! Ina maana shida zetu zimetufanya vipofu na viziwi tusiyosikia haya maovu...
Ebu tazama mfano tu wa watu wanaozidi kuomba kazi huko kupitia website za oman...

Tanzanian Embassy in Muscat, Oman

Tue, 19 Mar 2019 15:59 EDT
Natafuta kazi oman
Umri wangu ni 35,kwa heshima na taadhima naomba kusaidiwa kupata nafasi ya kazi ya usafi wa maofisini,nyumbani,kuhudumia bustani nk.namba yangu +255744068286/+258852052646 ahsante!
mz.png
Moza Sarah ally
Tue, 19 Mar 2019 15:47 EDT
Natafuta kazi oman
Aslykm,umri wangu ni 35natafuta kazi za kufanya usafi wa maofisini,nyumbani,hatakuhudumia mifugo shamba,Niko tayari kwa mazingira yeyote ilimuradi yasivunje haki zakibinadamu.
Ahsante katika ujenzi wa taifa!

is.png
Saidi Omary
Wed, 6 Mar 2019 14:34 EST
Natafuta kazi Oman
Naomba kusaidiwa kupata kazi nipo Tanzania
Umri wangu miaka 22
Fani yangu ni ufundi WA Magari Na Udereva
is.png
Saidi Omary
Wed, 6 Mar 2019 14:28 EST
Naitwa Saidi Omary, nipo Tanzania na mimi ni raia WA Tanzania nnaumri WA miaka 22
Nnashida natafuta kazi
Faniyangu ni udereva Magari madogo pia nnaujuzi WA ufundi magari
Whatssap 0692493025
Email Saidiomary1996@gmail.com
Naomba kusaidiwa kupata kazi
Ntashukuru sana
tz.png
Dave
Wed, 6 Mar 2019 05:10 EST
Im looking for any job abroad
My name is Dave a boy of 21 living in Dar es salam im looking for any job here in Tanzania or even outside the country im a o_level certificate holder,a driving cetificate with a class D driving licence also with some college education im good at english and that i have education to work anywhere please if there is any work contact me through my email:ashadavid040@gmail.com
is.png
Issa Ally
Thu, 28 Feb 2019 19:43 EST
Natafuta kazi oman
Kwa jina naitwa issa ally ni raia wa tanzanzia,na umri wangu ni miaka 22 nilikuwa natafuta kazi oman ya kufany usaf wa nyumbn au hat kwenye kampun, au hat kwenye supermarket, kwa mawasiliano zaid namba zangu ni +255685153224 au +255719571299
tz.png
shukuru hamis
Thu, 28 Feb 2019 08:37 EST
NATAFUTA KAZI OMAN UMRI WANGU NINA MIAKA 25 NATAFUTA KAZI FANI YANGU MIMI NI FUNDI UMEME WA MAGARI MAKUBWA KAMA VILE :SCANIA ,VOLVO ,ACTROS ,MAN .ETC NINAO UZOEFU KWA MUDA USIOPUNGUA MIAKA 7 *KWA MAWASILIANO WHATSAP 0763872249
tz.png
shukuru hamis
Thu, 28 Feb 2019 08:33 EST
NATAFUTA KAZI OMAN
KWA MAJINA NAITWA SHUKURU HAMISI NINAISHI DAR ES SALAAM NATAFUTA KAZI FANI YANGU MIMI NI FUNDI UMEME WA MAGARI MAKUBWA KAMA VILE :SCANIA ,VOLVO ,ACTROS ,MAN .ETC NINAO UZOEFU KWA MUDA USIOPUNGUA MIAKA 7 *KWA MAWASILIANO WHATSAP 0763872249
tz.png
KARIMU URASSA
Mon, 18 Feb 2019 05:33 EST
Driver
Natafuta kazi ya udereva umri wangu 19 nikipata hata wakumuendesha boss,wanafunzi hata familia ya nyumbani mm nipo tayali Nipigie kwenye no.0687715948
Naseeb hassan
Sun, 30 Dec 2018 17:02 EST
Natafuta msichana mwalabu kutoka omani..nipo tanzania 0752976856
Sasa hapa tunajiuliza, mnataka tuwasaidie kivipi wakati mnajitangaza kutafuta kazi wenyewe, hamtusikilizi kwamba msiende, ham...
Tumechoka kwa kweli...
 
SEHEMU YA MWISHO

Nilifumba macho wakati tendo hilo linafanyika ingawa niliusikia uchungu wa sindano ile hasa wakati daktari anaibinya sumu ya Tetrodotoxin kuingia ndani ya mishipa ya mwili wangu.
Sekunde tatu zilitosha kunifanya nianze kuona maluweluwe, nikajiona napatwa na maumivu makali mwili wote, yalikuwa ni maumivu kama vile nababuliwa na moto, nikataka kupiga kelele mdomo nao ukawa mzito, mara povu zito likaanza kunitoka modomoni, damu ikanitoka puani .
Giza la ajabu likazikumba mboni zangu, muda mfupi badae sikujua tena kilicho endelea duniani.
Nilikufa!!!!!
*********
“Agripina, we’ Agripina...Agripina amka...Amka upesi!” nilisikia sauti ikiniamsha, sauti hiyo haikuwa ngeni masikioni mwangu, nilifumbua macho kivivu, ingawa niliona kwa mbali lakini sura ya mtu ninaye mfahamu ilijidhihilisha mbele yangu.
“Mama!”
“Bee mwanangu.”
“Nmekufa na mungu ameniingiza peponi!”
“Hahaha! hapana mwanangu. Upo kijiji cha Makose wilaya ya Lushoto mkoani Tanga, hujafa”
“Nipo Makose!i inamaana niko Tanzania?” niliuliza huku macho yangu yakitizama huku na kule ndani ya chumba ambacho pia hakikuwa kigeni machoni mwangu.
Kabla mama yangu hajanipa jibu mara akaingia mtu ambaye sikumtegemea kumwona. A likuwa ni Mariamu Rashidi huyu ni yule wakala wa wasichana wa kazi wanaokwenda kufanya kazi za ndani nchini ya Oman, alikuja na kuketi karibu yangu.
“Mambo Agripina, naona mzimu wa kifo uliokukumba Oman umekurejesha Duniani,” alisema kwa masikhara huku akiachia tabasamu pana na kuketi karibu yangu.
Nikiwa sijakaa sawa nikendelea kushangazwa na utitiri wa ndugu walioingia ndani ya chumba kile nilichokuwa nimelala. Kila ndugu aliyekuja kuniona alionekana kufurahi kwa kuona nikiwa hai.
“Naombeni tusikilizane jamani,” alisema Mariamu. Ndugu wote waliokuwa mule ndani wakanyamaza.
“Kila mtu angependa kujua nini kilifanyika hadi Agripina kwa sasa yupo hai ilihali taarifa zilienea kuwa tayari binti huyu kisha chomwa sindano ya sumu na kafa...” aliposema sentesi hiyo watu wote walijenga utulivu zaidi ili kujua nini kilitokea.
“Kwanza kabisa shukrani na pongezi zote anastahili Mwenyezi Mungu kwakuwa ni yeye ndiye anayejua nini hatma ya maisha ya mja wake. Agripina alikuwa katika hukumu ya kifo na alikwisha ingizwa katika chumba cha kuhifadhia maiti tayari kwa kuchomwa sindano yenye sumu.
“Kitu ambacho wanajeshi na serikali ya nchi ya Oman hawafahamu hadi sasa ni kwamba mtu anayehusika na kutoa adhabu ya kuwachoma watu sindano ya sumu nilimuhonga Dolla zaidi ya 2000/= ili mradi afanye lolote lile kumwepusha binti huyu na kifo.
“Siku ya hukumu ya Agripina ilipowadia mipango yote ilikuwa sawa, alichofanya mtu yule ni kumdunga Agripina sindano yenye dawa ya Ketamine benzodiazepine ambayo ilimfanya apatwe na maumivu makali sanjari na kumtoa povu mdomoni lakini ambacho askari waliokuwa hawajui ni kwamba chupa yenye sumu aina ya tetrodotoxin chupa hiyo ilikuwa na dawa ya benzodiazepine ambayo ilikuwa ni dawa ya usingizi.
“Baada ya Agripina kupoteza fahamu kilichofuata ilikuwa ni kuusafirisha mwili ndani ya jeneza, kama ambavyo mahakama ya nchi ile ilivyokuwa imeahidi, kwa hiyo tulimsafirisha Agripina akiwa kama maiti hadi hapa Tanzania. Hivyo ndivyo ilivyokuwa jamani...” alimaliza kusimulia Mariamu.
Kila mtu mule ndani maelezo yale yalimsisimua mno. kwa kweli hata mimi nafsi yangu ilikiri kuwa Mungu hashindwi na jambo. Nilipewa pole nyingi na ndugu na jamaa, ilikuwa ni furaha kubwa mno kwa mama yangu, wakati wote alikuwa akibubujikwa na machozi. Kwa upande wangu, jambo lile nililiona ni kama ndoto nzuri inayopita kichwani mwangu.
Muda mfupi baadaye ilikuwa ni zamu yangu kusimulia mambo yote yaliyo nisibu tangu siku ya kwanza naikanyaga ardhi ya nchi ya Oman, hadi nagota nukta ya mwisho, kila kila mtu alibubujikwa machozi
Ndugu zangu waliumizwa zaidi kusikia naisha na maambukizi ya virusi vya Ukimwi, hata hivyo hapakuwa na mwenyekuweza kubadili ukweli wa jambo hilo.
Maisha yaliendela kama kawaida nikiwa kijijini kwetu Makose. Miezi michache badaye, nilijifungua salama mtoto mzuri wa kiume, ambaye kwa bahati mbaya, alizaliwa akiwa anamambukizi ya virusi vya Ukimwi.
Wito wangu kwa wasichana wenzangu wa kitanzani hasa wenye ndoto za kwenda kufanya kazi za ndani nchi za nje, ni vema mkawa makini huko mwendako, bila hivyo unaweza kujikuta unatumbukia katika shimo la mauti bila kutegemea.
Jifunze kusimamia dhamira yako, kazi na mapenzi ni mafuta na maji, lakini pia ningependa mjifunze kupamabana hapa hapa nyumbani, kwani fursa zipo nyingi. Ukipatwa na tatizo hapa, ni rahisi kukabiliana nalo. Waswahili husema, zimwi likujualo halikuli likakwisha.
Kabla ya kusema kwa heri. Napenda nimshukuru mwandishi wa mkasa huu wa maisha yangu. Kaka yangu, Ally katalambula, ambaye alibadilisha maelezo yangu na kuwa maandishi yaliyonakshiwa na kachumbali za kifasihi na kuchapwa kwa mara ya kwanza katika Gazeti la Risasi toleo la kila Jumatano kutoka Global Publishers.
Haikuwa kazi rahisi kumsimulia mkasa huu hadi mwisho, kwani mara nyingi maelezo yangu yalikatishwa na kilio na simanzi kila nilipokuwa nikimweleza hadithi hii.

***



ALLY KATALAMBULA:

Agripina alifariki Dunia January 12 mwaka 2016 huko mjini Tanga kwa maradhi ya UKIMWI. Ameacha mtoto mmoja wa miaka 7 ambaye analelewa kwenye kituo cha watoto yatima cha Umra kilichopo Magomeni jijini Dar es salam.

Bwana ametoa, Bwana ametwaa, jina leke lihimidiwe. Mungu na ailaze roho ya marehemu Agripina Joseph mahali pema peponi.

MWISHOOOO.

Jiandae kusoma kitabu changu kipya kiitwacho MAUJI YALIYOJAA UTATA. ni hadithi nzuri ya kipelelezi, kitabu ni kikubwa, bei shilingi elfu kumi.
 
Hakya Mungu leo nimetoa machozi kiukweli sikutegemea kama amefariki plz naomba no au namna ntakayoweza kumpata huyo mtoto nipo mbali sana ila plz nipeni anuani nijue namna ya kumsaidia huyo mtoto ila pia na kupata taarifa za kina kwa wazazi wake .usikumwema wadau.
 
Dah nipo mbali sana na Nchiyetu nduguzagu ila mimi kama mwanaume kweli leo chozi limenitoka nilitegemea agripina nimuone labda nimsaidie chochote ila nimekwazika sana kuwa Amefariki dah!!admn naombq nipewe contact zakuwapata ndugu wake coz me pia hom ni Muheza tanga
 
Dah nipo mbali sana na Nchiyetu nduguzagu ila mimi kama mwanaume kweli leo chozi limenitoka nilitegemea agripina nimuone labda nimsaidie chochote ila nimekwazika sana kuwa Amefariki dah!!admn naombq nipewe contact zakuwapata ndugu wake coz me pia hom ni Muheza tanga
Kasaidie kwanza ndugu zako huko vijijini waende ata shule
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom