MKASA: Hadi Lini?

MKASA: Hadi Lini?

HADI LINI! 25

Na Bishop Hiluka


“Hivi jema kwako ni lipi, tuendelee kugombana na hatimaye tuachane ili watoto wetu wateseke au tusameheane na tuanze ukurasa mpya?” Ibrahim alimuuliza Pamela huku akionesha mshangao mkubwa.
“Ukurasa mpya kauanze na mwanamke mpya, na mimi niache nianze ukurasa mpya kivyangu.” Pamela alisema na kumfanya Ibrahim ashtuke sana.
“Kama umekusudia kuachwa hapa sahau, mimi najua kuoa tu sijui kuacha,” Ibrahim aling’aka kwa hasira.
“Na ulipotaka kuniacha hukujua kama hujui kuacha? Naona unajitekenya na kucheka mwenyewe! Nasema hivi, leo bila talaka yangu humu ndani hakukaliki wala hakulaliki,” Pamela alisema kwa ukali huku akimkazia macho Ibrahim.
“Hivi uko yakini Pamela?” Ibrahim alimuuliza Pamela kwa mshangao.
“Niko yakini kabisa, nafahamu ninachokisema!” Pamela alijibu huku akiendelea kumtulizia macho Ibrahim.
Ibrahim akazidi kuchanganyikiwa, alimtazama Pamela kwa kitambo kirefu na kushusha pumzi, kisha akatingisha kichwa chake kwa masikitiko na kuondoka, akaelekea kwenye mlango, akaufungua na kutoka nje kimya kimya huku akiufunga ule mlango nyuma yake.
Pamela alimtazama kwa mshangao wakati akiondoka na kushusha pumzi, kisha akaketi pale kwenye kiti cha kupumzikia pale kwenye balcony. Baada ya muda mfupi alisikia hodi inabishwa mlangoni, akainuka na kwenda kufungua mlango na kuchungulia nje, akamuona Mama Bigirimana akiwa amesimama pale mlangoni akiwa na sura iliyosawajika kidogo.
“Mama yangu, kulikoni! Mbona tumepata taarifa za kutatanisha?” Mama Bigirimana alimuuliza Pamela huku akiwa bado katika sura iliyosawajika.
“Habari zipi za kutatanisha, mama?”
“Tumeambiwa eti hutaki kumsamehe mumeo ila unachodai ni talaka tu?”
Pamela akaachia mguno ulioambatana na tabasamu, alipotaka kusema neno Mama Bigirimana akamkatiza.
“Kama hutajali wazazi wako wanakuhitaji mara moja huko sebuleni. Najua hivi sasa ni usiku wa manane na ungependa kupumzika lakini nia yetu ni njema tu, mama yangu,” Mama Bigirimana alisema huku akishusha pumzi.
“wala usijali mama, nakuja sasa hivi,” Pamela alisema na kurudi chumbani huku akiufunga mlango nyuma yake.
Mama Bigirimana aliutazama ule mlango kwa wasiwasi kisha akazifuata ngazi na kuanza kushuka akielekea sebuleni. Pale sebuleni kimya kizito kilikuwa kimetawala, watu walikuwa wameketi wakiwa wametahayari huku kila mmoja akiwaza lake na wakionekana kusubiri kwa hamu kusikia kilichokuwa kinaendelea. Ibrahim alikuwa ameketi akiwa kajiinamia kwa huzuni.
Mama Bigirimana alifika pale sebuleni peke yake bila Pamela huku akiwa anatembea taratibu na kuwafanya wote wageuze shingo zao kumtazama kwa wasiwasi.
“Anakuja!” Mama Bigirimana alisema huku akiketi juu ya kochi baada ya kuona macho yote yalikuwa yanamtazama kwa wasiwasi.
Haikuchukua muda Pamela akafika pale sebuleni na kusimama akiwatazama wale wazee kwa mashaka kidogo. Mama Bigirimana alisogea na kuacha nafasi kidogo huku akimuashiria Pamela aketi jirani yake. Pamela alikwenda kuketi pale na kubaki kimya akiwatazama wale wazee kwa wasiwasi.
Kisha macho yake yakatua kwa Ibrahim ambaye alikuwa ameinamisha uso wake kutazama chini, hofu ikaanza kumtambaa Pamela mwilini mwake. Kitambo kifupi cha ukimya kikazuka pale sebuleni huku wale wazee wakitazamana kwa makini, kisha Mzee Tugiramahoro akakohoa kidogo kurekebisha sauti yake.
“Haya mama, hebu tuambie, kulikoni! Mbona tumepata taarifa za kutatanisha?”
Pamela alimtazama baba yake kwa makini kisha macho yake yakahama na kuwatazama wale wazee wengine, na mwisho akamalizia kwa Ibrahim na kushusha pumzi.
“Ndiyo baba, nadai talaka, ni Ibrahim ndiye anayeleta utatanishi kwa kutotoa talaka!” Pamela alisema na kuwafanya wale wazee wamwangalie kwa mshangao mkubwa.
Mzee Tugiramahoro alionekana kukerwa mno na ile kauli, hasira iliyochanganyika na mshangao mkubwa ikaibuka ndani yake.
“Hivi u mzima kweli wewe, au una wazimu?” Mzee Tugiramahoro alimuuliza Pamela kwa sauti kali.
“Mungu apishe mbali, sina wazimu, sikupagawa, sikurogwa na wala sina kichaa. Najua ninachokifanya baba! Nisaidieni kumwambia Ibrahim kuwa nataka talaka yangu sasa hivi!” Pamela alisisitiza huku akionekana kujiamini.
Mzee Tugiramahoro alitaka kusema lakini akasita na kugeuza shingo yake kumtazama mkewe kisha akainua mabega yake juu na kuyashusha akionekana kuchanganyikiwa huku akiwa hana la kufanya.
Wazee wote walionekana kuchanganyikiwa, walimtazama Pamela wakiwa hawaelewi ni kipi kilichomfanya awaite, maana mwanzoni walidhani alikuwa amewaita pale kuja kutatua mgogoro wa ndoa yao lakini sasa alionesha kuwa alitaka wamsaidie kudai talaka! Mama Bigirimana alimwangalia Pamela kwa huzuni.
“Mama, ni sababi zipi hasa zimekufanya utake mumeo akutaliki?” Mama Bigirimana alimuuliza Pamela kwa sauti tulivu.
Pamela alimtazama yule mama huku aking’atang’ata midomo yake na kufikicha ncha ya nguo aliyokuwa amejitanda kichwani.
“Ni kwa sababu nampenda sana na ninathamini maendeleo yake… mama!” Pamela alijibu huku akiiangalia ile ncha ya nguo na kuwafanya watu wote wamwangalie kwa mshangao.
Wale wazee waliendelea kumwangalia Pamela kwa muda kisha wakaangaliana wenyewe kwa wenyewe. Ibrahim aliduwaa na kubaki akimwangalia Pamela kwa mshangao zaidi.
“Sasa, kama unampenda sana na unathamini maendeleo yake mbona unataka akuache?” Mama Bigirimana alimuuliza Pamela huku mshangao ukiwa haujamtoka usoni kwake.
Pamela alinyanyua uso wake na kuwaangalia kwa makini wale wazee, hasa Mzee Tugiramahoro na Mzee Bigirimana. Akaonekana kusita na kumeza mate huku akimtupia jicho Ibrahim. Muda ule Ibrahim alionekana kuchanganyikiwa zaidi, jasho lilikuwa linamtoka.
“Kwa sababu sioni sababu kwa nini tumlazimishe kuishi na mtu aliyepanga kumtaliki badala ya kuheshimu maamuzi yake, mbona yeye haulizwi kwa nini alitaka kuniacha na kuoa mwanamke mwingine na kwa nini sasa hivi ananiona nafaa?”
Kauli ile ikafanya pazuke tena ukimya, wale wazee wote wakabaki kimya wakimtazama Pamela kwa makini. Mama Bigirimana akashusha pumzi ndefu huku akibetua kichwa chake akionekana kumwelewa Pamela na kuafikia naye.
“Hilo nalo neno! Mimi nipo upande wako mama, wanaume wanapaswa watambue kuwa mwanamke si mtumwa, tena wewe umekuwa muungwana sana, mwanzo alipokuja hapa alisema yake lakini sasa hayasemi… kwa nini tumuonee haya mtu asiyetuonea haya?”
Ibrahim aliwaangalia wale wazee huku akionekana kugwaya sana. Aliinamisha uso wake akiwa hana la kusema, machozi yalianza kumlengalenga. Pamela alimtazama Ibrahim kwa makini huku akijitahidi kuyazuia machozi ambayo yalianza kumtoka.
“Baba Samantha, nakupenda sana, kwa nini nisikuache huru ukaishi na mwanamke unayempenda. Ulipanga kuniacha ili uoe mwanamke anayekufaa na sasa unaniomba msamaha kwa kuwa wazee wamekulazimisha kufanya hivyo, sijui hapa pendo liko wapi? Hivi utalazimishwaje kuishi na mwanamke uliyemchoka eti kwa kuwa wazee wamekulazimisha? Ndiyo maana nataka unitaliki ili uwe huru kutafuta pendo la kweli…” Pamela alimwambia Ibrahim kwa sauti tulivu.
“Mwambie mama, mwambie mpumbavu huyu,” Mama Bigirimana alidakia na kuwafanya watu wengine wageuke kumwangalia kwa mshangao.
Sasa machozi mengi yalikuwa yanamtoka Ibrahim, alitaka kusema neno lakini akashindwa kuwa kuwa maneno yalikuwa hayatoki, akaanza kulia kilio cha kwikwi. Muda ule ule aliinuka, akamfuata Pamela na kuanguka miguuni kwake kisha akaishika miguu yake huku akiendelea kulia kwa uchungu.
Pamela alimtazama Ibrahim kwa huzuni, akajitahidi kuyazuia machozi yake. Mzee Tugiramahoro aliinuka na kumfuata Ibrahim, akamshika mabega na kumnyanyua kutoka pale alipokuwa amelala, kisha akampa ishara Mama Bigirimana akimtaka ainuke na kumpisha Ibrahim.
Mama Bigirimana alitii na kupisha, Mzee Tugiramahoro akamkalisha Ibrahim kando ya Pamela na kunyanyua kiganja cha mkono wa Pamela kisha akakikutanisha na kiganja cha mkono wa Ibrahim.
“Pamela, mumeo amejua makosa yake na sasa anataka muanze upya, sioni kwa nini usimsamehe…” Mzee Tugiramahoro alisema na kuwatazama wazee wengine.
“Na ikiwa mimi ni mzazi wenu, basi kwa niaba ya wazazi wenzangu wote naiombea kwa Mungu ndoa yenu idumu zaidi na zaidi, isiwe na migogoro tena wala visasi,” Mzee Tugiramahoro alisema na watu wote pale sebuleni wakaitikia, “Amina!”

MWISHO.
 
HADI LINI!

Na Bishop Hiluka

Yalikuwa yamemfika kooni baada ya kuitafuta haki yake kila mahali na kushindikana, akafikia uamuzi wa kuwaita wazazi wa pande zote mbili ili aweke wazi kuhusu msimamo wake juu ya ndoa yake. Kama noma na iwe noma lakini asingeweza kuendelea kuvumilia, avumilie hadi lini!...


JUMAMOSI, saa kumi na mbili na nusu jioni, kwa saa za Burundi, sauti tamu ya muziki laini wa kubembeleza ilikuwa inasikika kutoka katika spika zilizokuwa kwenye kona za ukumbi mkubwa wa kisasa wa burudani ndani ya Hotel Club du Lac Tanganyika.
Club du Lac Tanganyika ilikuwa hoteli yenye hadhi kubwa iliyokuwa imejengwa kwenye mandhari ya kuvutia ya ufukwe wa Ziwa Tanganyika jijini Bujumbura, Burundi. Ilikuwa hoteli ya kisasa kabisa iliyokuwa imezungukwa na mazingira yenye utulivu mkubwa ufukweni mwa ziwa, ikiwa kando ya barabara ya Chausse d'Uvira iliyokuwa inaelekea katika mji mdogo wa Uvira.
Ikiwa imezungukwa na uzio madhubuti ulioifanya kuwa mahali patulivu zaidi na penye usalama wa uhakika, ilikuwa sehemu tulivu zaidi ya kwenda kujirusha kwa watu wenye ukwasi, ikiwa umbali wa kilomita tatu tu kutoka katika Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Bujumbura.
Pia ilikuwa sehemu muhimu sana kwa burudani na wageni wengi kutoka nje walipenda kwenda sehemu ile, hasa mwisho wa wiki, kutokana na kuwa na kumbi mbili za kisasa: ukumbi mmoja ulitumika kwa ajili ya mikutano, ukiwa na sifa zote, na wenye viyoyozi na umeme wa uhakika saa 24, jambo linaloufanya kuvutia wageni mbalimbali. Ukumbi mwingine ulitumika zaidi kwa ajili ya burudani na matukio.
Ukumbi wa burudani ulikuwa na kila aina ya starehe, ukiwa na madirisha makubwa ya vioo yaliyofunikwa na mapazia safi marefu, na ulikuwa na kila kionjo cha daraja la kimataifa. Ndani ya ukumbi ule kulikuwa na wahudumu wazuri wa kike, warembo kwelikweli, waliokuwa wakihudumia wateja wachache waliokuwemo ukumbini muda huo wakiwa wameketi kwenye meza nzuri za mbao ya mti wa mninga na viti vifupi vyenye foronya laini.
Muda ule wa saa kumi na mbili na nusu za jioni idadi kubwa ya wateja waliokuwemo ndani ya ukumbi ule walikuwa raia wa kigeni, hasa kutoka katika nchi za Ufaransa na Marekani. Upande wa kulia wa ukumbi ule kulikuwa na mlango na dirisha dogo la jikoni, na humo ndani kulionekana wapishi waliokuwa katika mavazi yao ya kazi, wakiandaa chakula.
Katika ukumbi ule, mmoja wa wateja Waafrika walioonekana aliitwa Ibrahim Bigirimana, alikuwa mwanamume wa Kitanzania aliyekuwa na asili ya kutoka mkoa wa Kigoma, mkoa ambao uko pembezoni mwa nchi ya Tanzania katika mpaka wa Tanzania na Burundi.
Ibrahim Bigirimana alikuwa ameketi peke yake kwenye meza moja akionekana kuzama katika fikra fulani huku akiwa na shauku kubwa ya kusubiri kitu fulani muhimu sana, ambacho, ni yeye tu kati ya watu wote waliokuwemo mle ukumbini ndiye aliyekuwa akikijua.
Ibrahim alishusha pumzi za ndani kwa ndani na kutupa macho yake kuangalia nje kupitia ukuta msafi wa kioo cha dirisha, mkono wake mmoja alikuwa ameshika bilauri ndefu iliyokuwa na mvinyo mwekundu wa Kifaransa aina ya Navette de Marseille, na mkono wake wa kushoto alikuwa kauegemeza juu ya kiti alichokalia. Ibrahim akainua bilauri ya mvinyo na kupiga funda taratibu huku akionekana kuwaza mbali sana.
Alikuwa mwanamume mrefu na maji ya kunde, akiwa na sura bashasha ya kitoto iliyokuwa na muonekano uliomfanya mtu yeyote aliyemuona adhani kuwa hangeweza kuzidi miaka therathini, ingawa alishapita miaka hiyo.
Akiwa na umri wa miaka arobaini na mbili, kimuonekano, Ibrahim alikuwa na umbo kakamavu la kimichezo lililofanana na maumbo ya wachezaji wa ligi ya mpira wa kikapu wa nchini Marekani.
Alikuwa mcheshi sana na mtu wa kupenda kujichanganya na watu wengine bila kujali kipato, alikuwa muongeaji mkubwa mwenye kuzimudu vyema lugha za Kiswahili, Kiingereza, Kifaransa na hata Kirundi, lugha iliyokuwa ikizungumzwa zaidi na wenyeji wa nchi ile ya Burundi, jambo ambalo liliwafanya watu wengi kudhani kuwa labda alikuwa Mrundi mwenzao, hasa kwa kuwa hata jina lake la mwisho la ‘Bigirimana’ ni jina lililokuwa linatumiwa na Warundi.
Ibrahim alikuwa Muha kutoka mkoani Kigoma, kabila lililokuwa na utamaduni ulioshabihiana kwa kiasi kikubwa sana na ule utamaduni wa Warundi.
Ibrahim alikuwa ameishi jijini Bujumbura kwa takriban miaka kumi sasa. Na alikuwa akifanya kazi kama Meneja Mkuu wa CRDB Bank Burundi, benki iliyokuwa na makao yake katika barabara ya Chaussée du Prince Louis Rwagasore, ploti namba 490/A, jijini Bujumbura.
Kwa nafasi hiyo, Ibrahim alikuwa mtu mwenye mafanikio mema, ingawa alikuwa na kasoro moja iliyoonekana wazi, hakuwa na wala hakupenda kuwa na kitambi.
Wengi walidhani labda Ibrahim alikuwa amebebwa hadi kufikia nafasi ile, lakaini ukweli hakufikia nafasi ya ile ya umeneja mkuu wa benki hiyo kwa bahati au kama wasemavyo Waswahili ‘zali la mentali’, bali alikuwa nazo sifa zinazostahili ikiwemo elimu ya juu na uzoefu wa kazi.
Kabla hajakuwa Meneja Mkuu wa CRDB Bank Burundi, ibrahimu alikuwa amefanya kazi kama Manager Corporate Banking na baadaye akawa Senior Relationship Manager Corporate Banking katika Benki ya Biashara ya Burundi (Commercial Bank of Burundi) iliyokuwa na makao yake katika makutano ya barabara za Avenue des USA na Chaussée P.L. Rwagasore, ikiwa mkabala na jengo la CRDB Bank Burundi, jijini Bujumbura.
Ibrahim alikuwa msomi wa Shahada ya Umahili ya Business Administration aliyoipata kutoka Chuo Kikuu cha Oxford, Uingereza, ambacho kilikuwa chuo kikongwe zaidi katika ulimwengu wa nchi zinazozungumza lugha ya Kiingereza, na Shahada ya Kwanza ya Banking and Financial Services aliyohitimu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Tanzania.
Baada ya kumaliza chuo kikuu na kabla hajaenda kufanya kazi nchini Burundi, Ibrahim alikuwa amefanya kazi kaatika Benki Kuu ya Tanzania kwa miaka miwili kisha akaacha na kwenda kuishi jijini Bujumbura ambako aliajiriwa katika benki ya biashara ya Burundi. Hii ilitokana na yeye kuamua kumfuata mke wake aliyekuwa amerudishwa nchini Burundi baada ya kukumbwa na matatizo ya uraia alipokuwa akiishi nchini Tanzania.
Alipofika Burudni na kuajiriwa Commercial Bank of Burundi Ibrahim alifanya kazi kwa miaka kadhaa, na kutokana na uwezo wake na ufanisi kazini alichukuliwa na CRDB Bank Burundi, kama mwanzilishi na Meneja Mkuu wa benki hiyo jijini humo, nafasi ambayo aliweza kudumu nayo hadi wakati huo.
Huyo ndiyo Ibrahim Bigirimana, ambaye Jumamosi hiyo alikuwa katika ukumbi wa maraha wa Hotel Club Du Lac Tanganyika akiwa mwenye shauku kubwa. Alinyanyua bilauri yake na kunywa funda dogo la mvinyo kisha akaitazama saa yake ya mkononi kwa mara nyingine tena kisha akaonekana kutikisa kichwa chake.
Alishusha pumzi za ndani kwa ndani huku akisonya kwa huzuni, ni wazi alikuwa hapo akisubiria kitu muhimu sana lakini hadi muda ule alionekana kuanza kuishiwa na uvumilivu. Aliitazama tena saa yake na kuminya midomo yake akionekana kuwaza mbali, akabaki akiikodolea macho ile saa kana kwamba ilikuwa mbovu.
Laiti kama ingelikuwa saa ya kawaida labda angeweza kusema kuwa ilikuwa na kasoro, lakini hiyo saa kama ilivyo kwa vitu vyake vingi, haikuwa ya kawaida kabisa!

ITAENDELEA...

Cc the_legend Norshad bobefu zoefu Pablo PAKAYA Ibney blackstarline Bryece Tater, Bigjahman moneytalk marybaby, nipo2, ram, kisukari, Smart911, Madame S, carbamazepine, Astelia, culture gal , Prisoner of hope, Mine eyes, kuku mweus, Thad, hearly, Shunie, moneytalk,Tumosa, Mine eyes, Kudo, swahiba92, ludist, Toyota escudo, Clkey, macson3, Thad, boga la kiangazi, macson3, LEGE, Smart911, Richard irakunda, skfull, popie, Krizy Beat, hearly nipo2 MWINDAJI HARAMU kakhulu Katavi Norami mbududa iron2012 popie Bughy Harry Kinondoni Sweetheart SUPER EMILY
Ndio ndio..nipo hapa boss Bishop Hiluka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndio ndio..nipo hapa boss Bishop Hiluka

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi kazi yangu ni kuuombea huu mguu tu![emoji116][emoji6][emoji6][emoji6]
1554277337498.jpeg
 
HADI LINI! 5

Na Bishop Hiluka


Kuna kingine chochote?” yule mhudumu alimuuliza Ibrahim akiwa bado kamkazia macho yake.
Ndiyo,” Ibrahim alijibu yule mhudumu huku akimtupia jicho Bélise, kisha anaongeza, “Vitu tulivyoagiza vipeleke kwenye kile chumba maalumu, sawa?”
“Ondoa shaka,” alisema yule mhudumu huku akimtupia jicho la wizi Bélise na kuachia tabasamu pana. Kisha aligeuka na kuondoka haraka kutoka eneo lile na kuelekea kwenye kaunta ya jikoni ya ukumbi wa maakuli.
Ibrahim alishusha pumzi huku akimtupia jicho Bélise na kuachia tabasamu, “Chakula cha hapa kizuri sana,” alismema huku akiendelea kutabasamu.
* * * * *
Saa tatu usiku, kwenye chumba kizuri cha kifahari cha Hotel Club du Lac Tanganyika, taa mbili za rangi ya bluu zilikuwa zinatoa mwanga hafifu wenye mg’ao na kufanya nusu ya chumba kile kuwa kizani.
Kilikuwa chumba kikubwa chenye kitanda kikubwa cha samadari kilichokuwa katikati ya chumba, kitanda kile kilikuwa cha futi sita kwa sita, cha mbao ngumu za mninga na chenye droo mbili kila upande, na juu ya zile droo kulikuwa na zile taa mbili za rangi ya bluu.
Mbele ya kile kitanda kulikuwa na seti nzuri ya runinga pana aina ya LG ya inchi hamsini na mbili na chini ya ile runinga kulikuwa na meza nzuri nyeusi ya kioo, ambayo juu ya meza kulikuwa na simu mbili kubwa za kisasa za Smartphone na kando ya meza ile kulikuwa na briefcase nzuri nyeusi iliyokuwa imeegamishwa kwenye ukuta.
Upande wa kushoto wa kile chumba kulikuwa na jokofu la vinywaji lililokuwa kwenye kona, na hatua chache kutoka kwenye lile jokofu kulikuwa na dirisha pana la kioo lililokuwa limefunikwa kwa pazia zito na refu lenye nakshi za michoro ya maua yaliyodariziwa vizuri na kuyafanya yapendeze.
Kwa kutokea juu kwenye lile dirisha la chumba kile mtu angeweza kuona mandhari nzuri yenye nyasi nzuri za rangi ya kijani kibichi zilizopakana na maua ya rangi tofauti ya kuvutia na bwawa ambalo lilikuwa limezungukwa na nyasi zilizopandwa katika hoteli ile.
Pia mle ndani kulikuwa na kabati kubwa la kisasa la nguo ambalo hata hivyo lilikuwa limefungwa. Na pembeni ya lile kabati kulikuwa na kochi moja kubwa la sofa na meza ya kioo iliyokuwa mbele yake iliyokuwa na bilauri mbili ndefu, chupa kubwa ya mvinyo mwekundu wa Navette de Marseille na vyombo vilivyokuwa na mabaki ya chakula, vyote vikiwa juu ya ile meza.
Kando ya lile sofa kulikuwa na meza fupi ya mbao iliyokuwa na simu ya mezani na kitabu kidogo kilichokuwa ba orodha ya majina ya watu na kampuni zilizotumia huduma ya simu hiyo ya mezani. Kwenye kona ya chumba kile upande wa kulia kabisa kulikuwa na mlango wa kuelekea kwenye chumba kidogo cha maliwato na bafu.
Ukutani kulikuwa na picha mbili kubwa nzuri za kuchorwa zilizokuwa zimetundikwa sehemu mbili tofauti. Moja ilikuwa ni picha ya wanyama wa porini na picha nyingine ilikuwa ya ua zuri la rangi nyekundu na bluu lililochorwa kwa ustadi wa hali ya juu.
Picha zote mbili zilikuwa zimewekwa ndani ya fremu nzuri za kioo na kuzifanya zionekane vizuri katika hizo kuta nyeupe na safi za chumba kile. Chini sakafuni kulikuwa na zulia zuri lenye mchanganyiko wa maua ya rangi ya njano, bluu na kijani kibichi.
Hapo sakafuni zilionekana nguo za Ibrahim na Bélise zilizokuwa zimetupwa tupwa na kusambaa ovyo, na juu ya kile kitanda kikubwa cha kifahari walionekana Ibrahim na Bélise waliokuwa wamemezwa na ulimwengu wa anasa.
Muda ule Bélise alikuwa anajitahidi kumwonesha Ibrahim ufundi sanaa ya aina yake na kumfanya kutoa miguno kwa raha aliyojisikia huku akimimina ahadi nyingi ambazo aliapa kuwa angezitekeleza.
Ibrahim alimbusu mzinzi mwenzie na kumpapasa nyama za mgongo huku akihema kwa nguvu. Bélise naye alikuwa anatweta kwa mchoko lakini akionekana kuhisi faraja kubwa iliyokuwa inapenya kwenye mishipa yake ya damu, akajikuta akilia kilio kilichokosa tafsiri inayoweza kukubalika kwa haraka.
Akiwa anakaribia kumaliza safari yake ya kufika kileleni, Ibrahim alianza kutapatapa kama mtu aliyetaka kukata roho, jambo hilo likamfanya Bélise kupitisha vidole vyake laini ambavyo vilikuwa na kucha ndefu kwenye masikio ya Ibrahim. Kitendo hicho kikamfanya Ibrahim kuvunja dafu huku akilia kama mtoto mdogo.
Alitweta huku akionekana kuwa hoi na mapigo ya moyo wake yalikuwa yakimuenda mbio isivyo kawaida.
Bélise alijiinua taratibu kutoka pale kitandani na kumwacha Ibrahim akiwa bado amejilaza kwa uchovu aliokuwa nao, kisha aliingia bafuni na kujimwagia maji, na alipotoka alichukua taulo na kujifunga juu yake kupitia kifuani na kufanya lile taulo liache mapaja yake wazi, kisha alirudi tena katandani, akaketi juu ya kitanda huku akimtazama Ibrahim kwa aibu. Ibrahim alikuwa bado amejilaza huku akiwa amefumba macho yake kwa uchovu.
Mara simu ya Ibrahim ikaanza kuita na kumshtua Ibrahim. Alifumbua macho yake na kuinua kichwa chake kutazama mahali zilipo zile simu zake. Bélise aliinuka na kuichukua ile simu iliyokuwa inaita huku akipitisha macho yake kuiangalia namba ya mpigaji kabla hajampa Ibrahim.
Ibrahim aliitazama kwa makini ile namba iliyokuwa inampigia na kuguna huku akikunja sura yake. Aliipokea ile simu kwa shauku kubwa na kuiweka kwenye sikio lake la upande wa kushoto huku akiminya midomo yake.
“Hallo… unasema!” Ibrahim anamaka kwa mshtuko huku akijichomoa haraka kutoka pale kitandani.
Alimkodolea macho Bélise huku akiwa makini kusikiliza kile alichokuwa anaelezwa na mtu aliyekuwa upande wa pili wa ile simu. Akashusha pumzi ndefu huku aakiuma mdomo wake wa chini.
“Una uhakika? Okay, okay… nakuja sasa hivi…” Ibrahim alisema na kuamka kutoka pale kitandania akakimbilia bafuni bila hata kukata simu, kule bafuni alijimwagia maji chap chap na alipomaliza akaokota zile nguo zake pale sakafuni na kuanza kuvaa haraka.
Muda huo Bélise alikuwa anamtazama kwa mshangao uliokuwa umechanganyika na wivu, macho yake yalionesha wazi kumuonea Ibrahim.
Ibrahim alipomaliza kuvaa alichukua briefcase yake na kuanza kutoka nje haraka kabla hata hajamaliza kuvaa shati lake vizuri, mara akakatizwa na sauti kali ya Bélise kabla hata hajafungua mlango na kutokomea.
Mpenzi!”
Ibrahim aligeuza shingo yake kumtazama Bélise kwa mshangao, alionekana kukerwa kidogo.
“Unasemaje? Nachelewa!” Ibrahim alisema huku akimtazama Bélise kwa makini zaidi.
Bélise alikuwa amezishika mkononi zile simu mbili za Ibrahim na kumwonesha huku akimkazia macho.
Sawa, lakini umesahau simu zako,” alimwambia huku akiminya midomo yake akionesha dhahiri kuingiwa na wivu.

ITAENDELEA...
[emoji38]mzinzi akimbusu mzinzi mwenzie [emoji36]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HADI LINI! 25

Na Bishop Hiluka


“Hivi jema kwako ni lipi, tuendelee kugombana na hatimaye tuachane ili watoto wetu wateseke au tusameheane na tuanze ukurasa mpya?” Ibrahim alimuuliza Pamela huku akionesha mshangao mkubwa.
“Ukurasa mpya kauanze na mwanamke mpya, na mimi niache nianze ukurasa mpya kivyangu.” Pamela alisema na kumfanya Ibrahim ashtuke sana.
“Kama umekusudia kuachwa hapa sahau, mimi najua kuoa tu sijui kuacha,” Ibrahim aling’aka kwa hasira.
“Na ulipotaka kuniacha hukujua kama hujui kuacha? Naona unajitekenya na kucheka mwenyewe! Nasema hivi, leo bila talaka yangu humu ndani hakukaliki wala hakulaliki,” Pamela alisema kwa ukali huku akimkazia macho Ibrahim.
“Hivi uko yakini Pamela?” Ibrahim alimuuliza Pamela kwa mshangao.
“Niko yakini kabisa, nafahamu ninachokisema!” Pamela alijibu huku akiendelea kumtulizia macho Ibrahim.
Ibrahim akazidi kuchanganyikiwa, alimtazama Pamela kwa kitambo kirefu na kushusha pumzi, kisha akatingisha kichwa chake kwa masikitiko na kuondoka, akaelekea kwenye mlango, akaufungua na kutoka nje kimya kimya huku akiufunga ule mlango nyuma yake.
Pamela alimtazama kwa mshangao wakati akiondoka na kushusha pumzi, kisha akaketi pale kwenye kiti cha kupumzikia pale kwenye balcony. Baada ya muda mfupi alisikia hodi inabishwa mlangoni, akainuka na kwenda kufungua mlango na kuchungulia nje, akamuona Mama Bigirimana akiwa amesimama pale mlangoni akiwa na sura iliyosawajika kidogo.
“Mama yangu, kulikoni! Mbona tumepata taarifa za kutatanisha?” Mama Bigirimana alimuuliza Pamela huku akiwa bado katika sura iliyosawajika.
“Habari zipi za kutatanisha, mama?”
“Tumeambiwa eti hutaki kumsamehe mumeo ila unachodai ni talaka tu?”
Pamela akaachia mguno ulioambatana na tabasamu, alipotaka kusema neno Mama Bigirimana akamkatiza.
“Kama hutajali wazazi wako wanakuhitaji mara moja huko sebuleni. Najua hivi sasa ni usiku wa manane na ungependa kupumzika lakini nia yetu ni njema tu, mama yangu,” Mama Bigirimana alisema huku akishusha pumzi.
“wala usijali mama, nakuja sasa hivi,” Pamela alisema na kurudi chumbani huku akiufunga mlango nyuma yake.
Mama Bigirimana aliutazama ule mlango kwa wasiwasi kisha akazifuata ngazi na kuanza kushuka akielekea sebuleni. Pale sebuleni kimya kizito kilikuwa kimetawala, watu walikuwa wameketi wakiwa wametahayari huku kila mmoja akiwaza lake na wakionekana kusubiri kwa hamu kusikia kilichokuwa kinaendelea. Ibrahim alikuwa ameketi akiwa kajiinamia kwa huzuni.
Mama Bigirimana alifika pale sebuleni peke yake bila Pamela huku akiwa anatembea taratibu na kuwafanya wote wageuze shingo zao kumtazama kwa wasiwasi.
“Anakuja!” Mama Bigirimana alisema huku akiketi juu ya kochi baada ya kuona macho yote yalikuwa yanamtazama kwa wasiwasi.
Haikuchukua muda Pamela akafika pale sebuleni na kusimama akiwatazama wale wazee kwa mashaka kidogo. Mama Bigirimana alisogea na kuacha nafasi kidogo huku akimuashiria Pamela aketi jirani yake. Pamela alikwenda kuketi pale na kubaki kimya akiwatazama wale wazee kwa wasiwasi.
Kisha macho yake yakatua kwa Ibrahim ambaye alikuwa ameinamisha uso wake kutazama chini, hofu ikaanza kumtambaa Pamela mwilini mwake. Kitambo kifupi cha ukimya kikazuka pale sebuleni huku wale wazee wakitazamana kwa makini, kisha Mzee Tugiramahoro akakohoa kidogo kurekebisha sauti yake.
“Haya mama, hebu tuambie, kulikoni! Mbona tumepata taarifa za kutatanisha?”
Pamela alimtazama baba yake kwa makini kisha macho yake yakahama na kuwatazama wale wazee wengine, na mwisho akamalizia kwa Ibrahim na kushusha pumzi.
“Ndiyo baba, nadai talaka, ni Ibrahim ndiye anayeleta utatanishi kwa kutotoa talaka!” Pamela alisema na kuwafanya wale wazee wamwangalie kwa mshangao mkubwa.
Mzee Tugiramahoro alionekana kukerwa mno na ile kauli, hasira iliyochanganyika na mshangao mkubwa ikaibuka ndani yake.
“Hivi u mzima kweli wewe, au una wazimu?” Mzee Tugiramahoro alimuuliza Pamela kwa sauti kali.
“Mungu apishe mbali, sina wazimu, sikupagawa, sikurogwa na wala sina kichaa. Najua ninachokifanya baba! Nisaidieni kumwambia Ibrahim kuwa nataka talaka yangu sasa hivi!” Pamela alisisitiza huku akionekana kujiamini.
Mzee Tugiramahoro alitaka kusema lakini akasita na kugeuza shingo yake kumtazama mkewe kisha akainua mabega yake juu na kuyashusha akionekana kuchanganyikiwa huku akiwa hana la kufanya.
Wazee wote walionekana kuchanganyikiwa, walimtazama Pamela wakiwa hawaelewi ni kipi kilichomfanya awaite, maana mwanzoni walidhani alikuwa amewaita pale kuja kutatua mgogoro wa ndoa yao lakini sasa alionesha kuwa alitaka wamsaidie kudai talaka! Mama Bigirimana alimwangalia Pamela kwa huzuni.
“Mama, ni sababi zipi hasa zimekufanya utake mumeo akutaliki?” Mama Bigirimana alimuuliza Pamela kwa sauti tulivu.
Pamela alimtazama yule mama huku aking’atang’ata midomo yake na kufikicha ncha ya nguo aliyokuwa amejitanda kichwani.
“Ni kwa sababu nampenda sana na ninathamini maendeleo yake… mama!” Pamela alijibu huku akiiangalia ile ncha ya nguo na kuwafanya watu wote wamwangalie kwa mshangao.
Wale wazee waliendelea kumwangalia Pamela kwa muda kisha wakaangaliana wenyewe kwa wenyewe. Ibrahim aliduwaa na kubaki akimwangalia Pamela kwa mshangao zaidi.
“Sasa, kama unampenda sana na unathamini maendeleo yake mbona unataka akuache?” Mama Bigirimana alimuuliza Pamela huku mshangao ukiwa haujamtoka usoni kwake.
Pamela alinyanyua uso wake na kuwaangalia kwa makini wale wazee, hasa Mzee Tugiramahoro na Mzee Bigirimana. Akaonekana kusita na kumeza mate huku akimtupia jicho Ibrahim. Muda ule Ibrahim alionekana kuchanganyikiwa zaidi, jasho lilikuwa linamtoka.
“Kwa sababu sioni sababu kwa nini tumlazimishe kuishi na mtu aliyepanga kumtaliki badala ya kuheshimu maamuzi yake, mbona yeye haulizwi kwa nini alitaka kuniacha na kuoa mwanamke mwingine na kwa nini sasa hivi ananiona nafaa?”
Kauli ile ikafanya pazuke tena ukimya, wale wazee wote wakabaki kimya wakimtazama Pamela kwa makini. Mama Bigirimana akashusha pumzi ndefu huku akibetua kichwa chake akionekana kumwelewa Pamela na kuafikia naye.
“Hilo nalo neno! Mimi nipo upande wako mama, wanaume wanapaswa watambue kuwa mwanamke si mtumwa, tena wewe umekuwa muungwana sana, mwanzo alipokuja hapa alisema yake lakini sasa hayasemi… kwa nini tumuonee haya mtu asiyetuonea haya?”
Ibrahim aliwaangalia wale wazee huku akionekana kugwaya sana. Aliinamisha uso wake akiwa hana la kusema, machozi yalianza kumlengalenga. Pamela alimtazama Ibrahim kwa makini huku akijitahidi kuyazuia machozi ambayo yalianza kumtoka.
“Baba Samantha, nakupenda sana, kwa nini nisikuache huru ukaishi na mwanamke unayempenda. Ulipanga kuniacha ili uoe mwanamke anayekufaa na sasa unaniomba msamaha kwa kuwa wazee wamekulazimisha kufanya hivyo, sijui hapa pendo liko wapi? Hivi utalazimishwaje kuishi na mwanamke uliyemchoka eti kwa kuwa wazee wamekulazimisha? Ndiyo maana nataka unitaliki ili uwe huru kutafuta pendo la kweli…” Pamela alimwambia Ibrahim kwa sauti tulivu.
“Mwambie mama, mwambie mpumbavu huyu,” Mama Bigirimana alidakia na kuwafanya watu wengine wageuke kumwangalia kwa mshangao.
Sasa machozi mengi yalikuwa yanamtoka Ibrahim, alitaka kusema neno lakini akashindwa kuwa kuwa maneno yalikuwa hayatoki, akaanza kulia kilio cha kwikwi. Muda ule ule aliinuka, akamfuata Pamela na kuanguka miguuni kwake kisha akaishika miguu yake huku akiendelea kulia kwa uchungu.
Pamela alimtazama Ibrahim kwa huzuni, akajitahidi kuyazuia machozi yake. Mzee Tugiramahoro aliinuka na kumfuata Ibrahim, akamshika mabega na kumnyanyua kutoka pale alipokuwa amelala, kisha akampa ishara Mama Bigirimana akimtaka ainuke na kumpisha Ibrahim.
Mama Bigirimana alitii na kupisha, Mzee Tugiramahoro akamkalisha Ibrahim kando ya Pamela na kunyanyua kiganja cha mkono wa Pamela kisha akakikutanisha na kiganja cha mkono wa Ibrahim.
“Pamela, mumeo amejua makosa yake na sasa anataka muanze upya, sioni kwa nini usimsamehe…” Mzee Tugiramahoro alisema na kuwatazama wazee wengine.
“Na ikiwa mimi ni mzazi wenu, basi kwa niaba ya wazazi wenzangu wote naiombea kwa Mungu ndoa yenu idumu zaidi na zaidi, isiwe na migogoro tena wala visasi,” Mzee Tugiramahoro alisema na watu wote pale sebuleni wakaitikia, “Amina!”

MWISHO.

Daah Inahuzunisha...

Ingeendelea kidogo ili tuone Ibrahim anavyoipata joto ya jiwe...

Chapter Closed...


Cc: mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom